Salama Na TOUFIQ SE6 EP73| um'PENDAE PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 25 июн 2023
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Toufiq ni moja ya majina makubwa kati ya wafanya biashara wazuri na sasa mwanasiasa na Mbunge wa Mpendae, kwa wazee na vijana wa visiwani humo yeye ni mmoja wa mifano ya kuigwa ingawa kwake yeye yaliyo mengi kwenye maisha yake ni nguvu kubwa ilifanywa na Marehemu Mzee wake Ndugu Salih Hassan Abdullah Turky aka Mr White ambaye na yeye akiacha ukweli kwamba alikua tajiri na mfanya biashara nzuri huko visiwani ila yeye pia alikua kipenzi cha wananchi wa Jimbo la Mpendae ambapo sasa Toufiq ndo anaye liongoza jimbo hilo baada ya Mzee wake kutangulia mbele ya haki. Mwenyezi Mungu Amrehemu.
    Kwenye meza yetu ya kigae na kiti chetu kikukuu Taufiq anakumbuka wakati wa msiba wa Mzee wake bado wa moto kabisa watu walikua wanakuja nyumbani kwao na kumshauri yeye agombee ubunge wa jimbo hilo ambalo Mzee wake alikua akiliongoza. Ikumbukwe Mzee wake Mr White alifariki kipindi ambacho wananchi walikua wanajiandaa kwa uchaguzi wa wabunge wawakilishi na Rais, ananiambia kwanza aliwafukuza watu hao, wakarudi tena baada ya maziko bado Toufiq akawakatalia, baadae baada ya mambo kutulizana na kuombeleza kupungua watu ambao anawaheshimu walimfuata tena na kumueleza umuhimu wa yeye kugombea jimbo hilo. Wakamuelezea umuhimu wa Marehemu Mzee wake kwa watu wa Mpendae na kwamba kama hatofanya hivyo basi haitakua jambo zuri kwa wakazi wa eneo hilo. Ndugu Turky ilibidi akubaliane na ombi hilo na kutimiza matakwa ya wana Mpendae ambao walimpa kura nyingi za ndio.
    Yeye mawazo yake yalikua kwenye kuendeleza biashara zaidi ambayo kwa kiasi kikubwa Mzee wake alikua alimshirikisha nayo toka akiwa mdogo. Kuweza kufanya yote hayo kwa kijana mdogo kama yeye pengine ingekua mambo mengi sana so kwa heshima wakati mambo mengine yanaenda Toufiq ilibidi aachie majukumu mengine kwa Mdogo wake wa Kiume Ndugu Abdallah Salim na Dada yake Bi Khaytham Salim Turky, ingawa bado yeye ndo Mwenyekiti wa makampuni hayo ambayo yamejikita katika biashara mbali mbali ambazo zimestawi visiwani Zanzibar na nchi nyengine.
    Toufiq alikuja kwenye maongezi haya akiwa na mambo yake mengine ya ki majukumu kwenye meza yake na ki ukweli hatukupata wasaa teeele wa kuweza kuyachambua mengi kama ambavyo tungependa lakini pia hatukukosa lolote jambo la lolote jambo hilo ndo tumaini letu litasaidia kwenye kukusogeza kwenye sehemu fulani katika uelewa na uchambuzi wako wa mambo.
    Tafadhali enjoy hiki kidogo ambacho tuliweza kukukusanyia kwenye muda mchache.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪RUclips Link bit.ly/RUclipsSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • РазвлеченияРазвлечения

Комментарии • 37

  • @sundaylema249
    @sundaylema249 Год назад +3

    Huyu jamaa ni genious from day one nilimuona!appart from that he is down to earth person!

  • @barashially6136
    @barashially6136 Год назад +5

    Tuletee joel nanuka ni mtu mweny madini mengi sana

  • @ahmedhafidh3515
    @ahmedhafidh3515 Год назад +4

    Salama.....JOEL NANAUKA tuletee tafadhali..

  • @jumamuhammed7421
    @jumamuhammed7421 Год назад +11

    Salama jitahid kukumbusha sana unaowahoji wazungumze kiswahi.

    • @prof.ibrahim1883
      @prof.ibrahim1883 Год назад

      😂 pole

    • @salamisindimwo303
      @salamisindimwo303 Год назад +1

      yaaani, kidhungu cha jumla na reja reja...tulokimbia somo la ngeli darasani interview hiyi hatufui dafu...nimejua ku😂😂😂

    • @user-xf1xq3ky2w
      @user-xf1xq3ky2w 7 месяцев назад

      ​@@salamisindimwo303kingereza kutojua sio kukimbia shule tu unaweza jifunza

    • @raymoshmikidadi87
      @raymoshmikidadi87 3 месяца назад

      Kwani kingereza huelewi? Jitahidi ujifunze japo kidogo kama huelewi ndio usikwazike

  • @faridaalawy7290
    @faridaalawy7290 2 месяца назад

    I like him his is our brother may Allah bless him

  • @idrisanassor7744
    @idrisanassor7744 Год назад

    Hongeraa snaa

  • @jaaffarabuu6750
    @jaaffarabuu6750 Год назад

    Nzur❤

  • @susancharles1660
    @susancharles1660 Год назад +3

    Huyu ameishi nje ya nchi simlaumu kuongea kiingereza lkn unakuta mtu yupo bongo hata hajawahi kwenda Kenya ndio anajifanya km anatafuta maneno ya Kiswahili

    • @MrNdanguza
      @MrNdanguza Год назад +1

      Hahahaha duh nimecheka sana

  • @stevennyondo2215
    @stevennyondo2215 Год назад

    Thanks 👍

  • @flackomasterbaddest4155
    @flackomasterbaddest4155 Год назад +1

    Very bright guy

  • @josephmaganga9948
    @josephmaganga9948 2 месяца назад

    Salama safari hii umechemka kwenye lugha

  • @user-ik7wu5bi8g
    @user-ik7wu5bi8g 2 месяца назад

    Baba yko alikuwa Mtu Mzuri sana ila Chawa wake ndio walimuharibia Mzee.Kwa Jimbo La Mpendae Wabunge bora 2 tu.Issa Baharia na Turkey(Allah warehemu)

  • @bedabenson6576
    @bedabenson6576 Год назад +2

    Tuletee Juma Mgunda

  • @godfreymiho4927
    @godfreymiho4927 Год назад

    🔥💯👊

  • @tanganigga3499
    @tanganigga3499 9 месяцев назад +1

    Inakera show za kiswahili ziongelewe kingereza
    😎

    • @user-xf1xq3ky2w
      @user-xf1xq3ky2w 7 месяцев назад

      Watu wa aina tofauti wanapita hapo

  • @husseinwemmar6217
    @husseinwemmar6217 Год назад +2

    Mlete mzungu salamaaaa🤣🤣🤣

  • @lucianmartin-kn9xj
    @lucianmartin-kn9xj Год назад

    Tunamuomba dj joozey

  • @mrfashion1687
    @mrfashion1687 Год назад +1

    Tuletee soudy brown na ikiwezekana avue lile kofia lake

  • @user-mq6lu2po3y
    @user-mq6lu2po3y 7 месяцев назад

    Maziko ya baba yake Kuna watu hawakuweza ata kuiona nyumba ya marehemu Wala hawakuona jeneza la marehemu kwa watu walivyokua wengi

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 Год назад

    😘

  • @idrisanassor7744
    @idrisanassor7744 Год назад +4

    Ilkuwa tunaomba intavew ya jb

  • @yustomakangula2361
    @yustomakangula2361 Год назад

    Juma Mgunda fanya naye kipindi

  • @ahmuhally4430
    @ahmuhally4430 Год назад +2

    Anaboa anaongea sana Kingereza wengine hatuelewi

  • @stonetown578
    @stonetown578 3 месяца назад

    Masha'Allah

  • @Hakunamatata_shop
    @Hakunamatata_shop 2 месяца назад

    salama mtafute @sale said wa ZMMI Zanzibar