KAMA UNATAKA KUFUGA NYATI MAJI 'MILANGO IKO WAZI NJOO UCHUKUWE MBEGU SERIKALINI'

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 25 дек 2019
  • Shamba la Mifugo la Mabuki lililopo wilayani Misungwi mkoani Mwanza lilianzishwa mnamo mwaka 1966 baada ya Uhuru wa Tanganyika kwa ajili ya kuzalisha F1, hii ilikuja baada ya kugundua kuwa wafugaji wachache waliopewa ng’ombe wa kisasa kutoka Ulaya, wengi wao walishindwa kuwamudu wakafa ndipo wataalamu wa Mifugo waliokuwepo enzi hizo wakaona ni vyema kuzalisha ng’ombe wa maziwa wanaoweza kuhimili mazingira ya nyanda za nchi zenye joto ikiwemo Tanzania.
    Shuhudia ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina akizuru Shamba hilo la Mabuki kama sehemu ya mwendelezo wa Agenda ya Kitaifa ya Utafiti wa Mifugo, Uvuvi na Ukuzaji viumbe kwenye maji 2020 - 2025 ambapo pia amepata fursa ya kuwaona Nyati Maji wanaofugwa kituoni hapo, mbegu iliyoingizwa nchini enzi za utawala wa Rais wa Kwanza nchini Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere.
    Kwa wale wanaotaka kufuga Nyati hao, kitambo sana Serikali ilishafungua milango.
    TAFITI ZA AWALI.
    Kwa tafiti za URT za Mwaka 2015, Tanzania inashika nafasi ya pili kwa wingi wa mifugo barani Afrika ikiwa na ng'ombe milioni 25, mbuzi milioni 16.7, kondoo milioni 8, nguruwe milioni 2.4, na kuku milioni 36.
    Kati ya ng'ombe milioni 25 ng'ombe wa asili ni 98%. Hivyo, ni 2% tu ya ng'ombe wote Tanzania wanaofugwa kwa mfumo wa ufugaji wa kisasa.
    Tafiti hizo zinaonesha kuwa ufugaji wa asili unachangia 7.4% ya pato la Taifa na ongezeko la ukuaji la 2.2% kila mwaka. Ufugaji wa asili umethibitika kiuchumi kuwa na ufanisi mkubwa katika matumizi ya ardhi na uhifadhi wa mazingira.
    Ufugaji wa asili unategemewa na idadi kubwa ya Watanzania kwa kuendesha maisha yao; iwe kwa chakula, mavazi, na maendeleo kwa mapana yake.
    Mchango wake katika uchumi rasmi na usio rasmi (informal and formal economies) ni dhahiri hasa kupitia kodi na tozo mbalimbali katika masoko ya mifugo, usafirishaji wa mifugo, ukaguzi wa mifugo, na upatikanaji wa malighafi kwa matumizi ya viwanda mbalimbali.

Комментарии • 17

  • @frankjackson2784
    @frankjackson2784 2 месяца назад

    Nimeipenda

  • @matukiosafaris6508
    @matukiosafaris6508 2 года назад +2

    Maelezo mazuri lakini kila ukipiga simu ili ununue ngombe unaambiwa hakuna

  • @elisantemrita9894
    @elisantemrita9894 3 года назад +1

    Embu acheni siasa kwenye ufugaji Ongezeni akili katka ufugaji

  • @damasmaleo4845
    @damasmaleo4845 2 года назад

    Mbuzi mauza bei gani

  • @davidmsalilwa9687
    @davidmsalilwa9687 Год назад

    Wanapatikana wapi

  • @habibuluyangi2702
    @habibuluyangi2702 Год назад

    Mabuki iko mkoa gani na hao nyati maji bei gani

  • @amanibwire4423
    @amanibwire4423 3 года назад +1

    Pamoja na yote kama mfungaji nayeanza unapenda niwakumbushe kuwa ng'ombe wa kienyeji wana maziwa mazur na nyama nzr

  • @chuzilapweza6517
    @chuzilapweza6517 2 месяца назад

    kwanini sasa wanajitangaza kipindi cha nane nane na matasha peke yake?

  • @husseinhussein9971
    @husseinhussein9971 4 года назад

    Hao nyati ndio wale wa India?

  • @omarimnyeshani1810
    @omarimnyeshani1810 4 года назад +2

    Duuh!! Nyati tunao wengi tu mbugani halafu wataalamu mnaomba mbegu kutoka nje ya nchi? Hivi mnafeli wapi?

    • @avyalimanaathanassambuta6577
      @avyalimanaathanassambuta6577 3 года назад +1

      Nyati wanao tafutwa ni Domesticated

    • @TM.Sullusi
      @TM.Sullusi 3 года назад +1

      Usikariri mkuu, sio hao nyati wa mbugani kwetu. Ni aina tofauti kabisa ya nyati 😀😀😀😀😀

    • @matukiosafaris6508
      @matukiosafaris6508 2 года назад +2

      Kungekuwa na nyati wa mbugani hapo hao watu wote wangekuwa marehemu na wengine hospitali

    • @ndukulusudikucho_
      @ndukulusudikucho_ 2 года назад

      @@matukiosafaris6508 hahahahahaa

    • @mebumohammed6844
      @mebumohammed6844 Месяц назад

      @@avyalimanaathanassambuta6577naweza pata number naitaji madume tu