FISI AUA NA KUJERUHI CHUNYA MKOANI MBEYA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 7 апр 2024
  • Mnamo Aprili 07, 2024 katika Kitongoji cha Gengeni kilichopo Kata ya Kambi katoto, Tarafa ya Kipembawe, Wilayaya Chunya, Mkoa wa Mbeya, Mnyama Pori aina ya Fisi alivamia nyumba ya Shigela Ngasa [45] Mkazi wa Gengeni na kuwauwa kwa kuwang'ata watoto watatu wafamilia hiyo ambao ni Samweli Shigela [05], Kasunzu Shigela [03] na Ngasa Shigela mwaka 1 wote wakazi waGengeni.
    Aidha ,katika tukio hilo mnyama huyo aliwajeruhi wazazi wa watoto hao ambao ni Shigela Ngasa [baba] na mke wake aitwaye Limi Masanja [38] wote wakazi wa Gengeni. Baada ya tukio hilo Fisi huyo aliua kondoo wawili na kisha akakimbia uelekeo wa Hifadhi ya Rungwa eneo la Kambi katoto. Fisi huyo aliweza kuingia ndani ya nyumba hiyo kutokana na nyumba hiyo kutokuwa na mlango naikoporini karibu na Hifadhi hiyo.
    Majeruhi wamelazwa Hospitali ya Mtakatifu Gasper - Itigi, Wilaya ya Manyoni, Mkoa wa Singida kwa matibabu zaidi. Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Askari wa wanyama pori kutoka pori la akiba la Rungwa na Wananchi wa Gengeni limefanikiwa kumuua Fisi huyo ambaye alikimbilia Porini na baadae kurudi tena Kijijini hapo.
    Imetolewana:
    AbdiIssango - SACP
    KaimuKamandawaPolisi,
    MkoawaMbeya.

Комментарии •