MATHAYO 6: YESU AWAFUNDISHA WANAFUNZI WAKE KUSALI

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 10 сен 2024
  • #Sala#Kuomba#Ibada#Yesu#Wanafunziwake#Biblia
    Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao. 6Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
    7“Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi. 8Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba. 9Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali:
    ‘Baba yetu uliye mbinguni:
    Jina lako litukuzwe.
    10Ufalme wako ufike.
    Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
    11Utupe leo chakula chetu cha kila siku.
    12Utusamehe makosa yetu,
    kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
    13Usitutie katika majaribu,
    lakini utuokoe na yule Mwovu.’ [
    Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]
    14“Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nyinyi pia. 15Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe nyinyi makosa yenu.

Комментарии • 19