Fafanuzi rahisi ya kitabu cha UFUNUO WA YOHANA - Sura ya 11(Na Bishop Dr. Fredrick Simon)
HTML-код
- Опубликовано: 25 окт 2024
- Fafanuzi rahisi ya kitabu cha UFUNUO WA YOHANA - Sura ya 11(Na Bishop Dr. Fredrick Simon)
MASHAHIDI WAWILI AU MIZEITUNI MIWILI - SURA YA 11
11:1 Kipimo cha hekalu la kipindi cha Dhiki Kuu. Mwanzi mmoja ulikuwa na urefu
wa futi 20.
“2 ....... nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili. 3
Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku
elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia.”
Hao ni manabii wawili watakaotoa unabii kwa miezi 42 au siku 1260 (Hiyo ni
sawa na miaka 3½ ) ya mwishoni mwa kipindi cha Dhiki kuu. Manabii hao ni Eliya
na Henoko.
Wengine hudai ni Eliya na Musa, kwa kuzingatia miujiza inayotajwa; mimi naamini
ni Eliya na Henoko, kwa sababu:-
a. Wote wawili hawakufa katika nyakati zao - MWANZO 5:24;
2WAFALME 2:11.
Wakati huo watauwaliwa na Mpinga Kristo kwa idhini ya Mungu mwenyewe
(11:7,8). Kwa sasa wapo mbinguni wakiwa na miili ya duniani!.
b. Wote wawili walikuwa manabii - YUDA 1:14; 1WAFALME 18:22.
#UFUNUOWAYOHANA #mashahidiwawili #fredricksimon #ufunuo #mungu #siri #sikuzamwisho
Asante bishop MUNGU akubaliki
Asante sana kwa somo bishop Dr
Nimebalikiwaa