ALICHOKIFANYA DKT MPANGO KIGOMA MSAFARA NA ULINZI ANGANI NA ARDHINI NI "kwa makusudi UKAGUZI HUU..
HTML-код
- Опубликовано: 21 мар 2023
- #habari Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.
Philip Mpango amesema kukamilika kwa ujenzi barabara ya Kabingo- Kasulu-
Manyovu kutafungua mkoa wa Kigoma kiuchumi na biashara baina ya mkoa
huo na mikoa mingine pamoja na nchi jirani.
Makamu wa Rais amesema hayo akiwa eneo la Busunzu wilayani Kibondo
mkoani Kigoma leo tarehe 22 Machi 2023 wakati akizungumza na kamati ya
kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma inayokagua maendeleo ya
ujenzi wa miradi mbalimbali mkoani humo.
Amesema barabara hiyo ni mkombozi wa mkoa wa Kigoma kutokana na
wananchi wa mkoa huo kufanya biashara kwa wingi na mikoa ya Shinyanga
na Mwanza pamoja na nchi ya Burundi hivyo kukamilika kwake kutachochea
maendeleo ya mkoa huo na nchi kwa ujumla. Aidha Makamu wa Rais
amesema lengo la serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni
kuona mkoa wa Kigoma unapata maendeleo kwa haraka kadiri
inavyowezekana.
Makamu wa Rais ameagiza Wakala wa Barabara Nchini (TANROAD)
kumsimamia mkandarasi kikamilifu ili kuhakikisha barabara hiyo ya kilometa
260.6 inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyostahili. Aidha ametoa rai
kwa serikali ya mkoa wa Kigoma kusimamia vema miradi ya maendeleo
inayotekelezwa katika mkoa huo.
Makamu wa Rais amesema serikali itaendelea kusikiliza ushauri wa kamati za
bunge na kutoa wito kwa kamati hizo kuendelea kuangazia maeneo ambayo
serikali inapaswa kufanyia marekebisho.
LINDA SANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO, MUNGU AKULINDE.