Dizasta Vina - Hatia IV

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 2 фев 2025

Комментарии • 666

  • @dizastavina
    @dizastavina  4 года назад +103

    “JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE
    HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE
    MSICHANA ANAYEMPENDA
    LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI
    ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA
    LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI
    MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA…
    .ALIENDELEA KUNGOJA”
    Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba
    Sikuwa na mali za kufuja
    Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga
    Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa…
    Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’
    Nywele za kimasai na mkoba
    Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga
    Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani…
    Nilipomwambia nampenda hakujibu
    Akaweka moyo wangu maumivu
    Na mtima wangu akauweka ‘solemba’
    Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’
    Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa
    Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari
    Nikabadili mwenendo wa maisha
    Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali
    Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi
    Alikuwa na misimamo kuipita dini
    Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri
    Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri
    “JOHN ALIFAHAMU HALI YA JANE, KUWA JANE ALIZALIWA KWENYE
    FAMILIA MASIKINI, NA ALIUCHUKIA MNO UMASIKINI.
    ALIFAHAMU UMASIKINI ULIVYOCHUKUA UHAI WA MAMA YAKE KIPENZI,
    ALIYEFARIKI KWA KUKOSA MATIBABU. ALIIFAHAMAU NADHIRI ALIYOIWEKA JANE YA KWAMBA
    HATOKUBALI TENA KUISHI KWENYE MAISHA YA KIMASIKINI, NADHIRI ILIYO MWEKA JOHN NJIAPANDA”
    Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake
    Nilimwacha aende aufate moyo wake
    Alipata bwana wa kizungu magharibi
    Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake
    Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue
    Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka
    Ukipenda ua haulikati unaliacha likue
    Duka langu nilifunga biashara niliacha zote
    Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe
    Niliumwa bado kidogo moyo uzime
    Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine
    Alisema anakwenda jiji la Miami
    Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari
    Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali
    Na yupo tayari kumlipia gharama za safari
    Aliondoka na kipande kimoja cha mwili
    Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili
    Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie
    Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie
    “JANE ALIPOONDOKA ALIMWACHIA JOHN KIDONDA KILICHOCHELEWA SANA KUPONA
    NA YEYE AKAWEKA NADHIRI YA KUTOJIHUSISHA NA MAPENZI TENA MAISHANI MWAKE.
    ALIKAA KWA MUDA MREFU BILA MAHUSIANO. LAKINI…
    HAKUNA DAKTARI MZURI KAMA MUDA, JOHN ALIPONA MAUMIVU NA ALIIRUDIA HALI YAKE YA KAWAIDA”
    Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’
    Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali
    Nikamvisha pete nikalipia mahari
    Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali
    Aliuliza kama nampenda, nilimjibu
    Sikutaka kuweka moyo wake maumivu
    Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba
    Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’
    Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara
    Akanikabidhi tunda nikala
    Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa
    Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa
    “WAKATI KARNE YA 21 INAINGIA, JOHN ALIKUWA NI MIONGONI MWA
    VIJANA WALIOKUWA ‘FASCINATED’ NA UKUAJI WA TEKNOLOJIA YA MITANDAO YA KIJAMII.
    ALIJIUNGA NA DUNIA HII MPYA, MARA KADHAA ALIKAA KWENYE UBARAZA, AKIANGAZA SIMU YAKE.
    AKIPAPASA KILA KITUFE, NDIPO SIKU MOJA AKAPATA UJUMBE KUTOKA KWA JANE”
    “Habari naamini u bukheri wa afya
    Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa
    .nashukuru nahema ughaibuni si kwema
    Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa…
    Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo
    Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono
    Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani
    Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo
    Ukubwa umekuja kunisafisha jicho
    Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah
    Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo
    Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo”
    Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti
    Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi
    Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu
    Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi
    Nilivuka majangwa na majabali
    Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari
    Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa
    Penzi likanipeleka mbali
    “JOHN ALIFIKA UGHAIBUNI, AKAMTAFUTA MSAMARIA ALIYETAMBULISHWA NA UJUMBE,
    MSAMARIA AKAMWELEKEZA NJIWA WAKE ALIPO, NA NIKWELI… HAPAKUWA PEMA”
    Nikakutana na bopa la kizungu
    Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu
    Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe
    Pamoja na vishoka wenye mtutu
    Sio siri alizungukwa na wasichana wengi
    Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent”
    Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi”
    Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti
    “MASIKINI JOHN, ALIDANGANYA KWA KUJITAMBULISHA KAMA KAKA KWA JANE,
    AKIMSIHI YULE MAFIA AMRUHUSU AONDOKE NA JANE WAKAANZE MAISHA MAPYA,
    LAKINI… PALIPOSHINDWA SHOKA WEMBE HAUWEZI TAMBA. KWA KUZIDIWA NA UOGA WA KUUAWA…
    JANE ALIMKANA JOHN KWA KUSEMA HAMJUI…”
    Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu
    Akaweka moyo wangu maumivu
    Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda
    Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu
    Nilikiambia kifo kama unakuja njoo
    Maana sikuwa mtu ilishakufa roho
    Sikuumia kama alivyoniumiza yeye
    Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no
    Aliambiwa ambusu bosi hakubisha
    Alipewa bunduki hakusita
    Aliishika risasi akaiingiza
    Akaambiwa anipige kwenye kichwa
    JOHN ALIKUWA NI JINA JIPYA LA WAHANGA WA UPENDO WA DHATI, VIPOFU WA MAPENZI, WAJINGA WA MAHABA...
    JOHN ALIKUWA ROMEO KWENYE ROMEO AND JULIETH, ALIKUWA SAMSON KWA DELILAH KWENYE WAHUKUMU WA AGANO LA KALE, ALIKUWA JACK KWENYE TITANIC, FRED WEASLEY KWENYE HARRY POTTER..
    JOHN ALITUKUMBUSHA KUWA UPENDO NI SADAKA, SADAKA YA MUDA NA PESA, ALITUKUMBUSHA UPENDO NI SADAKA YA DAMU
    JOHN, ALIPOTEZA UHAI AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UPENDO WA MTU ALIYEMHUSUDU NA
    JANE ALIPOTEZA AMANI NA THAMANI YAKE KAMA MTU AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UTAJIRI ALIOUHUSUDU
    Hatia iko wapi?

    • @challymchaff374
      @challymchaff374 4 года назад +1

      Daaah dizasta wewe ni vina hivi naanzaje kuchoka kusikiliza nyimbo zako

    • @wilsontonga3728
      @wilsontonga3728 4 года назад +1

      🤝🏾

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад +4

      Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi!
      Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina.
      Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
      Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu!
      Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

    • @castorymwaipopo290
      @castorymwaipopo290 4 года назад

      Nakukubali sana bro 💪

    • @sautidawa2222
      @sautidawa2222 4 года назад

      Real talent

  • @gerrymainmunisi6677
    @gerrymainmunisi6677 5 месяцев назад +11

    Nani anasikiliza hiki chuma August 12, 2024... Dizasta mtu mbaya sana

  • @emilysaimon481
    @emilysaimon481 4 года назад +11

    Dizasta vina bro we ni mkaliii
    Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Kama tupo pamoja tia like 25-12-2020

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      Thanks.. Please share. Usisahau kuorder my new album

    • @emilysaimon481
      @emilysaimon481 4 года назад

      @@dizastavina pamoja bro nigei no yako

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад +2

      @@emilysaimon481 pre order kupitia tigo pesa 0655696811 au Mpesa 0762158871

  • @joshmangi
    @joshmangi 4 года назад +16

    "Nilimfanya ndoto, kumbe naye ana ndoto nyingine"

  • @shabannyamsalika
    @shabannyamsalika 4 года назад +25

    Hii ngoma ni zaidi ya albamu nzima ya Weusi, Prof Tungo we ni 🔥🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

    • @shabannyamsalika
      @shabannyamsalika 4 года назад

      @@dullywamashairi121 Hip hop inahitaj wenye uwezo mkubwa wa kufkr, pole sana kwako mwny uwezo mdogo nkushauri kasikilize waaah!!!

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад +1

      @@shabannyamsalika inaelekea wewe ndo hujanielewa Mimi. Wewe bado mbana pua. Wagumu wakipita wataelewa nimemaanisha nini.
      Umekurupuka mzee, maana kitaani wamenibatiza jina wananiita Dizasta vina!!💪💪💪

    • @shabannyamsalika
      @shabannyamsalika 4 года назад

      @@dullywamashairi121 We ndo umekurupuka kusema huu wimbo ni wawagumu, hii ngoma anasikiliza mtu yeyote na anaelewa. Tuondoe mawazo finyu ya kudhania kuwa hip hop inasikilizwa na watu wagumu, cjui makatiri km wewe ulivyosema mwanzo...

    • @obeidjoseph3610
      @obeidjoseph3610 4 года назад

      @@dullywamashairi121 mwanangu ww bado Sana na hilo jina la dizasta mwalichafua kitaan kwenu

  • @winfredykahwili1513
    @winfredykahwili1513 4 года назад +5

    Huu mziki wako ni dawa ya ubongo asee Viva dizasta vina 💪💪💪👊👊💥💥💥

  • @wawesttv
    @wawesttv Год назад +2

    ... nilipo mwambia nampenda hakujibu... 2024

  • @maishacenter-eastafricatv3976
    @maishacenter-eastafricatv3976 4 года назад +10

    Duuhh nlichelewa😪😪😪
    Dizzasta's fan number one from +257🇧🇮🇧🇮🇧🇮

  • @ashuramuhammed3257
    @ashuramuhammed3257 Год назад +1

    Dizasta hii nyimbo ni funzo tosha yani ww ndo mwalimu wangu najifunza vitu vingi nkasikiliza nyimbo zako$

  • @louiskhan7372
    @louiskhan7372 4 года назад +6

    Hii True story nimesikiza ×10....song imenipeleka mpaka gaibuni ....utahisi mkono wa mungu umeandika Hii✔✔#KingOfRap

  • @ARUSHA_NAILS
    @ARUSHA_NAILS 4 года назад +18

    Dah dizasta umezigusa hisia umenifanya nijione mwenye hatia

    • @erastompongo8400
      @erastompongo8400 4 года назад

      Dah Kama umeniimba mimi vile
      Haso za mapenzi duniani zinaumiza wengi

  • @msolidwagalilaya6094
    @msolidwagalilaya6094 10 месяцев назад +3

    Brother ushaandika HATIA nyingi sana lakini hii hatia IV ni funga kazi brother

  • @tiktoktv8678
    @tiktoktv8678 4 года назад +4

    Wasanii kama hawa Bongo ni wachache Sana... Big up bro....

  • @camillomakongwa8308
    @camillomakongwa8308 4 года назад +44

    This dude is a script writer, story teller inshort ni Verteller,,, he can compose a movies of 2 hrs in 7 mins,, daaaamn🔥🔥🔥🔥

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад +8

      Thanks, please share

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

    • @mussabutanwa8693
      @mussabutanwa8693 4 года назад +2

      @@dullywamashairi121 yes he's a genius we should support him lol!!!

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад

      @@mussabutanwa8693 dats true my blood
      Dizasta vina:
      The man one army 💪💪

    • @mussabutanwa8693
      @mussabutanwa8693 4 года назад

      @@dullywamashairi121 yes for really man

  • @jamesngadaya2791
    @jamesngadaya2791 4 года назад +3

    dizasta unao uwezo mkubwa sana wenye nguvu kama meli ya mizigo aiseee

  • @rachelgmartin6850
    @rachelgmartin6850 4 года назад +1

    Sauti yako tu mi hoiiiii🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🌹🥰❤️

  • @kelvinshayo608
    @kelvinshayo608 4 года назад +8

    Nilikwambia unajua na ctoacha kukwambia unajua💪💪

  • @jeovangisc7957
    @jeovangisc7957 3 года назад +1

    Daaaa bro unajua mpaka unaboa.. masikio yetu hayalali njaa kila unaposhika kipaza!!

  • @kangeyg6879
    @kangeyg6879 4 года назад +5

    Master vina fan toka 🇰🇪🔥✅ tumengoja sana umewakilisha kama kawaida

  • @revocatuscharles1512
    @revocatuscharles1512 Год назад +1

    Jamaa unaimba sana aiseh🔥🔥🔥🔥

  • @mdouharoon66
    @mdouharoon66 Месяц назад +3

    16/12/2024 Hili dude bado liko 🔥🔥🔥🔥🔥

  • @chibalevicent822
    @chibalevicent822 2 года назад +1

    You are so Genius, asante kwa uwezo wako wa kunifanya niamini kuwa wewe ndie Rapper Bora

  • @abdfattah883
    @abdfattah883 Год назад +2

    Kitu kinachoniuma ni kuona jamii inasikiliza miziki isiyo ya mafunzo yoyote na kuacha mziki wenye mafunzo Kama huu

  • @mwajumakarim8520
    @mwajumakarim8520 4 года назад +5

    Wewe wewe weeeeeewe🥺🥺🥺ulishushwa ututeke🇹🇿❤️

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @michaelmasanja6343
    @michaelmasanja6343 4 года назад +2

    Verteller ...Dah huwezi amini nimeiona movie yote kichwani mwangu the way Mwamba unavoflow... nilichofeli ni kuipata sura ya Jane.

  • @learntoearn9588
    @learntoearn9588 4 года назад +1

    Muda utafika Inshaallah dizasta utakua jina kubwa na ramani ya maarifa kwa kizazi kijacho

  • @KelvinEmersonSteven
    @KelvinEmersonSteven 4 года назад +5

    Aisee hii ni ya moto kushinda jua🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @BabaNasritz
    @BabaNasritz Год назад +2

    naikubali kinoma hingoma bigp bro

  • @awetubello5399
    @awetubello5399 4 года назад +2

    Brother unawezaaaaah na xo unaweza 2 we ni MWALIMU

  • @danielmalimi9890
    @danielmalimi9890 3 года назад +1

    Duuuhhh.... hii inabeba sababu muhimu ya muziki kwenye maisha....

  • @alextanzania
    @alextanzania 4 года назад +5

    Dizasta vina ni akina Joh 70.
    Mtiririko mzuri ,kazi nzuri. Big up brother.

  • @hassanihanzel
    @hassanihanzel 4 года назад +5

    Wa KUMI kutazama 🙌

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      👏🏾 👏🏾 👏🏾 👏🏾

  • @binyezanch8271
    @binyezanch8271 4 года назад +5

    Wimbo wangu wa mwaka kbsa Asante dizasta 2020

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      Apreciate, umeshaweka order ya album

  • @mosesbond202
    @mosesbond202 4 года назад +1

    Wewe mwamba ni mwehu sema tuu unafikiri sana
    Yaani movie moja classic

  • @lonely8682
    @lonely8682 4 года назад +1

    Najivunia kua shabiki ako bro...hujawahi kuniangusha🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @fadhilimponzi2242
    @fadhilimponzi2242 Месяц назад

    ni nyimbo niliyosikiliza mara nyingi kuliko nyimbo yoyote dizasta vina

  • @novatusanthony8563
    @novatusanthony8563 4 года назад +2

    Hii goma inatakiwa wasambaziwe wanafunzi Tanzania mzima maana hili ni somo linajitegemea.

  • @BrightoneAyubu
    @BrightoneAyubu 2 месяца назад

    Appeiciet mzee baba🔥🔥🔥

  • @meshack2559
    @meshack2559 4 года назад +1

    Mistar unachora Broo!!! Ni nomah ,we mkali aise,big up

  • @dullyhaleem6962
    @dullyhaleem6962 2 года назад

    Hii nyimbo itungiwe movie kummmke duuh😓😓🔥🔥🔥

  • @vandiddyy5733
    @vandiddyy5733 3 года назад +1

    Duuh..! sijui nikupe jina gani broh... una hatari kubwa sana. 🙌🙌🙌

  • @peterbenjaminpeterbenjamin9566
    @peterbenjaminpeterbenjamin9566 4 года назад +1

    Aisee dizastar noma Sana mshkaji wangu darasa Hilo namimi napenda Nije nipate mautundu ya asali ya hip-hop

  • @erickpaschaljr8667
    @erickpaschaljr8667 4 года назад +1

    Ahsante sana Dizasta Vina Kwa Muziki Mzuri unaoacha/utakaoacha Alama ya Milele

  • @kelvinmzopola5186
    @kelvinmzopola5186 4 года назад

    Daaaaah so sad 😌 ila we jamaa unajua kinoma

  • @shedzooytv4099
    @shedzooytv4099 25 дней назад

    Dizastavina greater thinker my best hip hop artist in tz nyimbo kama fasihi only for greater mind

  • @sayeedally8152
    @sayeedally8152 4 года назад +1

    kazi nzuri bro,,,, nakubali kazi zakoo

  • @jofreymfugale4752
    @jofreymfugale4752 4 года назад

    Aliondoka na kiungo cha mwili 😃🔥🔥

  • @bonnifacewilly3026
    @bonnifacewilly3026 3 года назад +1

    Daaah huyu jamaa anafanya mziki kwa bongo hakuna tena kama dizasta amani kwako brother

  • @sylvestermtweve2895
    @sylvestermtweve2895 4 года назад +4

    Dizasta..... you're very UNIQUE broo...Mungu akuzidishe maarifa na afya tele just because unajua kutupa Raha mashabiki zako..GOD BLESS TOUR TALENT

  • @harrismalone2316
    @harrismalone2316 4 года назад +1

    Disasta bro 💪 hiphop ngumu ya kiakil na yenye uelewa wa kwel💥💥

  • @franciscojonja1164
    @franciscojonja1164 4 года назад +1

    Asie elewa kazi ya hiki kichwa aisee hatokuja kuelewa milele @dizasta vina ndio nembo ya hip hop isio vunja nguzo ata moja ya hip hop brother umetisha sana

  • @shigangamussa2967
    @shigangamussa2967 4 года назад

    Si Movie kabisa hili la masaa2 kwenye dk7 mzee wangu 💥💥💥 Dizasta eeee We ni Mnooo Aseee

  • @Therealgayakidy
    @Therealgayakidy 4 года назад +1

    Kumamakeeeeee

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha💪💪
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @fanikishashoppingmall
    @fanikishashoppingmall 4 года назад +1

    Hujawahi niangusha brother,,,,,,🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥

  • @flovamanmusic3663
    @flovamanmusic3663 4 года назад +1

    jamaa unajua sana unaandika vizuri sana big up sana kwa kazi nzuri

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      Appreciate, please share and order my album now
      Tigo pesa 0655696811, mpesa 0762158871

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      Appreciate, please share and order my album now
      Tigo pesa 0655696811, mpesa 0762158871

  • @Tobey1988ful
    @Tobey1988ful 3 года назад

    New fan from +254 hapa.... Huyu kaka balaa sanaa dah

  • @clementactor5366
    @clementactor5366 20 дней назад

    USIJIITE MUHUNI KAMA HUMJUI DIZASTA VINA (THE VERTELLER) broo you always teach me many lessons kwa mistari yakoo daaaah

  • @furahinandrew9704
    @furahinandrew9704 4 года назад +1

    We jamaa nomaa

  • @gideonaire_ke
    @gideonaire_ke 4 года назад +2

    kazi safi sana Dizasta

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад +1

      Sijaona order yako brother?

    • @gideonaire_ke
      @gideonaire_ke 4 года назад +1

      @@dizastavina order ya nini bro?

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      @@gideonaire_ke the Verteller ALBUM.. Coming up this Sunday

  • @muddyjumaa604
    @muddyjumaa604 4 года назад +1

    Umetisha sana mzee baba bonge moja la ngoma

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @dullywamashairi121
    @dullywamashairi121 4 года назад +4

    Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi!
    Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina.
    Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
    Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu!
    Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo
    ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @fundi_nyata
    @fundi_nyata 4 года назад +3

    THE VERTELLER!! Wachache watakuelewa na kukusifia!!

  • @nickman4435
    @nickman4435 4 года назад

    Daaah!! Ama kweli wewe ni THE VERTELLER bro,. 👏👏👏👏🙌🙌

  • @aloycemaembe8116
    @aloycemaembe8116 4 года назад +1

    Nmekubar bro salut kwa hii kaz

  • @obeidjoseph3610
    @obeidjoseph3610 4 года назад +1

    Unatishaaa yaaaani hiii ngoma mengne live

  • @balikiabdala823
    @balikiabdala823 Год назад

    🤔🤔🤔🤔 Noma sana ngoma kali sana

  • @ramsmambea2318
    @ramsmambea2318 17 дней назад

    This is my number one hip hop artist in Tz

  • @GerrardTryphorn
    @GerrardTryphorn 8 месяцев назад

    Daaa hiingom Kali

  • @nashonshimba7997
    @nashonshimba7997 4 года назад +1

    Imenitoa machoz hii ngoma mapenz yanauma sana

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

    • @ramadhanally138
      @ramadhanally138 4 года назад

      My broo really umenitoa mazur kweli VINA NI HAFAHI KABISA

  • @directorluganongonya7212
    @directorluganongonya7212 3 года назад +1

    Daaah ! Shikamoo tena

  • @octavianmushi928
    @octavianmushi928 4 года назад

    Brazaaa umegusa maisha ye2 kwa hii ngoma

  • @allymarumbo1088
    @allymarumbo1088 4 года назад +1

    What a lesson..daaaaaah
    We jamaa ni zaidi ya hip hop bro.

  • @saidamour2635
    @saidamour2635 4 года назад +2

    Disasta unaweza sana amini wanakuelewa ila wanabana tu, fans wako tunasubri collabo yako na kaa la moto.

  • @johnkerrysibomana9062
    @johnkerrysibomana9062 2 года назад +1

    Nimerudi hapa baada ya mistari mingi kunigusa na kuendana na ninachikipitia kwenye maisha ya mahusiano

  • @oscarsospeter8034
    @oscarsospeter8034 2 года назад

    Wewe ni mtunzi Huru Dizasta vina God Abless njia zako

  • @emmabelljohn4086
    @emmabelljohn4086 4 года назад +3

    Nomaa sanaa

  • @raphaelhudson9699
    @raphaelhudson9699 4 года назад +1

    Bonge la talent big up ..unazungumza na mimi kama

    • @dizastavina
      @dizastavina  4 года назад

      Thanks, my album is out. Nunua kwa whatsApp au Email kwa namba hizi 0762158871 MPESA au 0655696811 TIGO PESA.

  • @salehekasangas3291
    @salehekasangas3291 Год назад +1

    Umeshushwa.brooo...yan.unajuaa.brooo

  • @aaronjohn9518
    @aaronjohn9518 4 года назад +1

    Deep sana hii ni kama movie

  • @boygavana4674
    @boygavana4674 4 года назад +1

    Dizasta ww sio binadamu wa kawaida aseee haijawahi tokea

  • @raymondtsumah6410
    @raymondtsumah6410 11 месяцев назад +1

    Ogopa mwanamke💔

  • @ombenedwin136
    @ombenedwin136 4 года назад +1

    Mungu ametupaga disaster vina

  • @johnmosha8285
    @johnmosha8285 4 года назад +1

    Makini sana mzee

  • @danchalzndyanabo9200
    @danchalzndyanabo9200 4 года назад +1

    Dizasta vina noma sana

  • @intavides
    @intavides 4 года назад

    daah..💯💯 shukrani sana

  • @ommymsomi4362
    @ommymsomi4362 4 года назад

    Ningekua baraza la sanaa ngomaa zako kaka zingetumika kujibia mitihan kaka...yan wanafunz ningewataka waskize kisha wachambue kila kipengele cha fasihiiiiiii

  • @richardtitus8539
    @richardtitus8539 4 года назад

    Daaah black maradona.. home boy unajua

  • @nafsitukuf7671
    @nafsitukuf7671 4 года назад +1

    Noma sana 🔥🔥

  • @legawayz6093
    @legawayz6093 4 года назад +9

    Hii ni movie kabisa bro one day andaa scripts then simama as diirector naamini itakuwa kazi kubwa BIG UP DIZASTA VINA

  • @kibafteshadau222
    @kibafteshadau222 2 года назад

    Yule dogo raptcha akae mbali....ajifunze kuchana, sio fujo nyingi ....dizasta ni disaster balaa🔥

  • @sabrisaleh1720
    @sabrisaleh1720 4 года назад

    We dizasta fundi ni kweli nikitaka mziki mzuri nimtafute dizasta

  • @hon-mlenga
    @hon-mlenga 7 месяцев назад

    🎶🎶🎶🎶Dizasta nadownlod nyimbo zako zote

  • @pudaboytz4956
    @pudaboytz4956 4 года назад

    Dizasta vina ujawai kosea big ✊✊

  • @ibuibu5247
    @ibuibu5247 4 года назад +1

    jamaa lnajua sanaaa .....

  • @dommie444
    @dommie444 4 года назад +1

    Dah! Hatimae mzigo umeachiwa.
    Hatia IV ni moto

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 4 года назад

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
      Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti
      ruclips.net/video/_vGu4l1MoMw/видео.html

  • @ebramaarifa203
    @ebramaarifa203 4 года назад

    We ni hatari sana bloo🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥

  • @mrundumo1326
    @mrundumo1326 4 года назад

    Namkubali Dizasta

  • @mrcoolboy5475
    @mrcoolboy5475 2 года назад

    Dah hatar sana

  • @bongeone
    @bongeone 4 года назад +1

    🔥🔥🔥🔥🔥🔥elimu kubwa sana hii

  • @mohammedyjshemweta1390
    @mohammedyjshemweta1390 4 года назад

    Daaah jiji lina habar kamil mzee,🙌🙌🙌