Zembwela Kuhusu Ndoa "Kuna Mke Mke, Mke Mke Wenu Na Mke Mkeo" | SALAMA NA ZEMBWELA PT 2

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 30 сен 2024
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    MSAFIRI HUFIKIRI
    Moja ya jambo ambalo nimejifunza kuhusu maisha na kufanikiwa ni KUTOKATA TAMAA wakati unatafuta ila kubwa kuliko ni wajibu wetu kutojiona tuko JUU zaidi ya wengine na kuamini kwamba pale ulipo hakuna siku ambayo utakuja KUTETEREKA. Katika makosa ambayo unaweza kuyafanya ni kuamini hilo jambo KUBWA.
    Hillary Daudi ni Kaka yangu na Rafiki yangu, mimi nilianza kwa kumuona yeye kwenye TV kabla sijakutana naye rasmi kwenye mwanzo kwa miaka ya 2013 kupitia Rafiki yangu mwengine aneyeitwa Mussa Hussein, Mussa na Zembwela ni washkaji ambao wali click tu mara ya kwanza walivyoonana na Mussa alipomsikia tu Zembwela aliona atamfaa sana kama atakua partner wake kwenye kile kipindi alichokua akifanya cha kuanzia saa tatu asubuhi pale EA Radio.
    Zembwela alikua mmoja wa waanzilishi wa kipindi cha vichekesho pale ITV akiwa na Rafiki yake Marehemu Max, na jambo ambalo mimi nilikua silijui ni kwamba Zembwela yeye ndiye aliyekua muandishi wa yale maigizo mafupi mafupi waliyokua wanafanya, na hilo swali nilimuuliza baada ya kusikia tetesi mtaani kwamba toka Max atangulie mbele ya haki yeye Zembwela amepoteza kabisa ile ladha na kwamba sasa si yule wa zamani. Ki kawaida tu kwanza hawezi kuwa kama yule wa zamani na zaidi ni kweli ladha pengine lazima ipotee maana sasa hivi yuko peke yake, ila je kipaji? Binafsi nadhani Zembwela ana kipaji na utashi wa hali ya juu ambao unamfanya aendelee kuwepo pale alipo na sasa akiwa anasimama kama Ndimu kwenye Radio ya Wasafi FM pale asubuhi anapokua anachambua magazeti.
    Mwanzo nilikuambia Zembwela alianzia EA Radio baada ya kuvutwa na Mussa pale, na alikaa kwa kipindi hata baada ya Mussa kuondoka yeye aliendelea kuzungusha gurudumu la Super Mix ila baadae mambo yakabadilika na ikambidi aende kutafuta ustaarabu mwengine na sehemu nyengine. Maisha yako wakati mwengine yanaweza kukupeleka sehemu ambayo wala ulikua huitarajii.
    Sasa pia amerudi kwenye TV na kaniibia siri pia kwamba hivi karibuni anatarajia kuanza series ambayo wao kama Wasafi TV wamekua wakiipika kwa kipindi sasa. Naamini hii itakua habari njema kwa wengi ambao wamekua wakiisubiria kwa hamu.
    Na pia kasema itaanza hivi karibuni.
    Mimi na Zembwela pia tumeongelea maisha yake binafsi, kuondoa kwa Max, kazi za kileo na mustakabali wa Siasa na wana Siasa na mengine tele. Moja kubwa ambalo naweza kukuahidi ni enjoyment na kucheka, hakika haya UTAYAPATA.
    Tafadhali enjoy,
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz

Комментарии • 235

  • @duncankabig9740
    @duncankabig9740 2 года назад +30

    Nime enjoy Sana Leo sister salama jamaa mkweli sanaa

  • @mahmoudaziz4717
    @mahmoudaziz4717 2 года назад +6

    Yani nakipenda sana iki kipande cha mke mke. Mke mkiwenu. Mke mkeo. Nimejifunza mambo mazuri sana. Big up zembwela na salama bin jabir.

  • @richardmmassy5857
    @richardmmassy5857 2 года назад +40

    Kuna elimu na kuna kuelimika... Huyu jamaa kila nikimsikiliza naelimika sana... Asante kwa maisha yako Zembwela, jua kwamba kuna watu tupo tunapata elimu sana.

  • @adamismailly1784
    @adamismailly1784 2 года назад +4

    Hebu muache km mienzi 2 halafu mlete tena salama huyo jambaa yuko vizuri sana na ana mambo mengi sana ya kutufunza

  • @SaumuHassan-sf5zk
    @SaumuHassan-sf5zk Год назад +3

    Mwamba huyu hapa, we are too blessed to have you till now. Akili nyingi mkweli mchekeshaji huchoki kumuangalia Wala kumsikiliza. Ahsante sana Salama kwa kutuletea huyu Mwamba muwe na afya njema tuendelee kujifunza

  • @kefamkv3743
    @kefamkv3743 2 года назад +7

    Siku ya nne sasa nairudia hii daaah🙌🙌🙌bonge la interview

  • @yohanacosmasmachalila9016
    @yohanacosmasmachalila9016 2 года назад +10

    Waoo! Kipindi kimenielimisha na kuniburudisha sana😊 Big up sana salama na kwa kaka yangu Zembwela

  • @officialrobeasy
    @officialrobeasy 2 года назад +23

    This guy is very fun, he made my night 😂😂😂😂

  • @kingndinyo9764
    @kingndinyo9764 2 года назад +9

    Gari bovu huvutwa na gari zima.... Fact Beberu 🍺

  • @sophiamazige705
    @sophiamazige705 2 года назад +6

    Hela ndo nguvu za kiume zilizobaki. Vijana tafuteni helaaaaaaaaaaaaa😅😅😅

  • @exclusvetztv9011
    @exclusvetztv9011 2 года назад +10

    Thanks my mom for this interview 😀😀😀😀😃🤣🤣🤣😂😅😂 appreciate madame salma j

  • @miracledamian2202
    @miracledamian2202 2 года назад +18

    One of my favorite shows wow

  • @hamzamoshi8275
    @hamzamoshi8275 2 года назад +7

    Asante dada salama, asante pia kwa zembwela babu nimeelimika sana leo napia nimeinjoy SHUKRANI 🙏🏻

  • @mozasaid3869
    @mozasaid3869 2 года назад +2

    Zembwela bhana eti ooh! Bugger zinanenepesha!😆😆😆😆😆😆😆🤣🤣🤣🤣 , nimefurahi sana maneno ya Zembwela,

  • @amanothmanhamimu1174
    @amanothmanhamimu1174 2 года назад +13

    Tunajifunza mengi sana kupitia interview

  • @mdomar4650
    @mdomar4650 2 года назад +7

    Zembwela kwa hakika naku SALUTE. Nimefaidika na mifano uliyoyapeana. Ufafanuzi wako ni Elimu tosha.. pongezi sana bro. Mimi nakukubali..

  • @josephlorri431
    @josephlorri431 3 дня назад

    Wanaosikiliza September 2024 tujuane.. bonge la kipindi..haichoshi

  • @winniekaria6334
    @winniekaria6334 2 года назад +5

    Nimeona muda wa kipindi mdogo leo jamaniii. ..Zembwela hachoshi kumskiliza wallah ukiplus na maswali yako Salama ndo kabisaaaa...

  • @nobodyfromnowhere1888
    @nobodyfromnowhere1888 2 года назад +23

    Sister Salama na Zembwela mmeua sana , y’all very smart people. Binamu Mb, Master , Salama and Zembwela to mention a few … Yall are the Cream of your trade of choice and talent. Fanyeni jambo….❤️

  • @ashminaabdulla8946
    @ashminaabdulla8946 2 года назад +4

    Zambi mpya 🤣🤣🤣🤣🤣😭😭😭

  • @thegreat6626
    @thegreat6626 2 года назад +5

    Pia vijana wanakosa nguvu za kiume kutokana na ku lose confidence kwa kuangalia sana porno na story za uongo za vijiweni wakikutana na madem zao wanajiona wanacheza tu wanajiona vibamia wakijilinganisha na abnormality, maladhi, overweight inayopelekea mzunguko wa damu kuwa hafifu, na janga zaidi ni hizi sms za "... nikwambie kitu... sijui utakubali..." au "...mwenzio naumwa.." too much invoices😀😀

  • @allinall9382
    @allinall9382 2 года назад +5

    Dah kipindi nimekiona kifupi san asee 😋😋, arudi tena ,ikibid muda uongezwe

    • @mdomar4650
      @mdomar4650 2 года назад +1

      Kweli kabisa.. Hapo sawa kabisa.

  • @alimuchiri6151
    @alimuchiri6151 2 года назад +6

    " Alaa moja panga mbili haikai, Babu zembwelaa chuma cha pua kabari yao." Naamia kamanda hujawai niangusha.

  • @saidimtera6665
    @saidimtera6665 2 года назад +5

    I like that mke mke,mke mkeo ,mke mke wenu😂😂😂

  • @zalubiasalim240
    @zalubiasalim240 2 года назад +6

    Thanks for the interview salama, madini ya kutosha, respect babuu zembwela

  • @universitylink
    @universitylink 2 года назад +3

    Utakula alafu ule au utakulaa kwanza, mkunga mwenyewe ameshachika

  • @officialteeh1213
    @officialteeh1213 2 года назад +5

    Thank you for you salama hua unatuletea watu kama hawa chuma kabari yao mbwa napata ziriki kwa mguu zake .I love him namejifunza vitu vingi sana kupiata Babu zembela Ak mume wangu 😂😂😂

  • @malickkasuga4805
    @malickkasuga4805 2 года назад +1

    Kwa max sikutegemea hiloo jibu umejibu kisilani

  • @pembemussa2804
    @pembemussa2804 2 года назад +2

    Msamiati wa Mke mke
    Mke mke wenu na
    Mke mkeo.
    Umenimaliza kk vijana tulio wengi tupo hapo kwenye Mke mke wenu.

  • @paulinekisaka4677
    @paulinekisaka4677 2 года назад +6

    One of the best Salama na episode.....kudos!!!

  • @universitylink
    @universitylink 2 года назад +3

    Watu wa dini, Bwana Yesu asifiwe, Shalom, Salaam aleykum, mi si mtu wa dini nisije tafuta dhambi mpya

  • @mwamvuajumatano1817
    @mwamvuajumatano1817 2 года назад +4

    Allah akupe uhayy,huwa na enjoy nikimfwata zembwela anajuwa sana hadi anakera,Allah azid kukubarik

  • @fatmazullu4933
    @fatmazullu4933 2 года назад +1

    Zembwela umetupiga hapo eti wanawake wa zamani wanavyotuma message! Looh wakati simu zimeanza miaka ya karibuni tu 😛😛😛

  • @mnenedrogba1218
    @mnenedrogba1218 2 года назад +4

    Very factual for sure Zembwela. I never knew u such an inspiration bro.i salute u man🤝👍👌🙏💯✔

  • @zeddeastafrica1032
    @zeddeastafrica1032 2 года назад +2

    Babu kaongea ukweli mtupu mwishoni facts respect sana kwake

  • @MonadiNadi-j6s
    @MonadiNadi-j6s 8 дней назад

    Nimependa sana watafute pesa sio mterezo wataanguka chali😂😂😂

  • @yusuphmipawa6340
    @yusuphmipawa6340 2 года назад +3

    Naomba Zembwela arudi tena

  • @AdamClassic-uj9ed
    @AdamClassic-uj9ed Год назад +1

    Daa Nimekubali Sana

  • @KalabashCreative
    @KalabashCreative 2 года назад +3

    Asante salama, asante Hillary(Zebwela) mbarikiwe kwa somo la maisha.

  • @jimmymeshack8725
    @jimmymeshack8725 2 года назад +3

    Wenye dini hawana imani na wenye imani hawa dini ..!

  • @fatmamussa5255
    @fatmamussa5255 2 года назад +7

    the show was great...nilitamani msingemalza☺

  • @shaqdizo7678
    @shaqdizo7678 2 года назад +1

    Swali la kipofu hapo nadhani Salama umekosea kuuliza swali kama hilo, upofu sio swala la kuliwekea utani maishani kuna wanaotaabika na upofu

  • @selemanimuhanga4018
    @selemanimuhanga4018 2 года назад +2

    Shoo Kali Sana! Producer Tunamuomba Mb Dog Mzee Wa Latifa Kwenye Shoo

  • @jumamohamed5174
    @jumamohamed5174 2 года назад +6

    salama and zembwela you guys are too smart ...

  • @babaetwaha8822
    @babaetwaha8822 2 года назад +2

    Nampenda sana bro zembwela ni mkweli cku zote pia kazi zake nzuri
    Asante dada salama kw kipindi chako naenjoy sana

  • @yahyaahmed1854
    @yahyaahmed1854 2 года назад +3

    Twataka part 3 salama

  • @merrymafole5180
    @merrymafole5180 2 года назад +4

    Utakula alafu ule au utakula kwanza 😂😂😂😂😂

  • @usanifumaandishi7519
    @usanifumaandishi7519 2 года назад +6

    Mke mke, mke mke wenu, mke mkeo🔥🔥🔥🔥

  • @ingabireritha3740
    @ingabireritha3740 2 года назад +4

    Oooh my Good one of the best busara nyingi na hekma thanks you for doing doing good job my sister

  • @kibajadaniel9887
    @kibajadaniel9887 Год назад +1

    "Hela ndiyo nguvu ya kiume pekee duniani "by babu zembwela

  • @alexkalonga5323
    @alexkalonga5323 2 года назад +3

    Madini ya kutosha Zembwela tunashukuru Sana kaka!

  • @vincentmushi1247
    @vincentmushi1247 2 года назад +2

    Hahahaaaa ila zembelwa nyoko sana ...maneno yake ni kiboko...amesema mengi...lkn ili la vijana tutafute hela limeenea...yaani salama ina bidi umrudishe tena babu zembwela hajamaliza bado ana mengi sana

  • @devotabashome1090
    @devotabashome1090 5 часов назад

    SALAMA NIITE NA MIMI NISONSOMOLE HIYO MISOSI😊😊😂

  • @princessbim6096
    @princessbim6096 2 года назад +1

    Kipofu utamfahamishaje kulijua hua😂😂😂😂😂😏😂😆😆😆😆😆😆

  • @malikzafarani172
    @malikzafarani172 2 года назад +2

    Safi saana nimenjoy saana pindi la lao zembwela katisha kinoma

  • @JOSKY-j8
    @JOSKY-j8 Год назад

    Huku wa prove wrong lakini ulihishi katk nyota za bahati may be za majina au ulikuwa unawategemea financially

  • @johnmalembeka3546
    @johnmalembeka3546 2 года назад +2

    Nmependa sna hii interview ya zembwela sna na chumvi katupiga sehem zaman emoji hazikuwepo 🤣🤣🤣🤣🤣🤣

  • @saidikobossa7489
    @saidikobossa7489 2 года назад +4

    I think this is one of the shows ambayo salama ame enjoy sana

  • @andrewmmbaga1665
    @andrewmmbaga1665 Год назад +1

    Zembwela katisha sana

  • @kilosa2000
    @kilosa2000 2 года назад +1

    Hivi ndivyo binadamu inatakiwa uwe ishi kiuhalisia sio kibongo movie, most of them are living fake life

  • @geofreymahally7115
    @geofreymahally7115 2 года назад +3

    Kwa kwl salama nme enjoy sn kipindi cha leo

  • @mateshasembuche2497
    @mateshasembuche2497 2 года назад +2

    Nimeipenda sana show yenu, nzuri sanaaa

  • @masoudnassor5332
    @masoudnassor5332 2 года назад +1

    Real zembwela mungu akupe kheri nyingi duniani

  • @salimumazige9497
    @salimumazige9497 4 месяца назад

    Salama nakuomba huyu jamaa uweunamwita marakwara anaelimisha jamii

  • @allywaziri9838
    @allywaziri9838 Год назад

    N rahisi San mtu kukuzungumzia na kutengeneza sentesi yakee🙈

  • @odrianinicolaus5353
    @odrianinicolaus5353 2 года назад +2

    Salama Tuletee yule Mbunge Mhe.Kishimba,mch.Gwajima au Mhe.Msukuma.

  • @willybaba9516
    @willybaba9516 11 месяцев назад

    Naomba hii kuijua mtu akigeuza samaki hapewi mke kivipi hii ??

  • @patrickpazza4764
    @patrickpazza4764 2 года назад +2

    Daaaaa dada asante Sana kwa kutuletea huyu jamaa n ukweli mtupu kaongea hapo

  • @esterutewele7143
    @esterutewele7143 2 года назад +1

    Dah ais

  • @godfreysanziki1461
    @godfreysanziki1461 9 месяцев назад

    Fresh akajibu hakuna mtindi kitambo sana,jamaa ana misemo uyu

  • @floramlowe7078
    @floramlowe7078 2 года назад +1

    Zembwela nomaaaa sanaaa!

  • @othumanlorenzo260
    @othumanlorenzo260 2 года назад +2

    Vyuma vimekutana

  • @manirakizaambula8605
    @manirakizaambula8605 2 года назад +1

    Asante kaka,🇧🇮

  • @josephlorri431
    @josephlorri431 3 дня назад

    16:10 salama anapenda paja

  • @rahmaawadh1695
    @rahmaawadh1695 2 года назад +2

    Hv salama haujamuelewa zembwela aloposema ushawahi kuona kituo cha polisi post cha bongo movie🤣🤣🤣 grill la nyumbani🤣🤣🤣

  • @paulmgoli4853
    @paulmgoli4853 2 года назад +1

    Iyo Zanzibar 😂

  • @dadygirija968
    @dadygirija968 2 года назад +3

    Zembwela👉🔥🔥🔥✌️

  • @mzhsk1386
    @mzhsk1386 2 года назад +3

    Zaman gani hiyo na simu zilikuwa hazipo

    • @yunusrnb5227
      @yunusrnb5227 2 года назад

      Simu zipo toka mwaka 90 ,Mimi nimemiliki simu mwaka 2000

  • @mahmoudaziz4717
    @mahmoudaziz4717 2 года назад +3

    Nimefurai sana Leo kumuona zembwela. Big salama.

  • @paulmgoli4853
    @paulmgoli4853 2 года назад +1

    Samba soti za shukrani 😂😂😂

  • @georgeosmund727
    @georgeosmund727 2 года назад +2

    Salama huyu mwamba inabidi awe na part 3 & 4

  • @kpol22
    @kpol22 Год назад +1

    This is excellent show. Hongera sana Salam J . Zembwela is too real!~

  • @soudbako5925
    @soudbako5925 2 года назад +2

    One of the best interview all the time anaitwa BEBERU kabali yao or BABU

  • @kassimnurdin9463
    @kassimnurdin9463 2 года назад +2

    hiki kipind ni Zaid ya darasa.
    kiludiwe tena

  • @karimumduma4048
    @karimumduma4048 2 года назад +1

    Dah nime enjoy sana

  • @prettypretty9745
    @prettypretty9745 2 года назад +1

    Nimechelewa Sana kuangalia hii interview mpaka Bwana zebwela ameanza ku trend huko tick tock na what's up stutus nikasema ngoja nije kuona utamu bonge moj ala rahaaaa na buridaniiii iliojaaa elimu toshaaaaa ama kweli junguu kuuu halikosi ukoko

  • @butogwaavelina5299
    @butogwaavelina5299 2 года назад +3

    Nimependa saan na nimejifunza vingi 🙏

  • @athumanipigo9295
    @athumanipigo9295 2 года назад +1

    Dada salama mlete pia Masoud Kipanya please!!!

  • @jumabarua3420
    @jumabarua3420 2 года назад +1

    Yani salama sikuzote nafuatalia kipindi lakini Leo nimetuliza akili sana kwa zembwela kaongea point sana

  • @husseinbuko9657
    @husseinbuko9657 2 года назад +1

    Nime enjoy na nimefurahi dada salama kumleta kaka zembwela kwenye kipindi chako nimejifunza mengi Sanaaaa kutoka kwa zembwela na kwako pia MSAFIRI HUFIKIRI

  • @mangisenya4012
    @mangisenya4012 2 года назад +2

    Zembwela big up

  • @kondokawambwa8398
    @kondokawambwa8398 2 года назад

    Utu uzima dawa

  • @paulmgoli4853
    @paulmgoli4853 2 года назад +1

    Ila Zembwela 😂😂😂🙌

  • @mssscorpion1611
    @mssscorpion1611 2 года назад +1

    😂😂😂😂 ili ndo jua

  • @dinotv1099
    @dinotv1099 2 года назад +1

    Yani utakula alafu ule au utakula kwanza...

  • @mr.africanatural-super_sta1130

    Hahahahahahahaaa

  • @frankkyomushula7588
    @frankkyomushula7588 2 года назад +12

    Great Show as usual Dada....

  • @mmbando
    @mmbando 2 года назад +1

    Vichwa viwili, hatari.. safi sana.

  • @othmanmulendelwa9622
    @othmanmulendelwa9622 2 года назад

    Assallam aleykum mlete tena zembwela kipindi kime chamka salama ongera kwa kumleta zambwela

  • @jumawaziri8501
    @jumawaziri8501 2 года назад +1

    ASANTE SAANA ZEMBWELA VIJANA TUAFUTE HELA .