HOTUBA KAMILI YA RAIS MAGUFULI AKIWA MUSOMA - 05/09/2018

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 5 сен 2024
  • Rais Magufuli leo tarehe 05 Septemba, 2018 ameendelea na ziara yake katika mkoa wa Mara ambapo amezindua mradi wa maji safi na usafi wa mazingira wa Manispaa ya Musoma, kufungua barabara ya Simiyu/Mara - Musoma na kisha kuhutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja Mukendo Musoma Mjini.
    Katika hotuba yake Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa na hatua zinazochukuliwa na viongozi wa Wizara, Mkoa wa Mara na vyombo vya dola dhidi ya mfanyabiashara Nyakilang’ani ambaye amelalamikiwa na wananchi wa Mwisenge katika Manispaa ya Musoma kuwa baada ya kuuziwa hoteli ya Musoma amezuia wananchi kukatiza katika eneo hilo wanapotaka kwenda katika mwambao wa ziwa Victoria na hivyo kulazimika kuzunguka umbali mrefu.
    “Hoteli hii imechukuliwa tangu miaka 10 iliyopita, haijaendelezwa, wananchi wanakosa ajira, Serikali inakosa mapato halafu viongozi mpo mnamuangalia tu, huyohuyo Nyakilang’ani amepewa mradi wa maji wa mji wa Bunda huu mwaka wa 8 na mpaka sasa hautoi maji, viongozi mpo hamchukui hatua.
    “Sasa nataka hoteli ya Musoma iliyojengwa na Baba wa Taifa kwa nia yake njema ya kuiendeleza Musoma ichukuliwe kwa sababu ameshindwa kuiendeleza” amesisitiza Rais Magufuli.
    Rais Magufuli pia amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Mara kuwa Serikali itahakikisha inaujenga kwa kiwango cha lami uwanja wa ndege wa Musoma ili uweze kupokea ndege kubwa na ndogo, na kukamilisha ujenzi wa hospitali ya Musoma haraka ili ifanane na hadhi ya hospitali iliyopo katika Mkoa aliozaliwa Baba wa Taifa.

Комментарии • 31

  • @henrysterling5133
    @henrysterling5133 2 месяца назад

    Mungu akuweke mahara pema😢

  • @mahmoudaziz6281
    @mahmoudaziz6281 6 лет назад +3

    my president magufuli. nakupenda mungu ndo anajua. napenda kwenye ziara zako niuzurie lkn sina uwezo. nakufuati kupitia RUclips.mi napenda utuongoze wewe miaka 50 tu. naisi akuna mtanzania yeyote atakae kwenda ulaya au nchi jirani kutafuta maisha.

  • @jamesngundateresia2600
    @jamesngundateresia2600 6 лет назад +5

    BABA DUNIA ZIMA INAKUELEWA SANA MIMI NI SHAHIDI MWAMINIFU

  • @shabanrajab3559
    @shabanrajab3559 6 лет назад +2

    Jamaa Yuko sawa duhh lahaja Zote anazipata duhh n

  • @joshuanjole578
    @joshuanjole578 6 лет назад +1

    Hongera raisi wetu

  • @jamesngundateresia2600
    @jamesngundateresia2600 6 лет назад +1

    Mambo ni hivi👏👏👏👏

  • @donyisrich2973
    @donyisrich2973 6 лет назад

    Chapa kazi my prsident

  • @jilugalamarco9308
    @jilugalamarco9308 6 лет назад +1

    do it and redo it tirelessly

  • @jackhans7708
    @jackhans7708 2 года назад

    Ninakukuri mzeee na nitakukubali daima

  • @jamesngundateresia2600
    @jamesngundateresia2600 6 лет назад +1

    Watu kama wote good kamanda
    LUGOLA UPO BABA

  • @philipojosephlukumay3965
    @philipojosephlukumay3965 6 лет назад +3

    Sijui kama Watanzania wengi wanafuatilia hizi hotuba kwa umakini kama mimi🤓
    Mimi naamini rais wetu JPM ni Mungu kamleta wakati huu
    Kama kweli gesi asilimia 70 inachukuliwa maana yake huo uchumi wetu hautokaa uboreke kama tutaendelea na mifumo iliokuwepo.
    Rais wangu endelea na moto huo huo watanzania wenye akili watakuelewa tu

  • @rashidiomary1324
    @rashidiomary1324 6 лет назад +3

    mzee Mimi nakushukuru kwa kitu kimoja mwaka huu nacho ni kutomtumbua makonda, amefanya mambo makubwa sana tangu umteue

  • @petermwenda5179
    @petermwenda5179 6 лет назад

    I m a respect my President

  • @frankmganda116
    @frankmganda116 6 лет назад +1

    Hakika ninge kuwa na uwezo kila ungekuwa unatembea mikoani ningekuwa na udhuria maana hotuba zako zote zinagusa maisha ya watanzania tulio wengi asa sisi masikini hakika tunaomba uendelee kuwepo niseme nini mzee

  • @abdulrazakyussef3177
    @abdulrazakyussef3177 6 лет назад +1

    Baada ya second term, (ukiondoka) angaza macho ili upate Sokoine mwingine aje awe rais wa wananchi siyo wa ''wenye-inchi''

  • @samsomkaziyoba9958
    @samsomkaziyoba9958 2 года назад

    mm GI. Vi YMCA fadw

  • @trophainamagogwa9590
    @trophainamagogwa9590 6 лет назад +2

    Lugha zooote unajua aise unafaa kuongoza

  • @kallahassan4896
    @kallahassan4896 6 лет назад +1

    baba osijali tupo pamoko

  • @rashidiomary1324
    @rashidiomary1324 6 лет назад

    ili kiongozi awe bora anatakiwa aingie gerezani kwanza asote akili ndo huwa zinakaa vizuri

  • @toshindugwa1085
    @toshindugwa1085 2 года назад

    Sijui wapi watanzania hawakukuelewa,ila sasa maneno yako yanaishi ulivyojitabiria mwamba

  • @rashidiomary1324
    @rashidiomary1324 6 лет назад +1

    watu wa musoma nyuso zao hazina stress

  • @habilicharles4410
    @habilicharles4410 6 лет назад +1

    Je ninani kama Magufuli? jibu hakunaaaaaa

  • @rashidiomary1324
    @rashidiomary1324 6 лет назад

    kwanza mzee ungeanza na lukuvi yeye kwa nini hakuumaliza huo mgogoro

  • @leonviskb8012
    @leonviskb8012 6 лет назад

    Tunawahona tunawahona munakula tu ubuyu ahhn subcriber chanily yetu pls