RAIS DKT. MAGUFULI ATOA MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU BEI YA KOROSHO NCHINI 2018
HTML-код
- Опубликовано: 10 фев 2025
- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 28 Oktoba, 2018 amekutana na wanunuzi wa zao la korosho na kutoa msimamo wa Serikali kuhusu bei ya zao la korosho kufuatia kuwepo kwa mvutano wa bei ya zao hilo kati ya wanunuzi na wakulima.
Mhe. Rais Magufuli amekutana na wanunuzi hao katika mkutano wa majadiliano uliokuwa ukiendelea kati ya wanunuzi wa korosho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Katika msimamo huo Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inaungana na msimamo wa wakulima kukataa bei zilizotolewa na wanunuzi katika mnada uliofanyika hivi karibuni ambapo kampuni za ununuzi wa korosho zilitangaza kununua korosho kwa bei ya kati ya shilingi 2,717/= na shilingi 1,900/= kwa kilo ikiwa imeshuka kutoka zaidi ya shilingi 3,600 ya msimu uliopita.
Mhe. Rais Magufuli amesema endapo wanunuzi hao hawatakuwa tayari kununua korosho kwa bei isiyopungua shilingi 3,000/= kwa kilo, Serikali ipo tayari kununua korosho kwa bei yenye maslahi kwa wakulima na kutafuta masoko yenye bei nzuri.
“Kama hamtanunua korosho kwa bei yenye maslahi kwa wakulima, Serikali itanunua korosho kwa bei nzuri kwa wakulima na tutaihifadhi, nipo tayari hata kutumia majeshi yetu kununua korosho na tutatafuta masoko ya uhakika ili tuuze kwa bei nzuri” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Wakizungumza katika mkutano huo, wanunuzi wa korosho wamekubali kununua korosho kwa bei isiyopungua shilingi 3,000 kama ilivyoelekezwa na Serikali na wameomba baadhi ya tozo zinazosababisha kupungua kwa bei ya zoa hilo kwa mkulima ziondolewe pamoja na kuruhusiwa kusafirisha korosho kupitia bandari ya Dar es Salaam ambako wanaweza kupata meli zinazotoza gharama nafuu za usafirishaji wa korosho kwenda kwenye masoko ya nje ya nchi.
Mhe. Rais Magufuli amekubali kuondolewa kwa utozaji ushuru wa mara ya pili wa ushuru wa halmashauri uliokuwa ukifanywa baada ya korosho kufikishwa Mtwara, kupunguza ushuru wa Bodi ya Korosho kutoka shilingi 17/- hadi shilingi 10/- kwa kilo na ameruhusu wafanyabiashara kununua magunia yao wenyewe kwa ajili ya korosho badala ya kuuziwa na vyama vya ushirika kwa bei kubwa.
Kuhusu bandari ya kusafirishia korosho Mhe. Rais Magufuli amekubaliana na maombi ya wanunuzi kutaka kusafirisha korosho kwa kutumia bandari ya Dar es Salaam ambapo kilo moja inasafirishwa kwa shilingi 47/- kwa kutumia meli ambazo zimeleta mizigo mingine ikilinganishwa na bandari ya Mtwara ambako kilo moja inasafirishwa kwa shilingi 203/- kwa kutumia meli zinazokodiwa kwa ajili ya kubeba korosho tu.
“Bandari ya Mtwara na bandari ya Dar es Salaam zote ni bandari za Serikali, mimi sina tatizo na kusafirisha korosho kupitia bandari ya Dar es Salaam lakini na nyinyi muwe tayari kutozidisha uzito kwenye magari mnaposafirisha kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, kutotorosha korosho na pia kutimiza masharti ya usafirishaji” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Ameagiza Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuweka utaratibu mzuri utakaowezesha usafirishaji wa korosho hizo kupitia bandari ya Dar es Salaam kama ambavyo wanunuzi hao wameomba.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka wanunuzi hao kuwekeza viwanda vya kubangua korosho ama kuwahamisisha washirika wao kuja kuwekeza katika viwanda hivyo na kwamba Serikali itaunga mkono juhudi hizo ikiwa ni pamoja na kuweka vivutio vya kikodi.
Mh.Rais,simamia maslahi ya wanyonge, hata mimi niliamini lazima utaliingilia Kati TU, wewe ni Rais wa mfano duniani sio tu Tanzania .mungu akulinde Sana na akupe maisha marefu.amin.
Raisi wangu, Mungu akulinde na akupe umri mrefu utuongoze miaka mingi, aaaaamin, asante baba
Hbdy to you Mr presidaaaa
Nimeiona hasira yako Mh. Rais ukiona wananchi wako wanataka kuonewa Mungu akubariki. Nikutakie tu heri ya siku ya kuzaliwa Mungu akupe maisha, siku moja nitakuwa kiongozi na nitakuwa na nitaongoza kwa mfano wako na Nyerere,
This man is a true and patriotic leader and above all he is absolutely genius
Definitely, you are really true
Mh Rais wetu JPM wewe ndie Rais muwazi,mkweli mchapa kazi, mtetezi wa wanyonge na unaetoa mwelekeo sasa wananchi wako.Mungu akupe maisha marefu Mh JPM. HAPPY BIRTHDAY RAIS WETU.
Nilikuwa mpinzani sana ila wewe ni rais unaejielewa sana nakupenda sana
Baba umenifurahisha sana asante sana mzee baba😂😂😂wanakuletea ujanja hapa wakat zao hili lina kazi c ya kitoto..... Hao wahindi wanajifanya wajanja wakat wao wenyewe ni middlemen pumbavu zao
Asante magu baba
Korosho yetu itanunuliwa tu alhamdulilah 👏👏👏👏👏👏👏
😭Kwenye direcrion ya Mzee Ukilaza unaondoka.
Rais 2020 usihangaike kuzunguka tena kupigakampeni tunakupakula mpaka washangae
Sikukupigia kula ila hakika unanidai kula yangu 2020 nakpenda huna mpinzan
Mungu atupe nini, this is the best president ever. Endelea kutawala hadi uchoke mwenyewe,hakuna shida,tunahitaji Maendeleo na wewe unatuletea maendeleo na pili ww n mtetezi wa WANYONGE. Nani kama Magufuli ,We love you our President, you're doing what every well minded Tanzanian needs. Rule even 40 years,we still need you.
Chapa kazi ,HAPA KAZI TU.
Enzi Za Mwl. JK. Nyerere tulisema UHURU NA KAZI sasa tunasema HAPA KAZI TU BIG UP MY PRESIDENT
Ongela
Raisi wangu umenifurahisha sana,hakika unafanya kazi ya kutetea wakulima tz.
Mheshimiwa Rais nakuombea mema asante sana Mungu akupe maisha
Sina cha kuongeza muheshimiwa Rais wangu..mwili unasisimka kila ninapokusikiliza , unayawakilisha mawazo yangu. Mungu akulinde na kila wabaya na aina ya ubaya! Pamoja tutaijenga Tanzania.
Nimejialika,..! Hehee umetisha mzazi
Asante rais wetu kwa kuwapigania wakulima ..... Mwenyezi Mungu azidi kukuongoza
Siku zote haki ikisimama malaghai wengi huumia sana wakati mwingi wanatafuta sehem wakosoe na si kutoa ushirikiano kwa yanayotendeka mh jpm pambana zid ya wanyonge usiwasikilize watakao kukatisha tamaa pambana zaid ya hapa ulipo yupo atakaye kulipa nayeye ni mwenyez mungu si mwanadam Mungu akujalie miaka mingi ili uitetee tanzania na fahari zake
Mweshimiwa rais alipo xema tuzae alikuwa anamanisha angalia nchi zote zilioendelea zina watu wengi xana angalia apo wahindi wengi na angalia kwetu kira sehemu kuna duka la muyindi mweshimiwa anaona mbali xana mungu amuongoze katika majukumu yake 👍👍👍👍
Hiki kichwa nihatari kinajua mambo mengi sana
Daah! Mheshimiwa Rais sina cha kuongezea, Mungu akubariki sana
Asante sana kwa yote unayoifanyia nchi yetu ..... Kipekee kabisa napenda nkushukuru kwa ujenzi wa barabara ya Mpemba kwenda Ileje unaoendelea .... Asante sana mh rais
Hakika MUNGU alikuleta kwa kusudi maalum ubarikiwe sana
I miss you Mangufuli. Rest in peace ✌️ byou are my hero up to now from Kenya 🇰🇪
Wanaompinga Mh, JPM watapata tabu sana maana utendaji kazi wake umetukuka sana. Hongera sana JPM, juhudi zako tunaziona,tunakuunga mkono na tunakuombea Mungu akubaliki.
Ila kumbe kuwa Rais si masihara. Nikisikiliza namna JPM anavyoongea kwa details na uelewa mkubwa wa mambo, najiuliza haya alijifunza lini. Anaongea vitu very technical kwa kweli.
Mungu akubariki kwa kuwa mzalendo wa Taifa letu tunakuombea sana wana nchi wamenyonywa sana
Yaani nikimsikia Rais wetu mpendwa John Pombe Magufuli natokwa na machozi kwa furaha. Kweli ni zawadi toka kwa Mungu.
nakuelewa sana baba magu thanx maana kuongoza ni kazi sana baba piga kaziiii
Rais wangu nchi yangu.
Haya tunayoyaandika tunatamani uwe unasoma mwenyewe ha ha ha
Kiukweli Raisi wangu unawapigania wakulima wanyonge kwa kiwango kikubwa sana
Tatizo watu wako (watendaji)wanakuangusha.
Haya mambo sasa ulitakiwa baada ya wewe kulipigia kelele mwaka Jana ilitakiwa sasa upumzike .wanakutesa sana sana.
Lakin tutafika tuu.
Good job JPM
mzee umenifurahisha speech yako yale,
Mungu akulinde maana wewe ni mtetezi wa kweli
The best leader in Africa
Mungu akulinde Mh.Rais
Nyerere II in the house.
mzee hongera sana jitahidi ufike maswa wananchi tunatahabika maji ayatoki wilaya nzima wiki ya tatu sasa fatilia mzee maji ni uhai
Ni kweli kabisa nmetka juzi huko tabu tupu
Nakupata vzur MH.Rais kutoka masharik ya kati kimsing hao wengi madalali huwa wanataka supernormal profit hayo matatzo mengi yako hata kwenye zao la ufuta na mazao mengine ya biashara
Asante baba jkt na majesh yetu yote hata kwa mdomo👏👏👏👏😂😂😂😂
Happy birthday Mr.President
Kwaajili ya maendeleo yanchi yetu huyu baba alizaliwa mungu ulitupa Bure zawad ya jpm mlinde muongezee muda waungozi siku kwasikuamina
Mnaenda kununua au hamuendi
This is the Man of Yes and No, no mbambamba
Ukisikia Raisi basi ndio huyu.
Mungu Akuzidishie Hekima Na Maarifa Raisi Wetu
mzee tunakukubali,we ni Rais wa wanyonge,asiekubali akafie mbali,
Huyu ndie aliekapaswa akabidhiwe nchi km alivyokabidhiwa rais wa China mpk afe
mahindi nayo vipi ndo basi tena mweshimiwa
Hahahaaaaaa, jkt. Mtabangua korosho kwa mdomo Kweli, chezea jembe we! Hakika Mh. Rais. Unakonga mioyo ya wakulima Mungu akuongoze baba.
haki ya Mungu ingekuwa ni amri yangu huyu Rais angeendelea angalu hata miaka ishirini maana kumpata kama huyu tena ni mtihani japo nina amini wapo ila kumpata ni shughuli kubwa.
VIVA magufuli VIVA
Bravo JPM
What a great president!
Hadi Bodyguard ametabasamu!!! Heshima yako mzee Magufuli
Hongera sana mkuu,
Huyo ndio mh. JPM, my favourite president
Mr Prisedent anglia uwezekano wa shirika la Tanganyika perkas yale maeneo ni muhimu sana kwani yamesahaulika kwa muda mrefu sana
Nawaza cha kufanya ili kukuongezea muda wa uongozi. Hakuna namna
ohooo hii ya kubangua kwa mdomo tusiende kichwakichwa asije akaangiza watanzania wote wabangue kwa mdomo
Ibadilishwe tu katiba ya Tanzania uwendelee mbaka kuzeeka kwako ayupo mwingine wa kuvaa viatu vyako
This is my president. ..
Mwenyez MUNGU yupo pamoja nawe raisi wetu
Good Mr president"
Kweli kabisa wakilaza = kilaza, fukuza tu, hata hii bodi jipu tu, watu wanunue tu hata wauza dagaa wanaweza jalibisha biashara ikiwashinda watavulia samaki
Hongera mtetezi wa wanyonge
Yessssssssssssssss assessed tanzaniaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
mungu akulinde siku zote!
🔥🔥🔥🔥
Jpm ever domination...we love u mo
Mr president anaijua korosho
Rais wa wanyonge
Nakuelewa Sana Kiongozi
BABA DUNIA ZIMA INAKUTAMANI UJUE UNA MADINI YASIYOISHA ALIKUZAAA ANASTAILI SIFA ZOTE
DUU HATUWEZI PATA TENA MTU HUYU MIMI NASEMA
HATA AKIPATIKANA ATAFIA TUU JANGWANI MAANA NCHI WATU KARIBIA WOTE NI WATUMWA WA WA WATU WEUPE TUU
My President big up
safisana
Raisi bora wa muda wote
😂😂 hata kwa meno jesh litabenguaa korosho..
Hakika huyu ni mtetezi Wa wanyonge. Kongole Rais.
Hongera waelemishe
baada yale kuongelea issue anazunguka kross
❤❤❤❤❤❤❤❤❤🎉🎉🎉🎉🎉
Kweli ulisema tutakukumbuka kweli nakukumbuka sasa
Ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kuyapa nguvu majeshi yetu yote ewe mwenyez MUNGU mkuu
jamani acheni siasa tunataka ela hadi mwezi wa kumi na mbili hatujapata ela kama hela haipo wapeni wahindi wanunue
good president
Nawapongeza sana Ikuilu mawasiliano pia kwa kuanzisha vyombo vyenu vya habaria na kwenda na wakati kama hivi mana hao waandishi wa TZ wengi tumeshawashtukia washanunuliwa na magaidi wa mabepari, wanakimbilia kutangaza habari za kuvuruga nchi zaidi kuliko habari za kuikomboa nchi. Watu wa hivyo wote wachunguzwe na wanyang'anywe uraia, tunataka watanzania wanaoitetea nchii kama Rr. Magufuli sio kuteketeza nchi na Wananchi.
Wale wanao jiita wapinza huwa hawakosi kukosoa watatia ujuaji wao et wao ndio wanajua ,upinzani huu ni chuki matusi na lawama ,zito atakosoa tu
Pongezi ziende kwa John
Mbele itabaki kuwa mbele tu speed hainashida nakuunga mkono raisi wangu hata kama tunaspeed ndogo naamini mbele tutafika tu HAPA KAZI TU
Leo ih atupo nawewe Jpm pumzika kwa Amani
Hongera President hili ndo tulikuwa tunalitaka kwa wananchi fukara
Kina "Kemcho" hapo wanachanganyikiwa 😃😃thumb up jembe!
Piga kazi Mr President, Watanzania tupo pamoja nawe
Mheshimiwa tunaomba tuangalie upande wa mbaazi hali ni mbaya kilo mia mbili 200 mkoa wa manyara
43:50 😅😅
Hakika huyu ni raisi mtetezi wa wanyonge mungu azidi kukulinda mkuu.
Ndomaana 2nakunda Rais. Jpm
Nmeona mzee mmja kama haelewi kabisa,hahaaaa
Ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kumuongoz kumsimamia kumrindi na kuzidi kuimalisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU pia enderea kuwaongoza vyema viyongoz wete wanaomsaidia raisi wetu turiongoza taifa retu
Uko vizur baba piga kazi
Hicho kichwa kaa nacho mbali
Happy birthday mzee wa kaz
😀😀😀
Tawala miaka yote Magufuli, hadi hao majambazi wa mabepari wakimbie nchi, kwanza wote wale sio Watanzani wanatumwa kuivuruga nchi. Kwa mwendo huu uwezo wa kuiendesha nchi unao hata bila msaada wa wanyonyaji wa nje, sisi hata njaa tutalala mradi ututoe utumwani, kunyonywa Tanzania ibaki kuwa historia, unaonesha njia ambayo wengi walishindwa kwasababu walikwamishwa na kuwaogopa hao wahalifu wa mabepari. Magufuli oyeee
nitaasisi maandamano ya kupinga kuondoka madaraka kwa anco magu bado tunakuhitaj
ndo uzuri wa
kuchagua rais msomi huwezi kumdanganya.
Natamani nione jinsi jeshi linavyobangua korosho kwa meno.. Lol
kama nikijana alafu huumpend magufuli inabidi ukapimwe akilii
👏👏👏👏😂😂😂😂😂👏👏👏👏
kigeugeu
chuma hiyo