CHATANDA AWA MBOGO KUHUSU VITENDO HIVI//TOENI TAARIFA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 15 окт 2024
  • #Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) amekemea vikali vitendo vya uvunjivu wa maadili vinavyojitokeza katika jamii.
    Chatanda ameitaka jamii kuungana pamoja kupinga na kukemea vikali uvunjivu wa maadili, pamoja na kuwaibua vinara wa vitendo hivyo katika jamii zao.
    Chatanda ameyasema hayo akiwa katika ziara inayolenga kuhuisha na kuimarisha uhai wa CCM pamoja, Kuhamasisha Wanawake wengi Kuhombea Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 na kuhamasisha wananchi, Wanachama wa CCM na Jumuiya zake kushiriki zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la Wapiga kura linarotarajiwa kuzinduliwa tarehe 20 Julai mkoani Kigoma.
    Ziara hiyo inayofanyika Mkoani Tabora, imeanza rasmi tarehe 10 Julai 2024 na inatarajiwa kumalizika tarehe 12 Julai 2024.

Комментарии •