Mvua zasababisha Mlima Kawetere kumeguka Ujiuji wafunika nyumba 20 kata ya Itezi Jijini Mbeya

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 13 апр 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Cde Juma Z. Homera amefika Mlima Kawetele uliopolomoka Alfajiri ya Leo na Kusababisha Kufukiwa kwa Nyumba 20, Ng'ombe Wanne na Kuharibika kwa Miundombinu ya Shule ya Generation katika Mtaa wa Gombe Kata ya Itezi Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
    Akizungumza baada Kuwasili eneo la Tukio RC Homera amekanusha Uvumi unaozagaa Mtandaoni ukidai Kuna Maafa katika tukio hilo ambapo amesema zaidi ya hivyo vilivyotajwa Aya ya Kwanza hakuna Madhara mengine Wala Maafa kama inavyoripotiwa na Baadhi ya Watu.
    Aidha Homera ameiagiza Halmashauri ya Jiji la Mbeya kufanya Tathimini juu ya Waathirika hasa wale wasio na Malazi ya Kulala wahakikishe wanapatiwa Sehemu hizo wakati huu ambao Serikali inaendelea kupambana kuhakikisha Hali inakuwa Sawa katika Maeneo hayo.
    Pia amekiagiza Kitengo Cha Ardhi Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuacha kuwapimia Wananchi Viwanja eneo lenye Changamoto hasa ya Mkondo wa Maji kwa kufanya Kwao hivyo kutasababisha Matatizo kama hayo ambayo yangeweza kuzuilika.
    Tukio hilo limetokea Alfajiri ya Kuamkia Leo ambapo chanzo Chake ni Mvua zinazoendelea Kunyesha Mfululizo na Matukio yanayofanana na haya yamekuwa yakitukia Mikoa Mbalimbali ikiwemo Mikoa ya Arusha na Lindi.

Комментарии • 150

  • @emmanuelgadau266
    @emmanuelgadau266 20 дней назад +2

    Poleni sana ndugu zetu Tuombe Mungu aturehemu wa Tz atuepushe na majanga yote

  • @user-ls2nq2eq3l
    @user-ls2nq2eq3l 21 день назад +3

    Ifikie wkt tuungane kumuomba Mungu msamaha mbona nyuma haya hayakuepo tukae chini tutafakari bila kujali itikadi za dini. Mungu anasamehe katikati ya ghadhabu anakumbuka rehema😭😭😭😭

  • @shabelibashili2064
    @shabelibashili2064 21 день назад +9

    Jaman mwaka wamajanga huu kila kukicha matukio

  • @Elias-gy8qu
    @Elias-gy8qu 8 дней назад

    Poleni sana ndugu zetuni. Ila tujueni kwamba mungu yupo na mungu anawesa tuwacheni kumuhuzi mungu tuwacheni kucheza na mungu maan kwasasa binadamu tumekua tukizecha na mungu kwa mufano watu wengine wamekua wakiabudu binadamu badala ya kumuabudu mwenyzi waongo tu ebu tumurudieni mungu wetu maan emeanza kuruonyesha kwamba yupo

  • @rosinamtauka9933
    @rosinamtauka9933 21 день назад +6

    Mungu baba tunaomba tusamehe sisi waja wako kwa kutenda maovu mbele zako , tuepushe na majanga ya aina yoyote yale

  • @simonissa-rz5rl
    @simonissa-rz5rl 13 дней назад

    Polen sana ndg zetu Mungu awatunze mliyokutwa na matatizo

  • @user-dx1hz3ow7k
    @user-dx1hz3ow7k 21 день назад +1

    Poleni sana ndg zangu wa Mbeya Mungu aweke wepesi mvua za mwaka huu kira sehem majanga kikubwa tumombe Mungu atuwekee wepesi

  • @user-ts8gy9rv2q
    @user-ts8gy9rv2q 21 день назад +3

    Poleni sana watanzania wenzetu tumombe sana mungu .

  • @solomondanny-1507
    @solomondanny-1507 21 день назад +1

    Poleni sana. Haya ndiyo yaliyotupata huku Katesh HANANG Manyara.

  • @nikodemmwahangila3334
    @nikodemmwahangila3334 20 дней назад

    Poleni sana wahanga poleni mkuu wa mkoa na mbunge na Rais wetu Mungu iponye Tanzania

  • @jordanmwamlima7579
    @jordanmwamlima7579 21 день назад +6

    Dah! Mkuu wa Mkoa instead of giving a way out kama mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama, wewe unazugumzia kuwa mbunge anatamani kupaa!? Sasa kupaa kwa mbunge kwenye madhira haya kusaidie nini!? wewe ndiye mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama sio huyo mbunge, so baadala ya kuzungumzia habari za ambaye hawezi kufika hapo Kwa muda huu, saidieni watu waliopata madhira common man, unasema mbunge ana protocol gani kwenda kuona watu wake walioathirika na hilo balaa jimboni kwake!?, hapo haendi kama speaker bali anaenda kama mbunge brother, please tunaomba saidieni watu hawa baadala ya hizo siasa.

  • @samwelrobertmwakatobe6467
    @samwelrobertmwakatobe6467 21 день назад +2

    Ilikua mwaka 2010 nikiwa mfanyakazi wa Sogea satom tulikua tunajenga tenk la itez lkn nikaona maajab ya wananchi wakulima katika mlima kawetere nakumbuka niliwahi kuandika kuhusu athali za kilimo Kando ya mlima na nikasema Wilayan ya Rungwe Ina mvua nyingi wilaya imepiga marufuku kilimo kwenye minuko hivo mlima kwetere ulitakiwa kua ni mlima wa hifadhi chini ya uangalizi wa wizara husika,kwa mgeni yeyote akififika mbeya atashangaa jinsi mlima ulivyo vamiwa na wakulima na wajenzi hii ndio mbeya

    • @evancedaniel-xp1kd
      @evancedaniel-xp1kd 21 день назад

      Wiki iliyopita nilishangaa watu walivyolima juu mlimani na makazi yapo chini na serikali ipo kimya, tusipochukua hatua tutashuhudia zaidi ya haya

  • @dicksonkilupa2258
    @dicksonkilupa2258 21 день назад +5

    SHIDA SANA, UKIKAA MLIMANI UNAPOROMOKEEWA NA UKIKAA BONDENI UNAFURIKIWA NAMAJI, SASA TUKAJENGEE WAPI?

  • @selinageogre2881
    @selinageogre2881 21 день назад

    Poleni sana ndugu zetu Mungu atusaidie sana majanga mengi huu mwaka

  • @mbokamwakalinga796
    @mbokamwakalinga796 20 дней назад

    Pole sana wenzetu Mungu awatie nguvu na awape faraja ya pekee.

  • @SolomonMwankuga
    @SolomonMwankuga 21 день назад +1

    Poleni sana ndugu zangu

  • @user-pm9fp9ib1o
    @user-pm9fp9ib1o 21 день назад +3

    Hii ni sauti ya Mungu inataka tubadilike

    • @mwanakombopopo5117
      @mwanakombopopo5117 21 день назад +1

      Tena nikazi dogo sana kwa mungu kutuondolea majanga kama tutarudi kwake kuomba toba na msamaa😢😢😢😢

  • @FredyRajabu
    @FredyRajabu 20 дней назад +1

    Poleni sana wahanga

  • @LuganoMwanjabala
    @LuganoMwanjabala 21 день назад +1

    Jamani poleni sana wapendwa

  • @ibrahimdotto5234
    @ibrahimdotto5234 21 день назад +1

    Poleni ndugu zetu

  • @jesusbrother7684
    @jesusbrother7684 18 дней назад

    Mbeya yote ina takiwa ku fanyiwa “MASTER PLAN”, ambayo ita saidia sana ku epusha maafa makubwa kama haya. Tuna mshukuru MWENYEZI MUNGU kwamba, hakuna kifo kilicho tokea kwa mwanadamu yeyote. Amen 🥺🙏🏾

  • @SaimonTanzaniaTanzania-ty5cz
    @SaimonTanzaniaTanzania-ty5cz 21 день назад

    Poleni Sana ndugu zangu watanzania na wanambeya, tumuombe MUNGU ni mwema kwetu

  • @zainabumartin9520
    @zainabumartin9520 21 день назад +2

    Jaman kunakitu tz siobure

  • @patrickmfundiri8669
    @patrickmfundiri8669 21 день назад +1

    Tuwe karibu na Mungu ndugu zangu

  • @MuhammadRukali
    @MuhammadRukali 17 дней назад

    poleni sana ndugu zetu

  • @MWASHOTA
    @MWASHOTA 21 день назад

    Poleni Sana ndugu zetu

  • @samsonmogire3975
    @samsonmogire3975 21 день назад

    Poleni ndugu zetu.

  • @rachelmapuli7482
    @rachelmapuli7482 17 дней назад

    Poleni ndg zetu wa Mbeya Mungu awasaidie

  • @laurianpatrice3711
    @laurianpatrice3711 21 день назад

    Pole sana🎉

  • @user-hf5uz3sm1x
    @user-hf5uz3sm1x 21 день назад

    Poleni sana ndugu wote mungu atawasimamia

  • @dicksonkilupa2258
    @dicksonkilupa2258 21 день назад +1

    Poleni sana ndg zetu huko mbeya Mungu awatetee mvuke hili janga. Lakini je wwatu wetu wore wako salama?

  • @laylayl5166
    @laylayl5166 19 дней назад

    Poleni sana nduguzetu

  • @user-gm1ry3ej9o
    @user-gm1ry3ej9o 21 день назад +1

    Mungu tuteee kwa kweli maana hatuelewi hii mvua ni mvua gani wakristo tuombe

  • @user-xx8jx6tb7d
    @user-xx8jx6tb7d 21 день назад +1

    Duu Polen jaman Maana hyo ni vurugavuruga eeee Mungu wang, chakushkru uzma upo Maana ingekua uck wa manane huenda yangetokea mengne

  • @WilibroadPatrick
    @WilibroadPatrick 21 день назад

    Poleni sana

  • @NeemaMateleka
    @NeemaMateleka 16 дней назад

    Ee mola utulehemu tanzani yetu ili tope linataka nn tanzania jamani tumludie mungu nyakati hizi mungu anataka kusema nasi amina

  • @MerkiorHerman
    @MerkiorHerman 20 дней назад

    Poleni sana watanzania mlioko mbeya Kwa majanga hayo ya land slide.mungu awatie nguvu.

  • @magdalenasirikwa517
    @magdalenasirikwa517 19 дней назад

    Tukumbuke semina ya Mwalimu Mwakasege ya mwaka jana mwezi wa 3 .mambo mabaya yatakayoipata nchi kwa miaka minne .tuombe sana

  • @user-gl1hw8sp3j
    @user-gl1hw8sp3j 16 дней назад

    Poleni ndugu zetu Kwa janga

  • @DavidMlaga
    @DavidMlaga 12 дней назад

    Polen Sana watu mbeya kwachangamoto za mafuliko

  • @user-om7lv9cj3n
    @user-om7lv9cj3n 18 дней назад

    Izi mvua ni kuomba Mungu tu Kila sehemu inanyeshaa na madhara ni mengi.. aisee tuombee uzima maana hali inatisha

  • @Gonga94tz
    @Gonga94tz 21 день назад

    Poleni Sana mbeya

  • @user-dk5kk4rf3v
    @user-dk5kk4rf3v 21 день назад +1

    Waaambiwe na watu wa mwanza linakuja kwao wahame

  • @user-bw8wp3ek4w
    @user-bw8wp3ek4w 18 дней назад

    Poleni sana ndugu zetu wanambeya

  • @user-jx4rx6jy6y
    @user-jx4rx6jy6y 21 день назад +1

    Kweli mwakahuu nimajanga jaman tumuombee sana mungu

  • @HosianaMwasibata
    @HosianaMwasibata 21 день назад

    Daa pole sana nduguzangu mbeya pole

  • @agnessmalyeek9387
    @agnessmalyeek9387 13 дней назад

    Poleni sana Mungu awalinde

  • @salummohamed2689
    @salummohamed2689 21 день назад +2

    Jamani Kuna watu mji wa Singida wamejenga karibu majabali makubwa, serikali fanyeni tathimini ya stability ya majabali hayo kumbe huenda Kuna siku yataanguka na kuleta madhara Kwa watu.

  • @LUCASJOHN-so5it
    @LUCASJOHN-so5it 18 дней назад

    Polen sana

  • @jonijonita1528
    @jonijonita1528 19 дней назад

    daa kuna mwamba naona nyumba yake pale pembeni kwakweli anamshukulu Mungu tu,

  • @mamachris6811
    @mamachris6811 18 дней назад

    Tatizo ni pale tulipo acha uongozi wa ki chifu
    Machifu walikuwa wanaheshimiwa na kuogopwa
    Walikuwa wakikataza uharibifu wa mazingira,lilikuwa linatejelezwa
    Sasa rushwa imetawala,mwenye jukumu la kutunza mazingira hawawajibiki😮

  • @mamapeace6730
    @mamapeace6730 21 день назад

    Pore ndugu zetu mungu amewasaidia

  • @ElizabethWanjiru-mg9sj
    @ElizabethWanjiru-mg9sj 17 дней назад

    Poleni Mungu na awafanyie njia kwa yote

  • @user-vp6ol3kq6g
    @user-vp6ol3kq6g 21 день назад

    Poleni ndugu zangu

  • @Donald-uz9du
    @Donald-uz9du 20 дней назад

    Pole

  • @VeronicaMangula-ck3wr
    @VeronicaMangula-ck3wr 21 день назад

    poleni wahanga

  • @jeremiahmalasusa3997
    @jeremiahmalasusa3997 21 день назад +1

    Poleni tunasikitika wote Hakuna anaye furahia jambo hili

  • @LucyJoseph-pb4um
    @LucyJoseph-pb4um 21 день назад

    Duuuh Pole sana

  • @SalminKhamis-ok1tf
    @SalminKhamis-ok1tf 18 дней назад

    Tunamuomba tulia na mama samia awasaidie haraka mkoa wa mbeya

  • @neemasiwakwi6528
    @neemasiwakwi6528 21 день назад

    Poleni jamani Mungu awafanyie wepesi. Kweli hizi ni siku za mwisho

  • @RubenMtuwaMungu-bz8ee
    @RubenMtuwaMungu-bz8ee 21 день назад +1

    Tuweke hazina zetu mbinguni.

  • @barakamkumbo-rq7tx
    @barakamkumbo-rq7tx 13 дней назад

    Mnawatukuza machifu kuliko Mungu bado mtajua mpaka mumheshimu Mungu mtajua kuwa Mungu ni mkuu tena anaogofya yeye ni wakuogopwa mnatuletea ushoga Tanzania haya mnayoyaona yalisha wakuta watu wa sodoma na gomola yani wanawake kwa wanawake waoane kweli kisa misaada eti haki za binadamu siushetani huu kisa mikopo msituletee laana mkono wa Mungu umekuwa mzito juu utawala huu kama wa Nebukadreza jitakarini wapi mnlipeleka taifa hili.

  • @LaehKaduma
    @LaehKaduma 18 дней назад

    Poleni

  • @JaphethButa
    @JaphethButa 19 дней назад

    Haya yote niutimilivu wa kumalizika kwa dunia yesu Yuko njiani kutuijia jiandaeni viumbe asili vinaashiria

  • @ahmadjuma-xx5nd
    @ahmadjuma-xx5nd 19 дней назад

    Turudieni kwa mungu sana allah atuhifadhi na mitihani

  • @magrethkapinga1811
    @magrethkapinga1811 20 дней назад

    Polen sanaaa ndugu zangu

  • @barnabasstanslaus6895
    @barnabasstanslaus6895 9 дней назад

    Poleni sana wapendwaaa😢😢😢

  • @SaimonTanzaniaTanzania-ty5cz
    @SaimonTanzaniaTanzania-ty5cz 21 день назад

    Poleni Sana wanambeya

  • @DM_15
    @DM_15 20 дней назад

    Siku zamwisho niza hatari,Mungu atusamehe makosayetu

  • @Lukiapaulo-xz6sf
    @Lukiapaulo-xz6sf 21 день назад

    Dah mungu atunusuru na majanga Aya

  • @RamsiFrayera
    @RamsiFrayera 18 дней назад

    Poleni wanambeya wenzetu

  • @eliakimrichardkyaruzi4985
    @eliakimrichardkyaruzi4985 18 дней назад

    Mbn matujio haya utokea jumapili

  • @benjaminiykamwelabenjaminiykam
    @benjaminiykamwelabenjaminiykam 21 день назад

    Polen wote mlio patwa na mahafa hayoooo mungu awaponye na mahafa yalio tokea Jana

  • @Ndushikayungilo722
    @Ndushikayungilo722 19 дней назад

    Poleni nyote mnaokubwa na janga hili

  • @OmaryNelson-bh8ij
    @OmaryNelson-bh8ij 20 дней назад

    Poleni saana jamaan

  • @veronicaaugust1793
    @veronicaaugust1793 18 дней назад

    POLENI SANA WAPENDWA

  • @EmmanuelSima
    @EmmanuelSima 21 день назад

    Poleni sana jamani

  • @BennyMahenge
    @BennyMahenge 20 дней назад

    Poleni jamani

  • @user-bw8wp3ek4w
    @user-bw8wp3ek4w 18 дней назад

    Eee Mungu tusaide tz

  • @user-qz8gp4im5z
    @user-qz8gp4im5z 20 дней назад

    Duuh poleni majirani zangu itezi😴

  • @MohdShaali
    @MohdShaali 21 день назад +1

    Ndugu jamaa na marafiki tuweni pole na hayo mafuriko

  • @EsitaDavid2-wp1uf
    @EsitaDavid2-wp1uf 10 дней назад

    NI WAKATI WA TOBA MATHAYO 24

  • @EliaMwakipesile-fz5is
    @EliaMwakipesile-fz5is 21 день назад

    Poren sana mungu atusaidie tu

  • @CandyMwahalende-yv2gs
    @CandyMwahalende-yv2gs 21 день назад

    Duuuu😢😢 polen sana ndugu zangu

  • @OscarManyamayangapigahao
    @OscarManyamayangapigahao 20 дней назад

    Power sana kwa mfuliko

  • @ZawadiSakamela
    @ZawadiSakamela 19 дней назад

    Mungu awasaidie

  • @PetroKalinga-jq6ih
    @PetroKalinga-jq6ih 19 дней назад

    Poleni watanzania wenzet

  • @user-kp2jf5jc2i
    @user-kp2jf5jc2i 20 дней назад

    KAULI YA KITAIFA YA KIONGOZI WA NCHI WA KWA WANANCHI KWA IMANI ZAO ITATOKA LINI?

  • @michaelkilimo8296
    @michaelkilimo8296 17 дней назад

    Polensa

  • @JosiaEnock
    @JosiaEnock 20 дней назад

    Polen ndugu zangu

  • @millitarybattalion7515
    @millitarybattalion7515 21 день назад +1

    Hii mvua.. daaa

  • @semeninyumayo2336
    @semeninyumayo2336 21 день назад

    pole sana hatari mwaka huu

  • @HasaniShija-ye5xg
    @HasaniShija-ye5xg 20 дней назад

    Atari sana jamani mungu atusamehe turipomkosea maana majanga kira kukicha

  • @janemushi850
    @janemushi850 21 день назад

    Tumuombe tuu Mungu atunusuru maana hatuna ujanja dunia na vyote vilivyomo ni mali yake

  • @gloriaamase9764
    @gloriaamase9764 21 день назад

    Wah pole mama😢

  • @BarakaGabrielMwampamba-kj8ci
    @BarakaGabrielMwampamba-kj8ci 20 дней назад

    Niongee ukweli tuu mazingira tunaharibu wenyewe binadamu rakin wataaramu wa majanga wanasema majanga yanayo tokea duniani % 96 tunasababisha binadamu % 4 tuu ndo majanga ya asili ya mwenyezi MUNGU mwenyewe

  • @NuruMbongo
    @NuruMbongo 21 день назад +1

    Poleni ndugu zangu wana mbeya hiii mvua inatisha tunashukuru Mungu kwa uzima aliowachia

  • @msafwatv432
    @msafwatv432 21 день назад

    Daaa pôleni sana jamani nyumbani hapo

  • @douglaskomba2304
    @douglaskomba2304 21 день назад

    Mwakasendo

  • @japhetgeofrey2063
    @japhetgeofrey2063 21 день назад

    E Mungu utusamehe maasi yamezidi