Ndege ya kwanza kutengenezwa Tanzania yaanza safari zake
HTML-код
- Опубликовано: 29 сен 2024
- Ndege ya kwanza kutengenezwa Tanzania, aina ya Skyleader 600, sasa ipo tayari kufanya safari zake mbalimbali nchini na nje ya nchi. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa AAL, David Grolig, wakati wa safari yake ya kwanza ambayo imefanyika mapema leoJumapili September 29, 2024, ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kuondoka mkoani Morogoro.
Grolig amesema ndege hiyo ina ubora wa juu, hivyo imepewa kibali cha kuanza safari zake nchini.
"Tulifanya utafiti wa kina ili kuelewa mahitaji ya wasafiri wa kibiashara, ambao mara nyingi hufanya safari za umbali mrefu. Kutokana na utafiti huo, tumeamua kutengeneza ndege hii ili kuwasaidia wafanyabiashara kusafiri kwa urahisi zaidi na kuhudhuria mikutano mbalimbali," amesema Grolig.
AAL ni kampuni ya kwanza nchini Tanzania kutengeneza ndege za aina hii, ambazo zina matumizi ya kibiashara na binafsi. Mwaka ujao 2025, kampuni hiyo inatarajia kuzindua Skyleader 500, ndege ya gharama nafuu itakayotumika katika shughuli za kilimo na nyingine zinazohusiana na maendeleo ya vijijini.
Grolig aliongeza kuwa kampuni hiyo inafanya kazi na timu ya wafanyakazi wa Kitanzania na Kicheki (Jmhuri ya Czech), na pia imewapatia fursa za ajira vijana wa Kitanzania. Baadhi ya wafanyakazi hao wamechaguliwa kufanya mafunzo kwa vitendo katika Jamhuri ya Czech, kuongeza ujuzi wao katika tasnia ya ndege.
Hii ni hatua muhimu katika maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini Tanzania, ikionyesha uwezo wa ndani katika kutengeneza vifaa vya kisasa vya usafiri.
Video na KHATIBU MGEJA.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highlights #cafconfiderationcup #riversunited #mashabiki #yangaleo #yanga #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko #entertainment #music #news #magoliyasimba #magoliyayanga #magoliyote #magoliyamayele #mayele #aziziki #manara #manaraleo #ikulumawasiliano #magufuli #kikwete #mayele #singidabigstars #magoliyamayele #magoliyasimba #magoliyayanga #highlights #azamsportsfederationcup #chama #Shot #mamelodisundowns #alahlytv #alahlysc #miraj
Mmmmh kwakuw imetengezwa bongo czan km watu watakuwa na Iman juu ya USALAMA wake, coz tunajuana sisi kwa sisi juu ya ufanisi wetu juu kwenye baaz ya mambo😂😂😂😂
Hamna haja ya kujinyonga tena chakufanya unapanda ndege iliyoandikwa made in Tanzania,utakufa mapema sanaaa
😂😂😂
Nilijua tuu ni wazungu..wabongo hata baiskeli hatutegenezi ndo tutengeneze pipa😂
Haaa haaaa 😂😂😂 asee nimechaka sana
Kuunda lazima kuwe na kipindi cha utafiti (scientific research ) ktk kuunda (manufacturing)vifaa vyake muhimu kwa asilimia kubwa mpk kukamilisha uundaji. ...kama ni hivi basi Tanzania imefanikiwa kuunda treni ya kisasa ya SGR😅 na uundaji wa speedboat ktk ziwa victoria. Watu wa media munatumiwa vibaya na wenye hela kupotosha taarifa! Wapo vijana wazalendo ambao muda huu wanavunja vichwa ktk utafiti ili waunde zana muhimu..watafuteni muwape publicity support!
Hapa inaonekana umuhimu wa Msamiati wa kiswahili...ndege ya mwanzo kutengenezwa au kuwa assembled?
Sasa inabeba watu wawili 2 tu...kanafaa kuchezea movie
😅😅😅😅kweli hii ni ya watanzania
Ka ndege ketu hoyeeee🙋🏿♂️🙋🏿♂️
Kutengenezwa au kuunganishwa😂😂 huu uandishi wa kifisiem kabisa😂😂
Acha ujinga
Imetengenezwa hapa na muwekezaji ni campuni ya nchini Czech republic, karakana ipo morogoro, ok mweusi hajafanya sawa ila imeundiwa Tanzania from the scratch. Na ni lini tutasifu vitu vinavyotokea hapa kwetu? Toyota zinazotengenezwa SA ni made from SA na kama Japan watasema but ni same brand campuni Moja nchi tofauti. Mpaka hii mindset ya kimaskini itoke kwenye vichwa vya watz wengi dunia itakua ishaisha. Ndoo maana Kenya ealisema Kilimanjaro ni wakwao na dunia ikaamini kwasababu mmiliki kalaza akili bongo lala kabisa
😂😂😂wacheni ujinga huu mnatufanya wapumbaaaavu
Hio ndege inaweza kukutelekeza kwa P dd😂
Mi nilifikiri ni wabongo wametengeneza kumbe wazungu 😅duhh au mimi ndo sijaelewa
Wametengezeza au wameunga unga
Ni wazungu kumbe aseee
Hongera kampuni, hongera awamu ya 6 Kwa kuwezesha wenye viwanda
Hivi hawa watangazaji mnawaokotaga wapi....eti Jamhuri Sizek hahahaha
Wakati naangalia Kuna ndege imekatiza apo inavyo tembea kama center bolt imekatiza imechooka 😂
Mbona haijafanana kua ndege, me ndege io siwezi kupanda 😂
😂😂😂😂😂😂😂😂kwa nin hutaki kupanda
Hata mimi😂😂😂😂
waluguru mashemeji zangu mshindwe wenyewee
Nilijua wametengeneza wabongo kumbe ni wazungu aishangazi sana
sh 18000 au
Da hongereni hadi ndege made in Tanzania zipo kweli Tanzania inaendelea
Wauze ata million mbili mbili tupate wote.
Tumeunda ndege sio kutengeneza ndege rekebisha usemi
Wtz Hawaii kusema mtengenezaji kapewa mtaji na Didi
Wtz Hawaii kusema mtengenezaji kapewa mtaji na Didi
Sasa mbona wazungu ndio wametengeneza
Hiyo ndege labda Jina lake mi Airbantu
Mbona hatuwasifu babu zetu wanao tengeneza flying saucer(nyungo) ni sound proof, pollution free kwenda canada na kurudi ndani ya saa moja. African technology.
Tatzo inasemekana fuel ni human blood.
Ndio pia na kutengeneza mapiramidi kutoa umeme na mengineo
Tena hauhitaji passport.
Maajabu hiyo itakua ni ndegeee au Ungo
That is good I appreciate thanks Tanzania
ONGERA SANA TANZANIA , TUNASONGA KIMYA KIMYA,
Ni Manufacturing au Assembling??
Uandishi unamashaka
Duu inatikisikass
Iyo ndege ama mkonga wa p didy
Ashakum sio matusi😂😂
Mgunduzi nani katumia nin
Dua zenu jamaniiii😂😂😂
Bei gani kama hiyo!
Kwl time improve ahead. Bravel
Kutengeza ama kuunganisha ,kila kitu inatoka inje wanakuja kuunganisha bana acheni ushamba
Kitu hujui hata airbus hawatengenezi kila kitu wao engine ni rolls Royce vioo makochi friji za ndani wananunua kwa watengenezaji na kufanya assembly hata toyota hawatengenezi kila kitu wenyewe
@@charlesolomi9514ni kweli ndege mpka kukamilika kuna mikono ya watu wengi humo ndani kila mmoja anakua na majukumu yake
Apa apa tz safi,
Kwl tume improve too. Great
Tuwape moyo
Safi sana 🎉❤
safi sana
Watanzania mbona auminjamini 😢😢😢😢😢
Sisi kazi yetu ni mambo ya UNGO
Ndege au nyuki
😂😂😂😅😅😂
Vipi; NYUKI?? NOGO SANA?
😂
Hiyo ni dege au drone?
😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅
Yani bodaboda ya anga
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
😢😢🎉🎉🎉
😂😂😂😂😂
😂😂
🎉🎉