MALANGO YA NDOTO YANAVYOTUMIKA NA ADUI (II) - PASTOR SUNBELLA KYANDO
HTML-код
- Опубликовано: 30 сен 2024
- Mathayo 13:24-26
[24]Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
[25]lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
[26]Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
Mpanzi alienda kupanda mbegu lakini adui alisubiri wakati wa usiku naye akaenda kupanda uharibifu.Adui huwa anasubiri wakati umelala(wakati ambao umetulia,hujui chochote kinachoendelea) ndipo wakati naye anakuja kupanda vya kwake.
Neno linasema kuwa majani ya ngano yalipoanza kumea ndipo wakagundua kuwa kuna magugu pamoja nayo.Ngano haioti kwa siku moja,mpanzi alikuja kugundua kuna magugu baada ya muda kupita.
Kumbuka adui alipanda magugu lakini hakusubiri yaote,alipomaliza kupanda akaondoka lakini madhara ya hiyo mbegu yalikuja kuonekana baada ya muda kupita.Ndio maana shetani anaweza kuzuia mwanamke kushika ujauzito toka akiwa mtoto mdogo lakini madhara ya hii mbegu inakuja kuonekana anapoingia kwenye ndoa na anapohitaji mtoto,hapa ndipo anakuja kugundua kuwa kuna ambacho sicho cha kiMungu kimepandwa.
Ni vizuri sana kutafuta kujua kama kila kitu kipo sawa kwenye maisha yako,unaweza kuona kuwa hakuna tatizo kabisa kwenye maisha yako kwa sababu tu bado magugu hayajamea.Kaa vizuri na Mungu naye atakuonesha mahali penye pando ambalo silo lake na atalitoa.
Katika ibada ya hii ambayo iliongozwa na Mtumishi wa Mungu Pastor Sunbella Kyando tulijifunza kuhusu namna adui ambavyo anatumia sana muda wa usiku kupanda uharibifu,na Jumatano ijayo tutakuwa na maombezi juu ya kuondoa kila pando ambalo silo la Mungu kwenye maisha yetu.
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our RUclips: www.youtube.co....
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz
Be blessed mtumishi
Am going to be good mapenzi ya Mungu yatimizwe🙏🏻
God bless u Pastor 🙏🏿
Thanks jesus😢🙏
One of the best teacher....
Pasta mungu akupe haja ya moyo wako ili tuendelee kujifunza hakika toka nimeamuamua kukufuatilia nimemuona mungu ktk maisha yangu amen
Wapenzi wenzangu wale hatuko tanzania tuna wasiliana vipi na hii kanisa
Mungu akubariki sana mtumishi
A good teacher through him I have learned alot
Amen ,God bless you man of God I have learned so much from you.
Nabarikiwa sana na mafundisho ya Reality Christ kupitia RUclips, Mungu ibariki Madhabahu ya Reality Chini kiongozi Mtushi Sunbella na wengine wote Mungu na awatie nguvu jamani kabla sija sahau naomba Ratiba yapo Kanisani.
Amen.Tuna ibada kila siku ya Jumatano kuanzia saa kumi na moja jioni, Ijumaa kuanzia saa kumi na moja jioni na Jumapili kuanzia saa tatu kamili asubuhi.Pia tuna ibada Dodoma kila siku ya Jumatano kuanzia saa kumi na moja jioni pale ukumbi wa Dear Mama, Area C njia panda ya kuelekea Arusha.
Karibu sana.
Aaaamen
Ameeen mtumishi be blessed ,nauliza hivi ,mimi huwa napenda kupeana sana mtu akihitaji msahada kwangu ,,,,,but me kupata mtu wa kunisaidia huwa sipati ,,,so nashindwa sana naomba unielimishe hapo
Mmh. wewe n Mtu Mzuri Sanaa
Mtumishi nina shida ya kuongea na wewe niko mtwara nimeokoka nampenda yesu nimesikiliza mafundisho yako nikaona naweza pata msaada kupitia wewe, hivyo kama nikipata kibali machoni pako na kwa bwana naomba msaada wa mawasiliano yako nikueleze matatzo yangu, asante sana mtumishi wa bwana mungu akupe mafunuo zaidi
Uko sahihi mtumishi nashukuru kulifahamu hili kuna nyakat mchana napata hofu sana lkn sikujua kama spiritual situation ucku nkiwa nmesinzia tu nkasikia kama jitu kubwa limeingilia dirishan likanikalia mgongon nkajaribu kupiga kelele saut haitoki nakemea haliondoki baada ya mda ile hali ikaondoka nkashtuka usingzn pastor huwezi amin ilikuwa halisia nlijawa na hofu San kiasi kwamba nlishindwa kulala tena, nashukuru sasa najua mamna ya kudili navyo
Amen, asante baba kwa mafunuo haya, asante MUNGU kwa kutupa mtumishi Sunbella. Jina lako litukuzwe milele Jehova.
Niulize unapo tuma sadaka nilazima mtu aweke code ukituma ukiwa Kenya..
Sio lazima ila ikikataa jaribu kuanza code ni +255
Woow!!!Jamani this man is blessed.I am learning so much
Mungu wetu akubariki sana baba. Kanisa lipo wapi kwa Dar?
Kanisa lipo Sinza Mori karibu kabisa na ofisi za TAMWA.Karibu sana.
Nimebarikiwa Sana
Njoo mpk sinza mori ukitokea shekilango mkono wa kulia kuna barabara inanyoosha mbele utakutana na geti jeusi imeandika tamwa pemben ake utaona kanisa
napata maarifa kila sku kupitia mafundisho yako Mungu akuinue zaidi
Amina baba
Mtumishi ninakuelewa Sana,napokkea kufunguliwa
Nimebarikiwa Sana na mafundisho yako , naimani Mungu atanisaidia
Amen
Amina
Mtumishi samahan naona kama imerudia ile ile ya kwanza au
Zipo mbili, sehemu ya kwanza na sehemu ya pili.
dah ahsante sorry mtumish kumbe zote nliziona ila nikasahau leo nukawa nmeona kama hii yote nimoja kwasababu nlikua naham sana kuiona inayofuata hii nmeifuatilia yote juzi nlipoona leo nikadhani ndo iliyofuata baada yapale nlipoishia ubarikiwe mtumishi
nnacho mshkuru Mungu kuhusu huduma yenu nikwamba kwaupande wangu naona nimuujiza sana kwasababu kipindi chanyuma baada yakuokoka nliwah kufunga nikimsihi Mungu anijaze Roho mtakatifu nipate wepesi kwenye wokovu lakini mpaka mwisho wamfungo sikuona nlichokua nakitafuta ila wakati napita pita RUclips nikaona mafundisho yako nikakuta nayaelewa isivyokua kawaida yani kutoka hapo haziwez kupita siku mbil sjafuatilia mafundisho yako wala sijadownload video zako yani ukifundisha kilasomo linanigusa sana na ndivyo lilivyo katika maisha yangu ubarikiwe saana sana mtumishi neema uliyonayo izidi kuwa hivo hivo isipungue mpaka hapo nmeamini kua Mungu ili atende kazi anatumia watu hashukagi yeye kama yeye kutufundisha kikubwa tu sisi nikumuomba kama vile mimi niliomba Roho mtakatifu awe mwalimu anifundishe sir zaufalme wa Mungu hakika sasahivi namimi pia naenjoy sana wokovu hata nikiskia jehanam na mbinguni hatuendi lakin siwez kuacha wokovu kupitia mafunzo yako misuli yangu yaimani imekua imara sana Sunbella mwalemi sana 👏👏👏
@@yustinmbilinyi671 Amen Amen,Mungu azidi kukubariki sana na kukufanikisha.
@@realityofchristchurch ubarikiwe mtumishi kwa Mara ya kwanza nimekusikiliza leo najuta kwa nini sikukusikiliza mapema, ushuhuda wako umenigusa natamani kuongea nawewe nakupataje
tuned
Amen Halelujah
AMEN
Amen
Uko sahihi kabisa baba
Mtumishi naomba no yako kama hutojali. Ubarikiwe sana.
Hallelujah