SERIKALI YASITISHA ZOEZI LA UKAGUZI WA RISITI KARIAKOO

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 23 июн 2024
  • SERIKALI imesitisha zoezi la ukaguzi wa risiti za Kielekroniki (EFD) na ritani za kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), iliyokuwa ikifanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kupitia mkoa wa kikodi wa Kariakoo, Jijini Dar es Salaam, wakati ukiandaliwa utaratibu mzuri wa utekelezaji wa suala hilo katika Soko Kuu la Kimataifa la Kariakoo.
    Hayo yamesemwa kwa niaba ya Serikali, jijini Dodoma, na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, wakati akitoa maazimio ya kikao kati ya Viongozi wa Wafanyabiashara Tanzania, Viongozi wa Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo na Taasisi zinazosimamia masuala ya wafanyabiashara, kikao ambacho kiliitishwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na kuhudhuriwa pia na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.

Комментарии • 9

  • @ndukulusudikucho_
    @ndukulusudikucho_ 2 дня назад +1

    Safi saana Serikali yetu sikivu

  • @abdull_hafidh
    @abdull_hafidh 4 дня назад +2

    Serekali msipoangalia mkaona wananchi ni wapuuzi kwa kutuongezea kodi kila mkiamka kuna siku watachoka

  • @usafiaps318
    @usafiaps318 День назад

    Mh.Waheshimuni Kwa Kiwango Kikubwa Wafanyabiashara Hawa Wazawa. Hawa Waiteni Mara Kwa Mara Sasikilizeni Sio Kwa Madharau.

  • @hassankongolilo8408
    @hassankongolilo8408 6 дней назад +1

    kuna kijusi kinatutishia uku ata busara halina

  • @mudhihirissa274
    @mudhihirissa274 3 дня назад

    Chalamila hatumtaki mkoa wa Dar es salam

  • @hassanmsangi1155
    @hassanmsangi1155 6 дней назад +1

    Nan kamtuma kwanza chalamila k/koo

  • @CheerfulCakeSlice-po2ht
    @CheerfulCakeSlice-po2ht 4 дня назад

    Yaani kamata kamata itarudi tena!!!

  • @obbybenitho5803
    @obbybenitho5803 17 часов назад

    Mshamba tu chalamila

  • @makelemohuya2723
    @makelemohuya2723 4 дня назад

    Chalamila hasa busara na hekima anakurupuka hovyo hovyo tu kama mganga wakienyeji