Ukiangalia hzi comments utaona waislamu bado tuna kazi kubwa ya kufanya. Sheikh zubeir anafanya kazi kubwa sana kwa hekima kubwa mno. Tuwe na tabia ya kusoma dini yetu badala ya kusoma mawazo ya watu. Allah atuongoze na asafishe vinywa vyetu mbele ya maulamaaa
Mufti ni MTU mzuri inshallah ataonyesha jitihada zake ili mashekhee wa uhamsho waachiwe huru nadhani ndicho kilio cha waislamu wengi kwani hakika wamejifunza kwa makosa yao na inshallah kama wakina babu seya waliachiwa basi raisi wetu mpendwa jpm inshallah atawaweka huru mashekhee amina.
Duh! Tuwe na hofu na Allah.Siku Rais alipokutana na viongozi wa dini, Mchungaji 1 aliomba kurejeshwa kwa mchungaji mwenzao aliye ughaibuni!!! Shekhe wew ulishindwa vipi kumwambia Rais awaachie huru Waislam wa UAMSHO???!!!
Mdomo ulimponza kichwa, uamsho waliponzwa na mdomo, hii nchi ni tofauti na nchi za kiharabu haiongozwi na Islamic sharia kwa hiyo ukitaka kulazimisha Tanzania hii watu wake wafate sheria za kiislamu lazima utaingia pabaya tu ndio kinachowaumiza uamsho. Wanavuka mipaka mpaka wanajisahau wanaona kama vile nchi hii haina serikali hiyo sio sawa lazima tujifunze kuheshimu mamlaka zilizowekwa kisheria hata mungu amearisha hivyo.
Povu lanini Sheikhe? mnazani kuwatisha watu ndio tuwaogope na tuwafuate hilo sahau hii sio nchi ya kidini kila mmoja atangaze imani yake bila ya kutishana.
Hakika BAKWATA ni chombo pekee cha kuendeleza uislam katika nchi hii mana mpaka kwenye kijiji uongozi wenu upo, lakini bahati mbaya sana hakuna uadilifu na mipango madhubuti ya kuendeleza uislam. Kama mngekuwa mnafanya kazi zenu vizuri kwa mujibu wa sheria za dini kweli, hakika hata omba omba na watoto wa mtaani pengine wasingekuwepo. Waislam wamepoteza imani na BAKWATA, inapaswa kurejesha imani iliyopotea kwa baadhi ya waislam. Msiwe kama viongozi ambao wapo wapo tu madarakani kwa kuwa wanapata maslahi binafsi, tuwe viongozi wenye kujali maslahi ya umma.
Weunasema tuu unajua kinachotokea zaidi katika huo upande wa pili Unaujua mkataba wa mou ww acha kujisemea kama hujui japo kweli madhaifu yapo lkn kwa kiasi kikubwa hujuma zimetawala
Kauli ya muft wa tz sio kauli ya mwisho kabisa maana hii sio nchi ya kiislam ingekuwa ya kiislam ingekuwa nchi ya kiislam ingekuwa ni kauli ya mwisho, mufti mwenye kauli za ni mufti wa Saudi Arabia, Oman, mascat nk ambako ni nchi za kiislam
A.alykm..ndugu yngu hemu kasome tena qur an ili ujue inasema nn juu ya viongoz wenu ktk nchi...yan uxije kusema kuwa mufti sio mtu wa mwsho katk nchi yetu coz utachekwa wakisikia waliosoma dini...
@@habibtalib5100 sheikh tz sio nchi kiislam, kauli ya muft wa tz haiwezi kuwa kauli ya mwisho kwa tz labda ni ya mwisho kwa bakwata wenyewe hili halina hoja
Wewe nani kwani umekua Mtume wewe fanya kazi ya serikali ndio waliokuchagua mambo ya uislam waachie waislam wenyewe sio kuitwa sheikh mkuu ww ndio wa2 wasiongee
Msafishe vinywa vyenu mbele ya maulamaa. Hamtafikia uchamungu wa mamufti wa Tz. Kuweni na heshima na adabu kwa akili hizi albabu ndgu yangu abajana unakoelekea siko
Mtihani kweli sasa kama nchi ambazo nyinyi mumefungua nazo 56 kama mlivyo sema je nchi zaidi ya 140 zimefungua Eid siku gani? Walifikiri duniani kunanchi 60 nini?
Naam uturuki ulingani na Tanzania kwa nn unalingabisha shughuli za serikali na dini kwa kutofautiana kulianza Tanzania kwa nn kuwabana masheikh wengine na wao wana mshango mkubwa wa kuhamasisha watu kwa nn ukataze watu kusema .
Ili uamike kwa WAISILAM kwanza utuungunishe WAISILAM WOTE, na pia uyarudishe mali zote za WAISILAM ambazo walio kutangulia waliyagujumu hapo tutakuamini
Mhhh mm nafikili taasisi hapa tz zip nyingi sasa mzee usijibebeshe mzigo usio uweza wewe ni mufti wa wafuasi wa bakwata sio wa waislam wote Tanzania uo ndio ukweri,,,na usiwalazimishe watu kufuata matakwa yako, kila mtu afuate zehebu lake bila kukashifu lingine
Bakwata ni taasisi kama taasisi zingine hivyo haina haki ya kuingilia uhuru wa taasisi zingine, yeye ni msemaji wa taasisi ya Bakwata hivyo awe na busara na hekima katika mambo ya dini, Bakwata ni taasisi ambayo mara nyingi iko kinyume na quran na Sunnah ambayo Ndio mihimili ya uislam popote duniani, bakwata ni wasimamizi wazuri wa bida'a na usufi jambo ambalo liko mbali na uislam wa Mtume swalla llaahu a'laihi wasallam na maswahaba zake, hivyo basi, hoja za mufti haziko kielimu kwani zimejikita zaidi katika jazba, ubabe na vitisho,... Jambo la funga ya arafah nilitarajia kumsikia mufti akisema kwamba ni jambo la khilaf lakini yeye anazungumza kama jambo la kukata, masuala ya khilaf kama ulivo utaratibu wa wanachuoni kwamba watu wapeane udhuru japokuwa katika khilaf Kunakuwa na msimamo /qauli yenye nguvu, kama mufti aombe radhi kwani maneno yake yako kinyume na utaratibu wa khilaf ambapo ziko qauli za wanachuoni wakubwa wenye fatawa mbalimbali ambao yeye bado ni mwanafunzi kwa wanachuoni hao mfano, sheikhul Islami ibn Taymiyyah na wengine miongoni mwa wanachuo wa tafsiir,." Hakuna kumtii kiumbe katika kumuasi Allah ".
Ndugu yangu nakushauri usirudie tena kauili kama hizi hasa kwenye hadhara kubwa km fb unayejaribu kumvunjia heshima sina shaka ni miongoni mwa Wachamungu jirudi ndgu kabla Allah hajakurudi
Said miraj kuwa wingi ndiyo unajiona mumeongoka Mimi nakwambia usijifaharishe kwa uwingiwenu aliye waumba ndiye anaetujua kwa iyo usijifaharishe kwauwingi inawezekana haokidogo unaowadharau kwa aliye tuumba wakawa wanathamani kubwa kuliko nyie wengi
Ungesoma historia usingesema hayo. Waislam hawakutambui wewe kama kiongozi wao. Taasisi yako imesajiliwa Rita kama ilivyo almallid au taasisi nyingine yeyote. Kwa upande wa wakristo kuna katoliki, Lutheran au SDA. Kila mmoja ana mipangilio yake na wana wasemaji wao. Acha kutafuta sympathy . Hii ni nchi isiyo na dini.
Kama wewe kiongozi wa waislam mbona huwatetei waislam wenzetu wapo jela masheikh wa Zanzibar upo kimya kazi unafiki tu subir Allah. Atakavyokuja kukuuliza .. Usitupotezee muda hapa huna kimoja bakwata ni taasisi ya ccm kwani hujui ivyo .. Washenzi wakubwa Allah atawalipa kwa dhulma zenu
Bakwata chini Muft Zuber ipo vzuri inajitambua majukumu yake nyie Wahabi mnafahamika ni wapotoshaji wa Dini.Kama leo mnalaumu kuwa Bakwata ni taasisi hyo taass ya Dini mnayoifuata huko Saudia ipo chini ya nani kama cyo chini ya Ufalme unaolindwa na Marekani ,Mayahudi na Uingereza.Tafuteni historia ya Saudia nn kilisababaisha Utawala wa kifalme kuundwa
BIG BROTHER ALWAYS RIGHT TUMEUCHEZEA SANA UISLAM KWA MASLAI YETU BINAFSI NA SASA IANZE KUWA MWISHO NAAM MUFTI MAANA BINADAM WANAANGALIA NETWORK TIME AWAANGALII NYAKATI........TENA UMEONGEA KIDOGO KIONGOZI WANGU ULITAKIWA UKOMESHE KABISA
@@hamidudongo1879 heri ya wewe ulie na elimu ya ghaibu na kutukana wakubwa na waliopass kukuongoza,kaa hivyo hivyo Wenzako ndio viongozi tayari na huna ulijualo hata vitabu vitatu tuu tofauti vya kuelekeza Uislam sijui kama unavyo ndani kwako.💣💣💣💣💣 wewe
@@akimmbwego797 Muislam mzima unakuwa Muongo. Kuna TUSI LOLOTE nililotoa hapo?? Tumia akili sio unafuata tu. Wewe mbona haufuati taasisi zengine na huambiwi umetukana?? Uwongo uwongo tu. Niambie TUSI nililotoa hapo kama umesema ukweli. Muislam mzima unazusha maneno maneno tu. Ukweli utabakia pale pale kwamba Waislam wengi wanahama kutoka Bakwata. Huo ndio ukweli hata akisema kama wewe unavyo sema angesema zaidi. Kama wewe unavyopenda kuwa Bakwata na wawe msemaji wako mkuu; wengine tunasikiliza Taasisi zetu kama Wasemaji wakuu wetu. Kuikataa Bakwata na kuona haturidhiki na uongozi wao- sio tatizo wala MATUSI. SINA SHAKA WALA WASIWASI NA UCHAMUNGU WAO BAKWATA AU ELUMU YAO HATA KIDOGO. Ila baadhi hatutaki kuongozwa na Bakwata pamoja wanasaidiwa na serikali pamoja na BAADHI ya Taasisi zisizo za kiislam. SIJATOA TUSSI LABDA NI WEWE NDIO UNAYETUKANA. ACHA UWONGO UONGO.
Kwanza ww nimufti gani unaeshindwa kuwatetea hata mashekh walikogerezani haija sikilika hata aikumoja sauti yako kuhusu mashekh halafu unatudaganya eti mswmaji wawa Islam hilo siobarza lawa isilam hilo nibaraza LA serekali we tetea tu ugali wako msemaji wawa isilam wote hayupo tena katka DUNIA hii limebaki jina lake na sifa zaketu utakua ww mnafiki WA uwisillam
HAO MASHEKHE WATETEWE ILI NINI NA HUKU NDIO WANAO LETA MGAWANYIKO BAINA YA WAISLAMU? HAO HAO SI NDO WALOKUWA WANAIPINGA BAKWATA?KWENYE MAAMUZI YENU YA HOVYO HAMUMJALI MUFTI,ILA MKIBANWA NA SERIKALI MWAMUONA MUFI NI WAMUHIMU
Mashaallah mufti umeongea,lakini tungependa kujifunza kutokakwako Hakuna wanawazuoni wakubwa kuliko au zaidi ya hao mamufti unao wataja walio toa fatwa zakukubali mwezi wa popote Duniani?kama wapo ndio haowasionaelimu?na wanahaki waliowakubali fatwa zao kuwafata au haifai?.
uturuki na tanzania tofauti na saudia huwezi kuilinganisha na tanzania maana tanzani sio nchi ya kiislam saudia ninchi ya kiislam lazima iwe na msemaji mmoja
Asitishe watu. BAKWATA ni taasisi kama taasisi nyingine. Hana mamlaka ya mwisho kwa waislamu wote. Alikuwa anaheshimika lakini sasa nahisi amechoka kuheshimiwa.
Alhamdulilah Shekh wetu umeongea uliyo yaongea ila tunataka video ya sudeis wakati unamuuliza maswali hayo yamwez atutaki stil picha maana ata mnazi unaweza ukapiganao picha ahaha!!!
Hakuna haja ya kulazimishana ktk dini Kila mtu Ana kaburi lake na atahukumiwa peke yake na ktk NEEMA ya AKILI Kila mtu Ana mgao wake na Kila mtu Ana mafhumu
ASLIMIA KUBWA YA WAISLAAM HATUKUPENDI WE ANGALIA TU HATA HAPA COMENT ZINAONESHA WAISLAAM HATUKUTAKI ILA UNAJIPENDEKEZA KWETU ILI TUKUPENDE KAA MBALI NASISI HUNA MASLAHI NA WAISLAAM
@@hassanalhakim8401 hapo utani uko wapi unafikiri hiidunia watu wanaweza kua juu yasheria nasio juu yamungu imani yangu nahofu kubwa nikwamola wangu kama wewe nimiongoni mwao nawe muogope allha uislamu hauko hivyo kama unakaelimu kidogo au huna kaakimya au tafuta wasomi wakuonyeshe aya juu yahayo kwakukusaidia
@@hassanalhakim8401 hayo ndo uliojifunza bora uwe mtumwa waallha na mtume wake unakua mtumwa kwabinaadamu wenzio ilichomwa qur-an pia ilikojolewa ilitoka kauli gani sasa vipi uwaamuru waislamu wote naona pia hujui bakwata ipo kwasababu gani kua naakili hujui kusoma hata picha huelewi katafute aya hii yaa ayyuhalladhiina aamanu innakathiiram minal ahbaari wallughubaan layakuuluna amuwala nnasi nilbaatwili wauasuduna aansabiilillah
Bakwata fanyeni kazi ya waislam sio kufanya kazi ya serikali . Waislam wana matatizo mengi sana siyo mwezi muandamo , waislam wamo ndani magerezani kwa tuhuma tu ushahidi hakuna zaidi ya miaka 5 sasa mufti upo kimyaa wale ni watu wana familia zao zinahitaji huduma
Haifai kutisha,Allah anakuona,na inshaAllah atawalinda,wale wanaifuata njia ya haki,mnasema Tanzania haina dini,au kuanzia leo ni jamhurui ya kiislamu ya Tanzania,mbona wakristo wana wasemaji wa madhehebu tofauti,kilutheri,kikatoliki,sabato na kadhalika,na kila madhehebu yana msemaji wake,wewe ni msemaji wa bakwata,haifai,kujipa cheo cha ukubwa wa kupindukia,ina maana mabokhora,mathnashiri,kenya hamufuati,ramadhani wao walifunga nyinyi ,hamkufunga,uislamu hauna serikali au chama,bakwata mnaipotosha serikali,kama mnafuata saudia basi msifanye bidaa ya maulidi,saudia hawaifuati hiyo,Allah anakuona na atakuhukumu,kwa kuwachia mamia ya waislamu kuwekwa majela,bila kushitakiwa.
@@rashidgontta7264 Usitetee jambo kwa kusema uwongo,maaskofu Tanzania wanakosoa kila leo,na hatujapata kusikia kukamatwa ama kukosolewa,mfano askofu wa kilutheru amekuwa akitoa maoni kwa kukosoa na kusimmamisha itikadi zake bila kuingiliwa,hilo liko wazi,bakwata haina haki ya kuwaamulia waislamu wote,Tanzania kuna madhebu tofauti ya kiislamu,yenye utikadi tofauti,kuanzia mashia ,ahmadia,sufia,kadaria,na ahlil sunna,sheikh itikadi yake anaijua mwenyewe,na wengi hawakubaliani na mitizamo yake ya madhehebu,kwa hiyo hana haki ya kuingilia wengine katika imani zao kidini,hana haki ya kushurutisha au kuletea vitisho kwa itikadi zingine,huko ni kwenda kinyume na sheria ya Tanzania,ambayo sheria zake kikatiba haina dini,na kila raia ana haki ya kuamini anavyotaka,mfano tumemuona nabii mpya ambaye anafuata Quran na Injili,tunamshauri sheikh asizibe macho/masikio aifuate njia ya haki,kwa Allah anamuona,ikiwa kakalia cheo chake kimaslahi au kwa ajili ya Allah.
@@sabraham5308 shekh uislam upo wa aina ngapi maana hizi madhehebu tumezitowa wapi mtume alikuwa mdhehebu gani ndiyo maana hata saudia usidhani wote ni wislamu kuna makafiri mashia suni nk lakini msemaji anabaki mmoja tu bc kwa hiyo yoyote atakaye ongea atachukuliwa ni maoni yake lakini akiongea mufti itaonekana ni sheria
@@rashidgontta7264 ingekua saudi arabia tungekubali hili,kwamba ni serikali ya kiislamu ya salafiya,na kauli ya mufti ingekuwa ndio sheria.lakini kwa Tanzania hilo si sheria,kwa sababu haina dini,na hakuna sheria inayomlazimisha mtu,unachokiamini wewe ndio iwe sheria,hapo unajidanganya.kisheria.
Nchi kuwa na khutbah moja kwa wakati tulionao ni kuulaza UMMAH, na ndio maana miongoni mwa mikoa iliyolala usingizi ni Tanga coz khutbah ni moja misikiti karibia yote
Dini ya Uislam inaamrisha Akhlaaq, Adaab na Nidham ya hali ya juu kabisa. Kweli Mufti Abubakar ni kiongozi wa Bakwata lakini haimaanishi kua sisi ambao hatukubaliani nae kiitikadi wala kiutendaji basi ndio tumseme kwa maneno yalikosa adabu. Ikiwa unamwona amekosea na wewe ukamkosea hapo panakua na makosa 2, sasa hapo utakua umeongeza makosa au umepunguza. Wallahu a'lam.
ukweli ni Kwamba Watanzania wengi hawajui Kazi ya Mufti.Yaan Ni Mtu wa Fatwa Mim labda niwasaidie Mufti Kazi yake ni Kuuulizwa Maswali Na kuyajibu. Sasa Hiyo Kazi Ya Kutangaza Mwezi Au Sijui Sikukuu za Eid Hilo sio jukumu lake Ni Jukumu la Kadhi Ambaye Sisi Kwa Tanzania Hatuna Huyo Mtu.
Hemedi bin Juma alitoka mlango wa nyuma ktk mnakasha wa mwezi sembuse wewe mpiga ramli? Bakwata si msemaji wa waislam wote ila ni msemaji wa taasisi yako.
BAKWATA sio chombo cha waislamu wote bali ni chombo cha wao wenyewe wachache. Mimi binafsi sio Bakwata. . Wakati wa kuchaguana mnawatenga waislamu mnajifungia wenyewe Dodoma halafu mkishapeana vyeo mnasema nyinyi mnawasemea waislamu wote
Mbona nyinyi Wakiristo mna TAASISI TOFAUTI TOFAUTI na kila Taasisi ina wasemaji wake wakuu? KWANINI na Waislam WASIWE hivyo hivyo? Bakwata has lost support from majority of Muslim population in Tanzania kutokana na poor management kwa Waislam katika mustakabar wa maendeleo & elimu. Taasisi ZA Kikristo waliwekeza na bado wanawekeza sana katika maendeleo ya Waumini wao kiasi kwamba mpaka sasa unaona Tanzania more than 90% ya wafanyakazi serikalini kuanzia chini mpaka juu ni Wakristo. Hatuwalaumu Wakristo kwa sababu Taasisi zao zimewekeza Mali na ideas kwenye mipango ya kimaendeleo for years kuanzia mashule bora, Mahospitali, vyuo vikuu na SHUGHULI zote ZA kimaendeleo for years. Waislam wanachoikatalia Bakwata kwa sababu hawana maendeleo waliyoyaleta toka Hayati Baba wa Taifa aanzishe hii Taasisi/Chombo. Waislam wengi wameikimbia na wanaendelea kuikimbia Bakwata na nobody will stop them. Bakwata ni chombo cha serikali ambacho kinafuata maamlisho ya serikali. Sasa hivi kwa sababu hawana jipya na hawawezi kuongoza Waislam towards progress- wanaitumia serikali. Pretty soon- Bakwata will be isolated institution. Kinachotakiwa serikali iwaachie Waislam wachague Taasisi wanazotaka kama vile WAKIRISTO wanavyofanyiwa sio kuleta double standard. Kwa hiyo dadaangu don't talk shits that you don't know kwa sababu tu you hate Muslims or you have pre-conceived misconceptions against Muslims. No one will protect Bakwata from gradual free fall. Si serikali wala Bakwata wenyewe kwa mfumo huu wanapokwenda nao. Waislam wa Tanzania wako so wise right now na tuna haki ya kufuata madhoebu tofauti kama Wakiristo wa Tanzania bila kuingiliwa na taasisi au serikali. Kinyume chake ndio kuvuruga amani yetu. We need to be left alone ili tuendelee kufuata dini yetu na madhoebu yetu kama vile WAKIRISTO.
Dunia Tz ni moja kwa nin kila mwaka Eid zinakuwa mbili Viongizi mnatuchanganya waumini kaeni chini viongoz wa taasis zote mpate muafaka kwa hili ,nashanga ,kibra, arafa ,shahada ni moja sasa kwa nn kunakuwa na Eid mbili????? Jaman Mfano muda wa saudia na Tanzania ni mmoja sasa nashangaa kwa nin tunapishana nao Amaaa kweli huyu aliyegawanya mipaka ya nchi na amefanikiwa kutugawanya waislam
KWANINI na wewe usisome au kujielimisha? Kwani wewe mwenyewe hauna akili ya kutafakali? Tafakali na halafu sepa ubazi unao kufaa. Dawa ya umbumbu ni kujielimisha.
mbona unaongea porojo tu hutowi dalili elimu gani unayoongea hapo chamsingi nikufuata haki sheikh ww ni kiongozi wa dini hutakiwi kuleta vitisho wala ubabe lete dalili muongozo wetu ni qur aan na sunnah sheikh kumbuka ww ni binadamu wapo walio kutangulia wakowapi? wameondoka nawew utakufa muogope Allah sheikh hii ni dunia tu.
Sikutarajia kama bin zuberi angeongea namna hiyo tena kwa mas'ala hayo ! Kuna mambo mengi mno waislam wanatarajia kuyasikia na kupata muelekeo mzuri na sio haya ya khutba nzima anazungumzia khitilafu zinazofahamika miaka yote tena kwa jazba kuubwa na kwa kufoka kukubwa kama vile anazungumza kuwasema makafiri.!!" Inna liy laahi wa inna ilayhi raajiwna"!!!
Tunapokua na maneno mengi tunawapa wenzetu waliotofauti kiimani kupata la kuongea inaonekana kama sisi sio wamoja kwanini kama shahada yetu moja tusiwe wa moja Allah atuhifadhi Wallahi ...
Kuna Othman Maalim ktk mashekh wakisuf ni shekh ambae anajitoa zaidi ktk dini chakushangza mtu kma huyu eti !! asiwe muft mtu from no ware twaambiwa huyu ndiye Mufty iko vipi ? hiyo
Adam Makoye mna waponda kisha mnawakubali wewe fuatilia recodi ya sheikh othman maalim utajua pia akiwa yeye mufti hutoacha kusema kwasababu ndo kawaidayenu
Hakuna usimamizi wa uislam wala uongoz bakwata ni chombo cha serekali na mm kama muislam siikubali wala haitatokea siku niikubali bakwata nyie ni sawa na taasisi ya ccm tu watumikieni mabwana zenu mulipwe mishahara.
Ma,shaa Allah, shukran jazakaAllahu khair. Allah atuongoze sote, Amiin.
Jazakkalwah khairan mufti wetu. Tekeleza majukum ya dini kadri upatapo fursa.
Ukiangalia hzi comments utaona waislamu bado tuna kazi kubwa ya kufanya. Sheikh zubeir anafanya kazi kubwa sana kwa hekima kubwa mno. Tuwe na tabia ya kusoma dini yetu badala ya kusoma mawazo ya watu. Allah atuongoze na asafishe vinywa vyetu mbele ya maulamaaa
Angekuwa ana hekima angetisha watu?
Mufti ni MTU mzuri inshallah ataonyesha jitihada zake ili mashekhee wa uhamsho waachiwe huru nadhani ndicho kilio cha waislamu wengi kwani hakika wamejifunza kwa makosa yao na inshallah kama wakina babu seya waliachiwa basi raisi wetu mpendwa jpm inshallah atawaweka huru mashekhee amina.
WEWE NDIO UMEONGEA BUSARA.SIO HAA WENGINE HAWAMWESHIMU MUFT LAKINI WANATAKA AWAPIGANIE HAO MASHEKHE
Mufti jitathimini ona comment nyingi hazikuungi mkono Allah atakulipa Kwa kupeleka dini kinyume na itakiwavyo.
Dini haipimwi kwa wingi brother,ndio maana wapo mitume waliopata wafuasi wachache na Allah aliwaridhia.
@@zaynabnyamsingwa3830 hebu nisaidie huenda napotea wewe unae jua arafa ni nini.
Sio waislamu wote tunaotambua bakwata tafadhali usitulazimishe
Mimi siipendi Bakwata
Usitutishe usitutishe usitutishe hii nchi haina dini kila mmoja atangaze imani yake bila ya kuvunja katiba ya nchi.
Maadamu ume quote sehemu ya sheria(nchi hii haina Dini) niambie huo msemo una maanisha nini ili baada ya hapo tuingie kwenye mjadala vizuri.
Duh! Tuwe na hofu na Allah.Siku Rais alipokutana na viongozi wa dini, Mchungaji 1 aliomba kurejeshwa kwa mchungaji mwenzao aliye ughaibuni!!!
Shekhe wew ulishindwa vipi kumwambia Rais awaachie huru Waislam wa UAMSHO???!!!
Kwa sababu they are COWARDS
Mdomo ulimponza kichwa, uamsho waliponzwa na mdomo, hii nchi ni tofauti na nchi za kiharabu haiongozwi na Islamic sharia kwa hiyo ukitaka kulazimisha Tanzania hii watu wake wafate sheria za kiislamu lazima utaingia pabaya tu ndio kinachowaumiza uamsho. Wanavuka mipaka mpaka wanajisahau wanaona kama vile nchi hii haina serikali hiyo sio sawa lazima tujifunze kuheshimu mamlaka zilizowekwa kisheria hata mungu amearisha hivyo.
Mungu ameamrisha hivyo
Hao ni mawahabi achana nao,wamewatukana sana masheikh,waache waonje dhambi ya matusi KWA wanawachuoni,washenzi nyinyi MAWAHABI.
Juma jembe allah atujaze iman ya dini
Nashkuru allah baadhi ya waislam tunayaon kam uloyaon wew
Povu lanini Sheikhe? mnazani kuwatisha watu ndio tuwaogope na tuwafuate hilo sahau hii sio nchi ya kidini kila mmoja atangaze imani yake bila ya kutishana.
msemaji ni wewe tu kwani Mungu wewe?huna lolote ni unafiki tu
Kuwa na hesma kwa viongozi wako wa dini,pimbi we kuwa mwelewa
Hakika BAKWATA ni chombo pekee cha kuendeleza uislam katika nchi hii mana mpaka kwenye kijiji uongozi wenu upo, lakini bahati mbaya sana hakuna uadilifu na mipango madhubuti ya kuendeleza uislam. Kama mngekuwa mnafanya kazi zenu vizuri kwa mujibu wa sheria za dini kweli, hakika hata omba omba na watoto wa mtaani pengine wasingekuwepo. Waislam wamepoteza imani na BAKWATA, inapaswa kurejesha imani iliyopotea kwa baadhi ya waislam. Msiwe kama viongozi ambao wapo wapo tu madarakani kwa kuwa wanapata maslahi binafsi, tuwe viongozi wenye kujali maslahi ya umma.
mimi nilijua utakua mkali kwa madhila wanayoyapata masheikh na ndugu zetu walioko gerezani.
hawezi.kuigiiris.wana.siasa.mashehe.wa.zanbar.siasasa.ndo.eme.waponza.warudi.kwa.mungu.wata.toka
Dah we jamaa umeongea point moja ambayo inaumiza san waumin
Allah akuongoze kaka
@@abubakarmahamudu1503 siasa au kupigania haki ya visiwa vya Zanzibar? Hawakuwa na bunduki wala panga. Wametiwa ndani bila ya kesi. Haki ikiwapi?
mnapenda sana kuabudiwa Alhah anawaona,university mmeshindwa kujenga,wenzetu upande wa pili wanazo kibao hazihesabiki
Weunasema tuu unajua kinachotokea zaidi katika huo upande wa pili
Unaujua mkataba wa mou ww acha kujisemea kama hujui japo kweli madhaifu yapo lkn kwa kiasi kikubwa hujuma zimetawala
huyu shekh vipi
hongera mufti tumekuelewa ww ni mufti wa kupigiwa mfano wafahamishe mashee wapotoshaji wasitudanganye
Ww na muft wk kasomeni tena
Mukhtar Abdulrahimu ....kwa kuwa sijamkubali shekhe mpotoshaji wa veteran
ماشاء الله تبارك الله شيخنا ومفتنا
Ingali kua ukali huohuo unautoa pale serekali inapowakandamiza waislam ningekuelewa lakini ukali kwetu tu kwa serekali huongei ,acha kutumikia mabwana wawili wewe
Hatuielewi bakwata hata uje na mizinga
Kauli ya muft wa tz sio kauli ya mwisho kabisa maana hii sio nchi ya kiislam ingekuwa ya kiislam ingekuwa nchi ya kiislam ingekuwa ni kauli ya mwisho, mufti mwenye kauli za ni mufti wa Saudi Arabia, Oman, mascat nk ambako ni nchi za kiislam
Oman ni inchi ya kiislam? Nadhani huijui oman...pia naungananawe kuwa muft sio mtu wa mwisho kwasababu hana mashiko ya kisheria ktk Daru twaahuut
Oman na saudia zote ni nchi za kiarabu sio za kiislam
@@ibnhassan9980 mmmmmmh!!!
A.alykm..ndugu yngu hemu kasome tena qur an ili ujue inasema nn juu ya viongoz wenu ktk nchi...yan uxije kusema kuwa mufti sio mtu wa mwsho katk nchi yetu coz utachekwa wakisikia waliosoma dini...
@@habibtalib5100 sheikh tz sio nchi kiislam, kauli ya muft wa tz haiwezi kuwa kauli ya mwisho kwa tz labda ni ya mwisho kwa bakwata wenyewe hili halina hoja
haya akhy zuberi Allah akuhifadhi mim nafaham utakua sawa in sha Allah.
unge ongelea masheikh wa lio kuwa jela ninge kuelewa sio unaongea mipashu tu apo
Nakupenda sana
Wewe nani kwani umekua Mtume wewe fanya kazi ya serikali ndio waliokuchagua mambo ya uislam waachie waislam wenyewe sio kuitwa sheikh mkuu ww ndio wa2 wasiongee
Muelewe sheikh kabla ya chuki sheikh anaeleza vizuri na amentaja sheikh mzito sheikh hemed bin jumaaa bin hemed mungu amrehemu amin
Et mufti
Msafishe vinywa vyenu mbele ya maulamaa. Hamtafikia uchamungu wa mamufti wa Tz. Kuweni na heshima na adabu kwa akili hizi albabu ndgu yangu abajana unakoelekea siko
Tumia akili ww acha siasa hii dini ina taratibu yake na mipaka yake...usiwe unaropoka tuuuu..
@@habibtalib5100 hujui lolote wewe kwenda huko.
Taasisi ya bakwata, inatakiwa ifanye marekebisho ya kiutawala, ishirikishe taasisi zote za dini ya kiislamu.
Ndugu yangu fuatilia vizuri kazi za Sheikh Zuberi utagundua unachokisema hujakifanyia utafiti
Hahahahaa Nikweli ndugu yangu
Allah akuhifadh, nmekuelewa vzuri.
Suleman Abbas soma dini uijue kijana
Nikweli wewe ni msemaji wa tanzania mzima kwa tasisi yako, na wengine ni wasemaji wa inchi mzima kwa mujibu wa tasisi zao pia.
Asante maan hatuongozwi na serikali Bali ni dini na kitabu
Mtihani kweli sasa kama nchi ambazo nyinyi mumefungua nazo 56 kama mlivyo sema je nchi zaidi ya 140 zimefungua Eid siku gani? Walifikiri duniani kunanchi 60 nini?
Wingi ni umoja lakini wingi si hoja. Tupatie dalili sheikh ili kusupport madai yako kwamba funga ya arafa na kisimamo cha arafa zinafungamana.
Hebu kasomeni waislam,unampinga muft huna hata hoja ya dalili,acha kuwa mwehu
قال الإمام مالك رحمه الله تعالى :"السنة مثل سفينة نوح من ركبها نجا ومن تخلف عنها غرك "....." نحن غرباء ":أي، الذين يصلحون إذ فسد الناس.
Nashukuru sana kwa nukuu hiyo sunnah nikweli mfano wa jahazi
Naam uturuki ulingani na Tanzania kwa nn unalingabisha shughuli za serikali na dini kwa kutofautiana kulianza Tanzania kwa nn kuwabana masheikh wengine na wao wana mshango mkubwa wa kuhamasisha watu kwa nn ukataze watu kusema .
Tatizo lenu ni kujigamba bila ya hekima, bakwata ilioudwa na nyerere ndiounayojigamba nayo,
Kuwa na adabu
Ili uamike kwa WAISILAM kwanza utuungunishe WAISILAM WOTE, na pia uyarudishe mali zote za WAISILAM ambazo walio kutangulia waliyagujumu hapo tutakuamini
Hiyo ndiyo point ya msingi sana
Mhhh mm nafikili taasisi hapa tz zip nyingi sasa mzee usijibebeshe mzigo usio uweza wewe ni mufti wa wafuasi wa bakwata sio wa waislam wote Tanzania uo ndio ukweri,,,na usiwalazimishe watu kufuata matakwa yako, kila mtu afuate zehebu lake bila kukashifu lingine
Hakuna dhehebu linaloitwa bakwata ktk Uislam. Na Bakwata ni chombo cha kuusemea uislam tanzania.tatizo ni nini nyie na bakwata?
basi uwe unatangaza pande zote ikifika sikukuu ya wenye itikadi ya mwezi wa kimataifa uwatangazie vilevile upande wa kitaifa ndio hautapata shida
Sh. Hao waliosoma saudi wanadharau mashekhe wetu wa Africa mashiriki na hawataki umoja wetu nahaki ya kuangalia mwezi.
Bakwata ni taasisi kama taasisi zingine hivyo haina haki ya kuingilia uhuru wa taasisi zingine, yeye ni msemaji wa taasisi ya Bakwata hivyo awe na busara na hekima katika mambo ya dini, Bakwata ni taasisi ambayo mara nyingi iko kinyume na quran na Sunnah ambayo Ndio mihimili ya uislam popote duniani, bakwata ni wasimamizi wazuri wa bida'a na usufi jambo ambalo liko mbali na uislam wa Mtume swalla llaahu a'laihi wasallam na maswahaba zake, hivyo basi, hoja za mufti haziko kielimu kwani zimejikita zaidi katika jazba, ubabe na vitisho,... Jambo la funga ya arafah nilitarajia kumsikia mufti akisema kwamba ni jambo la khilaf lakini yeye anazungumza kama jambo la kukata, masuala ya khilaf kama ulivo utaratibu wa wanachuoni kwamba watu wapeane udhuru japokuwa katika khilaf Kunakuwa na msimamo /qauli yenye nguvu, kama mufti aombe radhi kwani maneno yake yako kinyume na utaratibu wa khilaf ambapo ziko qauli za wanachuoni wakubwa wenye fatawa mbalimbali ambao yeye bado ni mwanafunzi kwa wanachuoni hao mfano, sheikhul Islami ibn Taymiyyah na wengine miongoni mwa wanachuo wa tafsiir,." Hakuna kumtii kiumbe katika kumuasi Allah ".
Bakwata na Waislam ni vitu tofauti..
Wewe unayejiita mufti umechaguliwa nani..?
Hebu acheni ushenzi wenu..
Usitukane ndugu yangu mpendwa kweli unatamani haki isimame na fahamu kuwa haki haisimami kwa matusi
Kauli ya huyu ni ya kipuuzi
Ndugu yangu nakushauri usirudie tena kauili kama hizi hasa kwenye hadhara kubwa km fb unayejaribu kumvunjia heshima sina shaka ni miongoni mwa Wachamungu jirudi ndgu kabla Allah hajakurudi
Me ni mpitiaj comment kiukweli bakwata watu hawawapendi na mnajua hampendwi fateni Uislam wa mtume Muhammad (s.w.s)
Huyu sheikh kavu kweli anajikuta kijukuu cha mtume et bakwata ikisema umeandama bas umeandama
🤣
Said miraj kuwa wingi ndiyo unajiona mumeongoka Mimi nakwambia usijifaharishe kwa uwingiwenu aliye waumba ndiye anaetujua kwa iyo usijifaharishe kwauwingi inawezekana haokidogo unaowadharau kwa aliye tuumba wakawa wanathamani kubwa kuliko nyie wengi
Ingekua nchi ya kiislam mufti ndio msemaji lakini Tanzania mmhh
Ungesoma historia usingesema hayo.
Waislam hawakutambui wewe kama kiongozi wao.
Taasisi yako imesajiliwa Rita kama ilivyo almallid au taasisi nyingine yeyote.
Kwa upande wa wakristo kuna katoliki, Lutheran au SDA.
Kila mmoja ana mipangilio yake na wana wasemaji wao.
Acha kutafuta sympathy .
Hii ni nchi isiyo na dini.
Kama wewe kiongozi wa waislam mbona huwatetei waislam wenzetu wapo jela masheikh wa Zanzibar upo kimya kazi unafiki tu subir Allah. Atakavyokuja kukuuliza ..
Usitupotezee muda hapa huna kimoja bakwata ni taasisi ya ccm kwani hujui ivyo ..
Washenzi wakubwa Allah atawalipa kwa dhulma zenu
Kwani wewe hutaulizwa?
Bakwata chini Muft Zuber ipo vzuri inajitambua majukumu yake nyie Wahabi mnafahamika ni wapotoshaji wa Dini.Kama leo mnalaumu kuwa Bakwata ni taasisi hyo taass ya Dini mnayoifuata huko Saudia ipo chini ya nani kama cyo chini ya Ufalme unaolindwa na Marekani ,Mayahudi na Uingereza.Tafuteni historia ya Saudia nn kilisababaisha Utawala wa kifalme kuundwa
BIG BROTHER ALWAYS RIGHT
TUMEUCHEZEA SANA UISLAM KWA MASLAI YETU BINAFSI NA SASA IANZE KUWA MWISHO NAAM MUFTI MAANA BINADAM WANAANGALIA NETWORK TIME AWAANGALII NYAKATI........TENA UMEONGEA KIDOGO KIONGOZI WANGU ULITAKIWA UKOMESHE KABISA
Uko kwenye ignorance my brother.
@@hamidudongo1879 heri ya wewe ulie na elimu ya ghaibu na kutukana wakubwa na waliopass kukuongoza,kaa hivyo hivyo Wenzako ndio viongozi tayari na huna ulijualo hata vitabu vitatu tuu tofauti vya kuelekeza Uislam sijui kama unavyo ndani kwako.💣💣💣💣💣 wewe
@@akimmbwego797 Muislam mzima unakuwa Muongo. Kuna TUSI LOLOTE nililotoa hapo?? Tumia akili sio unafuata tu. Wewe mbona haufuati taasisi zengine na huambiwi umetukana?? Uwongo uwongo tu. Niambie TUSI nililotoa hapo kama umesema ukweli. Muislam mzima unazusha maneno maneno tu.
Ukweli utabakia pale pale kwamba Waislam wengi wanahama kutoka Bakwata. Huo ndio ukweli hata akisema kama wewe unavyo sema angesema zaidi. Kama wewe unavyopenda kuwa Bakwata na wawe msemaji wako mkuu; wengine tunasikiliza Taasisi zetu kama Wasemaji wakuu wetu. Kuikataa Bakwata na kuona haturidhiki na uongozi wao- sio tatizo wala MATUSI. SINA SHAKA WALA WASIWASI NA UCHAMUNGU WAO BAKWATA AU ELUMU YAO HATA KIDOGO. Ila baadhi hatutaki kuongozwa na Bakwata pamoja wanasaidiwa na serikali pamoja na BAADHI ya Taasisi zisizo za kiislam.
SIJATOA TUSSI LABDA NI WEWE NDIO UNAYETUKANA. ACHA UWONGO UONGO.
Simama Katika Quran na sunnah sababu umebeba zimaa kubwa sana kuongoza uislam shekh
Ahaa kumbe anaongoza kwa kutumia katiba, siyo kitabu na sunnah,
Sasa nimejua
Mungu hatawifichua taratibu hawa watu
Kama hujui taratibu za uongozi kajifunze ujue nafasi yako,acha kuwa fikra finyu kwanza sikiza upime kwa mizani,acheni unafiki
Tutawaheshim kama wakituheshim lkn sio tuwaheshim kwa kuupoteza uislam wetu hayo labda ufanye ww na kundi lako sio ss
Kwanza ww nimufti gani unaeshindwa kuwatetea hata mashekh walikogerezani haija sikilika hata aikumoja sauti yako kuhusu mashekh halafu unatudaganya eti mswmaji wawa Islam hilo siobarza lawa isilam hilo nibaraza LA serekali we tetea tu ugali wako msemaji wawa isilam wote hayupo tena katka DUNIA hii limebaki jina lake na sifa zaketu utakua ww mnafiki WA uwisillam
HAO MASHEKHE WATETEWE ILI NINI NA HUKU NDIO WANAO LETA MGAWANYIKO BAINA YA WAISLAMU? HAO HAO SI NDO WALOKUWA WANAIPINGA BAKWATA?KWENYE MAAMUZI YENU YA HOVYO HAMUMJALI MUFTI,ILA MKIBANWA NA SERIKALI MWAMUONA MUFI NI WAMUHIMU
Wewe ndio utaingia pabaya kwa kuitwa mufti lakini hufanyi kazi ya Allah unafanya kazi ya siri kali
Kwa mjibu wa katiba ya JMT kila mtu ana haki ya kuabudu. Idi itaswaliwa kwa mtu kuamua
Nimekuelewa sana mufti wangu alhjj abubakar bin zuber Allah akujaalie afya njema
unatumika
Sasa wewe msemaji wa waislam? Sasa mashekhe akina mselem Ally hawakuhusu mbona hatujakusikia kuwasemea?
Kweli hatukatai kua namsemaji nakiongozi lakini imani natasisi hiyo hatuna kutokana namamboyenu
Mheshimiwa Mufti huko sahihi kwani hata Biblia katika Kutoka 22: 28 tunakumbushwa kutomtukana MUNGU, wala kumlaani mkuu wa watu wako.
hiyo ipo kanisani kwa wakristo sio kwetu sisi waislam
Kaishaza Bengesi wewe kafiri mambo ya kiislaam hayakuhusu unatuambia maswala ya bibilia hapa tuachi wenyewe tutayajenga
sheikh tuache mulumbano tumlejee allah sisi ni waislam haifai kulumbana
hiki ndio cha kusema allah atupe muongozo na tawfeeq ya kuungana wajua tukitukanana haipendez nakushukuru sana wewe ndugu ulio coment muungano
Mashaallah mufti umeongea,lakini tungependa kujifunza kutokakwako Hakuna wanawazuoni wakubwa kuliko au zaidi ya hao mamufti unao wataja walio toa fatwa zakukubali mwezi wa popote Duniani?kama wapo ndio haowasionaelimu?na wanahaki waliowakubali fatwa zao kuwafata au haifai?.
Wako na amewataja
Kuna ùhalali wafatwazao kufatwa?
Allah akulinde na kueshimu tueshumuni viongozi wetu
uturuki na tanzania tofauti na saudia huwezi kuilinganisha na tanzania maana tanzani sio nchi ya kiislam saudia ninchi ya kiislam lazima iwe na msemaji mmoja
Muhidin Ali kama sio nchi ya kiislaam hama ondoka nenda huko kwenye nchi ya kiislaam
Asitishe watu. BAKWATA ni taasisi kama taasisi nyingine. Hana mamlaka ya mwisho kwa waislamu wote. Alikuwa anaheshimika lakini sasa nahisi amechoka kuheshimiwa.
Alhamdulilah Shekh wetu umeongea uliyo yaongea ila tunataka video ya sudeis wakati unamuuliza maswali hayo yamwez atutaki stil picha maana ata mnazi unaweza ukapiganao picha ahaha!!!
Hakuna haja ya kulazimishana ktk dini Kila mtu Ana kaburi lake na atahukumiwa peke yake na ktk NEEMA ya AKILI Kila mtu Ana mgao wake na Kila mtu Ana mafhumu
ASLIMIA KUBWA YA WAISLAAM HATUKUPENDI WE ANGALIA TU HATA HAPA COMENT ZINAONESHA WAISLAAM HATUKUTAKI ILA UNAJIPENDEKEZA KWETU ILI TUKUPENDE KAA MBALI NASISI HUNA MASLAHI NA WAISLAAM
Acha porojo muogope mola wako unafananisha nchi yakitwaghut na zakiislamu mola hato kuacha salama fanya toba
Soma kwanza ndo mnyoshee kidole muft,unatumika bila kujua
Biasi Omari wewe unafanya utani na masheikh ndugu jihadhari usije ukapata tabu na usije chanzo nini
@@hassanalhakim8401 hapo utani uko wapi unafikiri hiidunia watu wanaweza kua juu yasheria nasio juu yamungu imani yangu nahofu kubwa nikwamola wangu kama wewe nimiongoni mwao nawe muogope allha uislamu hauko hivyo kama unakaelimu kidogo au huna kaakimya au tafuta wasomi wakuonyeshe aya juu yahayo kwakukusaidia
Biasi Omari innalillahi ibaada idha aradu arada sasa endelea kuwazingua tu ndugu
@@hassanalhakim8401 hayo ndo uliojifunza bora uwe mtumwa waallha na mtume wake unakua mtumwa kwabinaadamu wenzio ilichomwa qur-an pia ilikojolewa ilitoka kauli gani sasa vipi uwaamuru waislamu wote naona pia hujui bakwata ipo kwasababu gani kua naakili hujui kusoma hata picha huelewi katafute aya hii yaa ayyuhalladhiina aamanu innakathiiram minal ahbaari wallughubaan layakuuluna amuwala nnasi nilbaatwili wauasuduna aansabiilillah
Tumia hekima mzee wanaoipinga BAKWATA wanajulikana na sababu zao so vzr ni kuzungumza, kutumia nguvu pataleta chuki zaidi
Mwezi wa BAKWATA +ARAFA ya BAKWATA,,,,,hahahaaa huo ndio ukweli!!!!
@Juma Kapilima. Tuweke mjadala hapahapa tuufanye wa wazi kwa manufaa ya wengi. Unasemaje akhy?
@@muhsinmwambule9435 weka anuani ya mada
Mimi naeka mada: Je funga ya Arafa ni lazima ioane na kismamo cha Arafa Cha Mahujjaj Makka?
Binafsi nasema la×
Enyi mulioamini mtii m,mungu na mumtii mtume na wenye mamlaka juu yenu nyinyi aya hii hawaitaki
Yas alunaka anil ahilah (wanauliza kuhusu miandamo)umeona Aya hioo kwa iyo miandamo mingi
Unapo mkataa kiongozi Wa Uismlam kwa Chuki Na Hasadi tambuwa kiongozi Wako Ni Sheetani Mufti Hongera Hao Wanao Tutenganisha Yafaa Washuhulikiwe Waswali Misikitini Kwao Na Waache Kujipa Madaraka Dhamana Yote Ipo Kwako
Mwashirikiana na kenya wakati ramadhani kenya wameanza kufunga huku mmechelewa??
Wewe nani mpaka uwakataze waislam wasiyapange mambo yao mpaka wapangiwe na BAKWATA?
Kwa nini umeuliza hivyo?
IKHTILAFU ZILIKUEPO PIA ZITAENDELEA KUEPO KUA MAKINI WEWE NIMTIHAN KWA UMMAH
Bakwata fanyeni kazi ya waislam sio kufanya kazi ya serikali . Waislam wana matatizo mengi sana siyo mwezi muandamo , waislam wamo ndani magerezani kwa tuhuma tu ushahidi hakuna zaidi ya miaka 5 sasa mufti upo kimyaa wale ni watu wana familia zao zinahitaji huduma
Kwan wamehukumiwa na koti ya kiislam? Independence of institutions.
Haifai kutisha,Allah anakuona,na inshaAllah atawalinda,wale wanaifuata njia ya haki,mnasema Tanzania haina dini,au kuanzia leo ni jamhurui ya kiislamu ya Tanzania,mbona wakristo wana wasemaji wa madhehebu tofauti,kilutheri,kikatoliki,sabato na kadhalika,na kila madhehebu yana msemaji wake,wewe ni msemaji wa bakwata,haifai,kujipa cheo cha ukubwa wa kupindukia,ina maana mabokhora,mathnashiri,kenya hamufuati,ramadhani wao walifunga nyinyi ,hamkufunga,uislamu hauna serikali au chama,bakwata mnaipotosha serikali,kama mnafuata saudia basi msifanye bidaa ya maulidi,saudia hawaifuati hiyo,Allah anakuona na atakuhukumu,kwa kuwachia mamia ya waislamu kuwekwa majela,bila kushitakiwa.
Nitajie msemaji wa luteran msemaji mkuu wa wakristo wote ni kadinal pengo
@@rashidgontta7264 Usitetee jambo kwa kusema uwongo,maaskofu Tanzania wanakosoa kila leo,na hatujapata kusikia kukamatwa ama kukosolewa,mfano askofu wa kilutheru amekuwa akitoa maoni kwa kukosoa na kusimmamisha itikadi zake bila kuingiliwa,hilo liko wazi,bakwata haina haki ya kuwaamulia waislamu wote,Tanzania kuna madhebu tofauti ya kiislamu,yenye utikadi tofauti,kuanzia mashia ,ahmadia,sufia,kadaria,na ahlil sunna,sheikh itikadi yake anaijua mwenyewe,na wengi hawakubaliani na mitizamo yake ya madhehebu,kwa hiyo hana haki ya kuingilia wengine katika imani zao kidini,hana haki ya kushurutisha au kuletea vitisho kwa itikadi zingine,huko ni kwenda kinyume na sheria ya Tanzania,ambayo sheria zake kikatiba haina dini,na kila raia ana haki ya kuamini anavyotaka,mfano tumemuona nabii mpya ambaye anafuata Quran na Injili,tunamshauri sheikh asizibe macho/masikio aifuate njia ya haki,kwa Allah anamuona,ikiwa kakalia cheo chake kimaslahi au kwa ajili ya Allah.
@@sabraham5308 shekh uislam upo wa aina ngapi maana hizi madhehebu tumezitowa wapi mtume alikuwa mdhehebu gani ndiyo maana hata saudia usidhani wote ni wislamu kuna makafiri mashia suni nk lakini msemaji anabaki mmoja tu bc kwa hiyo yoyote atakaye ongea atachukuliwa ni maoni yake lakini akiongea mufti itaonekana ni sheria
@@rashidgontta7264 wewe unaona upo wa aina ngapi.
@@rashidgontta7264 ingekua saudi arabia tungekubali hili,kwamba ni serikali ya kiislamu ya salafiya,na kauli ya mufti ingekuwa ndio sheria.lakini kwa Tanzania hilo si sheria,kwa sababu haina dini,na hakuna sheria inayomlazimisha mtu,unachokiamini wewe ndio iwe sheria,hapo unajidanganya.kisheria.
Mufti upo sawa makundi 71ni shidaaa. Lakin ALLAH atawaongoza kwa Rehma zake
Nchi kuwa na khutbah moja kwa wakati tulionao ni kuulaza UMMAH, na ndio maana miongoni mwa mikoa iliyolala usingizi ni Tanga coz khutbah ni moja misikiti karibia yote
Dini ya Uislam inaamrisha Akhlaaq, Adaab na Nidham ya hali ya juu kabisa. Kweli Mufti Abubakar ni kiongozi wa Bakwata lakini haimaanishi kua sisi ambao hatukubaliani nae kiitikadi wala kiutendaji basi ndio tumseme kwa maneno yalikosa adabu. Ikiwa unamwona amekosea na wewe ukamkosea hapo panakua na makosa 2, sasa hapo utakua umeongeza makosa au umepunguza.
Wallahu a'lam.
Kuna mchungaji aliomba mchungaji mwenzao kwa serikali
Mufti wetu anashindwa hata kuwatolea sauti waislamu wanaodhulumiwa haki zao
Katiba ya wapi.
hakuna alietoa laana acha uzushi wako mufti mtu halaaniwi kwa hilo jmbo sisi tutasimama ktk haqi
Uniwie radhi sheikh, hakuna nchi kubwa mbele ya nchi nyingine labda ukubwa wa eneo.
ukweli ni Kwamba Watanzania wengi hawajui Kazi ya Mufti.Yaan Ni Mtu wa Fatwa
Mim labda niwasaidie Mufti Kazi yake ni Kuuulizwa Maswali Na kuyajibu.
Sasa Hiyo Kazi Ya Kutangaza Mwezi Au Sijui Sikukuu za Eid Hilo sio jukumu lake Ni Jukumu la Kadhi Ambaye Sisi Kwa Tanzania Hatuna Huyo Mtu.
Hemedi bin Juma alitoka mlango wa nyuma ktk mnakasha wa mwezi sembuse wewe mpiga ramli? Bakwata si msemaji wa waislam wote ila ni msemaji wa taasisi yako.
Kwa nini usikae na viongozi wengine ili muwe mnakubaliana kwa pamoja pia ukumbuke kuna madhehebu mengi
kama ndvyo, Baraza lako liwe na wajumbe wa taasisi zote, sio mashehe wa Bakwata wa mikoa au wilaya
Mufti tambua hata ukristo una madhehebu na taasisi na wana Uhuru wakutangaza wanachoaminj....
Nalamuhimu zaidi Qurani na swala na saumu wanafundishwa na hawa hawa mashekhe wetu.
BAKWATA sio chombo cha waislamu wote bali ni chombo cha wao wenyewe wachache.
Mimi binafsi sio Bakwata. .
Wakati wa kuchaguana mnawatenga waislamu mnajifungia wenyewe Dodoma halafu mkishapeana vyeo mnasema nyinyi mnawasemea waislamu wote
mufty umeongea maneno makali sana ila nimekuelewa sana ni kweli kabisa waache kuvuruga nchi
Mbona nyinyi Wakiristo mna TAASISI TOFAUTI TOFAUTI na kila Taasisi ina wasemaji wake wakuu? KWANINI na Waislam WASIWE hivyo hivyo? Bakwata has lost support from majority of Muslim population in Tanzania kutokana na poor management kwa Waislam katika mustakabar wa maendeleo & elimu. Taasisi ZA Kikristo waliwekeza na bado wanawekeza sana katika maendeleo ya Waumini wao kiasi kwamba mpaka sasa unaona Tanzania more than 90% ya wafanyakazi serikalini kuanzia chini mpaka juu ni Wakristo. Hatuwalaumu Wakristo kwa sababu Taasisi zao zimewekeza Mali na ideas kwenye mipango ya kimaendeleo for years kuanzia mashule bora, Mahospitali, vyuo vikuu na SHUGHULI zote ZA kimaendeleo for years. Waislam wanachoikatalia Bakwata kwa sababu hawana maendeleo waliyoyaleta toka Hayati Baba wa Taifa aanzishe hii Taasisi/Chombo.
Waislam wengi wameikimbia na wanaendelea kuikimbia Bakwata na nobody will stop them. Bakwata ni chombo cha serikali ambacho kinafuata maamlisho ya serikali. Sasa hivi kwa sababu hawana jipya na hawawezi kuongoza Waislam towards progress- wanaitumia serikali. Pretty soon- Bakwata will be isolated institution.
Kinachotakiwa serikali iwaachie Waislam wachague Taasisi wanazotaka kama vile WAKIRISTO wanavyofanyiwa sio kuleta double standard.
Kwa hiyo dadaangu don't talk shits that you don't know kwa sababu tu you hate Muslims or you have pre-conceived misconceptions against Muslims. No one will protect Bakwata from gradual free fall. Si serikali wala Bakwata wenyewe kwa mfumo huu wanapokwenda nao. Waislam wa Tanzania wako so wise right now na tuna haki ya kufuata madhoebu tofauti kama Wakiristo wa Tanzania bila kuingiliwa na taasisi au serikali. Kinyume chake ndio kuvuruga amani yetu. We need to be left alone ili tuendelee kufuata dini yetu na madhoebu yetu kama vile WAKIRISTO.
kaa kimya wewe kafir mkubwa hujui chocho kuhusu uislam hivyo basi hauruhusiwi kucoment chochote
Dunia Tz ni moja kwa nin kila mwaka Eid zinakuwa mbili
Viongizi mnatuchanganya waumini kaeni chini viongoz wa taasis zote mpate muafaka kwa hili ,nashanga ,kibra, arafa ,shahada ni moja sasa kwa nn kunakuwa na Eid mbili????? Jaman
Mfano muda wa saudia na Tanzania ni mmoja sasa nashangaa kwa nin tunapishana nao
Amaaa kweli huyu aliyegawanya mipaka ya nchi na amefanikiwa kutugawanya waislam
sahihi kiongozi wetu simama katika kazi yako ya uongozi
Tatizo wako masheikh hujiona wanajua zaidi ya masheikh wengine jawabu kangu wafate bakatwa siwaoni na makosa ni chuki tu za masheikh wazushi
KWANINI na wewe usisome au kujielimisha? Kwani wewe mwenyewe hauna akili ya kutafakali? Tafakali na halafu sepa ubazi unao kufaa. Dawa ya umbumbu ni kujielimisha.
kwani wewe nani?taasisi zipo nyingi sana na zinakubalika na wengi,siyo hugo Bakwata ya wazee tena wa miaka 70 na kuendelea
Nenda.ukacheze.kwaya
@@brunojosenampassa614 mimi au wewe ndiyo unatakiwa ukacheze kwaya
Wewe ninani ktk dini hii,tatizo nielim mnahadaika na vimilioni kumi
acha.kumtuka.shehe.ogea.hoja.kama.yeye
Aaww_IKHITILAFU_zipo_ila_kutukanana_Ndio_vibaya_hata_mimi_nachukia_wanavyo_tukana_SIPENDI_jaman_,haipendezi
mbona unaongea porojo tu hutowi dalili elimu gani unayoongea hapo chamsingi nikufuata haki sheikh ww ni kiongozi wa dini hutakiwi kuleta vitisho wala ubabe lete dalili muongozo wetu ni qur aan na sunnah sheikh kumbuka ww ni binadamu wapo walio kutangulia wakowapi? wameondoka nawew utakufa muogope Allah sheikh hii ni dunia tu.
Ya waislam muwaachie waislam na ya serikali iachieni serikali
Wewe mufti wa serikali
Hakuna muumin aliyekuchagua
mufti sema tena sema tunaotambua bakwata tupo wengi kuliko hiki kikundi cha fecbook kilichoandika coment zao hapo
Povu la nini kwani lazima tukufuate wewe umekuwa Mungu au mtume wewe? A
Sijui huyu
Nikweli kabisa lakin wewe sio kiongozi wa waislaamu wewe ni kiongozi wa bakwata..hata haya huoni mzee
Uislamu wa bakwata ni upi mbona inaonekana kama mikakati maalum?
Sikutarajia kama bin zuberi angeongea namna hiyo tena kwa mas'ala hayo ! Kuna mambo mengi mno waislam wanatarajia kuyasikia na kupata muelekeo mzuri na sio haya ya khutba nzima anazungumzia khitilafu zinazofahamika miaka yote tena kwa jazba kuubwa na kwa kufoka kukubwa kama vile anazungumza kuwasema makafiri.!!" Inna liy laahi wa inna ilayhi raajiwna"!!!
Tunapokua na maneno mengi tunawapa wenzetu waliotofauti kiimani kupata la kuongea inaonekana kama sisi sio wamoja kwanini kama shahada yetu moja tusiwe wa moja Allah atuhifadhi Wallahi ...
Kuna Othman Maalim ktk mashekh wakisuf ni shekh ambae anajitoa zaidi ktk dini chakushangza mtu kma huyu eti !! asiwe muft mtu from no ware twaambiwa huyu ndiye Mufty iko vipi ? hiyo
Adam Makoye mna waponda kisha mnawakubali wewe fuatilia recodi ya sheikh othman maalim utajua pia akiwa yeye mufti hutoacha kusema kwasababu ndo kawaidayenu
sio kma ndiyo niko ktk msimamo wake Othman Maalim laa ! Ni kutaka kuonyesha tu kwamba vipi ? isiwe hivyo
Tanzania sio nchi ya kiislam kama Saudi Arabia au uturuki
Jaffar saudia ingekuwa ya kiislam ingekuwa na ufalme
Kwanini uwe na tatizo lauchumi wakat waislam wapo,tatzo hapo elim hakuna kingine
Bakwata mbona ipo kwenye hafla za kiserikali tu.huku chini kwa waumini haionekani.
kwani uislam huendeshwa kwa katiba? nyinyi mnataka kuleta fitna
Hakuna usimamizi wa uislam wala uongoz bakwata ni chombo cha serekali na mm kama muislam siikubali wala haitatokea siku niikubali bakwata nyie ni sawa na taasisi ya ccm tu watumikieni mabwana zenu mulipwe mishahara.
fahamisha wat itilafu yamwez acha kukwambia watu hote wafuat mwez wandan Hali yakuw una juwa hayo nimasuala yaitilaf