VIDEO! KAULI ya IRENE UWOYA AKIHUBIRI KANISANI MORO, AMWAGA HELA
HTML-код
- Опубликовано: 9 июл 2022
- #nia24tv #morogoro #Irineuwoya
Leo mkoa Morogoro Mwigizaji maarufu nchini Irene Uwoya amealikwa kuwa mgeni rasmi katika kanisa la Ufunua lililopo Mkundi Manispaa ya Morogoro katika sherehe ya wanawake wa kanisa hilo pamoja na kutimiza miaka 8 tangu kuanzishwa kwake.
katika ibada hiyo Uwoya alipewa fursa ya kuhubiri neno la Mungu ndipo akatumia nafasi hiyo kutoa wito kwa jamii kuacha kuwachukulia wasanii kama watu wenye dhambi kuliko watu wote Duniani jambo ambalo halina ukweli huku akiahidi kuchangia milioni tano ya ujenzi wa kanisa hilo.
Sasa jamani mtu kaokoka Leo unataka afanane na wewe una miaka 20 ktk wokovu? Yesu amemkuta na tattoo yeye mwenyewe amemkubali hivyo wewe mwanadamu unaongeeeea. Sote tuongeze BIDII ktk kujifunza na kumtafuta Mungu. Hongera dada Mbingu zimefurahi msimkatishe tamaa Mungu anazidi kutengeneza maisha yetu kidogokidogo. Hadi tutamlaki Yesu mawinguni.
Hapa kinachoongelewa siyo Irene kuokoka hapana,bali kinachoongelewa hapa ni suala la kujiita mchungaji.
Irene bado ni mchanga kiroho kupewa wajibu wa kuchunga wengine.
Biblia hairuhusu mtu aliyeokoka hivi karibu kupewa kuhudumia wengine kabla ya kukaa chini afundishwe aive ili afae kuwaongoza wengine
Kwa wale wanaosoma Biblia wanaelewa ninachosema. Ukisoma habari za Musa kabla hatajtumwa kwenda kuwakomboa wana wa Israel alipitishwa shule kwanza, Paulo baada ya kuokoka hakuruhusiwa kutumika mpaka alipofundishwa,na wengine kama akina Daudi na Samweli
*Hatari inayoweza kujitokeza mtu aliyeokoka hivi karibu na kuanza huduma hapo hapo ni kujikuta anapotosha anaowaongoza pasipo kujua.
Ni utaratibu wa Mungu kumwandaa mtu kabla hajawa,mtume,nabii,mchungaji na kadharika. Ni nia njema ya kufanya hivyo,ili uwe umejengewa misuli ya imani itakayokusaidia kumudu changamoto katika kuwahidumia wengine. Lkn pia itskusaidie kuyaishi yale kwa matendo yale unayowafundisha wengine.
Mungu amekuonekania jamanii hongera❤😊 ila sasa vikuku hvy miguuni jamniii
Atabadilika tu msimhukmu mungu yupo atambadilisha
Hivi kweli sisi ni wasafi kiasi cha kumuhukumu huyu dada?? Mimi naamini kama Ameamua kumgeukia MUNGU, basi MUNGU mwenyewe atambadilisha na anaweza kuja kuwa Mtu tofauti Kabisaaa hatubadiliki Mala moja tuuu. Mungu akusaidie dada ili uje uwavute wengi kwa Bwana.
Mungu akutangulie na azidi kukutia nguvu
Ubarikiwe Irene, acha wapige kelele ww kaza mwendo kwani mtume Paulo mbona alikuwa akiua watu wa Mungu alipokuwa akiitwa Sauli lakini Mungu alimwita kwa kazi yake,
Mahali ulipofikia Mungu ni mwema ! Pamebaki muonekano tu dada yetu na Mungu akuwezeshe
Nakuona mbali Irene❤❤❤❤, Yesu ni mzuri jmn
Kweli Mungu akusaidie kama umeamua kuokoka kweli kutoka ndani ya moyo wako. Naomba tusimuhukumu ata SIsi Mungu alitutoa mbali atatengenezwa tu. Mungu ndiye anayetengeneza watu wake wanaokubari kunyenyekea kwake.
Umeanza hatua ya kwanza, hatua nyingine ni kuachana na kucha za kubandika, kope za bandia, mavazi ya waziwazi, na nywele zitofautishwe na wasio mjua MUNGU..zisichachamae kichwani..na mengine roho mtakatifu atakavyookuelekeza kwa ajili ya hekalu lake.. Barikiwa sana..
Toa miwani hiyo labda kama unaumwa macho
Hongera sana dada, MUNGU akutangulie ❤❤❤❤❤❤
Mungu akubarik dada uendelee ivyo ivyo
Nikupongeza Sana Irene...kwa uamuzi..wako ..na Mungu azidi kukutetea japo utatukanwa Sana na watu ila hata Yesu alitukanwa songa mbele
Ataweza kuweza kuacha kuuza mwili ?
Mungu akakutumie vema amina🙏🙏🙏🙏
Mwachen dada wawatu amtumikie mungu ,wokovu sio wasku moja kila sku tunakoka ebu achani kujihesabia haki wapendwa we mwenyewe mungu alikokutoa unajua ulifanya uovi gani unajua mwenyewe ,mungu msmamishe dada huyu alietambua kuwa Maisha bila wewe no bure
Amen pastor maana sio mwenzetu tena
Amen Mungu akubariki
Kuna mtu kuokoka ni jambo moja na ni muhimu zuri .
Lakini mtu kuwa mchg si jambo jepesi kama tunavyodhani.
Biblia imeonya sana kabla mtu hujawa muhudumu kwa wengine baada ya kuokoka anapaswa kukaa kwanza chini ya watu maalum walio na uwezo kuliko yeye ili kumtengeneza na kumpa miongozo sahihi.Ndivyo ilivyokuwa utaratibu wa Biblia tangu Agano la kale na Agano jipya.
*Ni sawa na kutaka kuwadereva wa chombo chochote kabla hujajifunza namna ya kukiendesha,mwisho wa siku nikuingiza abiria kwenye magorongo.
* Tujifanze kwa Musa kabla haijatumwa kwenda Misri kabla kuwakombo wana wa Israel,Sauli kabla hajawa Paulo, Kornelio,Samwel n.k.
Nimekupenda sana dada iren kaza mwanangu utapitia mengi wengi watakusema ila kaza aliyekuita anakujuwa kuliko mwanadama pambana mwanangu
Hongera sana
Mungu aendelee kukupandisha kwa viwango ili uyafikie malengo yako.Tunakuombea,hakika umechagua fungu lililo jema.
Amen!!!
Irene Mungu akubariki sana kwa uamuzi huo ulio uchagua
Hahahaaaaa ushajiunga rasmin na chama cha kuwauwa maalbino
Ivi mbn hueleweki kucha kama sheytani minyelele hata nguo ulovaa eti umerudi kwa mungu na uvaa wavu jamani uyo mungu mmh
Atabadirika kwani we msafi Sana?
Mungu anataka kutumikiwa ivo?...
Mbona sioni anamtaja Yesu? Anamwogopa maana anafanya kinyume na utaratibu wake, embu acha kuekt ww mama ipo utakuja Lia na huwo uchangaji wako bandia angalia ata unavyo ongea Ni uwongo mtupu, Wala kwel haimo ndani yako, eti mchungaji umevaa vikuku mguuni
Mungu haangalii mwanzo anaiangalia hatma wewe unaehukumu kazana tu
Hongera sana kwa kuchaguliwa
Mapenzi Ya Bwana yatimizwe
Hiyo miwani sasa mmmm
Nenda shule bas ukasome kwanza. Ndo uje.elimu ya kimbingu inahitaji roho mtakatifu na maarifa.sasa ili upate maarifa.nenda shule.
Afiche tatuu za nini? Kuna watu hawana hizo tatuu lakini mambo yao balaa. Mwacheni
Mungu akubariki ulicho kifuata kwa sasa ni sahihi kwa maisha ya binadamu kumjua Mungu
Nimeona tattoo😂
Hata Rahabu Wa Yeriko alikuwa kahaba mnoo lakini Mungu alimkuta hukohuko akamwokoa ,huyu ni mama Mchungaji tu wala hawezi fanana na Rahabu shida yetu ni kumchukua Mungu na ukuu wake na Kumuweka kwenye vichwa vyetu vidogo
Sasa hiyo nguo uliovaa si njema......ungejaribu kuvaa nguo ambayo inaficha hizo tattoo
Yesu alikuja kwa ajili ya hao wenye tattoo hata akiificha kwenu wanadamu Mu gu anaiona
Kweli tenabkama zinafutika akazifute
Hata akizificha Mungu bado anaziona,na ameamua kumchagua na kumkubali hivyo hivyo na tatoo zake,kwahyo wewe unayejikuta mtakatifu tuliza komwe kakojoe ulale.
Mungu hana shida na hiyo michoro.matendo ndio Anachokiangalia