Ndege ya kwanza kutengenezwa Tanzania yaanza safari zake

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 29 сен 2024
  • Ndege ya kwanza kutengenezwa Tanzania, aina ya Skyleader 600, sasa ipo tayari kufanya safari zake mbalimbali nchini na nje ya nchi. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa AAL, David Grolig, wakati wa safari yake ya kwanza ambayo imefanyika mapema leoJumapili September 29, 2024, ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kuondoka mkoani Morogoro.
    Grolig amesema ndege hiyo ina ubora wa juu, hivyo imepewa kibali cha kuanza safari zake nchini.
    "Tulifanya utafiti wa kina ili kuelewa mahitaji ya wasafiri wa kibiashara, ambao mara nyingi hufanya safari za umbali mrefu. Kutokana na utafiti huo, tumeamua kutengeneza ndege hii ili kuwasaidia wafanyabiashara kusafiri kwa urahisi zaidi na kuhudhuria mikutano mbalimbali," amesema Grolig.
    AAL ni kampuni ya kwanza nchini Tanzania kutengeneza ndege za aina hii, ambazo zina matumizi ya kibiashara na binafsi. Mwaka ujao 2025, kampuni hiyo inatarajia kuzindua Skyleader 500, ndege ya gharama nafuu itakayotumika katika shughuli za kilimo na nyingine zinazohusiana na maendeleo ya vijijini.
    Grolig aliongeza kuwa kampuni hiyo inafanya kazi na timu ya wafanyakazi wa Kitanzania na Kicheki (Jmhuri ya Czech), na pia imewapatia fursa za ajira vijana wa Kitanzania. Baadhi ya wafanyakazi hao wamechaguliwa kufanya mafunzo kwa vitendo katika Jamhuri ya Czech, kuongeza ujuzi wao katika tasnia ya ndege.
    Hii ni hatua muhimu katika maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini Tanzania, ikionyesha uwezo wa ndani katika kutengeneza vifaa vya kisasa vya usafiri.
    Video na KHATIBU MGEJA.
    #samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highlights #cafconfiderationcup #riversunited #mashabiki #yangaleo #yanga #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko #entertainment #music #news #magoliyasimba #magoliyayanga #magoliyote #magoliyamayele #mayele #aziziki #manara #manaraleo #ikulumawasiliano #magufuli #kikwete #mayele #singidabigstars #magoliyamayele #magoliyasimba #magoliyayanga #highlights #azamsportsfederationcup #chama #Shot #mamelodisundowns #alahlytv #alahlysc #miraj

Комментарии • 73

  • @JustinMwakalukila
    @JustinMwakalukila 8 часов назад +2

    Mmmmh kwakuw imetengezwa bongo czan km watu watakuwa na Iman juu ya USALAMA wake, coz tunajuana sisi kwa sisi juu ya ufanisi wetu juu kwenye baaz ya mambo😂😂😂😂

  • @ceciliaathanas3135
    @ceciliaathanas3135 43 минуты назад +2

    Hamna haja ya kujinyonga tena chakufanya unapanda ndege iliyoandikwa made in Tanzania,utakufa mapema sanaaa

  • @mrdaslam301
    @mrdaslam301 10 часов назад +2

    Nilijua tuu ni wazungu..wabongo hata baiskeli hatutegenezi ndo tutengeneze pipa😂

    • @robertphilip385
      @robertphilip385 10 часов назад +1

      Haaa haaaa 😂😂😂 asee nimechaka sana

  • @bajomba2010
    @bajomba2010 7 часов назад +1

    Kuunda lazima kuwe na kipindi cha utafiti (scientific research ) ktk kuunda (manufacturing)vifaa vyake muhimu kwa asilimia kubwa mpk kukamilisha uundaji. ...kama ni hivi basi Tanzania imefanikiwa kuunda treni ya kisasa ya SGR😅 na uundaji wa speedboat ktk ziwa victoria. Watu wa media munatumiwa vibaya na wenye hela kupotosha taarifa! Wapo vijana wazalendo ambao muda huu wanavunja vichwa ktk utafiti ili waunde zana muhimu..watafuteni muwape publicity support!

  • @bajomba2010
    @bajomba2010 8 часов назад +1

    Hapa inaonekana umuhimu wa Msamiati wa kiswahili...ndege ya mwanzo kutengenezwa au kuwa assembled?

  • @archbordygodfrey2614
    @archbordygodfrey2614 4 часа назад +1

    Sasa inabeba watu wawili 2 tu...kanafaa kuchezea movie

  • @Revelation1412.
    @Revelation1412. 13 часов назад +1

    😅😅😅😅kweli hii ni ya watanzania
    Ka ndege ketu hoyeeee🙋🏿‍♂️🙋🏿‍♂️

  • @barakajohn8005
    @barakajohn8005 14 часов назад +2

    Kutengenezwa au kuunganishwa😂😂 huu uandishi wa kifisiem kabisa😂😂

    • @majaliwabwitonde6900
      @majaliwabwitonde6900 12 часов назад +1

      Acha ujinga

    • @jamesjerome9476
      @jamesjerome9476 9 часов назад

      Imetengenezwa hapa na muwekezaji ni campuni ya nchini Czech republic, karakana ipo morogoro, ok mweusi hajafanya sawa ila imeundiwa Tanzania from the scratch. Na ni lini tutasifu vitu vinavyotokea hapa kwetu? Toyota zinazotengenezwa SA ni made from SA na kama Japan watasema but ni same brand campuni Moja nchi tofauti. Mpaka hii mindset ya kimaskini itoke kwenye vichwa vya watz wengi dunia itakua ishaisha. Ndoo maana Kenya ealisema Kilimanjaro ni wakwao na dunia ikaamini kwasababu mmiliki kalaza akili bongo lala kabisa

  • @AdrusHassan-c5m
    @AdrusHassan-c5m 8 часов назад +1

    😂😂😂wacheni ujinga huu mnatufanya wapumbaaaavu

  • @blues4life633
    @blues4life633 12 часов назад +1

    Hio ndege inaweza kukutelekeza kwa P dd😂

  • @allymanyika3502
    @allymanyika3502 Час назад

    Mi nilifikiri ni wabongo wametengeneza kumbe wazungu 😅duhh au mimi ndo sijaelewa

  • @montegokellix1227
    @montegokellix1227 11 часов назад +1

    Wametengezeza au wameunga unga

  • @octavianmgode3868
    @octavianmgode3868 12 часов назад +1

    Ni wazungu kumbe aseee

  • @kalingaasukile8730
    @kalingaasukile8730 3 часа назад

    Hongera kampuni, hongera awamu ya 6 Kwa kuwezesha wenye viwanda

  • @hoseastephen4508
    @hoseastephen4508 2 часа назад

    Hivi hawa watangazaji mnawaokotaga wapi....eti Jamhuri Sizek hahahaha

  • @saidimussa8200
    @saidimussa8200 14 часов назад

    Wakati naangalia Kuna ndege imekatiza apo inavyo tembea kama center bolt imekatiza imechooka 😂

  • @NoufelSalim
    @NoufelSalim 14 часов назад +1

    Mbona haijafanana kua ndege, me ndege io siwezi kupanda 😂

  • @ISACKKILEO-e7z
    @ISACKKILEO-e7z Час назад

    waluguru mashemeji zangu mshindwe wenyewee

  • @onesmomwakasege5215
    @onesmomwakasege5215 12 часов назад

    Nilijua wametengeneza wabongo kumbe ni wazungu aishangazi sana

  • @mussamaganga2764
    @mussamaganga2764 12 часов назад +1

    sh 18000 au

  • @rahimzuberi2673
    @rahimzuberi2673 10 часов назад

    Da hongereni hadi ndege made in Tanzania zipo kweli Tanzania inaendelea

  • @hallin9561
    @hallin9561 2 часа назад

    Wauze ata million mbili mbili tupate wote.

  • @venancerutta6875
    @venancerutta6875 14 часов назад

    Tumeunda ndege sio kutengeneza ndege rekebisha usemi

  • @aboudasilver6541
    @aboudasilver6541 13 часов назад

    Wtz Hawaii kusema mtengenezaji kapewa mtaji na Didi

  • @aboudasilver6541
    @aboudasilver6541 13 часов назад

    Wtz Hawaii kusema mtengenezaji kapewa mtaji na Didi

  • @hamidamussa-sy4fm
    @hamidamussa-sy4fm 4 часа назад

    Sasa mbona wazungu ndio wametengeneza

  • @furgencejustinian7283
    @furgencejustinian7283 14 часов назад

    Hiyo ndege labda Jina lake mi Airbantu

  • @DavidSemu-gu6wp
    @DavidSemu-gu6wp 12 часов назад +4

    Mbona hatuwasifu babu zetu wanao tengeneza flying saucer(nyungo) ni sound proof, pollution free kwenda canada na kurudi ndani ya saa moja. African technology.

    • @visionstudios6804
      @visionstudios6804 2 часа назад +1

      Tatzo inasemekana fuel ni human blood.

    • @kingjoshuamhuamk2559
      @kingjoshuamhuamk2559 49 минут назад

      Ndio pia na kutengeneza mapiramidi kutoa umeme na mengineo

    • @zully756
      @zully756 45 минут назад

      Tena hauhitaji passport.

  • @robertphilip385
    @robertphilip385 10 часов назад

    Maajabu hiyo itakua ni ndegeee au Ungo

  • @tediusmakwara3931
    @tediusmakwara3931 Час назад

    That is good I appreciate thanks Tanzania

  • @ikulunimahalipatakatifu7642
    @ikulunimahalipatakatifu7642 14 часов назад

    ONGERA SANA TANZANIA , TUNASONGA KIMYA KIMYA,

  • @furgencejustinian7283
    @furgencejustinian7283 14 часов назад

    Ni Manufacturing au Assembling??

  • @dicksonulotu7427
    @dicksonulotu7427 2 часа назад

    Uandishi unamashaka

  • @deodathrobertquacker3879
    @deodathrobertquacker3879 54 минуты назад

    Duu inatikisikass

  • @maxmakombe6750
    @maxmakombe6750 13 часов назад

    Iyo ndege ama mkonga wa p didy

  • @tops-brand
    @tops-brand 12 часов назад

    Ashakum sio matusi😂😂

  • @IvanSaid-ef8tb
    @IvanSaid-ef8tb 13 часов назад

    Mgunduzi nani katumia nin

  • @halfankallah7173
    @halfankallah7173 14 часов назад

    Dua zenu jamaniiii😂😂😂

  • @omarymbaraj8072
    @omarymbaraj8072 12 часов назад

    Bei gani kama hiyo!

  • @ReubenRaymond-zh4yw
    @ReubenRaymond-zh4yw 12 часов назад

    Kwl time improve ahead. Bravel

  • @LuckymusyokiMueni
    @LuckymusyokiMueni 13 часов назад

    Kutengeza ama kuunganisha ,kila kitu inatoka inje wanakuja kuunganisha bana acheni ushamba

    • @charlesolomi9514
      @charlesolomi9514 13 часов назад +1

      Kitu hujui hata airbus hawatengenezi kila kitu wao engine ni rolls Royce vioo makochi friji za ndani wananunua kwa watengenezaji na kufanya assembly hata toyota hawatengenezi kila kitu wenyewe

    • @MursalLusinde
      @MursalLusinde 12 часов назад

      ​@@charlesolomi9514ni kweli ndege mpka kukamilika kuna mikono ya watu wengi humo ndani kila mmoja anakua na majukumu yake

  • @LucasMayunga
    @LucasMayunga 14 часов назад

    Apa apa tz safi,

  • @ReubenRaymond-zh4yw
    @ReubenRaymond-zh4yw 12 часов назад

    Kwl tume improve too. Great

  • @AbuuRamadhani-o7k
    @AbuuRamadhani-o7k 14 часов назад

    Tuwape moyo

  • @eaglecrown1101
    @eaglecrown1101 14 часов назад

    Safi sana 🎉❤

  • @tanzanaire
    @tanzanaire 13 часов назад

    safi sana

  • @HeboniBabu
    @HeboniBabu 12 часов назад

    Watanzania mbona auminjamini 😢😢😢😢😢

  • @MedardNtara
    @MedardNtara 13 часов назад +1

    Ndege au nyuki

  • @Godfreyolekidongo
    @Godfreyolekidongo 2 часа назад

    Hiyo ni dege au drone?

  • @tanzanaire
    @tanzanaire 13 часов назад

    Yani bodaboda ya anga

    • @Revelation1412.
      @Revelation1412. 13 часов назад

      😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

  • @SadikiKisubi
    @SadikiKisubi 3 часа назад

    😢😢🎉🎉🎉

  • @fadhilimhagama2650
    @fadhilimhagama2650 12 часов назад

    😂😂😂😂😂

  • @aboudasilver6541
    @aboudasilver6541 13 часов назад

    😂😂

  • @LEDINASHEMZIGWA-r9t
    @LEDINASHEMZIGWA-r9t 14 часов назад

    🎉🎉