Kunambi :Tanzania ndio nchi pekee duniani wakurugenzi wanateuliwa, wanatakiwa kuomba nafasi....
HTML-код
- Опубликовано: 21 апр 2024
- Mbunge wa Mlimba (CCM), Godwin Kunambi ameshauri nafasi za uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri wasiteuliwe wanasiasa na badala yake watu wafanye usaili ili mamlaka ya uteuzi ipelekewe majina ya watu watatu ambao wanatokana na utumishi ili mmoja wao awe mkurugenzi.
Kunambi ameyasema hayo leo Jumatatu, Aprili 22, 2024, wakati akichangia maoni yake kwenye makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji kwa mwaka 2024/25 ambapo amesema kwa kufanya hivyo nchi itakuwa na watu waliopo kwenye fani hivyo kuleta maendeleo.
Kunambi amesema Tanzania pekeyake ndio nchi inayoteua Wakurugenzi wa Halmashauri huku akisema nchi nyingine Duniani hazifanyi hivyo na kutaka kuwa wakurugenzi wasiteuliwe kutokana na historia zao za nyuma kwenye siasa.
Godwin Kunambi alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kabla ya kwenda kugombea ubunge kwenye Jimbo la Mlimba, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM na kuibuka kidedea kwenye uchaguzi uliopita wa mwaka 2020.
Uko vizuri hongera kwa muongozo wako na kuwapa maarifa mawaziri na kazi zao UBARIKIWE SANA .. NAKISIFU PIA UNA SAUTI YA UTENDAJI .. .
Hapo hawapigi makofi kwenye point nzito kiasi hicho! Kuna shida kubwa Sana ktk siasa yetu bado!
Mungu aku aukupe maisha marefu sana maana ulitupambania sana Wana ndachi ila ss wamebaki vidabwa vidabwa tu
you deserve to save the country
Hua mnapoteza muda mwingi kwenye shukrani ambazo hazina kichwa wala miguu
wambie viongozi wetu huwezi kuweka mkurugebz kuwa mwanasiasaaa
Tukiendelea na mtindo wa kuteua watendaji wa serikali nchi yetu itaendelea kuwa kichaka cha wizi.
Ccm wanajitoa ufahamu hapa ni katiba tuu
Kunambi ni madini matupu safiii tunataka wabunge kama hawa
Kaka Bado huja iva
C useme tuuu kuwa katiba mpya ni sasa au unaogopa kuitwa na kuhojiwa kuwa au umetumwa na Mbowe🤣🤣🤣🤣
Katiba waka ku vyote ni bure kama hakuna utashi wa uzalendo.
Kenya wanakatiba mpya OG ila kila uchaguzi ukikaribiya wanakufa watu na uchaguzi ukimaliza katiba unarudi kuheshimiwa tena.
Kikubwa ni uzalendo wa kujenga nchi kuliko ubinafsi wa kujifaidisha mifuko na familiya zao.
Katika jambo la kurekebishwa haraka bila kusubiria katiba ni kuondoa huo uteuzi wa watendaji wa ngazi za watendaji kuteuliwa na rais.
hawawezi ndg mjomba atapeleka jina kwa mhusika atapea
Tukipata KATIBA mpya itaondoa cheni ya teuzi ambazo hzina mshiko.
Hiyo imepenya