MAOMBI YA KUMFUNGUA MUME WAKO - MWL. ISAAC JAVAN

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 30 сен 2024
  • Haya ni maombi maalum kwa mwanamke aliyeolewa ambaye anapitia mambo yafuatayo:-
    1. Mume wake ana mahusiano nje ya ndoa.
    2. Mume wake ametelekeza familia.
    3. Mume wake ametoka kwenye nafasi yake kama mume na kama baba wa familia.
    Lengo la maombi haya ni kufungua vifungo vya kiroho ambavyo nyuma yake kuna mtu au watu. Mungu anapotaka kufanya jambo kwenye maisha, anatumia mtu. Shetani pia anapotaka kuharibu jambo, anatumia mtu. Kuna mtu au watu ambao shetani anawatumia kuharibu ndoa. Zipo ndoa zilizovunjika kwa sababu ya watu ambao shetani aliwatumia. Zipo familia zilizopoteza muelekeo na maono ya ki-Mungu kwa sababu kuna mtu au watu waliotumiwa na shetani kupitisha uharibifu. Ni maombi yetu ya kwamba maombi haya yafanyike msaada kwako, na Mungu aliye hai, kwa jina la YESU afanye urejesho kwenye ndoa yako.
    Unapofanya maombi haya, simamia mstari huu, "Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe" [MARKO 10:9].
    MUHIMU!
    Usiombe maombi haya kwa mazoea! Omba kwa kumaanisha. Pata eneo lenye utulivu, paza sauti yako mbele za BWANA. Haya ni maombi ya vita, kwa hiyo omba kwa kumaanisha, usikae kimya katikati ya maombi. Hakikisha unapambana kwa ajili ya mume wako. Ukiona machozi yanatoka, usizuie, endelea. Mahali pa kukemea, kemea. Mahali pa kuamuru, amuru. Mungu anaenda kufanya kitu kikubwa kwa utukufu wa jina lake.
    Mungu akubariki. Mshirikishe na mwanamke mwingine ambaye anaweza akanufaika na maombi haya.

Комментарии • 849

  • @IsaacJavan
    @IsaacJavan  2 года назад +57

    TAFADHALI FUATA MAELEKEZO
    BWANA YESU asifiwe. Haya maombi ni maalum kwa mwanamke aliyeolewa. Haya maombi si kwa ajili ya wachumba. Haya si maombi kwa ajili ya watu wanaoishi pamoja lakini hawajafunga ndoa. Haya ni maombi ya wanawake ambao wamefunga ndoa mbele ya madhabahu ya BWANA.
    Lengo la kuweka maombi haya ni kuwasaidia wanawake wanaopitia changamoto kwenye ndoa zao waweze kuomba na kumuona Mungu akiwatendea jambo. Tunashauri, jenga tabia ya kusimama wewe kama wewe kumuombea mume wako. Usijidharau. Amini ukiomba Mungu anasikia.
    Maono ya Channel hii ni kuwasaidia watu wafike mahali ambapo wanaweza wakajiombea wao wenyewe, na ndiyo maana tunaweka muongozo wa namna ya kuomba. Tamani kujua kuomba. Tamani kusimama wewe kama wewe mbele za BWANA kwa ajili ya ndoa yako. Tamani kuwa muombaji, kwa sababu inawezekana. Ng'ang'ana na YESU na atakujibu mwanangu.

    • @magdalenesyombua8085
      @magdalenesyombua8085 2 года назад +1

      Na wale ambao.wameachana na mume akaoa tena.

    • @festodivule6555
      @festodivule6555 2 года назад +6

      Kama unamchumba Ako ila kashikiliwa uko je haupasw kuyaomba

    • @festodivule6555
      @festodivule6555 2 года назад +1

      Kama ni mchumba angu ila Kuna mwanamke kamshikilia kichaw je spaswi kuomba

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      @@magdalenesyombua8085 Unaweza kuomba mwanangu

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      @@festodivule6555 haya maombi ni kwa ajili ya wanandoa mwanangu.

  • @castorkanuti
    @castorkanuti Год назад +19

    Mchungaji Mungu akutumie zaidi nimefanya maombi haya mida ya saa 4 maana mwanaume alikua ameNizimia cm hataki kabisa kuongea na anataka tuachane gafla tu bila Sababu ilikua jpl nikaona Hali inazidi kua mbaya ndo gafla leo RUclips ndo naona maombi hayo nikaomba baada ya maombi sauti ikaniambia kimbia haraka katoe sadaka na sikua na hela nilikua na. Ela. Ya kula tu lakin ilibidi nitimue mbio kwenda kutuma. Saa hizi kapiga sm kwa upole na. Unyenyekevu .Nakushukuru Sana Mungu anaewatumia watu wake

    • @verenasemgen8873
      @verenasemgen8873 Год назад +1

      Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад

      Amen jina la BWANA YESU libarikiwe na kutukuzwa milele. YESU azidi kuwatetea na kulinda ndoa yenu. Amani ya YESU itawale na upendo wa kwanza urudi. Katika jina la YESU

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад

      Amen ubarikiwe sana na BWANA YESU milele yote

    • @taboochendi8474
      @taboochendi8474 11 месяцев назад

      Nasisi ambao tuko kwenye mahusiano natunafuatilia Haya maombi hatutasaidika ju hatujaoana

    • @agnesspaul1866
      @agnesspaul1866 3 месяца назад

      ❤❤ Aminaaa

  • @surmiseatter73
    @surmiseatter73 11 месяцев назад +6

    Leo trh 28/10/2023. Nimesikiliza na kuomba pamoja na wewe Mtumishi..... Kuanzia sasa Nina amini Mumewangu amefunguliwa, sitalia tena. Mumewangu Emma ametoka ktk kifungo..... Asante yesu kwa kumkomboa Mumewangu.... ... Kwa Jina La Yesu ninaenda kuuanza mwezi 11 kwa Amani na vicheko ktk Ndoa yangu...... Kwakuwa Mungu Umekwisha Ijenga upya Ndoa yangu. Nami nakuhaidi SITOKUACHA SIKUZOTE ZA MAISHA YANGU... NITAKUSHUKURU NA KUSHUHUDIA UKUU WAKO KUPITIA NDOA YANGU.........nami pia ninawaombea wanawake wenzengu wote wakafunguliwe leo kwa jina la YESU KRISTO AMEEEEN

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen mwanangu YESU akupe amani na akutetee na kukulinda daima. Damu ya YESU inene maneno mazuri kwa ajili yako. Amen

  • @freretoms5119
    @freretoms5119 7 месяцев назад +8

    Aya ma ombi niya wana wake pekeyake Ila mimi natumiya nafasi iyi kwa ajili ya muke wangu kipenzi guilaine Tom's popote alipo damu ya yesu imufinike ilete Amani kila Léo kwenyi ndowa yetu na watoto wetu Isaac Tony Ibrahim Tony pamoja na Tatiana Tony watoto wangu wote hawa wazidi ku ishi ki MUNGU katika jina la YESU CHRISTU Amen Amen Amen nawa ombeya wana wake wote waliyo kuwa na ndowa Amani idumu kwenyi ndowa zawo na omba vile vile kwama binti wote ambawo hawaja olewa MUNGU Awa epusha natama za uli mwengu na awape ndowa zenyi kudumu hadi uze narudiya tena MUNGU akubariki ndowa zenyi kudumu Amen Amen Amen 🙏 bila kumu sa Abu ndugu yangu prunelle popote alipo MUNGU amu epushe naki buri natama kwa jina la YESU CHRISTU amu epushe nakila hasira kali namaneno makali kwa jina la YESU CHRISTU Amen Amen Amen 🙏🙏🙏🙏 mtu mishi wa MUNGU Isaac Java MUNGU akubariki sana popote ulipo baba

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  7 месяцев назад +1

      Amen Mungu akubariki na akupe haja za moyo wako. Pokea sawasawa na imani yako

  • @JosphineMwasame
    @JosphineMwasame 3 дня назад +1

    Asante mtumishi wamungu amen 🙏

  • @happynescostat7420
    @happynescostat7420 Год назад +6

    AMINA,NIMEANZA na wewe nimemaliza na wewe Asante Yesu akutetee,mme wangu amenikimbia na anaishi na mwanamk aliepewa taraka,asikii Wala aoni ataki kuniona Ila kwa maombi haya amerudi kwangu,

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад +1

      Amen YESU akutendee makuu na akupe ushindi kwa utukufu wa jina lake takatifu

    • @zabiburashid
      @zabiburashid 2 месяца назад

      ​@@IsaacJavanhabari baba

  • @VioletKaitila
    @VioletKaitila Месяц назад +1

    tumeomba pamojja NAONA USHINDI MKUBWA KWA NGUVU ZA MUNGU

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Месяц назад

      Amen zidi kupokea ushindi, kibali na neema. Ubarikiwe na BWANA YESU

  • @sakatamsooh3190
    @sakatamsooh3190 6 месяцев назад +1

    Mchungaji tufanyie video ya maombi ya mahusiano yaliovunjika( a broken relationship) kindly

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  6 месяцев назад +1

      Amen Mungu akubariki. Yatapatikana hivi karibuni

  • @kabibipea3062
    @kabibipea3062 Год назад +4

    Asifiwe yesu bishop naoba ushauri kutoka kwako kwa sababu mm nime changaniykiwa mume wangu amenisaliti na mwanamke mwengine nilivo juwa nika muliza akakubali makosa yake anasema nimsamee hata rudia tena lakini mm inaniuma sana sija mkosea bona anisaliti mm aliaza kunidarau aliacha kunijali kube alikuwa na mwanamke mwengine aki na huyo mwanamke pia amenioba msamaa aka sema atamacha mume wangu 😭😭

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад +1

      Pole mwanangu kwa yote unayopitia kwenye ndoa yako. Ninaelewa umeumizwa na moyo wako umevunjika kutokana na yote yaliyotokea kwenye ndoa yako. Lakini, huu si mwisho wa ndoa yako, bado Mungu anakuwazia mema. Nakushauri, umsamehe mume wako kwa sababu ameshatubia makosa yake. Muombe Mungu akutie nguvu ya kusimama tena na kusahau yaliyopita ili muweze kusonga mbele. Lakini anza kutumia maombi kama silaha yako kuu kwa ajili ya ulinzi na ustawi wa ndoa yako. YESU anakupenda. Usiogope.

  • @moumou2856
    @moumou2856 Год назад +6

    Eeee mungu wangu narudia tena kwenye haya maombi nina imani yana nguvu sana....Eeee mungu baba asante kwa neema yako...Eeee baba narudia tena mbele zako ninamfukuza mke mwenza alie leta majonzi,machozi na vurugu kwenye ndoa yangu namfukuza naweka ukutu kati yake na mume wangu....Eee Bwana ninakuomba huu mwaka uwe wa mwisho nakataaa uke wenza kwenye ndoa yangu ameeeen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад +2

      Amen Amen YESU akushindie na aiponye ndoa yako kwa utukufu wa jina lake. Damu ya YESU isimame upande wako na kufanya ukombozi wa nafsi kati yako na mume wako. Amani na upendo wa kwanza urudi na YESU awalinde na kuwatunza.

    • @HappyJ-lr9sn
      @HappyJ-lr9sn 4 месяца назад

      Ameni kipenzi.

    • @HappyJ-lr9sn
      @HappyJ-lr9sn 4 месяца назад

      ​@@IsaacJavan
      Same to me Pastor

    • @moumou2856
      @moumou2856 4 месяца назад

      🙏🙏

    • @christinaoyye4059
      @christinaoyye4059 4 месяца назад

      Amen yaani nimepata nguvu ya ajabu wakati naomba maombi nashukuru sana sasa nasubiri matokeo kwa damau ya yesu

  • @dgjkkkvbjkk6041
    @dgjkkkvbjkk6041 Год назад +1

    Hello pastor bwana yesu asifiwe Mm naitwa secilia Akenyan ..nlikua nakutafuta whatsapp

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад

      Amen mwanangu, unaweza kuwasiliana nasi kwa njia ya WhatsApp kupitia namba ya simu +255 745 76 45 72

  • @MaryanaPatrick-x4s
    @MaryanaPatrick-x4s 5 месяцев назад +1

    Nashukuru umenifundisha kuomba nimejua kunena kwa lugha leo

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  5 месяцев назад

      Mungu akubariki sana. YESU azidi kukuonekania. Karibu pia uungane nasi kwa maombi ya kila siku na kusoma biblia. Mungu akikupa nafasi, unaweza kuungana nasi kupitia link hii:
      youtube.com/@NenoLaSiku?si=4ZlJKyvQA1Z_cqoZ

  • @judymwende571
    @judymwende571 Год назад +1

    Joseph makao mwelu nakuita urudi kwa nyumba

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      YESU akupe haja ya moyo wako kwa utukufu wa jina lake

  • @emilyamani2016
    @emilyamani2016 11 месяцев назад +1

    Pastor nikumbuke kwa maombi mme wangu amepotezwa na ulevi na wanawake niombee

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen YESU akupe haja ya moyo wako kwa utukufu wa jina lake

  • @elishamarco521
    @elishamarco521 Год назад +1

    Naweza kumuombea mme wangu tuliyeacha nae ila mm Bado nampeda yy hanipedi

  • @raelsarange638
    @raelsarange638 2 года назад +8

    Thanks for the good prayer, I will come soon with the testimony in Jesus mighty name Amen 🙏🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen my daughter may the power of the Holy Spirit minister to you and grant you victory in Jesus name. God bless you forever

    • @magrethmsaky4153
      @magrethmsaky4153 2 года назад +1

      @@IsaacJavan amem

    • @magrethmsaky4153
      @magrethmsaky4153 2 года назад

      Amen

  • @RachelMallya-gx1sv
    @RachelMallya-gx1sv 10 месяцев назад +1

    Damu ya yesu inene mema leo Kwa erinest anitoea block atume ela mtoto nampenda

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Damu ya YESU inene mema kwa ajili yako na kukushindia katika yote

  • @victoriamaige2862
    @victoriamaige2862 Год назад +1

    Nimejiungamanisha mtumishi lkn utanisaidia niongee na wewe maana shida ya mume wangu ht humu haimo ila Kuna shida

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Mungu akubariki na akutane na haja za moyo wako

  • @rosemwasha9944
    @rosemwasha9944 2 года назад +1

    Kwakumfungua,mumewangu,kwa,damu,yasu

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen mwanangu ubarikiwe na BWANA YESU milele

  • @pendomwaringa7597
    @pendomwaringa7597 20 дней назад

    Nimepokea ushindi kwa jina la yesu🙏🙏🙏🙏

  • @suzanne9517
    @suzanne9517 Месяц назад

    Bwana Yesu asifiwe mtumishi wa Mungu naomba kupitia maombi haya Mungu akubariki ndoa kwa jina la Yesu kristo 🙏🙏

  • @MarthaGeogre
    @MarthaGeogre Год назад +1

    Amina

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele

  • @waleedbahar5275
    @waleedbahar5275 Месяц назад

    Amen MUNGU akubariki sana mtumishi Kwa maombi

  • @RoidaMgaya
    @RoidaMgaya 11 месяцев назад +3

    Asante kwa maono maana tunapitia changamoto juu ya waume mungu wa mbinguni azidi kukutumia juu ya watu wake ubalikiwe kwa huduma hii.

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  11 месяцев назад +1

      Amen mwanangu ubarikiwe sana na BWANA YESU milele yote. Damu ya YESU inene mema kwa ajili yako na kukushindia daima 🙏

  • @ismaiyamusa1277
    @ismaiyamusa1277 6 месяцев назад +1

    Asante mtumishii 🙏🙏🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  6 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU

  • @edinarwamgira5712
    @edinarwamgira5712 Месяц назад

    Kupitia maombi haya ndoa yangu ikafunguliwe sasa

  • @lilianwambui1325
    @lilianwambui1325 2 года назад +7

    Amen , Amen this was really powerful. I prayed and felt something in the spirit. God is faithful

    • @lilianwambui1325
      @lilianwambui1325 2 года назад +1

      Mungu wa mbinguni akutende mema mtumishi wa Mungu

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen my daughter, to JESUS be the praise and honor. May God meet you at the point of your need for His name's sake. God bless you and keep on praying till you receive it. Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen mwanangu ubarikiwe pia na BWANA YESU milele yote. Amen Amen

  • @priscamutheu7350
    @priscamutheu7350 2 года назад +4

    Nimebarikiwa na hayo maombi sana najua Kuna jambo mungu anaenda kutenda amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen mwanangu. YESU akutendee kwa utukufu wa jina lake. Ubarikiwe

  • @AlisiaAgusitino
    @AlisiaAgusitino 9 месяцев назад +1

    Mngu naomba mme wangu aje

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele yote

  • @victoryndugutse296
    @victoryndugutse296 28 дней назад

    Amina amina amina amina ❤

  • @maureenshinavuli2381
    @maureenshinavuli2381 8 месяцев назад +1

    Thanks pastor

  • @aishawaziri2701
    @aishawaziri2701 7 месяцев назад +1

    Nmepokea

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  6 месяцев назад

      Amen YESU akutendee makuu kwa utukufu wa jina lake takatifu

  • @ElizabethWanjiru-w3q
    @ElizabethWanjiru-w3q 6 месяцев назад +1

    Blood above all

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  6 месяцев назад

      Amen to JESUS be the praise and glory. God bless you

  • @esterfaida7357
    @esterfaida7357 Год назад +1

    Nafugua ufaham wako

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад

      YESU akupe ushindi mkuu mwanangu. Ubarikiwe sana

  • @ruthmuja7792
    @ruthmuja7792 8 месяцев назад +1

    Amen Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад +1

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU kwa baraka za milele

  • @NasraSaidi-dq7fh
    @NasraSaidi-dq7fh 5 месяцев назад +1

    Amen 🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  5 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele yote

  • @BethsaidaMacrean
    @BethsaidaMacrean Месяц назад

    Naomb mungu umlind na kumfungua mume wang kifungon na malengo tutimize bila kipingamiz na amini imekua asante mungu

  • @miriammagarinza8807
    @miriammagarinza8807 9 месяцев назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele yote

  • @suzanne9517
    @suzanne9517 Месяц назад

    Mungu akubariki mtumishi kwa maombi haya

  • @bahatichenje5722
    @bahatichenje5722 11 месяцев назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU

  • @LucyGaceri-x7f
    @LucyGaceri-x7f Год назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад

      Amen ubarikiwe sana na BWANA YESU milele yote

  • @edinafelicin9523
    @edinafelicin9523 Год назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  Год назад

      Amen ubarikiwe sana na BWANA YESU milele yote

  • @doreenshayo1272
    @doreenshayo1272 3 дня назад

    Amina

  • @RabsonManswet-pc1co
    @RabsonManswet-pc1co Год назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele

  • @getrudemollel705
    @getrudemollel705 Год назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele

  • @dorcasasia2819
    @dorcasasia2819 2 года назад +3

    Msamaha ni uponyaji hakika nimemwona Mungu kwa ndoa yangu jina la Bwana Yesu libarikiwe hao maadui wameshindwa kupitia maombi haya be blessed servant of God 🙏🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen Amen mwanangu. YESU azidi kukuonekania katika mambo yote. Ubarikiwe sana

  • @RachealKukunde
    @RachealKukunde 25 дней назад

    Namini katika haya maombi mume wangu alinitenga na kuishi na mwana muke mwengine atarudi kwangu mana sijui hata anapoishi

  • @anny-gal...4097
    @anny-gal...4097 Год назад +1

    Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen Mungu akubariki kwa baraka za milele

  • @gracekanyanza4816
    @gracekanyanza4816 2 года назад +1

    Aaa

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Mungu akubariki mwanangu

  • @MeryMbaga-y4n
    @MeryMbaga-y4n Месяц назад

    Ameeen barikiwa mungu akutunze

  • @aisiamkonyi4977
    @aisiamkonyi4977 9 месяцев назад +1

    Ameen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад

      Amen ubarikiwe kwa baraka za milele yote

  • @AisiaMoshi
    @AisiaMoshi 2 месяца назад

    Asante kwa maombi haya mungu akubariki Sana amen

  • @NatashapraizzyPraizzy-p7u
    @NatashapraizzyPraizzy-p7u 2 месяца назад

    Amen mtumishi tumebarikiwa🙏

  • @MeryMbaga-y4n
    @MeryMbaga-y4n 29 дней назад

    Mungu akutunze baba na kukuinua kwa viwango vingine

  • @LoiceOngachi-j9e
    @LoiceOngachi-j9e Год назад +3

    Amen nakomboa doa yangu Kwa damu ya yesu uadui ulioko kati yangu na mume wangu u kaondoke Kwa damu ya yesu madawa aliyo lishwa ya kiuchawi ukaondoke Kwa tumbo lake katika damu ya yesu na upendo ukarije Kwa damu ya yesu

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen Amen YESU akupe ushindi mkuu kwa utukufu wa jina lake

  • @victoryndugutse296
    @victoryndugutse296 Месяц назад

    Amina amina❤

  • @priskywangui6529
    @priskywangui6529 2 года назад +6

    Amen Amen.So powerful and believing that it will change my husband

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen my daughter, may Jesus change your husband and heal your marriage for His name's sake. God bless you

    • @winiwill
      @winiwill Год назад +1

      Bwana Yesu asifiwe Asante naamini nimemfungua mme wangu Kwa jina la Yesu

  • @GetrudeSwai
    @GetrudeSwai 2 месяца назад +1

    Kupitia maombi haya ninaamin mume wangu atrurudi kwangu na atanipenda na atanijal mimi pamoja na mtoto amen

  • @estermeshack610
    @estermeshack610 9 месяцев назад +2

    Ameen Baba namuombea mme wangu aache kunywa pombe na aache kuchelewa kurudi nyumbani.kila siraha iteketee kwa jina la yesu ameeni.

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen YESU akutane na haja za moyo wako na akupe ushindi

  • @beatricewanza2995
    @beatricewanza2995 2 года назад +2

    Niko kwa maombi mume wangu Frank nakuitisha urudi kwa ndoa yetu na huyo kavuna amekuweka akuachilie kwa damu ya yesu na urudi nyumbani katika NJINA lA YESU.DAMU YA YESU INENE REHEMA.

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад +1

      Amen Amen mwanangu, YESU akutane na haja ya moyo wako na aiponye ndoa yako kwa utukufu wa jina lake takatifu

    • @beatricewanza2995
      @beatricewanza2995 2 года назад

      @@IsaacJavan AMEN

    • @maryhumble6470
      @maryhumble6470 2 года назад

      Amen

  • @GraceJumwa-h8n
    @GraceJumwa-h8n Месяц назад

    Mungu akubariki mchungaji

  • @AnithaAhadiel
    @AnithaAhadiel Месяц назад

    Mchungaji niombe sana

  • @jaelbabie12
    @jaelbabie12 3 месяца назад

    Amen in Jesus Christ Name Amen Amen.

  • @janemothama2387
    @janemothama2387 2 месяца назад

    Amen God do miracles I trust in you

  • @fezakabala6589
    @fezakabala6589 3 года назад +4

    Bwana asifiwe 🙏🙏

  • @victoryndugutse296
    @victoryndugutse296 Месяц назад

    Amina amina amina amina umbarikiwe mtumi shiwangu

  • @tausamon5844
    @tausamon5844 5 месяцев назад +1

    Ameni

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  5 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU

  • @kitunganochristine1346
    @kitunganochristine1346 2 года назад +6

    Naamini kupitia mahombi haya mume wangu amefunguliwa tayari kupitia damu ya bwana wetu yesu christo
    Naamini nitarudi tena apa kutowa ushuuda na kumshukuru mungu wangu kwa makuu na mahajabu yenye atanitendea kupitia mahombi haya
    Mungu akubariki sana mtumishi wa bwana na akuhongezeye siku za kuishi wewe na familia yako yote kwa ujumla
    Bwana yesu asifiwe sana

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад +1

      Amen mwanangu, YESU ni mwaminifu, nami ninaamini anaenda kukutendea makuu kwa utukufu wa jina lake. Mungu akubariki na akutane na haa ya moyo wako mwanangu. Amen

    • @kitunganochristine1346
      @kitunganochristine1346 2 года назад

      @@IsaacJavan Amen

    • @bahatimaige6666
      @bahatimaige6666 2 года назад

      Naamini kupitia maombi haya mume wangu amefunguliwa kutoka kwa makahaba na kurudi nyumbani kuleta amani na familia yetu! Amina!

  • @agenithaleonard6804
    @agenithaleonard6804 2 года назад +2

    Nakushukulu kwa maombi yako kupitia maombi haya mme wangu anafunguka naamini anafunguka mngu akubaliki amee

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen mwanangu. YESU akutane na haja ya moyo wako. Ubarikiwe sana

  • @verenasemgen8873
    @verenasemgen8873 Год назад +2

    Mtumishi ubzrikiwa sana kwa maombi haya naombanukupigie

  • @MeryMbaga-y4n
    @MeryMbaga-y4n Месяц назад

    Mungu akubariki sana baba

  • @MeryMbaga-y4n
    @MeryMbaga-y4n Месяц назад

    Ameeni barikiwa

  • @macfadyneminja
    @macfadyneminja 8 месяцев назад +2

    Amen Natii Haya Maombi. Mapenzi yako Mungu na Yatimie Amen

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Mungu akubariki sana na kukupa ushindi kwa utukufu wa jina lake takatifu

  • @ezekiakaminyoge5198
    @ezekiakaminyoge5198 2 года назад +1

    Mim ckufunga ndoa ila alitoa mali nakunipeleka kwao nikaishi nae miaka 6 badae akawa mzinzi sana nikagundua anamahusiano na dada mmoja nika mfata yule dada ila alichofanya yule dada akajitolea mali akaendesha arusi wakafunga ndoa na alifanya makusudi kunikomoa je huyo si mume wangu?

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Hapana mwanangu. Mume ni yule uliyefunga naye ndoa.

    • @ezekiakaminyoge5198
      @ezekiakaminyoge5198 2 года назад +1

      Amina baba nashukuru🙏🙏🙏🙏🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      @@ezekiakaminyoge5198 Amen mwanangu ubarikiwe na YESU

  • @matildaff6728
    @matildaff6728 3 года назад +5

    Ubarikiwe sana na bwana kwa maombi mazuri 🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  3 года назад +1

      Amen Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele

    • @matildaff6728
      @matildaff6728 3 года назад +1

      @@IsaacJavan Amen 🙏

    • @wazirichiduo52
      @wazirichiduo52 3 года назад +1

      Amen ubarikiwe kwa maombi mazuri

    • @wazirichiduo52
      @wazirichiduo52 3 года назад +1

      Naitaji kuawasiliana nawe

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  3 года назад

      @@wazirichiduo52 Amen ubarikiwe na BWANA YESU

  • @AliceAlice-ol5zv
    @AliceAlice-ol5zv 2 года назад +2

    Asifiwe yesu dady asante kwa maombi haya mungu akubariki sana🙏🙏🙏🙏🙏

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад +1

      Amen mwanangu ubarikiwe na BWANA YESU akutendee makuu

  • @ritha8110
    @ritha8110 2 года назад +2

    Libarikiwe jina la Bwana Yesu...Ahsante kwa maombi haya.Nimeomba na nitaendelea.Ninaamini Mungu atatutendea soon kwa jina la Yesu.

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen Amen mwanangu. Zidi kubarikiwa na BWANA YESU. Mungu akutane na haja za moyo wako na akutendee makuu kwa utukufu wa jina lake. Ubarikiwe sana. Amen.

  • @wivinendege
    @wivinendege 3 года назад +3

    AMEN UBARIKIWA BABA YANGU MTUMISHI ISAAC.MUNGU AMESIKIYA MAOMBI YETU 👏🤝🤝🤝✊✊✊♥️♥️♥️

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  3 года назад

      Amen Amen mwanangu, Mungu akubariki kwa baraka za milele

  • @angelfelician5389
    @angelfelician5389 8 месяцев назад +2

    Amen namkomboa mume wangu aliyeniwekea chuki kwa kusikiliza maneno ya watu

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen YESU akupe ushindi

  • @SallyMaina-lg3uw
    @SallyMaina-lg3uw 9 месяцев назад +2

    This prayer is powerful

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen may God meet you at the point of your need

  • @priscahshemkunde7256
    @priscahshemkunde7256 Год назад +2

    Ameeen kubwa mtumishi wa mungu alishaanikimbia na kukata mawasiliano kwa maombi haya naamini mungu amesikia na atarudi kwa jina na kwa damu ya yesu ameeen ubarikiwe Sana mtumishi

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  9 месяцев назад +1

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele

  • @NancyLazaroTanzania
    @NancyLazaroTanzania 2 года назад +2

    Amen. Amen. Amen. Mungu wetu ni mwaminifu. Alitenda, ametenda, anatenda na atatenda. Yeye ni yule yule jana, leo na hata milele. Shetani anaenda kuaibishwa kwa Jina la Yesu. Naamini Mungu amejibu maombi kwa jina la Yesu Kristo. Amen.

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад +1

      Amen mwanangu YESU anaweza yote. YESU anakupenda. YESU akutane na haja ya moyo wako kwa utukufu wa jina lake. Ubarikiwe sana kwa baraka za milele yote

  • @deogratiussingano3814
    @deogratiussingano3814 Месяц назад

    Ameen

  • @Rashneyirene
    @Rashneyirene Месяц назад

    Ameeeeeen

  • @JoyceHaule-o7b
    @JoyceHaule-o7b 26 дней назад

    Amen

  • @Rashneyirene
    @Rashneyirene Месяц назад

    Ameen

  • @LilianBosibori-l1m
    @LilianBosibori-l1m Месяц назад

    Amen

  • @suzyamos9589
    @suzyamos9589 4 месяца назад

    Amen🙏🙏🙏

  • @heleminaamani5810
    @heleminaamani5810 3 года назад +2

    Namushukulu Mungu kwaajili yako maana nilikuwa nahangaika niombeje ili niweze kuludiana naye na tuweze kusameheana makosa yetu naomba Mungu akutunze na kuku tumia zaidi ikikupendeza naomba kuongea na wewe

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  3 года назад +1

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU. Mungu akushindie na damu ya YESU inene mema kwenye maombi yako.

  • @HeriethMalonza
    @HeriethMalonza 2 месяца назад

    Amen🙏

  • @HappyKabogo
    @HappyKabogo 3 месяца назад

    Amen

  • @augustinarichard3029
    @augustinarichard3029 3 месяца назад

    Amen

  • @saramtei4371
    @saramtei4371 2 года назад +1

    Amen mungu akubarik past maana kusema ukweli kupitia maombi haya ndoa yangu imepone mungu akuweke mika elf na aendelee kukupa maarf il tuendele kupna amn

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  2 года назад

      Amen mwanangu, ubarikiwe sana, na BWANA YESU azidi kukutendea makuu kwa utukufu wa jina lake

  • @GraceKibelenge
    @GraceKibelenge 4 месяца назад

    Amen

  • @Romana77-m4o
    @Romana77-m4o 4 месяца назад

    Amen

  • @SalimaKalambo-id3te
    @SalimaKalambo-id3te 4 месяца назад

    Amen

  • @HappyKinyaiya
    @HappyKinyaiya 5 месяцев назад

    Namkomboa na mume wangu kwa roho zote chafu zinazo mfwatilia

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  5 месяцев назад

      Amen YESU akupe ushindi mkuu

  • @brightnessbajuta9666
    @brightnessbajuta9666 Год назад +2

    Amen ubarikiwe naamni mume wangu atarudi kwa maombi hay miaka miwili sasa

    • @verenasemgen8873
      @verenasemgen8873 9 месяцев назад +1

      Mungu atukumbuke miaka miwili mie miezi 5 naona kama miaka

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      YESU akupe ushindi kwa utukufu wa jina lake

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Mungu akupe ushindi

  • @JoyceJohn-n7l
    @JoyceJohn-n7l 10 месяцев назад +3

    Naikomboa ndoa yangu kwa damu ya yesu dawa zote alizowekewa zikaharibike zivunjike tupendane kama mwanzo

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  8 месяцев назад

      Amen ubarikiwe na BWANA YESU milele

  • @elvinantangeki9907
    @elvinantangeki9907 3 года назад +2

    Mtumishi Mungu akubariki kwa maombi yako najua mine wangu atafunguliw

    • @IsaacJavan
      @IsaacJavan  3 года назад

      Amen Amen Damu ya YESU ikupambanie na kukupa ushindi