Safari Ya Dina : Asimulia Msoto Aliopitia Kabla Kuwa Mtangazaji | SALAMA NA DINA MARIOUS PART 1
HTML-код
- Опубликовано: 14 окт 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Dina Marious ni STAR ambaye amakua akijenga jina lake kwa miaka mingi sana. Kama sote tunavyofahamu hakuna mtu ambaye anaibuka tu siku moja na kupata heshima na kuaminiwa kama hajafanya kazi ambayo itamfanya watu wamuamini na kumpenda. Dina yeye ameteka kabisa soko la Wanawake, kitu chochote kinachohusiana na wanawake na madhila, raha na mambo yao ya kijamii basi ukiangalia kushoto na kulia lazima utamkuta Dina yuko hapo akitoa mchango wake kwenye suala hilo. Iwe kuanzia maandalizi au uwepo wake tu. Hicho ndo ambacho yeye kama Mama na Dada na Binti ameamua kufanya, na anaweza haswa.
Alianzia Radio ya watu ya Clouds FM na baada ya kupata mtoto wake wa kwanza mitihani mingi aliipitia, ile maternity leave ambayo alikaa wakati anamkuza kijana wake ilileta mabadiliko makubwa kwenye maisha yake. Zion (mtoto wake) alipo zaliwa ilimbidi Dina aache kazi kwenye Taasisi ambayo alikua ameizoe mno na kutafuta ustaarabu mwengine bila ya kuwa na mipango hiyo wakati alipochukua likizo yake ya kwenda kujifungua. Mipango ilikua akitoka kwenye likizo yake hiyo ya uzazi basi arudi tu kazini kwake kama kawaida lakini Bosi wake wa wakati huo, Marehemu Ruge Mutahaba alikua na mipango mengine na Dina mipango ambayo kwa mujibu wake anaamini alikua akipigwa chenga tu na hakukua na mpango thabiti ambao ulikua umeekwa kwaajili yake.
Dina anakumbuka nenda rudi alizokua akizipata na kulipwa mshahara bila ya kufanya kazi yoyote, kwa kweli hilo lilikua likimsubua sana na anasema kila akiangalia kushoto na kulia alikua haoni dalili zozote za yeye kuanza kufanya kazi muda wowote wa karibu na kwasababu maswali yake mengi mazito yalikua yakipatiwa majibu mepesi mepesi aliona basi si vibaya kama atatafuta challenge nyengine kwenye maisha yake. Kwanza hiyo plan ambayo alikua amepewa hakua ameifurahia na pili majibu ambayo alikua anapatiwa nayo yalimfanya ajue pale hapakua sehemu sahihi kwake tena.
Kumuuma ilikua ikimuuma sana kama anavyosema mwenyewe, hakukua na sababu yoyote ya kutaka kufanya mabadiliko yale ambayo yalifanyika, ya kutaka kumpeleka yeye kwenye TV wakati tayari alikua ameshatengeneza kundi kubwa la mashabiki kwa wakati huo, na pengine approach iliyotumika pia haikua sahihi na hilo liliacha ladha mbaya kwenye moyo na kinywa chake, na baada ya hapo kwasababu kulikua na ofa nyengine hakufanya ajizi kuziskiliza na uzuri zaidi kwanza hapakua mbali na ofisi yake ya zamani hapo alipokua anatakiwa na pili ambalo ndo KUBWA kabisa, alikua anapewa muda ule ule wa hewani kama ambao alinyang’anywa baada ya kuenda likizo ya uzazi kwenye ajira yake ya zamani. Alikua na kila sababu ya kuchukua hatua nyengine na kujisogeza mbele zaidi, kama ambavyo tunafahamu, mtu huenda aitwapo. Na mengine ndo haya, yamebaki story tu.
Nafasi yake kwenye jumuia za wanawake ni ya kipekee na anaiweza kuikaimu vizuri tu, amekua akifanya shughuli mbali mbali za kutatua baadhi ya adha na pia kuwatunza wale ambao anadhani wanastahili ili kuwafanya wapate nguvu zaidi ya kuendelea kufanya wanayofanya kwa uzuri zaidi. Na amekua mfano mzuri hata kazini kwake maana kipindi chake cha Radio ni moja ya vipindi vinavyo sikilizwa zaidi kwa wakati ule. Hilo halina ubishi.
Kama binadamu wengine na yeye nae ana ushindi mwingi na kushindwa kwingi kwenye maisha yake na kwenye session hii tukiyagusia hayo na zaidi. Kuhusu mapenzi, mtoto, familia yake alitokea, elimu na malezi lakini pia muajiri wake wa zamani na jinsi ya kukabiliana na mambo mbali mbali maishani.
Yangu matumaini uta enjoy na kujifunza mambo kadhaa kuhusu kazi na jinsi na kujua kutafuta na kupata kutoka sehemu nyengine ukiachana na ile ulokua umeizoea.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Jamani Da salama siamini nilichoomba kimefanyika nakupendaje 💖💋uwiiiii hongera sana mpz hakuna kama ww in East Africa Mungu akusimamie..nampenda sana huyu Da Dina 😍💖❤
#Yahstonetown naomba mumlete stara thomas...naamini ana mingi ya kuuongelea huu mziki wetu na maisha yake kwa ujumla. Regards🙌🏾💛
daah umewaza mbaali ni kwl yule mdada kitamboo wamletee
Dada mlete Babalevo
Ni “Chawa” but kwenye serious issues he’s so smart 🧠
Wallai watu walopitia maisha magumu ndio nahisi wana maendeleo sana na niwapiganaji wa maisha vizuri
Madam salama. Nashauri interview ya Salama na Maulid kitenge
Ooh nliwatch part 1 nkisubiri part 2, kumbe leo dada Salama kabadilisha kidogo
Marlaw tunaomba umlete Salama🙏🙏🙏
THIS WAS GOOD AS USUAL....NEXT AJE STARA THOMAS BASI
Dah kweli mahasidi wanaanzia udogoni😄😄
Yaan ya kwanza ni ya pili na ya pili ni ya kwanza😅😅😅
Next county wizzy,tuleteee yule boy
huyu dada jamani,nampenda mnoooooooo
Hasidi hana sababu 👌🏽👌🏽👌🏽
Your enemy does not need a reason to do bad things, ama adui huwa hana sababu ya kutaka kukutendea mabaya.
Mtu mwenye kukufanyia hila au ubaya fulani huwa hana sababu za msingi kufanya hilo nalo fanya #salama
Iam Dina,fAns
Penda Sana salama na Dina Mungu awalinde
Salama-Tuletee marlow 🇰🇪🇹🇿
Kweli kabisa marlaw
Wap Salama na Fred Vunjabei
Yea hii n part I
Nice
Hujambo!
Hongera.
Dinaa🔥🔥
UMEKOSEA SALAM, hii ndo Part1, but umeadika part2, Na part 2 umesema Part1
Of course wakwanza mimi #1
nilidhani hivyo pia lakini soma tittle vizuri mwenye kuwahi hakosi part 2
@@ramansitv3292
Smart,
Salama Niletee Juma Nature Au a Upendi kumhojii
Kwanini aspende 😊
Huyu da Dina mmi nampenda namkubaliigi,nilikuwa nakushangaaa ukuwahi kumhoji Dina,Dina ni balaa
Jamani napenda kicheko Cha salama dah
Nampenda sn Dina Marious
Hapo kwenye kuishi na mahasidi kwa akili ndio shida, bora kumtema tu
Good
Finally
Mlete aunty sadaka twamuhitaji
Hasidi ni mtu ambae akiamua kukufanyia Ubaya sio lazm uwe umemkosea Hua anaamua tu kukufanyia Without any reason
❤️
Hii ni part 1 salama
Heey sorry, mme label hizi parts wrongly. Part 1 imekuwa as Part 2 and vice versa.
Awesome c Ya kukosa ii
hasidi hana sababu " mtu akitaka kukuletea jam anakuletea tu hatakama haujamkosea
Salama Tutafutie Na Watu Wa Football Sio Watu Walio Kwenye Media Tu
Live you dada Dina🥰
Typing error Leo kwenye episode but 🔥🔥
Soma virzuri kichwa cha habari... Wee ndo umetafsiri kimakosa... #MwemyeKuwahikakosiPart2
Dina Anazungumza Kiswahilin Kabsa Kwel EFM imekubadili Sana Tofaut Na Dina Yule Wa Clouds
Tuna miss interview yako na Millard ayo
Salama mwambie Dina yeye kazaliwa Arusha,alafu hapendi kuleta mwanamke wa shoka kaskazinii,
Tuletee Nikki mbishi pia tumsikie akijibu maswali yako yakijanja
kabisa mzee
Nakuunga mkono
Next episode fred saganda atishe humu please
Part 1 imeandikwa part 2 na part 2 imeandikwa part 1
She’s goes 😍
Either write She's gone or She goes,
There's no She's goes in English!
@@abdallahcooper3111 jamaa kwani lugha iyo yake au wee ndo unajua sana
@@abdallahcooper3111 qqppp²q
Hasidi hana sababu,mtu mwenye ubaya au akitaka kukufanyia ubaya anafanya bila hata ya kuwa na sababu
Salama niaje nakuomba tulete juma nature
Bonge moja la interview c lakukosaaaa Nature km Nature
SALAMA m na Albart Chalamila tunamuomba
Ya da dina toka umeanza kujipunguza mbona upungui we kula tu ndo mwili wako uwo
Stamina na afande sele walete hapo sijawaona kwa kiti
Stamina n afande sele walete bado sijawaona kwa kiti
Hasidi ni mtu anakuharibia hk anajifanya anakuhurumia au anakupeti peti
Nizaid ya mchawiiii hasidi muharibu wamambo yaaani ktk watu nawachukia ni awa
@@mapekhamis3882 yani hasidi na mnafiki wametofautiana kdg tuu
"#TITLE" YA KWANZA ILIKUWA "#VERYPHILOSOPHICAL..." Laiti aliyefanya "#editing" angejua alichoondoa kilikuwa na thamani kubwa mmno.
Kuna watu wana bahati
mbona husemi umesoma shule zipi majina yake!!
Salama tuletee Max Rioba
Nampenda sana dina mazungimzo yake na no mzuri sana
Yy na Salma Msangi co wakujishaushaua wako real kama ulikula dagaa sema kama ulitembea posta mpk temeke kwa miguu sema tu ni maisha yakawaida binaadam upitia nimependa walivojiachia kwa interview cjui ni kwavile wako ktk iyo section km Salama🙌