NIMEONA YANAYOFANYIKA HUKO, KWETU YANAWEZEKANA PIA.

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 окт 2024
  • Mhe.Mwanaidi Ali Khamis Naibu Waziri wa
    Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Makundi Maalumu amepongeza kikundi cha Twaweza Kilichopo Kata ya Mji mwema Halmshauri ya Mji Njombe kwa kutumia Fursa za Mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na Halmashauri .
    Naibu waziri ametoa Pongezi hizo Julai 05,2024 alipotembelea eneo la uzalishaji la kikundi cha Twaweza ambacho kinazalisha bidhaa mbalimbli za Ushonaji jambo ambalo limepelekea kuzalishwa kwa ajira nyingine ambazo zimetokana na mkopo huo ambao walipewa na Halmashauri .
    "Tumezoea kuyaona mambo haya China lakini kwa juhudi za Serikali tunayaona katika Nchi yetu niwapongeze vijana kwa uthubutu wenu wakufika na kujiunga na kikundi hiki na pia niombe vijana kuweni mabalozi wazuri kwa wale ambao bado hawazijuwi fursa hizi " Alisema Mhe.Mwanaidi Ali Khamis Naibu Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Makundi Maalumu.
    Aidha Mhe Naibu waziri ameiomba Idara ya Maendeleo ya Jamii kuendelea kutoa elimu juu ya ujio wa mikopo ya asilimia kumi ambayo itatolewa na Halmashauri kupitia Benki.

Комментарии • 1