MAUAJI YA KUTISHA: MWALIMU NA MWANAFUZI WAKUTWA WAMEUAWA KIKATILI CHUNYA MKOANI MBEYA
HTML-код
- Опубликовано: 31 мар 2024
- Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamtafuta mtu au watu waliohusika katika tukio la
mauaji ya aliyekuwa Mwalimu wa Shule ya Msingi Mbugani Heriety Lupembe [37] na
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Isenyela Ivon Tatizo [15] wote
wakazi wa Kijiji cha Kiwanja Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.
Tukio hilo limetokea Machi 31, 2024 majira ya saa 2:30 usiku wakati marehemu akiwa
nyumbani kwake sebuleni na watoto wawili Ivon Tatizo na Haris Barnaba Mtweve [06]
Mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Ken Gold aliyejeruhiwa kwa
kupigwa kitu butu kichwani.
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, mtu huyo aliwavamia marehemu na kuanza
kuwashambulia na baada ya kufanya hivyo alifunga milango kwa nje na kuondoka na
funguo. Chanzo cha tukio hili bado kinachunguzwa. Majeruhi mtoto Haris Mtweve
anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa tukio hili ikiwa ni Pamoja
na msako dhidi ya mtu au watu waliohusika. Aidha, linatoa wito kwa mtu yeyote
mwenye taarifa za mtu au watu waliohusika