Kufungua Akaunti ya Uwekezaji ya UTT AMIS: Hatua kwa Hatua
HTML-код
- Опубликовано: 4 окт 2024
- Uwekezaji katika mifuko ya pamoja ni rahisi kuliko unavyofikiria. Ni njia nzuri ya kukuza mtaji kwa wale wenye malengo ya muda mfupi, kati na ya muda mrefu.
Mifuko hii ni aina ya uwekezaji wa pamoja ambayo inaruhusu wawekezaji walio na malengo sawa kuwekeza fedha zao kwa pamoja kwenye jalada la dhamana au mali zingine.
Wawekezaji (wenye vipande) hawamiliki dhamana hizo za mfuko moja kwa moja. Umiliki wa mfuko umegawanywa katika umiliki wa vipande. Kadiri mfuko unavyoongezeka au kupungua kwa thamani ndivyo thamani ya kipande huongezeka au kupungua ipasavyo. Idadi ya vipande inategemea bei ya ununuzi wa kipande,wakati wa uwekezaji na kiwango cha pesa kilichowekezwa.
Kawaida, faida ya uwekezaji kwa wamiliki wa vipande hupatikana kwa mfumo wa gawio la mapato na kukua kwa mtaji, inayotokana na uwekezaji wa pamoja. Kila kipande kinapata mapato sawa, yaliyotokana na kiwango kilichowekezwa kama mtaji katika kipindi chochote.
Uwekezaji katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja, huhamisha utaalam wote wa uwekezaji kwa wale wenye uwezo wa kusimamia masuala ya uwekezaji na hao ndiyo sisi, UTT -AMIS (Wasimamizi wa Mfuko)
soma zaidi
"Uwekezaji wa pamoja kwa muhtasari | DHAMANA YA UWEKEZAJI NA USIMAMIZI RASILIMALI TANZANIA" www.uttamis.co...
Kama tayali Nina vupande vya utt nifanyeje ilikupata taarifa zangu.
Asanteee kaka
Ahsante sana
Tunashukuru kwa elimu
Shukran kaka
Je naweza jiunga utt nikiwa nje ya Tanzania?
Thanks bro
Msaada nimedeposit ile initial deposit ya liquid fund 100k lakini kutumia nmb yangu lakini ni kicheck balance inaonyesha 0
Na kama umeshafungua form unataka kufungua account simu yangu app unafajanje
Form zipo nne naomba unielekeze namna ya kuzijaza
Nikiweka namba ya simu hawaleti taarifa kama nimefungua akaunti mbona?
Jmn mbona mim kila nikifungua haifunguki wala acount siipati
Hatua kwa hatua
Anaeielewa hii elimu naomba maarifa
Elimu zaidi kwenye vipande nenda utube kasome zaid
Mmmh hakuna ujanja ujanja
Naweza kufungua Account mbili kwenye App Moja?!
Ndio inawezekana kama ni mifuko tofauti, au iwapo utatumia line mbili tofuati
Mimi nimeweka 100000 na nimepoteza ile namba na sijafika ofis zao je nikienda bila namba nitakubaliwa
Namba ya akaunti?kama ni ya akaunti sio shida tumia namba yako ya simu kupata namba yako ya akaunti
Huyu muhun
Kwa Dar ofisi yao ipo wapi
Sukari house posta
Kwa mfano mm nipo simiyu nikienda crdb wananikamilishia usajili
Ndio ,popote ulipo Tanzania,pakiwa na tawi la CRDB unakamilisha usajili
M nimeenda crdb wameniambia hawaungi watu wakanipa namba 150*82 sa sielew@@ElimikaMtandaoni
Mimi nikifungua akaunti wanasema niweke namba ya simu niliyojisajiri,
Ndio namba ya simu ni muhimu ,maana akaunti yako itahusianishwa na namba yako ya simu
Na ukienda crdb pia wanakusaidia kukamilisha form sindio
Ndio utasaidiwa
Mbona account haifunguki?
Na mm nimejaribu haifunguki
Mh
Dah ingekuwa rahisi sana kama mtu unajifungulia account mwenyewe pia unakamilisha mwenyewe sio mpaka kwenda kwenye mabenk au kuna namna?
unaweza kuingia kwenye website yao, www.uttamis.co.tz download application form then unawatumia kwenye email uwekezaji@uttamis.co.tz
KYC ni muhimu ,nadhani watafanya namna ya kuiwezesha KYC online kama ilivyo kwa soko la hisa
Mbn kwenye website yao haionyeshi application form?
www.uttamis.co.tz/forms/scheme_account_opening_form
Asante kwa maelezo. Je mfano mimi nina account NMB bank nikishajaza form na kuwatumia online nikitaka kuanza kuchangia naweza hamisha hela kutoka NMB na kutuma huko UTT Amis au naweza kutuma kwa kutumia mfano mpesa au tigo pesa km namba ya simu niliyoandikisha wakati najaza form?