Tamko la JWTZ Juu ya Wanajeshi 14 Waliouawa Congo DR

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 9 фев 2025
  • Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania limesema kikundi chake cha ulinzi na usalama kilichopo DRC kwaajili ya kutekeleza jukumu la ulinzi na amani kilivamiwa na Waasi waliojilikana kuwa ni ADF na kusababisha mauaji kwa wanajeshi 14.
    Amesema kwamba tukio hilo lilitokea katika eneo la kambi iliyopo daraja kwenye mto Simulike barabara ya kutokea Oicha kwenda Kamango mpakani mwa nchi ya Uganda Kaskazini Mashariki ya wilaya ya Beni Jimbo la Kivu Kaskazini.
    Akithibitisha mauaji hayo muwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania (CDF) Luteni Jenerali James Mwakibolwa amesema shambulio hilo lakuvamiwa lilizusha mapigano baina ya kikundi hicho na kile cha waasi na yalidumu kwa takribani masaa kumi na tatu (13) na kusababisha vifo vya askari wa Tanzania 14 na wengine 44 kujeruhiwa na askari wawili bado hawajulikani walipo ambapo jitihada zaidi za kuwatafuta zinaendelea.
    Amesema shambulizi la tarehe 7 kuamkia tarehe 8 Desemba lilikua baya zaidi kuwahi kuitokea tangu vikosi hivyo vianze kushiriki ulinzi wa amani nchini DRC mwaka 2011 kwakua limeleta madhara makubwa, hata hivyo kikundi hicho ambacho bado kipo huko kinauwezo mkubwa wa kutekeleza majukumu husika kwa uhodari wa hali ya juu ,ushupavu, weledi mkubwa na umahiri stahiki.
    Kwa niaba ya mkuu wa majeshi Luteni Jenerali Mwakibolwa amewathibitishia watanzania kuwa tukio hilo halitawavunja moyo na kamwe Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania halitatetereka kupeperusha bendera yake ndani na nje ya nchi kwani tukio hilo limewaongezea nguvu, ari ,ushupavu na uhodari zaidi katika kutekeleza majukumu yake.
    Aidha amesema nchi pia iko salama na itaendelea kuwa salama na yeyote ambaye anataka kuwajaribu atashughulikiwa ipasavyo kwani historia ya jeshi inadhihirisha uwezo thabiti.
    Kuhusu taratibu za kusafirisha miili ya marehemu kuirejesha nchini zinafanyika chini ya utaratibu wa Serikali na umoja wa mataifa na JWTZ na serikali wanaendelea kuchukua hatua stahiki kufuatia tukio hilo ikiwemo kufanya uchunguzi katika eneo husika sambamba na kuangalia taratibu za kuwajulisha familia za wafiwa zimekamilika na ndio maana hawakuweza kutoa taarifa hizo bila kuwaweka sawa familia za mashujaa hao.
    Kwa umoja wa watanzania amewataka kuwaombea dua roho za mashujaa hao zipumzike mahali pema peponi kwa amani na majeruhi wote wapone haraka iwezekanavyo ili warejee kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa ulinzi wa taifa na dunia nzima.

Комментарии • 122

  • @assimmhamed1851
    @assimmhamed1851 4 года назад +1

    Mwenyezi mungu awalaze pahala pema amiin mashujaa wetu

  • @selincharles3383
    @selincharles3383 7 лет назад +1

    mapigano yalikuwa makali Sana.. Mungu awapokee na roho zao mahali pema Peponi.amina

  • @ussikhamisussi4882
    @ussikhamisussi4882 7 лет назад +1

    Ndio mitihani bhana! Poleni sana.

  • @michaelshayo2747
    @michaelshayo2747 7 лет назад +1

    mungu ibariki tanzania mungi libariki jeshi letu amina

  • @wcbwanatishakiranikirudiab2349
    @wcbwanatishakiranikirudiab2349 7 лет назад +1

    Mashujaa wetu mungu awapokee na mungu awaponyeshe jeshi retu riko imara poreni wakuu

  • @privatestudiotz
    @privatestudiotz 7 лет назад +2

    Mungu alito na Mungu ametwaa Jina la Bwana Libarikiwe Amen.

  • @tambwealmasi7510
    @tambwealmasi7510 7 лет назад +1

    Mungu ibariki Tanzania pamoja na vyombo vya usalama

  • @AbdallahSuede
    @AbdallahSuede 5 дней назад

    😊na marehemu wetu au nmeskia vby

  • @rukiaabdallah92
    @rukiaabdallah92 7 лет назад +4

    Kukosea lazima kuongea maana wanajeshi walioko huko mipakan ndo tunao wategemea 💃Allah azipumzishe roho za marehem 😢👏

  • @gracemanyori7273
    @gracemanyori7273 7 лет назад +1

    Mungu azilaze pema roho za marehemu amina

  • @abdurazakijuma2857
    @abdurazakijuma2857 4 года назад +1

    Awalaze Mahal pema pepon amen

  • @mathalusako4108
    @mathalusako4108 7 лет назад

    Mungu aliye muumba wa vyote na mwamuz wayote kwa namna ya pekee naomba umtume roho wako Mt. Akawafariji wafiwa wote.

  • @saumuhassan1365
    @saumuhassan1365 7 лет назад +2

    Innalilah Wainnalilah rajiun, Allah warehem waliotangulia Ameen👏

  • @brightmpanda211
    @brightmpanda211 7 лет назад +6

    Jamani kwann tupoteze ndugu zetu waludi wote hatutaki kumalizwa namba hii sawa niuchujaa lakini hawafanyii kwawenyewe ni majonzi kwa inchi yetu mungu azilaze roho zamarehemu pema peponi

  • @stephenjonas4866
    @stephenjonas4866 7 месяцев назад

    Mungu azipokee roho za makamanda wetu, Amen.

  • @richardnyamahanga4159
    @richardnyamahanga4159 7 лет назад +1

    Poleni sana Jeshi la Wananchi la Tz, Mungu awapumzishe mahala pema mashujaa wetu, na awaponye majeruhi wote ili wawe na afya njema na warejee katika majukumu yao ya kudumisha amani. Ila Mnadhim mkuu hapo mwisho sijamuelewa, anasema na marehem wetu wapote haraka na weendelee na kazi. Marehem wanaweza kupona kweli?

    • @mctidohondoa1652
      @mctidohondoa1652 7 лет назад

      Richard Nyamahanga na wewe umesema wapote ulimi hauna mfupa

  • @Fatima-v9k6f
    @Fatima-v9k6f 11 дней назад

    From 🇧🇮 inalillah wa inalillah rajiun

  • @fabianikapesa1157
    @fabianikapesa1157 7 лет назад +1

    sawa kaka mwakibolwa nimekuelewa naomba amani itawale kwani mdogo wangu yuko huko

  • @halawsmalimi7287
    @halawsmalimi7287 7 лет назад +1

    single soldier attack under enemy fire ni noma sana poleni wapiganaji we2 mungu awatangulie

  • @petermwanyondo6459
    @petermwanyondo6459 7 лет назад

    duu wanaume kazi poleni xana

  • @eliudedwin3424
    @eliudedwin3424 7 лет назад

    kuzaliwa ni siku moja na kufa ni siku moja poleni sana familia Kwa kupoteza na taifa ila Pongezi Kwa jeshi kuthibitishia Uma kuwa jeshi ndo limeimalika zaidi

  • @ashazaharan1750
    @ashazaharan1750 7 лет назад +1

    daa inasikitisha saaan polen wote mloondekewa na wapendwa wenu mungu ibariki Tz lakin watoen huko jaman

  • @jumamwengwa4309
    @jumamwengwa4309 7 лет назад +2

    R. I. P, ndugu zangu. Mungu nakuomba uwapokee ndugu zangu kwa upendo wako na kwa aman yako ktk ridhaa yako. Inshaallah. TANZANIA NGUVU MOJA.

  • @husseinmuhammad9067
    @husseinmuhammad9067 7 лет назад +3

    Mungu awape subra ndugu na jamaa waloondokewa na wapendwa wao.

  • @NdikumanaSebakunziNorbert
    @NdikumanaSebakunziNorbert Год назад +1

    Jameni laiti Nyerere angali Jua hayo ayatendayo Suluhu? Ange jutia sanaaaaa!

  • @godfreyleka5839
    @godfreyleka5839 7 лет назад +3

    ni Leteni jenerali sio meja jenerali,. fuatilieni vizur alama Za vyeo,. Wana habari

  • @cliffsalija4692
    @cliffsalija4692 Год назад +1

    Mwakibolwa.. tanzania

  • @shukurkatembo2807
    @shukurkatembo2807 4 года назад +1

    Ni Lt. Gen siyo Maj. Gen

  • @mtoshugilbert5540
    @mtoshugilbert5540 7 лет назад +5

    majeruh bhana siyo marehem

  • @HijaSaid-t6c
    @HijaSaid-t6c 7 дней назад

    Marehemu wetu wapone haraka iwezekanavyo, Hii imenda

  • @mariamlameckelifuraha5114
    @mariamlameckelifuraha5114 7 лет назад

    Mungu fariji familia zao

  • @RubayitaRukaka
    @RubayitaRukaka Год назад +1

    Hhhh mtalia sana kwa hivi wamekufa mamia wameuliwa na m23

  • @mponjolimwakasege782
    @mponjolimwakasege782 7 лет назад +1

    Poleni Sana wapi ganajiwetu

  • @MWilly-xu1ki
    @MWilly-xu1ki 7 лет назад +1

    Aksanteni Tanzania kwa kujitolea kutulinda sisi wakongo tuna waheshimu

  • @veronicamagesa1752
    @veronicamagesa1752 9 месяцев назад

    Jaman mbona nguvu kazi zetu wanajeshi wetu wanateketea uko congo? Nchi yenyew haitak aman leo wanaili kesho lile kama mashekwani tu 😭😭inauma sn iseee 😭😭😭😭😭😭

  • @PascalChimatu
    @PascalChimatu 9 дней назад

    Acheni kutupigia kelele kwann msiwapige mpaka alie watuma kila siku wanajeshi wauwawa kila siku mpo tu tunataka wapigwe walio shiliki

  • @dimokcee8403
    @dimokcee8403 7 лет назад +3

    Huyo Ni luteni generali sio meja jenerali

  • @khamisjuma7616
    @khamisjuma7616 7 лет назад +1

    Jamani kamanda hakutuambia hayo mapigano wamekufa waasi wangapi ?

  • @stn4873
    @stn4873 Год назад +1

    Saa 13 chuma zinalia tu daah sio poa

  • @salehsaleh1305
    @salehsaleh1305 7 лет назад +1

    Kwanin waasi hawaoneshwi wanapokufa wao

  • @davidnicholas8772
    @davidnicholas8772 7 лет назад +1

    jamani kaka zetu na dada zetu warudi nyumbani poleni familia za wanajeshi hawa

  • @jumamakuri9176
    @jumamakuri9176 7 лет назад

    Askari wetu hawajazoea kukabiliana na waasi ila wamezoea kupambana na wananchi wanaoandamana tena wasio na silaha. Ni vema kuwaandaa askari vijana wetu kabla ya kuingia katika uwanja wa mapambano, vinginevyo watkwisha wote . Tutaambulia makaburi.
    Ndiyo maana askari waliouawa ni Watanzania japo kulikuwa na askari toka nchi mbalimbali.
    God bless Tanzania. Amen.

    • @robsonalen2649
      @robsonalen2649 2 года назад

      Usiongee ujinga uwo kijna una unacho kijuwa kakimya

  • @athanaskameja6128
    @athanaskameja6128 7 лет назад +1

    waje home haraka

  • @monamackey569
    @monamackey569 7 лет назад +1

    et naomba kuuliza. iv uko congo wanaofanya matukio ni wanajesh pia. maana nshawah kuona kuna kipind iv wanajesh wanauwa watu then wanawatupa kwenye uwo mto wa mamba

  • @iviejustified8109
    @iviejustified8109 7 лет назад +1

    Rest Easy Fallen Heroes!

  • @geofreymaghali183
    @geofreymaghali183 7 лет назад

    Poleni jeshi la wananchi wa Tanzania, Amiri jeshi mkuu na Watanzania Kwa ujumla. Lakini tuna maswali: hao waasi wanafadhiriwa nani? Nini malengo yao? Kijografia wanatokea wapi ktk DR Congo? Shughuli zao kiuchumi ni zipi? Wanapata wapi silaha na chakula? Mungu tusaidie kuifanya Africa kuwa sehemu salama ya kuishi na kupiga hatua kimaendeleo

  • @alhamdulillah5796
    @alhamdulillah5796 7 лет назад +5

    Plse serikali watunzieni wazee na wake zao waliowaacha uhai wao wote na muwasomeshee watoto wao pia. Isie km baada ya kupewa kiunua mgongo baadae bac.

  • @MwitaSenso
    @MwitaSenso 4 месяца назад

    Nmesikia roho za marehem zipone haraka

  • @benimagaya7966
    @benimagaya7966 7 лет назад

    Pole Sana 😭😭R.I.P

  • @idrissasaidy-bs1cw
    @idrissasaidy-bs1cw 10 месяцев назад

    tutafika tu kwenye lengo

  • @radhiasalum833
    @radhiasalum833 7 лет назад +1

    inauma jamani bora waliobaki warudi

  • @billebaraka6534
    @billebaraka6534 7 лет назад +1

    Ni luteni general siyo meja muwe making mnapoandika

  • @jworld1480
    @jworld1480 8 дней назад

    sasa hapo mkuu marehe,u wanaponaje tena

  • @HabibuUrasa
    @HabibuUrasa 4 месяца назад

    Idf siyo mchezo rudisheni wanajeshi wataishia huko waasi wa congo🇨🇩 wameshindikana umoja wa mataifa wameshindwa. lengo la kupeleka jeshi ni nn au ni kutafuta sifa UN

  • @asiakheir3846
    @asiakheir3846 7 лет назад +4

    Bado mna waachatuu huko.mungu ibarikiTanzania.

    • @حسامالراشدي-د9ن
      @حسامالراشدي-د9ن 7 лет назад

      Hapana Amani gani unaenda kulinda inchi ya jirani wenyewe awana Amani kwenye Inchi yao warudisheni Ndgu zetu hari yanini Ndgu zetu kila cku wanahuliwa inje ya inch i inauma sana hata kama warudi walide Amani hapa nyumbani

  • @kassimramadhani5378
    @kassimramadhani5378 7 лет назад

    Kiukweli inasikitisha sana aisee daaah bora ndugu yangu hakurudishwa tena huko, sasa na huyo mkuu anasema marehem wapone duuh ni kuchanganyikiwa ama kama yeye kapagawa hivi sasa walioko kule wako katika hali gani

  • @masandaretv898
    @masandaretv898 7 лет назад +1

    Aisee inauma

  • @veronicamagesa1752
    @veronicamagesa1752 9 месяцев назад

    😭😭😭😭😭

  • @ramadhaniathumanimlenge6641
    @ramadhaniathumanimlenge6641 7 лет назад +7

    Daaah Ndiyo maana niligoma kwenda jeshi

  • @NdikumanaSebakunziNorbert
    @NdikumanaSebakunziNorbert Год назад

    Mnatafuta dhahabu , alimasi, Uranium lakini jueni kwamba mtavilipa Kwa damu ya watanzania!!! Je mbona munahivyo vyote kwenu? Simurudie kwenu!

  • @ebenezerurioh9610
    @ebenezerurioh9610 7 лет назад +1

    r.i..p solder

  • @verdianabanabi2205
    @verdianabanabi2205 7 лет назад +3

    Muwafate wote watoke huko si kwao.

  • @shawarbakar7587
    @shawarbakar7587 7 лет назад

    marehem wetu waponee haraka 😂😂😂😂😂😀😀

    • @emmysam7938
      @emmysam7938 Год назад

      Usicheke kachanganyikiwa..inaumiza sana

  • @ezlonlony3588
    @ezlonlony3588 7 лет назад

    Meja kachapia😂😂😂😂

  • @majaliwaking4500
    @majaliwaking4500 4 дня назад

    Huyu si ndio Yule jamaa alisema marehem wapone haraka si ndio Huyu au vipi?

  • @husseinkonz5192
    @husseinkonz5192 Год назад

    Damu ya mtanzania haipotei bure

  • @mahmadougronkjaer8316
    @mahmadougronkjaer8316 7 лет назад

    ETI MAREHEMU WETU WAPONE HARAKA IWEZEKANAVYO ..haupo serious kamanda

  • @mariammwambungu3174
    @mariammwambungu3174 7 лет назад

    RIP 😭😭😭😭😭😭😭😭

  • @elisianajohn5655
    @elisianajohn5655 7 лет назад

    dah

  • @salehsaleh1305
    @salehsaleh1305 7 лет назад

    uchunguzi ufanyike na kujua uwezo wa silaha za waasi na wanajeshi wetu
    ikitokea pana uzembe uwajibikaji uchukue nafasi yake kwa pande yeyote

  • @frenkjoseph3948
    @frenkjoseph3948 7 лет назад

    ndo jeshi hiyo,poleni ndugu zangu

  • @suzyfrednand983
    @suzyfrednand983 7 лет назад +1

    mi naona Tanzania ni nchi yenye aman kwa nn tunajipendekeza kwenye mataifa ambayo wao wenyewe wameshindwa kulinda amani yao

  • @allyahamedy6567
    @allyahamedy6567 7 лет назад

    Meja kavulugwa

  • @sebastiansalamba8236
    @sebastiansalamba8236 7 лет назад +3

    Wapigeni tu hao waasi mnawalea wa nini piga

  • @jumabaruti9845
    @jumabaruti9845 7 лет назад

    mkuu marehemu haponi maana ameshakufa

  • @fatmaalliy3547
    @fatmaalliy3547 7 лет назад +1

    Yeyote atakayetaka kutujaribu atashughulikiwa ipasavyo

  • @joemaabdala622
    @joemaabdala622 7 лет назад

    R.I.P MAKAMANDA WETU

  • @diwanilemomo3117
    @diwanilemomo3117 7 лет назад +1

    rudisheni majeshi yetu wate kila nchi ibebe msalaba wake

    • @deodatuspolla8272
      @deodatuspolla8272 7 лет назад

      rip mungu awabrk família YA marehemu wawe na Subra ktk kipind hik kigumu?

  • @mavoajunior7163
    @mavoajunior7163 7 лет назад

    RIP Makamanda wetu.

  • @melickjohn5141
    @melickjohn5141 7 лет назад

    R I p makomando

  • @hassanisadiki824
    @hassanisadiki824 7 лет назад +4

    Eti Na marehemu wetu wapone Kwa haraka iwezekanavyo khaaa😂😂😂

  • @husseinmuhammad9067
    @husseinmuhammad9067 7 лет назад +3

    Hahahah eti marehemu wetu wapone haraka iwezekanvyooo!!!!!!

    • @joycemashikolo9096
      @joycemashikolo9096 7 лет назад +1

      Hussein Muhammad usimcheke msiba kubwa huo hawezi kuwa sahihi katika kuongea.

    • @ngometvarusha4030
      @ngometvarusha4030 7 лет назад +1

      wewe husen Mungu anakuona kwani wewe hua hukosea ktk kutamka

  • @omarylugusha
    @omarylugusha 7 лет назад

    R.I.P makamanda

  • @samueljohn7560
    @samueljohn7560 7 лет назад

    R I P

  • @hamadibrahim6275
    @hamadibrahim6275 7 лет назад

    askari wa f

  • @simonmlowe2675
    @simonmlowe2675 7 лет назад

    RIP

  • @jumamwengwa4309
    @jumamwengwa4309 7 лет назад

    Mbona mkuu huna ht kielezo ktk mwili wako kwa Taifa lina msiba mzito ?!!!!. Mfano kitamba cheusi au vazi jeusi. Au huko sio smdestuli yenu ?

  • @ibrahimpius893
    @ibrahimpius893 7 лет назад

    R.I.P

  • @amaryahmedkusaka3841
    @amaryahmedkusaka3841 7 лет назад +1

    r.i.p infactia

  • @obedkitandala8150
    @obedkitandala8150 6 лет назад

    siri majini

  • @benimagaya7966
    @benimagaya7966 7 лет назад +1

    Pole Sana 😭😭R.I.P

  • @linahdavid9660
    @linahdavid9660 7 лет назад

    R.I.P

  • @obedkitandala8150
    @obedkitandala8150 6 лет назад

    siri majini