Ripoti Maalumu|| Vivuko Kigamboni, Bomu linalosubiri kuingiza nchi kwenye maafa
HTML-код
- Опубликовано: 25 май 2024
- Usalama wa zaidi ya watu 60,000 wanaotumia huduma ya vivuko kuvuka Kigamboni na Magogoni kila siku upo katika mashaka.
Mashaka ya usalama wa watu hao, yanatokana na ubovu wa vivuko hivyo, unaosababishwa na kutofanyiwa matengenezo makubwa kwa mujibu wa sheria, ratiba na matakwa ya kitaalamu.
Hali hiyo inazua hofu ya kuharibika kwa vivuko hivyo vikiwa safarini, kama ilivyowahi kutokea mara kadhaa vyombo hivyo vya usafiri wa majini vilipozima vikiwa na abiria katikati ya maji.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), kwa siku ni zaidi ya abiria 60,000 wanaohudumiwa katika vivuko vya Magogoni-Kigamboni.
Uchunguzi wa Gazeti la Mwananchi, umebaini vivuko hivyo aghalabu hupitiliza muda wa matengenezo makubwa, ambayo ndiyo msingi wa uhai na ufanisi wake.
Soma kwa undani kupitia www.mwananchi.co.tz
Asante MUNGU umesikia kilio cha wana kigamboni
kwan serikal s imejenga daraja kapiten darajan bana
Serikali ya CCM imechoka
Piteni darajani
DUH HTR XNA
Mbaya zaidi ni idadi kubwa ya abiria wanaoingia bila idadi mpaka unaogopa kupanda
Pia watu wanaingia wengi inafaa waweke idadi yawatu na magari
Si naona kunajengwa Daraja lakini?
Mpaka watu wafe ndiyo wanaanza uchunguzi