TUNDA MAN - Full Interview na Bongo Project
HTML-код
- Опубликовано: 5 окт 2024
- Tunda Man au Khalid Ramadhan Tunda katika haya mazungumzo marefu na ya kufurahisha anasimulia juu ya safari yake nzima ya muziki na maisha. Anaelezea kuhusu maisha yake ya shule, ndoto za udaktari, utundu, kucheza mpira n.k. Anasimulia kuhusu ngoma zake za awali ikiwemo Neila, Demu Sio, Msambinungwa, Nipe Report na nyingine nyingi alizofanya na Tip Top Connection kama Bado Tunapanda na nyingine nyingi. Pia ameelezea mahusiano yake na wasanii maarufu wa Bongo akiwemo Profesa Jay, Ali Kiba na Diamond Platnumz. Ni mazungumzo mazuri na yenye visa vya kuchekesha...Usikose!
#tundaman #bongoproject #bongofleva #tiptopconnection #
Bongo Project ni "project" mpya Tanzania inayojihusisha na kazi za sanaa na yenye lengo la kuhifadhi taarifa, historia na takwimu muhimu za sanaa ya Tanzania pamoja na wasanii wake.
--------------------
WEBSITE
--------------------
bongoproject.org
--------------------
SOCIAL MEDIA
--------------------
Instagram: / bongo_project
Facebook: / bongo-project-10256641...
--------------------
CONTACT
--------------------
Email: info@bongoproject.org
Nmeangalia yote jamaa uchoki kumsikiliza. Na amefunguka mengi saana hii ni historia nzima ya maisha yake. Hapo hata hasipofanya interview tena hii itabaki ni kumbukumbu kwa vizazi vijavyo. Safi sana tundaman.
Shukrani sana mkuu! Tunda alitupa moja ya interviews bora kabisa.
Dah zote nzuli ulizoweka blessing sana bongo project
Shukrani sana. Endelea kutufuatilia
Napenda Sana interview ambayo watu wanaulizwa historia zao
Pamoja sana. Shukrani
Interview kalisana tunda yupo really life🤜
Shukrani
Mpe I S T kwel huyo teacher TUNDAMAN
Nimefuatilia interview zenumnafanya poa sana, ila sound bado haiko poa inakua na mawingu mawingu sana,tunaomba mjitahidi kurekebisha hilo.ila show ni kali sana.#Naomba tuvutie dully sykes hapa mzee.
Shukrani mkuu. Tunaendelea kufanya marekebisho mbalimbali. Tutalifanyia kazi hilo suala. Dully atafika mezani usijali.
Hapo mm sitaki watu wa hip hop nimecheka sana
Neillah 🔥
Demu sio huo wimbo umegusa wengi saana. Anavyosema kuwa ameimba tabia zilizopo ni kweli kabisa... Ni nyimbo ambayo inaishi kabisa.😂