HOSPITALI BINAFSI ZAVUTIWA NA HUDUMA ZA MADAKTARI BINGWA WA HOSPITALI YA RUFAA KANDA MBEYA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 23 май 2024
  • Ni Madaktari Bingwa wa Samia
    #Kwenda Kujifunza hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya
    Hospitali ya Rufaa Kanda Mbeya, imeendelea kushiriki katika kukuza na kuimarisha ubora wa huduma za afya nchini na kitovu cha huduma za afya katika Nyanda za Juu Kusini kuwa na madaktari bingwa na bobezi, vifaa tiba vya kisasa katika kuwahudumia wananchi.
    Timu ya Viongozi na Wataalamu kutoka Kituo cha afya cha Mt. Theresia Wenda Iringa vijijini ikiongozwa na Mganga Mfawidhi na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani Sr. Dkt. Sabina Mangi, wamefanya ziara ya siku moja katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa lengo la kujionea na kujifunza mambo mbalimbali ya utoaji huduma na pia kuanzisha ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya kwaajili ya kuwajengea uwezo watumishi wa kituo hicho cha afya.
    Sista Mangi ameeleza kuwa msukumo huwo wa kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya umetokanana na Madakati bingwa na bobezi kutoka hospitali ya kanda Mbeya waliokua wakitoa huduma mkoba ya Madaktari wa Samia katika kituo hicho kuonekana ni watumishi ambao namna wanavyofanya kazi zao kwa furaha, ukamilifu na kwa taaluma hivyo, wakaona ni vyema kuja kujifunza kutoka na ufanisi huo mkubwa walioonyesha
    “Tumefika hapa tumeona kweli ni hospitali ambayo watumishi wake wanaonekana ni wanafuraha, wanaonekana wananmwamko, wanaonyesha ownership ya hospitali,na Mkurugenzi ametupokea vizuri akatueleza siri za mafanikio hayo na jinsi wanavyofanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na watumishi. ” - Sr. Mangi
    Amesema kupitia ziara hiyo kuwa wamejifunza mambo mnegi ikiwemo kufanya kazi kama timu na ushirikiano, maswala ya ubora kwa utekelezaji wa 5s KAIZEN na ushirikiano mkubwa kati ya Uongozi na watumishi kwa kuishi kama familia na kwa pamoja.
    Sr. Mangi ameeleza kuwa na dhamira ya kushirikia na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya katika kuwa na huduma mkoba pia kuanzisha programu ya kubadilishana wataalamu kwenda kituo cha afya cha Mt. Theresia na wengine kuja MZRH kwa lengo la kujengewa uwezo na kujifunza
    “Tunataka kufanye kazi na ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya kwa kuwa na huduma mkoba kila baada ya miezi 3, pili kwapata watumishi watakaokuja kufanya kazi pamoja na sisi kwaajili ya kuwajengea uwezo watumishi wa kituo chetu, tatu kuwaleta watumishi wetu hospitali ya rufaa ya kanda Mbeya kwaajili ya kujifunza na kujengewa uwezo ili wakirudi waje watujengee uwezo wale hatukupata nafasi ya kuja huku”. - Sr. Mangi
    Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji, ameupongeza Uongozi wa kituo cha afya cha Mt. Theresia kwa kuichagua Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kamakituo cha mafunzo kwao na kuamua kushirikiana katika nyanja mbalimbali za kutolea huduma za afya kwa wananchi na kuwasihi kufanya kazi kwa furaha na amani ili jamii inapowakuja kupata huduma wanapokea uponyaji haraka hata kabla ya matibabu.
    Nae Jofrey Ngumba Muuguzi Mfawidhi wa kituo cha Afya cha Mt. Theresia ameushukru Uongozi wa hospitali ya rufaa ya kanda Mbeya kwa mapokezi mazuri na kupongeza ushirikia ambao wamejifunza kutokana na ziara yao kuwa ya mafanikio.

Комментарии •