Dina Afunguka Chanzo Cha Kuacha Kazi Clouds : "Akufukuzaye Hakwambii Toka" | SALAMA NA DINA PART 2
HTML-код
- Опубликовано: 14 окт 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Dina Marious ni STAR ambaye amakua akijenga jina lake kwa miaka mingi sana. Kama sote tunavyofahamu hakuna mtu ambaye anaibuka tu siku moja na kupata heshima na kuaminiwa kama hajafanya kazi ambayo itamfanya watu wamuamini na kumpenda. Dina yeye ameteka kabisa soko la Wanawake, kitu chochote kinachohusiana na wanawake na madhila, raha na mambo yao ya kijamii basi ukiangalia kushoto na kulia lazima utamkuta Dina yuko hapo akitoa mchango wake kwenye suala hilo. Iwe kuanzia maandalizi au uwepo wake tu. Hicho ndo ambacho yeye kama Mama na Dada na Binti ameamua kufanya, na anaweza haswa.
Alianzia Radio ya watu ya Clouds FM na baada ya kupata mtoto wake wa kwanza mitihani mingi aliipitia, ile maternity leave ambayo alikaa wakati anamkuza kijana wake ilileta mabadiliko makubwa kwenye maisha yake. Zion (mtoto wake) alipo zaliwa ilimbidi Dina aache kazi kwenye Taasisi ambayo alikua ameizoe mno na kutafuta ustaarabu mwengine bila ya kuwa na mipango hiyo wakati alipochukua likizo yake ya kwenda kujifungua. Mipango ilikua akitoka kwenye likizo yake hiyo ya uzazi basi arudi tu kazini kwake kama kawaida lakini Bosi wake wa wakati huo, Marehemu Ruge Mutahaba alikua na mipango mengine na Dina mipango ambayo kwa mujibu wake anaamini alikua akipigwa chenga tu na hakukua na mpango thabiti ambao ulikua umeekwa kwaajili yake.
Dina anakumbuka nenda rudi alizokua akizipata na kulipwa mshahara bila ya kufanya kazi yoyote, kwa kweli hilo lilikua likimsubua sana na anasema kila akiangalia kushoto na kulia alikua haoni dalili zozote za yeye kuanza kufanya kazi muda wowote wa karibu na kwasababu maswali yake mengi mazito yalikua yakipatiwa majibu mepesi mepesi aliona basi si vibaya kama atatafuta challenge nyengine kwenye maisha yake. Kwanza hiyo plan ambayo alikua amepewa hakua ameifurahia na pili majibu ambayo alikua anapatiwa nayo yalimfanya ajue pale hapakua sehemu sahihi kwake tena.
Kumuuma ilikua ikimuuma sana kama anavyosema mwenyewe, hakukua na sababu yoyote ya kutaka kufanya mabadiliko yale ambayo yalifanyika, ya kutaka kumpeleka yeye kwenye TV wakati tayari alikua ameshatengeneza kundi kubwa la mashabiki kwa wakati huo, na pengine approach iliyotumika pia haikua sahihi na hilo liliacha ladha mbaya kwenye moyo na kinywa chake, na baada ya hapo kwasababu kulikua na ofa nyengine hakufanya ajizi kuziskiliza na uzuri zaidi kwanza hapakua mbali na ofisi yake ya zamani hapo alipokua anatakiwa na pili ambalo ndo KUBWA kabisa, alikua anapewa muda ule ule wa hewani kama ambao alinyang’anywa baada ya kuenda likizo ya uzazi kwenye ajira yake ya zamani. Alikua na kila sababu ya kuchukua hatua nyengine na kujisogeza mbele zaidi, kama ambavyo tunafahamu, mtu huenda aitwapo. Na mengine ndo haya, yamebaki story tu.
Nafasi yake kwenye jumuia za wanawake ni ya kipekee na anaiweza kuikaimu vizuri tu, amekua akifanya shughuli mbali mbali za kutatua baadhi ya adha na pia kuwatunza wale ambao anadhani wanastahili ili kuwafanya wapate nguvu zaidi ya kuendelea kufanya wanayofanya kwa uzuri zaidi. Na amekua mfano mzuri hata kazini kwake maana kipindi chake cha Radio ni moja ya vipindi vinavyo sikilizwa zaidi kwa wakati ule. Hilo halina ubishi.
Kama binadamu wengine na yeye nae ana ushindi mwingi na kushindwa kwingi kwenye maisha yake na kwenye session hii tukiyagusia hayo na zaidi. Kuhusu mapenzi, mtoto, familia yake alitokea, elimu na malezi lakini pia muajiri wake wa zamani na jinsi ya kukabiliana na mambo mbali mbali maishani.
Yangu matumaini uta enjoy na kujifunza mambo kadhaa kuhusu kazi na jinsi na kujua kutafuta na kupata kutoka sehemu nyengine ukiachana na ile ulokua umeizoea.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Utu, hekima,uvumilivu Dina ❤❤❤❤ Golden heart interview imetulia na imenipa majibu mengi sana hakika Subra ina malipo
Dina somo yangu hongera kwa kuwa jasili na mpambanaji nimependa story sana
Dina uko real xan, i can feel ur humanity through ur words
Nime jifunza sana hapo kwa baba mtoto 🙏👌🏽
Dina You're the Best.... I think this is the interview I was waiting to hear. Hongera Sana Salama
Unaweza sana Salama, big up sister....hongera sana Dina kwa kujibu maswali vizuri
Maisha ya kazi yana changamotooo sometimes!!!!! Dah 🙌🏻
Exclusive interview ni njia kuu ya kujifunza.Ahsante salama
Good inrerview. Waswahili wanasema Milango ikifungwa upande mmoja Mola anakufungulia upande mwengine
Dina nakupendaga Sana mpenzi
Namkubali Sana Dina umepambna Sana Mungu akuzidishie baraka
Dina since day 1
DINA YOU ARE THE BEST
Nampenda Sana Dina...kibonge mwenzangu...leo nimefarijika sana ...ila bado sijaelewa ile Salma Msangi imepotea wapi?mn pia nampenda Sana Somo.yangu
Alimuhoji Salma Msangi Mpnz Nae Yuko vzr Kwny Kujibu Maswali 🙌
Nakumbuka kipindi cha leo tena wakati ule kilikuwa 🔥 hapa Dina pale da Suzy na kule Geàh Habib balaam lilikuwa zito. Nilikuwa malini nacho sana kipindi cha leo tena.
Dina we mkaliiiii hatariiii🔥🔥🔥
Nakupenda Dina unajielewa Sana darling🌹
Super 👌 good 👍 excellent interview 👏 I love dinnar
I love the story, and i love Dina 😘❤️
Interview ni nzuri sana sana sana...! Hongereni sana
Nilisoma gazette la udaku kipindi hicho kuhusu kuondoka clouds ni sababu alikuwa haelewani na zamaradi ambae alikuwa in relation na Boss
Asante sana dina
Penda Sana Salama na Dina Mungu awalinde
Ilove you salama 💪🤲🙏
Dina Marios Mimi Ni shabiki yako tangu 2006 ndio kwanza naingia mjini adi Leo japo apo katikati nilisafiri ila ckujua uko efm Mana niliachana na kusikiliza radio kipindi Cha magufuli mana radio nyingi zilibadilika na kuamua kumsifu magu tu Ila yote kwa yote nimejifunza mengi kutoka kwako wee ni shujaa .
Nimeinjoy Sana kusikiliza iki kipindi
Dina I love youuuu🥰🥰🥰🥰🥰😍😍🥰🥰🥰
Kwl akufukuzae akuambii toka hy
best kipindi ever seen.
Wana RUclips mmetusahau wiki hii Jamani ama? Salama na ya wiki hii Hamna?
Keep it up sis...Salama!! We love u
Natamani sana kukutana na Dina
Huyo ex ni Ruben Ndege"Ncha Kali!
Ohkay!!!
💯💯
Nimejifunza kitu jmn
Kumbe Salama ana mtoto uwiii duh
Cha ajabu nini
19:21....📌
Anae toa uhai ni mmoja tu aliyeumba ww umebeba tu kwa uheri ila muumba ni mmoja tu
💜🎉
unajua understand zinakuja baadaye baada ya why nyingi...dina marios bonge 1 la mtu mwanamke na nusu
Uyu mdada nilikuwa nampenda kabla sijamuona kila mtoto anakusudio lake akuna bahati mbaya
Leo kupindi kimeanza mwisho kwenda mwanzo
UMEKOSEA SALAM, hii ndo Part2, but umeadika part1, Na part 1 umesema Part2
Of course wapili mimi #2
hata mm.naiona kama 2
Ndio
Soma vizuri alivyoandika.....
@@ebenezanatse9436
Got you son
Umenena vyema
Kwani nani baba wa mtoto wetu dina ?
Ukijibiwa nitag tafadhali
Kwani aliza nanani???
Ncha kali (Ruben Ndege)
Kwani Dina alizaa nani?natamani kujua mzazi mwenzake msahada please
Ncha kali mzee wa ubunifu pale mawinguni
Nchakali hatari sana
Nani huyo ncha kali?
Sebastian Maganga
Reuben ndege a k a ncha Kaliiiii
Kumbukumbu zangu dina Mario's aliwahikumohoji mond kipindi kile bando mdogo kweny gemu mlete tenabando anamadini mengi sana
Dina anajielewa sana kwakweli hana ushamba wa mabifu ila swali alivyolazwa hosptl mwez ilikuwa ni haya matatizo ya baba mtt wake??
Interview nzuri ila alizaa na nani sijui,umbea huu utanipeleka pabaya wooiii
Ruben Nchakali
Nae ni mtangazaji
Huyu dada nmempenda zaidi, mkweli mno.
Apo baadh ya watu maarufu(co woote) watizame waone vile majibu yanatakiwa co kujibu swali km umevurugwa au unajickiiiia kujibu swali 😀😀😀
HII MBONA IMEANZA TUU 🤣🤣🤣
Hata mimi nimeshangaa nilijua part 2
@@muna1744 aah kumbe wamekosea heading tuu.. part one ndio 2 na two ndio 1
@@mkaapwekekariakoo6417 wewe ndio hujaelewa, kaa kimya
@@Hashdough 🙏🙏
@@Hashdough sijaelewa nini sasa mbona unanitaja biala sababu????
Mualike mwaisa siku moja
🥰🥰🥰🥰🥰🥰
Na walifanyana nini na Zamaradi
Hhhhhhhh
Mbona hatumjui huyo ex wa dada Dina? Natamani kumjua. Ila hongera sana dada kukuza mtoto wako
Anaitwa nncha kali yuko pale clauds
Nakumbuka kipindi cha leo tena wakati ule kilikuwa 🔥 hapa Dina pale da Suzy na kule Geàh Habib balaam lilikuwa zito. Nilikuwa malini nacho sana kipindi cha leo tena.