SIMBA YARUDI KWENYE MAFAILI/ KUIBOMOA TP MAZEMBE/MGUNDA APETA MAZIMA/KIBU DENIS, MENEJA WAKE WAHUKA!
HTML-код
- Опубликовано: 2 май 2024
- Baada ya kuondoka kwa Abdelhak Benchikha, Uongozi wa Simba SC kwa haraka umeanza mchakato wa kutafuta Kocha Mkuu mpya atakayerithi mikoba ya Mualgeria huyo ukipanga kukamilisha ishu hiyo kabla ya msimu huu kumalizika Mei 28, 2024.
Mabosi wa Simba SC walikaa kikao baada ya kuondoka kwa Benchikha aliyesepa na wasaidizi wake Farid Zemit na Kamal Bougnan, na kuamua kuanza mara moja mchakato wa kupata mrithi wake ambaye atakinoa kikosi cha klabu hiyo walau katika michezo mitatu ya mwisho msimu huu, ili ajue wapi pa kuanzia katika usajili wa dirisha kubwa likifunguliwa baada ya kumalizika kwa msimu.
Licha ya Simba SC kufanya kuwa siri, lakini taarifa zinabainisha kuwa Wekundu wa Msimbazi wanatafuta kocha haraka ili aweze kusimamia shoo nzima ya usajili ambao klabu hiyo imepanga kufanya kufuru kwa kushusha majembe yatakayoipambania na kurejesha ufalme ilioupoteza misimu mitatu sasa.
--
Dar24 ni chanzo namba moja cha habari kwa watanzania mahali popote walipo duniani. Kwa habari za uhakika kutoka nyanja mbali mbali.
JE, NA WEWE UNA HABARI?
⚫️ WASILIANA NA DAR24 MEDIA: +255 679 979 786
⚫️ Email: dar24newsroom@gmail.com
⚫️ Website: www.dar24.com
⚫️ Instagram: @Dar24news
⚫️ Facebook: @dar24
⚫️ Twitter: @Dar24News
#simbasc #ahmedally #usajilisimbasc - Спорт
Aendeeeee
Hata aje Pep Guardiola bila ya wachezaji wa maana hamna kitu...mtaburuza mkia kila uchwao!
Kibu aende tu sodhani kama kweli ana thamani kubwa kiasi hicho lazima kwanza awashukuru wale waliomnyanyua akaonekana wachezaji hawa watawayumbisha sana viongozi na timu kwa ujumls wanajivunja sana kwenye mechi
Yeye asepe tuu asiwe anajivunja kwenye mech
Mie naona bora aende tu kwasababu akibaki hatacheza kwakujituma, wamwache aende akatafute changamoto zingine
SIMBAA MRUDISHENI SVEN NDIO MTAFAULU HUYO NDIO MWALIMU BORA KWA SASA MPENI TIMU AIJENGE
Viongoz wanapaparuka tu mwacheni mgunda timu