MAUAJI YA KUTISHA: MWALIMU NA MWANAFUZI WAKUTWA WAMEUAWA KIKATILI CHUNYA MKOANI MBEYA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 31 мар 2024
  • Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamtafuta mtu au watu waliohusika katika tukio la
    mauaji ya aliyekuwa Mwalimu wa Shule ya Msingi Mbugani Heriety Lupembe [37] na
    Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Isenyela Ivon Tatizo [15] wote
    wakazi wa Kijiji cha Kiwanja Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.
    Tukio hilo limetokea Machi 31, 2024 majira ya saa 2:30 usiku wakati marehemu akiwa
    nyumbani kwake sebuleni na watoto wawili Ivon Tatizo na Haris Barnaba Mtweve [06]
    Mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Ken Gold aliyejeruhiwa kwa
    kupigwa kitu butu kichwani.
    Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, mtu huyo aliwavamia marehemu na kuanza
    kuwashambulia na baada ya kufanya hivyo alifunga milango kwa nje na kuondoka na
    funguo. Chanzo cha tukio hili bado kinachunguzwa. Majeruhi mtoto Haris Mtweve
    anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
    Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa tukio hili ikiwa ni Pamoja
    na msako dhidi ya mtu au watu waliohusika. Aidha, linatoa wito kwa mtu yeyote
    mwenye taarifa za mtu au watu waliohusika

Комментарии •