TFRA YAWATAKA WAZALISHAJI WA MBOLEA KUTUMIA MALIGHAFI ZINAZO PATIKANA NCHINI

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 5 окт 2024
  • TFRA yawataka wazalishaji wa mbolea
    kutumia malighafi zinazopatikana nchini
    DAR-Wazalishaji wa mbolea nchini wametakiwa kutumia malighafi za kutengeneza mbolea zinazopatikana ndani ya nchi ili kupunguza gharama za uzalishaji kwa kuagiza malighafi hizo kutoka nje ya nchi.
    Wito huo umetolewa leo Oktoba 3, 2024 na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent alipofanya ziara kwenye kiwanda cha kuchanganya mbolea cha kampuni ya mbolea ya Yara Tanzania kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam.
    Akieleza lengo la ziara hiyo, Mkurugenzi Laurent amesema, ni moja ya majukumu ya mamlaka kutembelea wadau wake ili kujiridhisha na uwezo wa uzalishaji wa viwanda vilivyopo nchini.
    Laurent amewataka waingizaji wa mbolea nchini kuwekeza katika viwanda vya kuchanganya mbolea ili kuwawezesha wakulima kupata mbolea inayoendana na mahitaji ya zao pamoja na aina ya udongo unaolimwa na si kutumia mbolea kimazoea.
    Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mbolea ya Yara Tanzania Limited, Winstone Odhiambo amesema, kampuni yake inajikita katika kuzalisha mbolea kulingana na mahitaji ya wakulima ili kuhakikisha wakulima wanapata pembejeo hiyo kwa wakati na ubora unaokubalika kimataifa.
    Amesema, mpaka sasa wamewekeza kwenye mitambo miwili ya kuchanganya mbolea yenye uwezo wa kuzalisha tani 120 kwa saa na hivyo kuwahakikishia uwezo wa kuzalisha tani 720,000 kwa mwaka.
    Kwa upande wake Meneja wa kiwanda, Santus Chonya amesema, wanazalisha aina mbalimbali za mbolea kulingana na mahitaji ya wakulima wanayoyabaini baada ya kupima udongo na kujua mahitaji ya virutubisho yanayolingana na aina ya zao linalilimwa.
    Amezitaja mbolea hizo kuwa ni micro planting (mbolea ya kupandia), micro mbogamboga,micro top (mbolea ya kukuzia) na micro tobacco zinazofanya kazi vizuri kwenye mazao yaliyokusudiwa.
    Naye Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Ndani na Ununuzi wa Mbolea kwa Pamoja wa TFRA, Louis Kasera ameeleza kuwa, ziara hiyo inaipa picha halisi Mamlaka ya kutambua uwezo wa viwanda vya ndani katika kuhudumia wananchi wake kwa kuwafikishia pembejeo hiyo kwa wakati.

Комментарии •