UFUNUO WA YOHANA sura ya 14 | MWANA-KONDOO (YESU KRISTO) NA WAISRAELI 144,000 & DUNIA KUVUNWA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 10 сен 2024
  • Na Bishop Dr. Fredrick Simon
    MWANA-KONDOO (YESU KRISTO) NA WAISRAELI 144,000 - 14:1-5
    Wanaonekana wakiwa mbinguni katika mlima Sayuni.
    Dunia kuvunwa 14:6-20.
    Malaika watatu watahubiri wakati wa kipindi cha miaka 3½ ya mwisho.
    1. Malaika mwenye Injili ya milele - 14:6,7
    2. Malaika atangazae anguko la Babeli - 14:8
    3. Malaika atahadharishaye watu wasipokee chapa ya mnyama 14:9-20.
    Katika 14:14 -19, Yesu na malaika zake wanaonekana wakiwa wanaivuna dunia, maana Yohana aliwaona wakiwa na miundu mikononi mwao, wakionyesha kuwa dunia inapaswa kuvunwa kwa ajili ya hukumu.
    Vichala vya mizabibu vinavyotajwa katika 14:18-20 huonyesha kwamba, kutakuwa na mauaji makubwa sana wakati wa vita ya Har-magedoni - 16:16. Hiyo ni vita kati ya Israeli ambalo ni taifa la Mungu, na nchi za mataifa.
    Wakati wa vita hiyo ya Har-Magedoni, Mungu atawapa Waisraeli roho ya neema na kuomba.
    “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma, nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake ... “ ZEKARIA 12:10.
    Ndipo Bwana atawatetea watu wake na kuwaponya, Yesu Kristo atashuka kama jemedari mkuu wa vita ili kuwapigania watu wake Israeli - 19:11-16
     Ataruhusu mvua kubwa ya mawe inyeshe juu ya majeshi ya Mpinga Kristo - Ufu 16:21
    Jiwe moja lina uzito wa Talanta 1. Talanta 1 ni sawa na Kilo 45½ .
     Atawapiga maadui kwa ugonjwa wa tauni, na damu, nk EZEKIELI 38:22,23
     Mungu ataruhusu kazi ya kuzika maiti za wa watakaokufa katika vita hivyo ya Har-Magedoni 39:11-14.
    #fredricksimon #ufunuo #suraya14 #ufunuowayohana #yohana

Комментарии • 5

  • @kizandume3015
    @kizandume3015 Год назад

    Amena mtumishi wa mungu nime barikiwa sana

  • @micomanasseh3497
    @micomanasseh3497 Год назад

    Hakika tumebalikiwa Mwalimu.

  • @ALENKUMBURU-rt6jl
    @ALENKUMBURU-rt6jl Год назад

    Ameeen mwalimu wetu🙏🙏🙏

  • @micomanasseh3497
    @micomanasseh3497 Год назад

    Asante sana Mchungaji.

  • @EliyaMunkwa
    @EliyaMunkwa 6 дней назад

    Jambo mutumishi wa Mungu nilikuwa wapendwa ni juwe je? Kuna watu wata kufa marapili??