Dina Afunguka Chanzo Cha Kuacha Kazi Clouds : "Akufukuzaye Hakwambii Toka" | SALAMA NA DINA PART 2

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 окт 2024
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Dina Marious ni STAR ambaye amakua akijenga jina lake kwa miaka mingi sana. Kama sote tunavyofahamu hakuna mtu ambaye anaibuka tu siku moja na kupata heshima na kuaminiwa kama hajafanya kazi ambayo itamfanya watu wamuamini na kumpenda. Dina yeye ameteka kabisa soko la Wanawake, kitu chochote kinachohusiana na wanawake na madhila, raha na mambo yao ya kijamii basi ukiangalia kushoto na kulia lazima utamkuta Dina yuko hapo akitoa mchango wake kwenye suala hilo. Iwe kuanzia maandalizi au uwepo wake tu. Hicho ndo ambacho yeye kama Mama na Dada na Binti ameamua kufanya, na anaweza haswa.
    Alianzia Radio ya watu ya Clouds FM na baada ya kupata mtoto wake wa kwanza mitihani mingi aliipitia, ile maternity leave ambayo alikaa wakati anamkuza kijana wake ilileta mabadiliko makubwa kwenye maisha yake. Zion (mtoto wake) alipo zaliwa ilimbidi Dina aache kazi kwenye Taasisi ambayo alikua ameizoe mno na kutafuta ustaarabu mwengine bila ya kuwa na mipango hiyo wakati alipochukua likizo yake ya kwenda kujifungua. Mipango ilikua akitoka kwenye likizo yake hiyo ya uzazi basi arudi tu kazini kwake kama kawaida lakini Bosi wake wa wakati huo, Marehemu Ruge Mutahaba alikua na mipango mengine na Dina mipango ambayo kwa mujibu wake anaamini alikua akipigwa chenga tu na hakukua na mpango thabiti ambao ulikua umeekwa kwaajili yake.
    Dina anakumbuka nenda rudi alizokua akizipata na kulipwa mshahara bila ya kufanya kazi yoyote, kwa kweli hilo lilikua likimsubua sana na anasema kila akiangalia kushoto na kulia alikua haoni dalili zozote za yeye kuanza kufanya kazi muda wowote wa karibu na kwasababu maswali yake mengi mazito yalikua yakipatiwa majibu mepesi mepesi aliona basi si vibaya kama atatafuta challenge nyengine kwenye maisha yake. Kwanza hiyo plan ambayo alikua amepewa hakua ameifurahia na pili majibu ambayo alikua anapatiwa nayo yalimfanya ajue pale hapakua sehemu sahihi kwake tena.
    Kumuuma ilikua ikimuuma sana kama anavyosema mwenyewe, hakukua na sababu yoyote ya kutaka kufanya mabadiliko yale ambayo yalifanyika, ya kutaka kumpeleka yeye kwenye TV wakati tayari alikua ameshatengeneza kundi kubwa la mashabiki kwa wakati huo, na pengine approach iliyotumika pia haikua sahihi na hilo liliacha ladha mbaya kwenye moyo na kinywa chake, na baada ya hapo kwasababu kulikua na ofa nyengine hakufanya ajizi kuziskiliza na uzuri zaidi kwanza hapakua mbali na ofisi yake ya zamani hapo alipokua anatakiwa na pili ambalo ndo KUBWA kabisa, alikua anapewa muda ule ule wa hewani kama ambao alinyang’anywa baada ya kuenda likizo ya uzazi kwenye ajira yake ya zamani. Alikua na kila sababu ya kuchukua hatua nyengine na kujisogeza mbele zaidi, kama ambavyo tunafahamu, mtu huenda aitwapo. Na mengine ndo haya, yamebaki story tu.
    Nafasi yake kwenye jumuia za wanawake ni ya kipekee na anaiweza kuikaimu vizuri tu, amekua akifanya shughuli mbali mbali za kutatua baadhi ya adha na pia kuwatunza wale ambao anadhani wanastahili ili kuwafanya wapate nguvu zaidi ya kuendelea kufanya wanayofanya kwa uzuri zaidi. Na amekua mfano mzuri hata kazini kwake maana kipindi chake cha Radio ni moja ya vipindi vinavyo sikilizwa zaidi kwa wakati ule. Hilo halina ubishi.
    Kama binadamu wengine na yeye nae ana ushindi mwingi na kushindwa kwingi kwenye maisha yake na kwenye session hii tukiyagusia hayo na zaidi. Kuhusu mapenzi, mtoto, familia yake alitokea, elimu na malezi lakini pia muajiri wake wa zamani na jinsi ya kukabiliana na mambo mbali mbali maishani.
    Yangu matumaini uta enjoy na kujifunza mambo kadhaa kuhusu kazi na jinsi na kujua kutafuta na kupata kutoka sehemu nyengine ukiachana na ile ulokua umeizoea.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz

Комментарии • 84

  • @hawaaman3172
    @hawaaman3172 9 месяцев назад +1

    Utu, hekima,uvumilivu Dina ❤❤❤❤ Golden heart interview imetulia na imenipa majibu mengi sana hakika Subra ina malipo

  • @BernadethaMihele
    @BernadethaMihele 2 месяца назад

    Dina somo yangu hongera kwa kuwa jasili na mpambanaji nimependa story sana

  • @lotilazaro8845
    @lotilazaro8845 2 года назад +5

    Dina uko real xan, i can feel ur humanity through ur words

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 2 года назад +5

    Nime jifunza sana hapo kwa baba mtoto 🙏👌🏽

  • @dr.sarahbusongo
    @dr.sarahbusongo 2 года назад +3

    Dina You're the Best.... I think this is the interview I was waiting to hear. Hongera Sana Salama

  • @catherinemwanga6227
    @catherinemwanga6227 2 года назад +2

    Unaweza sana Salama, big up sister....hongera sana Dina kwa kujibu maswali vizuri

  • @agnessjoseph9069
    @agnessjoseph9069 2 года назад +1

    Maisha ya kazi yana changamotooo sometimes!!!!! Dah 🙌🏻

  • @mgenikisinzah1564
    @mgenikisinzah1564 2 года назад

    Exclusive interview ni njia kuu ya kujifunza.Ahsante salama

  • @rehemamakuburi8254
    @rehemamakuburi8254 2 года назад +2

    Good inrerview. Waswahili wanasema Milango ikifungwa upande mmoja Mola anakufungulia upande mwengine

  • @moshielfesty7992
    @moshielfesty7992 8 месяцев назад

    Dina nakupendaga Sana mpenzi

  • @leaherasto929
    @leaherasto929 2 года назад

    Namkubali Sana Dina umepambna Sana Mungu akuzidishie baraka

  • @brainsngaugula6075
    @brainsngaugula6075 2 месяца назад

    Dina since day 1

  • @happymilangasi5904
    @happymilangasi5904 2 года назад +1

    DINA YOU ARE THE BEST

  • @salmadulazi6876
    @salmadulazi6876 2 года назад +1

    Nampenda Sana Dina...kibonge mwenzangu...leo nimefarijika sana ...ila bado sijaelewa ile Salma Msangi imepotea wapi?mn pia nampenda Sana Somo.yangu

    • @mapekhamis3882
      @mapekhamis3882 2 года назад

      Alimuhoji Salma Msangi Mpnz Nae Yuko vzr Kwny Kujibu Maswali 🙌

  • @asiaasia5025
    @asiaasia5025 2 года назад +1

    Nakumbuka kipindi cha leo tena wakati ule kilikuwa 🔥 hapa Dina pale da Suzy na kule Geàh Habib balaam lilikuwa zito. Nilikuwa malini nacho sana kipindi cha leo tena.

  • @rehemarwanda6039
    @rehemarwanda6039 Год назад

    Dina we mkaliiiii hatariiii🔥🔥🔥

  • @kissamwamunyange1018
    @kissamwamunyange1018 2 года назад

    Nakupenda Dina unajielewa Sana darling🌹

  • @ibrahimkibira9943
    @ibrahimkibira9943 2 года назад

    Super 👌 good 👍 excellent interview 👏 I love dinnar

  • @sky-wz5zi
    @sky-wz5zi 2 года назад

    I love the story, and i love Dina 😘❤️

  • @mc_mrope
    @mc_mrope 2 года назад

    Interview ni nzuri sana sana sana...! Hongereni sana

  • @felixjunior4772
    @felixjunior4772 2 года назад +3

    Nilisoma gazette la udaku kipindi hicho kuhusu kuondoka clouds ni sababu alikuwa haelewani na zamaradi ambae alikuwa in relation na Boss

  • @hamidasaif4065
    @hamidasaif4065 Год назад

    Asante sana dina

  • @niriacatering172
    @niriacatering172 2 года назад

    Penda Sana Salama na Dina Mungu awalinde

  • @ahmedaliabdallaali7946
    @ahmedaliabdallaali7946 Год назад

    Ilove you salama 💪🤲🙏

  • @bntrashidi3083
    @bntrashidi3083 Год назад

    Dina Marios Mimi Ni shabiki yako tangu 2006 ndio kwanza naingia mjini adi Leo japo apo katikati nilisafiri ila ckujua uko efm Mana niliachana na kusikiliza radio kipindi Cha magufuli mana radio nyingi zilibadilika na kuamua kumsifu magu tu Ila yote kwa yote nimejifunza mengi kutoka kwako wee ni shujaa .
    Nimeinjoy Sana kusikiliza iki kipindi

  • @yurisongoro2895
    @yurisongoro2895 2 года назад

    Dina I love youuuu🥰🥰🥰🥰🥰😍😍🥰🥰🥰

  • @khadijahali4837
    @khadijahali4837 2 года назад

    Kwl akufukuzae akuambii toka hy

  • @khaleedmakiya8892
    @khaleedmakiya8892 2 года назад +2

    best kipindi ever seen.

  • @Annie-tt8fi
    @Annie-tt8fi 2 года назад

    Wana RUclips mmetusahau wiki hii Jamani ama? Salama na ya wiki hii Hamna?

  • @mustaphareginald3264
    @mustaphareginald3264 2 года назад

    Keep it up sis...Salama!! We love u

  • @annaabraham6999
    @annaabraham6999 2 года назад

    Natamani sana kukutana na Dina

  • @tonyriziki37
    @tonyriziki37 2 года назад +2

    Huyo ex ni Ruben Ndege"Ncha Kali!

  • @muniramunira9941
    @muniramunira9941 2 года назад

    💯💯

  • @GloryMsopa
    @GloryMsopa 5 месяцев назад

    Nimejifunza kitu jmn

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 2 года назад +1

    Kumbe Salama ana mtoto uwiii duh

  • @maryshirima1234
    @maryshirima1234 2 года назад +2

    19:21....📌

  • @mankacharles4559
    @mankacharles4559 2 года назад

    Anae toa uhai ni mmoja tu aliyeumba ww umebeba tu kwa uheri ila muumba ni mmoja tu

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 2 года назад

    💜🎉

  • @husseinibnuhassan1272
    @husseinibnuhassan1272 2 года назад +3

    unajua understand zinakuja baadaye baada ya why nyingi...dina marios bonge 1 la mtu mwanamke na nusu

  • @uwezomabava3949
    @uwezomabava3949 2 года назад

    Uyu mdada nilikuwa nampenda kabla sijamuona kila mtoto anakusudio lake akuna bahati mbaya

  • @dianerditto
    @dianerditto 2 года назад

    Leo kupindi kimeanza mwisho kwenda mwanzo

  • @RamazaniMulongeca
    @RamazaniMulongeca 2 года назад +2

    UMEKOSEA SALAM, hii ndo Part2, but umeadika part1, Na part 1 umesema Part2
    Of course wapili mimi #2

  • @rosetasuleiman6799
    @rosetasuleiman6799 2 года назад

    Umenena vyema

  • @xkingx8041
    @xkingx8041 2 года назад +1

    Kwani nani baba wa mtoto wetu dina ?

  • @nickolatharwelamila776
    @nickolatharwelamila776 2 года назад +2

    Kwani aliza nanani???

  • @Jassmin-media-official
    @Jassmin-media-official 2 года назад +4

    Kwani Dina alizaa nani?natamani kujua mzazi mwenzake msahada please

  • @hamadgakwaya3466
    @hamadgakwaya3466 2 года назад

    Kumbukumbu zangu dina Mario's aliwahikumohoji mond kipindi kile bando mdogo kweny gemu mlete tenabando anamadini mengi sana

  • @roseurio9600
    @roseurio9600 2 года назад

    Dina anajielewa sana kwakweli hana ushamba wa mabifu ila swali alivyolazwa hosptl mwez ilikuwa ni haya matatizo ya baba mtt wake??

  • @elizabethhonere2931
    @elizabethhonere2931 Год назад

    Interview nzuri ila alizaa na nani sijui,umbea huu utanipeleka pabaya wooiii

  • @josephk90
    @josephk90 2 года назад

    Huyu dada nmempenda zaidi, mkweli mno.

    • @mapekhamis3882
      @mapekhamis3882 2 года назад

      Apo baadh ya watu maarufu(co woote) watizame waone vile majibu yanatakiwa co kujibu swali km umevurugwa au unajickiiiia kujibu swali 😀😀😀

  • @Hashdough
    @Hashdough 2 года назад +1

    HII MBONA IMEANZA TUU 🤣🤣🤣

    • @muna1744
      @muna1744 2 года назад

      Hata mimi nimeshangaa nilijua part 2

    • @Hashdough
      @Hashdough 2 года назад

      @@muna1744 aah kumbe wamekosea heading tuu.. part one ndio 2 na two ndio 1

    • @Hashdough
      @Hashdough 2 года назад

      @@mkaapwekekariakoo6417 wewe ndio hujaelewa, kaa kimya

    • @mkaapwekekariakoo6417
      @mkaapwekekariakoo6417 2 года назад

      @@Hashdough 🙏🙏

    • @mkaapwekekariakoo6417
      @mkaapwekekariakoo6417 2 года назад

      @@Hashdough sijaelewa nini sasa mbona unanitaja biala sababu????

  • @abdallahmdangadachi7030
    @abdallahmdangadachi7030 2 года назад

    Mualike mwaisa siku moja

  • @yurisongoro2895
    @yurisongoro2895 2 года назад

    🥰🥰🥰🥰🥰🥰

  • @muna1744
    @muna1744 2 года назад

    Na walifanyana nini na Zamaradi

  • @kazkaz1943
    @kazkaz1943 2 года назад

    Hhhhhhhh

  • @ilovejesus9303
    @ilovejesus9303 2 года назад

    Mbona hatumjui huyo ex wa dada Dina? Natamani kumjua. Ila hongera sana dada kukuza mtoto wako

  • @asiaasia5025
    @asiaasia5025 2 года назад

    Nakumbuka kipindi cha leo tena wakati ule kilikuwa 🔥 hapa Dina pale da Suzy na kule Geàh Habib balaam lilikuwa zito. Nilikuwa malini nacho sana kipindi cha leo tena.