Mke wa Mbunge mstaafu Mbeya Afariki dunia Atimiza miaka 90 ni mama wa Meya wa jiji Dodoma

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 24 апр 2024
  • #mbeyayetutv
    Mke mkubwa wa Mbunge mstaafu wa jimbo la Mbeya mjini Obel Benson Mwamfupe,Bi Sosisyo Kalasya Mwamfupe amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90 na kuzikwa nyumbani kwake Lugombo Mwakaleli wilayani Rungwe.
    Mwamfupe alipata kuwa Mbunge jimbo la Mbeya mjini kati ya mwaka 1985-1995.
    Mtoto mkubwa wa marehemu ambaye ni Meya wa Jiji la Dodoma Prof Davis Obel Mwamfupe amemzungumzia marehemu Mama yake Sosisyo Kalasya Mwamfupe kwamba ukarimu wake ulisababisha nyumbani kwake Lugombo kutopungua wageni mara kwa mara.
    Naye Binti wa marehemu Irene Mwamfupe alisema kuwa mama yake mbali ya kuwa ni mzazi wake alikuwa rafiki na msiri wake mkubwa ambaye alikuwa kiunganishi kikubwa cha watoto na familia nzima ya marehemu Obel Mwamfupe.

Комментарии • 4

  • @irenemwamfupe8994
    @irenemwamfupe8994 22 дня назад +1

    Barikiwa kaka Asante kwa kuja

    • @MbeyaYetuOnlineTV1
      @MbeyaYetuOnlineTV1  19 дней назад

      Alikuwa mama yetu mwenye upendo mkubwa nisingekuja ningeumia sana moyoni, kila tulipopita Lugombo kumsalimia hakukosa kutupa zawadi ya Maparachichi na Mkungu wa ndizi aliwaambia majirani zake hawa ni wanangu rafiki zake Mbasa,pole sana dada Irene

  • @Aminmwansile-we8vn
    @Aminmwansile-we8vn 23 дня назад

    Mwee yaani mke wa mbunge mstaafu na mitoto yote hiyo wameshindwa kujengea mama Yao kaburi la maana mama Yao anazikwa kimasikini hivyoooo?