"MARUFUKU HOSPITALI KUZUIA MAITI"- RC MAKONDA
HTML-код
- Опубликовано: 26 май 2024
- "MARUFUKU HOSPITALI KUZUIA MAITI"- RC MAKONDA.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amepiga marufuku hospitali za Mkoa wa Arusha kuzuia maiti kutokana na gharama za matibabu na badala yake zibuni njia mbadala za kudai malipo hayo.
Mkuu wa Mkoa Mhe. Makonda ametoa katazo hilo leo Mei 27, 2024 alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli kukagua maendeleo ya Ujenzi wa jengo la mionzi na la upasuaji pamoja na kuzungumza na wahudumu wa hospitali hiyo na kuangalia namna huduma zinavyotolewa hospitalini hapo.
Mhe. Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa na Waganga wakuu wa wilaya zote za Mkoa wa Arusha kusimamia agizo hilo ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alilolitoa kupitia kwa Waziri wa afya.
Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Arusha akiwa Hospitalini hapo amewataka wahudumu wa afya mkoani Arusha kutoa huduma nzuri kwa wananchi wanaofika hospitalini na kwenye vituo vyote vya afya ili kuwa sehemu ya kuwapunguzia maumivu wananchi kutokana na magonjwa yanayowasumbua.
Mhe. Makonda amesema Mkoa wa Arusha unafaa kuwa Mfano wa huduma nzuri za afya ili kuendana na uwekezaji mkubwa wa serikali ya awamu ya sita kutokana na Rais Samia Suluhu Hassan kutoa fedha nyingi za kuwezesha miundombinu bora ya utoaji wa huduma za kiafya.
Mhe. Paul Makonda anaendelea na ziara yake ya Kikazi Wilayani Monduli ambapo pamoja na mambo mengine amepangiwa pia kukagua mradi wa maji wa Kijiji cha NAFCO kabla ya kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara unaotarajiwa kufanyika eneo la Meserani maarufu kama Duka bovu.
Makonda wetu hoyeeee🙏💪
Safi sana Mh Makonda Mungu akubariki sana. Hakika tunajivunia uwepo wako na Rais Samia kukuteua 🎉🎉🎉🎉
T M U
Mungu azidi kuwatangulia, asante mama Samia mama, Mungu azidi kuwalinda wote, uongozi wako na washauri wako...
Makondaa unapambana sana hata kama unachengamoto nyingi sanaaa
Mkuu wa Mkoa wa wakuu wa mikoa yote Tanzania Makonda akiongea
MWENYEZI MUNGU azidi kukupigania makonda.
Kwakweli sio vzr kukataza maiti itoke hosptal kisa pesa
Niukweli, usio pimika kabula makonda hajateuliwa kua mwenezi CCM Nani kiongozi Alie jitwika jukumu la kuwasikiliza WA tz kama sio makonda, halihii tukua tunaiona kwa magufuli pekee
Safi sana. Nakushauri uandike mwongozo upelekwe hospitali zote. Vinginevyo ukiondoka tu, yamekufa. Au ichagize Wizara ya Afya iandike mwongozo huo kwa hospitali zote za serikali na binafsi, na adhabu ya asiyefuata.
Kuna namna nyingi za kistaarabu kuwadai wafiliwa. Kwa mfano, kuwauliza wana uwezo wa kulipa kiasi gani kila mwezi (kama wafanyavyo huku Ulaya watu waliostaarabika). Pia anzisheni bima za mazishi au katika bima ya afya include hiyo (lakini msiwawekee watu kulipa laki mbili kwa mwezi. Elfu tatu kwa mwezi tosha). Of course, itatazamwa mtu anaikata wakati gani, siyo yuko mahtuti .....
Mambo mengi Tanzania yanasababisha usumbufu kwa wananchi kwa vile watendaji wengi hawana/ hawatumii akili tu.
Nakubaliana nawe!mtu Kesha kufa ..daini hizo 3000 kila mwezi hata miaka 3..potelea mbali lkn siyo kuzuia maiti?
Makonda atakuja kifitiniwa maana kashawafunika wengine sasa tusubiri tuone
Arusha mshukuruni mungu kuwaletea mwamba huyu
Ilo kwel
Makonda wape somo hajuwi kitu viongozi wa arusha
Kwakweli Makonda anajitahidi, hakuna mkuu wa mkowa anaefatilia matatizo ya wananchi wamkoa wake km huyu mtumishi wa Mungu,,
😭😭😭😭😭🙏🙏🙏🙏🙏
Mbona ilikuwa Ni shida sana Ni Kwa nini wanganganie maiti ?
Twayeeeeeb ❤
raisi ajae mbeleni
Rais ajaye baada ya mama
Hyo turizika chato hakuna daktari au muuguzi mwenye tabia nzuri saiz ukienda hospital za serikal awamu hii nisawa na kusaini hati ya kifo
Kabisa
pongezi kubwa kwako binafsi
Makonda rais jerry silaa waziri mkuu = Magufuli ( hapa kazi tu)
T M U chini ya uongozi wa mama Samia na Serikali yake, sisi wanyonge tuko nyuma yenu kwa maombi kila mmoja kwa imani yake,
Mtu ambae hajapitia hayo Makonda na timu yake wanayafanyia kazi katu hawatamuelewa!!
Lkn upo usemi usemao mwenzio akinyolewa .......
🫡🇹🇿
Kiongozi wa hovyo
Kwakusema maiti zisitozwe hela kwa wananchi wasio na uwezo au?
Ww ndio wahovyo huna akili hata kidogo
MAKONDA, HONGERA TWASHANGA HOSPITALI ZOTE NCHINI TZ ZINAZUIYA MAITI WAKATI DADA UUMI ALIKATANZA KUZUUIWA MAITI LAKINI BADO WANAZUIYA TATIZO NN
AMRI BILA KUPELEKA BARUA INAYO ELEKEZA HLO.HYO TUNAITA SIASA.
Kwa hiyo uambiwe itapopelekwa barua amri zoote zitolewazo hutoka na barua
Huelewi wewe.
HIVI unadhani Makonda anafanya siasa!!
Ww jinga
Makonda piga spana watu waby sn
Mmesikia alichosema waziri au hamjamsikia na Kila AMRI unakuwa na barua hakuna AMRI bila barua, tukiangalia kwa majini ni siasa vipi AMRI aliyoitoa kumhusu yule mdada Sabrina ilitekelezwa au alienda kulimwa talaka