Salama Na Fid Q Ep 7 | NGOSHA WA MBASA Part 1

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 5 сен 2024
  • #YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast
    Listen our Podcast on
    ‪Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcasts Link apple.co/2Ou1bru‬
    ‪RUclips Link bit.ly/RUclipsS...
    NGOSHA WA MBASA
    Nakumbuka kipindi ambacho Fidi alikua anaamini kabisa kama kuweka ‘uso wa mbuzi’ ndo kulikua kunakufanya uwe ‘hard core’, sina uhakika lini aliachana na dhana hiyo ila kwa kipindi cha miaka miwili au zaidi tabasamu na bashasha vimekua havibanduki kwenye uso wake, jambo ambalo mimi kama rafiki nalifurahia sana. Nakumbuka baadhi ya marafiki zangu wa kike ambao ni wapenzi haswa wa mziki wake walikua wakiniambia eh, sema rafiki yako mgumu jamani, Kha! Mi hucheka tu na baadae wakishazoeana basi sidhani kama kuna hata mmoja anaweza kusema kitu kibaya kuhusu yeye. Nilikua nacheka kwasababu mimi naamini namfahamu rafiki yangu huyu, yeye hupenda sana matani, na kucheka na marafiki wa karibu wanaweza wakathibitisha hilo maana katika watu ambao unaweza ukawatania weeee mpaka asubuhi, na utani mpaka wa vitu vyengine ambavyo wewe wa karibu unaweza kusema ey, hiyo sasa imepitiliza, yeye waala... Atacheka tu!
    Mwenye kipaji chake cha kujifunza mwenyewe, nasema hivyo kwasababu nadhani kufahamiana kwetu na kuelewana kwetu pia kunatokana na kuwa na vitu vinavyofanana ndani yetu. Kajifunza jinsi ya kupenda kusoma vitabu mwenyewe, kujifunza jinsi ya kuandika na kurap mwenyewe, kajiendeleza mwenyewe (bila ya shaka kuna watu walomsaidia kwa tafu za hapa na pale ila walitokea baada ya kuona jitihada zake). Alihakikisha anasafiri kwenda nje ya nchi na Africa kwa jitihada zake mwenyewe na mpaka leo, kukiitwa watu ambao wamesaidia kwa kiasi kikubwa kufikisha Hip Hop ya nyumbani hapa ilipo basi jina lake litakua ni miungoni ya yale yatakayopata heshima ya juu kabisa. Pia anachekesha sana. Uelewa wake wa baadhi ya vitu unaweza ukakuacha mdomo wazi wakati mwengine. Kwenye uwepo wake? Vicheko lazima vitawale.
    Hii siku nilitia nae story haikua kama kazi, bali kama mtu na rafikiye tu wakitia story juu ya njia za maisha ambazo tumepitia mpaka sasa. Fidi amekuzwa na Mama yake ambae alikua ni mfanyakazi wa serikalini (ameshastaafu), alikulia mkoani kama wengi wetu, alifika Dar akakaa kwa ndugu kama wengi wetu, alianzia sehemu na kutoka hapo mdogomdogo akajijenga kufikia hapa alipo. Humu tumeongelea hayo, watoto, muziki, ndoa, maisha ya wasanii na maendeleo kwa ujumla. Yangu matumaini uta enjoy na kuelewa baadhi ya vitu zaidi na zaidi.
    Here’s to Ngosha wa Mbasa.
    Love,
    Salama.
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown

Комментарии • 241

  • @innocentmushi1550
    @innocentmushi1550 4 года назад +62

    Wanawake huhofia maisha kabla ya ndoa. Wanaume huhofia maisha na future baada ya ndoa

    • @veronicadaniel1122
      @veronicadaniel1122 4 года назад +1

      Innocent Mushi Naona mnaokota madini ya ngosha😍

    • @innocentmushi1550
      @innocentmushi1550 4 года назад

      @@veronicadaniel1122 yah ngosha ana madini mengi sana..ukitaka mengine nicheki kwa email yangu mushiinnocent19@gmail.com

    • @djunction4127
      @djunction4127 4 года назад

      point hyosiomakudhuzi ya thuglife nailele

  • @sharifamfaume9342
    @sharifamfaume9342 4 года назад +40

    Naomba like zamamaake fraridi jamani🤲

  • @fettymanyo438
    @fettymanyo438 4 года назад +41

    Mwanaume ni kichwa cha familia lkin mwanamke in shingo inayofanya kichwa kizunguuke

  • @fazeelshomary2704
    @fazeelshomary2704 4 года назад +61

    Only two artists nikiangaliaga au kusikiliza interviews zao nachota vitu vipya, 1. FID Q na 2. MwanaFA

    • @ericagerald4486
      @ericagerald4486 4 года назад +7

      Ukweli mtupu ukimuongeza na AY

    • @Jxcjs
      @Jxcjs 4 года назад +3

      We jamaa kama Mimi kaaaabiiiisaaaaa

    • @Yegon254
      @Yegon254 4 года назад +4

      hawa majamaa wana akili sana, ukisikiliza nyimbo zao unashiba

    • @Jitu_Lisilofikirika.
      @Jitu_Lisilofikirika. 4 года назад

      Niki wa 2

    • @dullyzungu536
      @dullyzungu536 4 года назад

      Mmoja wa mwisho mwamba wa kaskazini

  • @rishmizuka
    @rishmizuka 4 года назад +28

    Naheshimu Fid- Q Sana toka long tym, big up dadangu Salama kwa kumleta

  • @cheaffundikila9727
    @cheaffundikila9727 4 года назад +11

    Salama unamuoji mshikaji Kuna maswali kabla ya kuhoji unataka kucheka unajikaza

  • @augustinojerome7001
    @augustinojerome7001 4 года назад +3

    dah nimejifunz meng san kupitia mtu huy coz story ya maish yak aijaend mbal san na story ya maish yang thnks fid umenitia moyo wa maisha leo bigup pia salam kwa kuandaa kipind kizur km hiki i will be no 1 kukitazam kipind chako...

  • @baloziubalozini5074
    @baloziubalozini5074 4 года назад +19

    Hii ya "Ongeza Bando" nimeielewa sanaa..😂😂
    So far, fid yuko very specific in details, unakua km unatizama movie hv

  • @emmanuelbukuku1
    @emmanuelbukuku1 4 года назад +24

    (Wabongo wa majuu hamna upendo mnajigawa) Yani ukweli wa msemo huu ni asiimia 88%

  • @gthegamer5866
    @gthegamer5866 10 месяцев назад

    The way mwamba anavochana mistar katik nyimbo na interview ataendelea kuwa the best on my soul

  • @ezekiambise2595
    @ezekiambise2595 4 года назад +9

    Brain with potential

  • @convilsabato7596
    @convilsabato7596 2 года назад +3

    Kazi nzuri sana Salama. Mlete Jay Moe kwa interview

  • @denismakweba3870
    @denismakweba3870 4 года назад +11

    "Farid Kubanda,alizaliwa Aug 13 katika hosp ya bugando jijini mwanza,kwakuwa mtoto kwa mama akui aliamua kwenda kulelewa kwa bibi.....salama napenda
    "Kwanini wasinitafute kupitia mimi"

  • @nahyialetomia9284
    @nahyialetomia9284 4 года назад +6

    Liberia, Senegal, Ivory Coast

  • @davidsomi451
    @davidsomi451 4 года назад +9

    nimemuelewa vizur Mr mbuzi naomba hii interview irudiwe

  • @abdallahmakombo3866
    @abdallahmakombo3866 4 года назад +5

    Historia ya malezi ya fid q inaumiza Sana

  • @kijokombao5345
    @kijokombao5345 4 года назад +5

    Mwalimu wa kitaaa and the truth speaker,

  • @saumuhassan6365
    @saumuhassan6365 4 года назад +7

    Much love my dear Brother *FAREED* unamadini Mengi sana Bro ❤️😍

    • @abujuhaifah7461
      @abujuhaifah7461 4 года назад

      Yani ww hongera kila nikisoma koment za kipindi hiki lazima nikuone hongera hatar ila ue wajifunza mamy hata kama nakuona upo kwneye ndege ya ethiopia

  • @alkaullahmediaTz
    @alkaullahmediaTz 3 года назад +1

    the G.O.A.T farid qubanda
    .... "nawapa ofa ya mswaki alaf mnaning'oa meno!!!!" hatar sanaa huu mstar

    • @maesryclassic456
      @maesryclassic456 3 года назад +1

      Time is money nafasi hujali kuzuga, wema anataka saa ya almasi zari anaujali mda

  • @fashiontrendstv3207
    @fashiontrendstv3207 4 года назад +5

    Ila Wakaka wa hip hop wanaonekanaga hardcore lakini wanakipenda wanamapenzi ya kweli

  • @kisalaurence6177
    @kisalaurence6177 Год назад

    SalamaNaFidQ among the best talk siku zote ya kuangalia to us young generation ✊🏿🤍🧠

  • @abdulkarimmohamed4616
    @abdulkarimmohamed4616 Год назад

    Hichi kimewahamasisha vijana wengi sana wawe na matumaini kwa maisha hasa mimi Salama dadangu mkubwa vipindi vyako navifwatilia mbaya

  • @judamsaki5609
    @judamsaki5609 3 года назад +2

    brain ..Fid Q...GREAT

  • @tafawasaid4740
    @tafawasaid4740 4 года назад +6

    Salama Jabir The Greatest Of All Time #Goat she can do each and everything in this industry

  • @UgandanAllstarTales
    @UgandanAllstarTales 4 года назад +4

    My nigga Q always been a great story teller. Liked alivyo simulia the way he met his girl

  • @josehaulee1508
    @josehaulee1508 Год назад

    Wana sanaaa waliobaki ni fd pr j sugu na fa

  • @andrewjulius3951
    @andrewjulius3951 4 года назад +4

    Leo kali,,,umekutana na mtu mwenye upeo mkubwa kiakil na saikolojia,,,,ulizeni maswali ya kikubwa.

    • @vevo3130
      @vevo3130 4 года назад +1

      kama yapi?? yaweke wazi ili wajue tujifunze...

    • @advocatekarama4917
      @advocatekarama4917 4 года назад

      Vivian Charlz 😅😅

  • @thomasbutingo17
    @thomasbutingo17 3 года назад

    Fid q kalelewa vzr xn uyu jamaa ana hekima na busara xn npo jiran na nymbn kwao apa nyegezi Mwanza jamaa anakujaga home Hana sifa yan ana maisha ya pekee xn

  • @ujudiabdull9442
    @ujudiabdull9442 4 года назад +2

    Yaani FidQ nkikuangalia tu nacheka big up broo nakukubali sana 💪💪

  • @alshabihnjuck
    @alshabihnjuck 10 месяцев назад

    Perfect Mwanamalundi fid Q

  • @habeebboost1342
    @habeebboost1342 4 года назад +1

    Point ya mama fid umenikosha Allah akujazie kheri

  • @bigboyben6932
    @bigboyben6932 4 года назад +1

    ‘Nilichekechaaaaaaa nikandua sijafanya chochote cha kumfurahisha huyu headmaster’ fid Q nakukubari sana man

  • @clarasteven1802
    @clarasteven1802 3 года назад

    Mr aron wa nyakabungo,ni shidaaaa

  • @deogratiusjohn4502
    @deogratiusjohn4502 4 года назад +9

    Msanii bora wa hip hop Africa nzima na duniani kubali san bro

  • @masudiwaukweli468
    @masudiwaukweli468 2 года назад +1

    Nimeipenda sana tangia agost 13 mpaka sasa maneno ya kikubwa heshima kwenu👍👍👍👍

  • @rehemamrutu5596
    @rehemamrutu5596 4 года назад +4

    Salama always I love you

  • @sidval-el5816
    @sidval-el5816 4 года назад

    "Sehemu niliopo huku hamna access kabisa ya pilau" imenichekesha sana na kunihuzinisha pia. Bittersweet moment!

  • @stellaedmund7071
    @stellaedmund7071 4 года назад +4

    Legends re perfect 🙏🙏🙏🙏

  • @brayanphilipo1851
    @brayanphilipo1851 4 года назад +3

    Natumia Akili nyingi Kuilewa Mistari Yako Bro 💪🏼

  • @hamispeter9043
    @hamispeter9043 4 года назад +2

    Hii interview qali sana....fid q amepoa sana.

  • @fubanjenjele521
    @fubanjenjele521 4 года назад +3

    Bonge LA ex interview Kati ya Ng'wanamarundi na salama
    Nimecheka sn ety ninaappetite ya msosi

  • @bahatilusambo2757
    @bahatilusambo2757 Год назад +2

    Fid anaweza kumlaumu Baba yake lakini haja fanya utafiti kuwa kilicho mfanya Baba yake kubadilika Ni Nini?mke anaweza kuwa mzuri kwa watoto lakini asiwe mzuri Kwa mme au mme anaweza kuwa mzuri kwa watoto lakini asiwe mzuri Kwa mke wake kwa hiyo kujua chanzo kikubwa cha tatizo ndio ukomavu wa fikra pana na utafiti, asilimia kubwa ya mke au mme kuna kosa kubwa sana wanalo fanya kuhamishia upendo kwa watoto Ni kosa kubwa sana katika ndoa, mme na mke wakipendana wao kwa wao Ni jambo jema na la busara, Mimi nina mwanangu lakini mwanangu akikua ataniacha na mke wangu

    • @zedekiahmagwega8044
      @zedekiahmagwega8044 3 месяца назад

      Hapo alipotoka huko kwa mwanae na akaamua kumsamehe nafikiri aliambiwa ukweli ulivyo

  • @Ishengoma1
    @Ishengoma1 4 года назад +10

    Single monthers and fathers mjifunze hapa, msiwatie sumu watoto, haisidii. Baba ni baba na Mama ni Mama. Period!!

  • @AfiSoul103
    @AfiSoul103 4 года назад +7

    Love u my sisSalamA ... 🤗your hair 😋

  • @KaoratajrMD
    @KaoratajrMD 4 года назад +2

    some brains conversations...safi sana

  • @edwalks4922
    @edwalks4922 4 года назад +1

    Mmetisha sana

  • @jimmymangao5698
    @jimmymangao5698 4 года назад +4

    Best interview Salama n Fid Q

  • @ramadhaniabdi9530
    @ramadhaniabdi9530 4 года назад +4

    Leo story za malezi tu na familia

  • @hellenmawere9284
    @hellenmawere9284 4 года назад +1

    Kaka mkubwa wewe ni zaidi ya kiyoo... Mashairi yako, maisha yako hua najifunza Sana kupitia nyimbo zako... 🤪 Mzee wa appetite

  • @danielsama1576
    @danielsama1576 4 года назад +7

    😂😂😂😂😂kila akichekecha hajamfraisha mwalimu

  • @shesheejumaa578
    @shesheejumaa578 4 года назад +3

    sister salama please nitafurahi sana kama utarudia tena interview na brother fid coz daaah maneno yake ni kuntu

  • @abdalamhamed1748
    @abdalamhamed1748 4 года назад +1

    ukiniuliza msanii bongo,kichwani inakuja fid q.

  • @malickabbas8271
    @malickabbas8271 4 года назад

    Ni kweli Salama aliwah kutembea na fid q

  • @mkoakaskaziniu8132
    @mkoakaskaziniu8132 2 года назад +1

    Wewe hatar sana salama
    Unajua

  • @bittersweet1683
    @bittersweet1683 Год назад

    Fid Q's music changed how I see the world

  • @queenkiruwa3499
    @queenkiruwa3499 3 года назад +1

    Salama uyo Alisha kua mtu wako gonga like km unajua iloo

  • @chumayaoinvestment1647
    @chumayaoinvestment1647 4 года назад +1

    Neat

  • @benardmartine244
    @benardmartine244 4 года назад

    mbasa Gete

  • @zedekiahmagwega8044
    @zedekiahmagwega8044 3 месяца назад

    Rudia hii interview SALAMA

  • @andrewbabaako6972
    @andrewbabaako6972 2 года назад

    usinikubali halaka moja kat ya ngoma nzuri sana inayotukosesha mademu

  • @ibrahamkalu9069
    @ibrahamkalu9069 4 года назад +1

    Salama twataka sura ya Jesca,,. interview iko 🔥🔥

  • @jacksonmishwaro7460
    @jacksonmishwaro7460 4 года назад +5

    mimi nikishamuona jessica tu...Show imeisha

  • @hamzaabdulhalimissa7184
    @hamzaabdulhalimissa7184 4 года назад +1

    Mwanamalundi,ngosha,mwanza mwanza,cheusi dawa sijawahi kuchukia interview zake

  • @mercymakundi3582
    @mercymakundi3582 4 года назад +4

    Bonge la intavyuuuuu aiseee

  • @frexalphonce9387
    @frexalphonce9387 4 года назад +4

    Dar fid nimependa maneno yako ofxa

  • @zuleikhakhamis3303
    @zuleikhakhamis3303 4 года назад +2

    kweli 100% wabongo wa majuu wanagombana na kujigawa kila cku mpk wengine wanasema mtu akifa asiende mazikoni kwake hongera kaka kwa mda mchache State kuliona ilo mucpinge mie pia naishi State hali iyo ipo ukweli mtupu

  • @Ivy-pn2gc
    @Ivy-pn2gc 4 года назад +7

    Salaama uko makini ...eti apo ushaita mpenzi.

  • @michaelgermany173
    @michaelgermany173 4 года назад +3

    Respect to you fid q your big thinker

  • @thomasbutingo17
    @thomasbutingo17 3 года назад

    Fid q fundi wa mziki we proud of u Wana lake zone

  • @Majambo_Duniani_Tv
    @Majambo_Duniani_Tv 4 года назад +1

    Jeska kula gwara👊

  • @ashminaabdulla8946
    @ashminaabdulla8946 Год назад

    Sijutiii kukutizama

  • @benjo_brighter
    @benjo_brighter Год назад

    King 👑 of Rock City 🙌

  • @nelsonmwombeki5243
    @nelsonmwombeki5243 3 года назад +4

    Fid Q, the Legendary OG GOAT

  • @oscarjohn477
    @oscarjohn477 4 года назад +12

    nakumuintaviu ex veepee 😂

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 2 года назад

    *FARID QUBANDA* nakukubali sana 💕

  • @marymichael6635
    @marymichael6635 4 года назад +8

    wooozaaah😍😍😍

  • @hajiabdalla2034
    @hajiabdalla2034 2 года назад

    very nice

  • @lovenessgodson1075
    @lovenessgodson1075 4 года назад +1

    Mbona haifunguki kwangu

  • @rajabudau7478
    @rajabudau7478 4 года назад +3

    Salama upo active sana .. unajua sana hii kazi siku choki kwenye kamera

  • @berthamtenga2091
    @berthamtenga2091 4 года назад +1

    Namkubali saana fid

  • @anisiamedard3775
    @anisiamedard3775 4 года назад +1

    Nimekuja baada ya kuona Ngosha wa Mbasa

  • @ombenmichael3473
    @ombenmichael3473 4 года назад +1

    Great interview

  • @allimwakalebella3789
    @allimwakalebella3789 4 года назад +2

    Salama na #Dj_Fetty itakua poa

  • @kelvinsichone2359
    @kelvinsichone2359 4 года назад

    You are so conscious mwanamalundi

  • @richardkirongo4835
    @richardkirongo4835 4 года назад +1

    August 13

  • @nellykasanda825
    @nellykasanda825 3 года назад

    Good

  • @chunanachu2529
    @chunanachu2529 4 года назад

    Yani kuna watu huwezi kuangalia interview zao lkn kwasababu yupo na Salama unapata ushawishi wa kuangalia na unaenjoy sanaaaa I love u salama

  • @scripturetz1056
    @scripturetz1056 4 года назад +1

    #madsoft

  • @watidowalid7744
    @watidowalid7744 4 года назад

    Sawa

  • @africanyoung5410
    @africanyoung5410 4 года назад

    Salama naskia goma hlo kitambo mshagusisha nyaya

  • @jumamichael4083
    @jumamichael4083 4 года назад +1

    Duh

  • @mababiyoo8099
    @mababiyoo8099 4 года назад

    One love

  • @veronicadaniel1122
    @veronicadaniel1122 4 года назад

    My kaka WA mbasa

  • @Yegon254
    @Yegon254 4 года назад +9

    huwa siangalii episodes zako lakini wasanii kama Fid q, FA, AY na professor Jay akiibukia lazima niangalie

  • @erickbmaxunga6019
    @erickbmaxunga6019 3 года назад

    Mnyama kabixa

  • @ashminaabdulla8946
    @ashminaabdulla8946 Год назад

    Mpaka leo 👌🥰🥰👌💯

  • @binbaya923
    @binbaya923 4 года назад +1

    Kipindi kizuri🇹🇿🇦🇷

  • @pascalanthony2542
    @pascalanthony2542 4 года назад

    Nakukubali sana fid q

  • @johashisamson1915
    @johashisamson1915 4 года назад

    Jamaa anajua sana

  • @majadotto9513
    @majadotto9513 4 года назад

    Mwanamalundi nakubari