WANAKIJIJI''TOKA MWAKA 1970 WAZIRI YEYOTE HAJAWAHI FIKA KIJIJINI WAKWANZA KAWAWA,NDALICHAKO WAPILI''

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 5 сен 2024
  • Waziri wa elimu sayansi teknolojia na mafunzo ya ufundi Prof Joyce Ndalichako ametoa mchango wa mabati 72 na mifuko 50 ya saruji kwajili ya ujenzi wa Kituo cha afya katika Kijiji cha Marumba kata ya Muhunga wilayani Kasulu Mkoani Kigoma jambo litakalowasaidia wakazi wa kijiji hicho kuacha kutembea umbali wa kilomita 50 kufuata huduma za afya .
    Waziri Ndalichako ametoa mchango huo katika harambee ya kuchangia ukarabati wa kanisa la mtakatifu Agustino kijijini hapo kanisa ambalo lilianzishwa tangu mwaka 1945 ambapo zaidi ya shilingi million 20 zilipatikana.
    Aidha wakazi wa kijiji hicho wameeleza kuwa ni takribani miaka 70 sasa tangu hayati Waziri Rashidi Mfaume kawawa kufika kijiji hapo hakuna kiongozi yoyote mkubwa aliyewahi kufika ambapo waziri Ndalichako amewahidi kuwa kuanzia sasa viongozi mbalimbali wataanza kufika kijijini hapo.

Комментарии • 160

  • @princeramsay6638
    @princeramsay6638 5 лет назад +12

    Nakushukuru millardayo kuonesha kijiji chetu mungu akubalik

  • @erickfene1642
    @erickfene1642 5 лет назад

    hongela umi mwalim kwa kwenda kijiji cha marumba nashauli kila wazili afike kijiji cha marumba

  • @mudystarog1381
    @mudystarog1381 5 лет назад +6

    Aisee poleni Sana ndugu zangu wa kigoma kwa changamoto mnazozipata

  • @m.mmarckus6298
    @m.mmarckus6298 5 лет назад +9

    Ilitakiwa kila mbunge anayegombea kwenye eneo flani akakae huko alikogombea,siyo wanajazana mjini tu

  • @musasimba3689
    @musasimba3689 5 лет назад +24

    Nikisema katika media Mirradiayo ni Namba moja piga kazi waonyeshe kijiji Kama hawana mbunge du!

  • @petermbalawata1102
    @petermbalawata1102 5 лет назад +14

    Nakbl bro millardayo 🔥🔥

  • @alexmmary8887
    @alexmmary8887 5 лет назад +25

    duuuu na mm ndio
    mwanakijiji ambaye nina smart hapa kijijini kote haijawahi tokea tokea1970

  • @hapyness2504
    @hapyness2504 5 лет назад +2

    Millardayo kazi nzuri proud of kigoma

  • @linkreuben5804
    @linkreuben5804 5 лет назад

    Mawazili mme lala!
    Kazi ya kuisaidia Tanzania kama inawashinda vile! But the people of Kasulu they're so smart. God bless them!

  • @kelvinvitalis175
    @kelvinvitalis175 5 лет назад

    Inamaana mpaka wahitaji waziri aendee kijijini kwao inamaana hata mb'unge wao hawamfahamu hatari viongozi wajibu wenuu sasa ni hupi watembeleeni wananchi itakua safi Sana

  • @katibatanzania3089
    @katibatanzania3089 4 года назад

    Ivi ata rahisi nyny mwamjuwa kweli jamani poleni sana wakija kuomba kura mwawapa wanafki hao

  • @muniraahmed624
    @muniraahmed624 5 лет назад +21

    Kiukwel baadhi ya viongozi wakishapata madaraka wanawasahau wananchi wao😬 inauma sana

  • @happymsaki1720
    @happymsaki1720 5 лет назад +2

    Kanisa Hongra kwa kazi nzri ya kuhudumia jamii,

  • @happymsaki1720
    @happymsaki1720 5 лет назад +2

    Kwa kweli mko vzr ndgu zangu kwa mambo ya maendeleo msiogope Mheshimiwa RAISI RAISI wetu na mawaziri wa awamu hii wako vzr jiandae na ugeni pamoja na misaada kama YOTEEEEE VIVA JPM

  • @idayagangs124
    @idayagangs124 5 лет назад +12

    Watu wanafumukiana vitambi mijini kazi kwelikweli

  • @allyrussinga3703
    @allyrussinga3703 5 лет назад +1

    Hyo kwakuwa imerushwa ktk mitandao lakini vijj vingi sana vipo namna hii au zaidi tz yetu

    • @mamachris6811
      @mamachris6811 5 лет назад

      Vijiji ni Vinci sana
      Viongozi wawajibike kwa ngazi zao

  • @gapablessgadison6863
    @gapablessgadison6863 2 года назад

    Yaaani,,inauma jamani😭😭😭 et tangu 1990 kawa waziri wa pili kufika huko marumba,VERY SAD

  • @michaelkabeta7974
    @michaelkabeta7974 5 лет назад +17

    Duuh viongoz wamejazana mjini tu

  • @tinyaanosiatha1118
    @tinyaanosiatha1118 5 лет назад +3

    Ama kweli kigoma wamesahaulika kimaendeleo Jamani inauma sana , Ni mbunge gani mliyemuchangua ambaye hatatui kelo za wananchi wake. 2020 msimupatia kula chagueni mwingine ambaye atawatatulia kelo zenu.

    • @giftgodson5603
      @giftgodson5603 5 лет назад

      zito kabwe

    • @tinyaanosiatha1118
      @tinyaanosiatha1118 5 лет назад

      Kweli ni zitto kabwe au umenidanganya.

    • @giftgodson5603
      @giftgodson5603 5 лет назад

      nadhani ni yeye ila huyu waziri yeye ni mbunge wa viti maalum huko lakini alie na jimbo nadhani ni zito labda nisahihishwe kama nimekosea

    • @arexmerck2324
      @arexmerck2324 5 лет назад

      apana sio zito kabwe yure nijembe yye anaongoza kgm mjini iro nijimbo riko chini yambunge mwingine Kasul

    • @tinyaanosiatha1118
      @tinyaanosiatha1118 5 лет назад

      Arex Merck Alex sikubaliani wewe zitto katika jimbo lake kawafanyia nini wananchi wa ujiji pesa za jimbo anasunda yeye na familia yake leo unasema eti ni jembe sikubalini na wewe.

  • @agathaagustino2820
    @agathaagustino2820 5 лет назад

    Hinayo karisana vijijihivi tunakushululu kwakufika nyumbani karibu sana

  • @kbpfurniture4358
    @kbpfurniture4358 5 лет назад +4

    Aisee nimefurahi sana kuona leo kijiji chetu kimekumbukea, nakumbuka toka nizaliwe ndio mala ya kwanza kuona kiongozi mkubwa anafika kijijini kwetu, hadi leo ni na miaka (26) dah?

    • @kbpfurniture4358
      @kbpfurniture4358 5 лет назад +2

      Na sikuwahi kusikia eti kuna kiongozi aliwahi kuja kwetu, binafsi niwaombe viongozi watujengee sekondari pamoja na kumalizia zahanati, tutafurahia sana sana, tunateseka sana wana Marumba,

  • @tedymwandara5480
    @tedymwandara5480 5 лет назад

    Sura zao nzuri kweli km hawaishi kijijini!

  • @felixmuzambele9031
    @felixmuzambele9031 5 лет назад +1

    Mawaziri wengi wa Kigoma hawapendi ktumbelea Kigoma iwe kikaz au kwa mapumuzko, wabunge wanakaa Dodoma na Dar wakuu wa wilaya wapo maofisin hawajui kero za wananchi wao,hawatoki maofisin,n ss Kigoma vijijin hatujamfaidi Magufuli kwa miaka hii mitano sabubu ya uongozi wa chini huku ni mbovu.

  • @anuaryally6177
    @anuaryally6177 5 лет назад +2

    Zito je yupo ubeligiji au ujerumani

  • @wemakalamu3538
    @wemakalamu3538 5 лет назад +1

    Duuu balaa poleni kwa kweli 🙋‍♀️🙋‍♀️🙋‍♀️

  • @godfreylyimo4177
    @godfreylyimo4177 5 лет назад

    Hongera sn Wazari hiyo ndio faida ya Mama kupewa nafasi kubwa,sifa ya huruma na Upendo. Mawaziri inakuwaje hawajafika? Mkuu wa wilaya pia wananchi hawakujui?? Bado hamjaelewa Kamanda wetu JPM anataka nini

  • @mrholela7906
    @mrholela7906 5 лет назад +4

    Watu wa Kigoma nadhani Mzee kaongea ukweli wa moyoni .... Kigoma kiukweli duuh cjui km tuko wapi !??

  • @ilovejesus9303
    @ilovejesus9303 5 лет назад +4

    Ndio shida ya kukaa vijijini, haiwezi kuwa Kama mjini lkn angalau mpate vitu muhimu Kama umeme,maji, elimu Bora na zahanati jmn.

  • @isaacvtv547
    @isaacvtv547 5 лет назад +3

    Kasulo hoyeeeeeeeee!!!!!!!!

  • @ManaseBuhanza-cl1lc
    @ManaseBuhanza-cl1lc 3 месяца назад

    Saratani ya tanda nchi wakina mama ,hususa titi ya kansa kimbembe tena wapaswa kufanyiwa uchuguzi zaidi

  • @salamaseif4032
    @salamaseif4032 3 года назад

    Poleni xana

  • @hawasaid8262
    @hawasaid8262 5 лет назад

    Arafu nimekipenda ichokijiji

  • @gullaalex6590
    @gullaalex6590 5 лет назад +1

    Kigoma yangu

  • @japharikarume7887
    @japharikarume7887 5 лет назад

    safi sana

  • @maxcharles5436
    @maxcharles5436 3 года назад

    marumba ndoo nimesoma apo nimekulia apo

  • @jostamzxkaole3113
    @jostamzxkaole3113 7 месяцев назад

    HAKUNA HAJA YA ONGERA.. kama miaka yoote iyo hawajaja wamekuja mwaka wamwisho,, kazi nikazi tuu na nijukumulao viongozi kuwatimizia wananchi wa malumba.
    (Napo hakuja kwa ziara ya serikali)👁

  • @pinnawilson825
    @pinnawilson825 5 лет назад

    viongozi wengine ni wasaliti jamani.........poleni ndugu zangu....

  • @deokimena5168
    @deokimena5168 5 лет назад

    Place of Domicile!!!! Umenikumbusha mbali sana!!

  • @bebisheni4380
    @bebisheni4380 5 лет назад

    makubwa kumbe ratio ramani ya tanzania hawaangali ndio maana hawafiki maeneo y'a nchi hawajui waziri wa elimu gawa ramani

  • @neemajosephati8403
    @neemajosephati8403 5 лет назад

    Hongereni Wana Marumba

  • @robertjagad5826
    @robertjagad5826 5 лет назад +2

    tunavijiji vingi tanzania hii msilete mchezo, ndo maana kukawa na center huko kweingine wakuu wa wilaya na ma katibu kata inatosha otherwise mmmh tunavijiji vingiiiiii

    • @mamachris6811
      @mamachris6811 5 лет назад

      Kweli kabisa so rahisi Waziri akafika kila kijiji
      Muundo wa Serikali na vyama upon vizuri
      Uwajibikaji ndio la msingi

  • @mwigakatumpula2175
    @mwigakatumpula2175 5 лет назад +2

    Harafu uchaguzi ukikalibia waanza kuja kuwapatia vijihela nakuwasahaurisha yaliopita

  • @edwardmkwelele
    @edwardmkwelele 5 лет назад +1

    Kwani kufika tu kunasaidia nini?

  • @ramadhanisuru1822
    @ramadhanisuru1822 4 года назад +1

    Huko kweni cmlimchaguwa zito kabwe

  • @jumaigoti8676
    @jumaigoti8676 5 лет назад +1

    Kijana akija mjini. Harudi tena marumba.

  • @deograciakashaigili5973
    @deograciakashaigili5973 5 лет назад +4

    Mawaziri wote mnapaswa kufika hapo sio hao 3 tu. Inaonyesha dhahiri hawana Mbunge pia. Inasikitisha sana Juhudi zote anazofanya Mhe.Rais. Mnakisahau vipi kijiji hiki?

    • @kamicholo2669
      @kamicholo2669 5 лет назад

      Hii kali wabunge kila mwezi washukuwa pesa daa inasikitisha

  • @athumanmrisho1762
    @athumanmrisho1762 5 лет назад

    Ayo tv unakipaji

  • @OnlyRuky
    @OnlyRuky 5 лет назад

    Jamaniii huko sasa ndiyo anatakiwa apelekwe joketi 💃💃💃

    • @mamymamiza2924
      @mamymamiza2924 5 лет назад +1

      🤣🤣punguza sauti wanakisarawe wakikusikia watakuroga🤣🤣🤣

  • @markoernest4958
    @markoernest4958 5 лет назад +3

    Vijiji vingi Tz huu nd uhalisia wake

  • @deustutu1162
    @deustutu1162 5 лет назад +4

    viongoz wanakula baga mjin polen sana ndugu zetu

  • @centywid9051
    @centywid9051 5 лет назад +1

    wasaidien

  • @husnatgamaah1335
    @husnatgamaah1335 5 лет назад

    Mmmmh kuna vijiji vinasahaulika jamani hamna wawakilishi huko wabunge n.k? Nimejiskia vibaya mtu unajihisi hata kama haupo tanzania, maskini na hiyo zahanati nani atawaletea madaktari na manesi sasa kama miaka miaka yote hiyo hamna kiongoz amefika huko😢

  • @hiralidismasi6164
    @hiralidismasi6164 5 лет назад

    asante kawhata

  • @yusrahamad1085
    @yusrahamad1085 5 лет назад +1

    tunamsubr Mh JPM atalipokeaje tariff hii

  • @madawakemikali776
    @madawakemikali776 5 лет назад +3

    Heri ya nyie sisi wezenu ( kijiji cha Nyang'wambe - taarifa ya mikese) tangu tupate uhuru,,inasikitisha.

    • @jafaringogomela1658
      @jafaringogomela1658 5 лет назад

      Mwenzangu kwa kina kizigo ngogomela , nitafute ndugu yangu

    • @madawakemikali776
      @madawakemikali776 5 лет назад

      @@jafaringogomela1658 ....nitakutafuta ndugu yangu usijali

  • @msafiriiddy3135
    @msafiriiddy3135 5 лет назад

    tatizo huko ni mbali sana bwana mpaka kunatisha sikai hata kwa kupewa nyumba ya bure

  • @dottopeter3187
    @dottopeter3187 5 лет назад

    Hataree

    • @nooras6404
      @nooras6404 5 лет назад +1

      Eleweni zito ni mbunge was Kigoma mjini wakasulu ni pita selukamba

  • @nusulaally6379
    @nusulaally6379 5 лет назад

    Hiii sio haki kbx jmn wa2 mpk wamekuwa wabb nawamm hawawajui insikitisha🤔🤔

  • @cydemanchester2368
    @cydemanchester2368 5 лет назад

    Ningesimuliwa ningebisha sana

  • @idrissajumakona5871
    @idrissajumakona5871 5 лет назад

    Duh..jamaa tangu azaliwe hajawahi kumuona..ila leo tu ndio ameckia kama kaja

  • @mawazoselemani614
    @mawazoselemani614 2 года назад

    tangia uzaliwe ndio kwa mara ya kwanza ndalichako anakuja hapo kwenu hei!wajameni Huyu ndalichako mboni kachelewa kuja huko.angekuja wakati unazaliwa eti😀

  • @FlorenceDDR
    @FlorenceDDR 5 лет назад

    Aww 🥰

    • @nestorycharleskelegwa526
      @nestorycharleskelegwa526 4 года назад

      Ahsante sana Mirad Ayo Tv sub sisi hapo ni home coz Serikali ililala fursa ni nyingi ktk kijiji hicho cha Marumba! Asante Joyce Ndalichako tunamtegemea Philipo mpango naye mda wowote

    • @nestorycharleskelegwa526
      @nestorycharleskelegwa526 4 года назад

      Viongozi mtu kwao kwanza!!!

    • @nestorycharleskelegwa526
      @nestorycharleskelegwa526 4 года назад

      Kauli yako kwa wazee wetu uilinde uikumbuke kama ilani ya CHAMA TAWALA

  • @mhthesamemh7303
    @mhthesamemh7303 5 лет назад

    Duh 😷😷😷😷

  • @Chiefmukama
    @Chiefmukama 5 лет назад

    Naiona nyumba yetu ileee

  • @luizabahati5198
    @luizabahati5198 5 лет назад +1

    Dah...nimeshtuka Sana...hata sio kidogo Yani watu wanamjua hayati Kawawa Tu?OMG uongozi ni dhamana nadhani hata viongozi WA level ya chini kabisa hawapazi sauti kuikomboa maramba na waliofanikiwa/kubahatika kutoka maramba wameisahau maramba.HONGERA BABA PAROKO USIZIMIE MOYO

  • @yohanabundala9162
    @yohanabundala9162 5 лет назад

    Hivi jamani hicho kijiji Wanainchi wake hawakupiga kura!? UKWELI inauma mpaka huruma sana..

  • @joshuanyamweru8410
    @joshuanyamweru8410 2 года назад

    Wanamarumba oyeee

  • @kojjagulimuyesenga8025
    @kojjagulimuyesenga8025 5 лет назад

    Kagoma ni Burundi sio Tanzania

  • @neemakilomoni4258
    @neemakilomoni4258 5 лет назад +1

    Hivi Zitto kabwe alisha fika huko??

  • @yohanabundala9162
    @yohanabundala9162 5 лет назад

    Eti livumbi lekundu Kama hili,, Poreni sana jamani.

  • @sudymgeni701
    @sudymgeni701 5 лет назад

    Mbuge wenu yuko wapi jamani

  • @saidhassan1104
    @saidhassan1104 5 лет назад +1

    Zitto yupo wapi

    • @zenobyomary9482
      @zenobyomary9482 5 лет назад

      Zito hahusiki apo ndg yy anhusk kgm mjn na ap yup mhuska

    • @ilovejesus9303
      @ilovejesus9303 5 лет назад

      @@zenobyomary9482 Kuna mbunge wa kijijini na mjini? Mie najua mbunge ni mmoja

  • @kanjanjamwimikes9228
    @kanjanjamwimikes9228 4 года назад

    Ndalichakoo ?? haendagii?

  • @godfreysanga2405
    @godfreysanga2405 5 лет назад

    Tatuzo la waha mnasahau kwenu sana mkipata vyeo maana mmetikea huko ila hata kutembelea mnashindwa

  • @princemgambwa9143
    @princemgambwa9143 5 лет назад

    Sasa mmeanza kufanyia mikutano yenu hata bila haya kanisani

  • @mbingaheaven9899
    @mbingaheaven9899 5 лет назад

    Kwa nn vumbi jekundu africa tuu?

  • @yessecharles3155
    @yessecharles3155 5 лет назад +1

    Zitto ni mbunge dar tuu jmn dah

    • @sulleyjones6321
      @sulleyjones6321 5 лет назад +1

      Acha ujinga kuna wabunge wa kigoma mjini na vijijini
      Zitto ni mbunge wa kigoma mjini

    • @kamicholo2669
      @kamicholo2669 5 лет назад

      Musiwape kura washezi hao daa mama shukuwa uongozi uwasaidie

  • @khadeejaabdullah7083
    @khadeejaabdullah7083 5 лет назад

    Daah kwan huko hakuna mbunge

  • @hemedindunguru5021
    @hemedindunguru5021 5 лет назад

    Napataga tabu sana kuelewa vichwa vya habari za bongo kwani ukisema tangu 1970 ni mawaziri wawili tu ndio waliotembelea kijiji hiki utakuwa umekosea mkuu

  • @mohamedjuma1878
    @mohamedjuma1878 5 лет назад

    Dah kudadeki olewako upelekwe kufanya kazi huko

  • @rahmamgoo7518
    @rahmamgoo7518 5 лет назад

    Viongozi tunawachagua lakini hamtutendei Haki walah hadi huruma

  • @centywid9051
    @centywid9051 5 лет назад +3

    hadi huluma viongoz munaenda kubeba kura zen tu

  • @fantsonmpango7742
    @fantsonmpango7742 5 лет назад

    Mama mpaka povu

  • @shefaashefaa1930
    @shefaashefaa1930 5 лет назад

    Wananenepeyana 2 mijini hakuna kujuwa shida za watanzania

  • @happymsaki1720
    @happymsaki1720 5 лет назад

    Hamna mbunge wa kuwatetea huko????

  • @isaacvtv547
    @isaacvtv547 5 лет назад

    Zittooooooooo yuko wapiiiiiiiiii!

  • @jumaigoti8676
    @jumaigoti8676 5 лет назад +1

    Isaka rudini kwenu mkaboreshe kwenu.

  • @samoramdemu2834
    @samoramdemu2834 5 лет назад

    POLENI WATU WA KIJIJI CHA MARUMBA KASULU KIGOMA, KWA KUTOMUONA WAZIRI YEYOTE TANGU 1970.

  • @bintymwaliwanga565
    @bintymwaliwanga565 5 лет назад

    Naona uko kasulu kuna baba levo?

  • @mrholela7906
    @mrholela7906 5 лет назад

    Wanafaidi wengne

  • @gabrielisack7786
    @gabrielisack7786 5 лет назад

    Viongozi liangalieni hili

  • @bernardalethace5281
    @bernardalethace5281 5 лет назад

    Kasulu fanyeni ujinga tn kumrudsha gwanko wenu

  • @tgeofrey
    @tgeofrey 5 лет назад

    Nyie ndio mawaziri achananeni nao

  • @gadielpaulo8925
    @gadielpaulo8925 5 лет назад

    Dah kweli Ona wanavyoshangaa Ujio wake. utafikiri wameshukiwa. na mtume inasikitisha sana mawaziri

  • @gm7045
    @gm7045 5 лет назад

    Hii ni ukweli kabsa!
    Niliona Masanja tu akiwa anawacheki akili.

  • @patrickmadiwa3845
    @patrickmadiwa3845 5 лет назад

    Viongozi nyie Mungu anawaona!

  • @bintymwaliwanga565
    @bintymwaliwanga565 5 лет назад

    Mmeona uchaguzi uko karibu ndio mmeanza mambo yenu ya kundanganya wanaichi

  • @maricelajohn4241
    @maricelajohn4241 5 лет назад +3

    Bora hata nyie mmekumukwa Mimi hata kabila langu halijulikani utasema ni wakimbizi ukimwmbia mtu mm ni mmbugwe anakushangaa, mmbugwe! Ndiyo nini? Kwakweli najiskiaga vibaya sana, wambugwe tunaishi mkoa wa mayara wilaya ya babati vijijini.

    • @gloriousnp
      @gloriousnp 5 лет назад +1

      Maricela John mayara ndo wapi?🤷🏽‍♀️🤷🏽‍♀️🙄

    • @ilovejesus9303
      @ilovejesus9303 5 лет назад +1

      @@gloriousnp alimaanisha Manyara. Ilikuwa Arusha wakaitenganisha maana Arusha ilikuwa kubwa

    • @maryamdounga2290
      @maryamdounga2290 5 лет назад +1

      Me mwenyewe ndo nalisikia leo hilo kabila

    • @rashidkajara4328
      @rashidkajara4328 5 лет назад +2

      Maricela John wakikuulza waambie ni jamii ya warangi nawafahamu ni ndugu zangu nami ni Wa babati vjjn kata ya Magugu tarafa ya mbugwe na ndo mnakopatkana kwa wingi

    • @maricelajohn4241
      @maricelajohn4241 5 лет назад

      @@rashidkajara4328 kweli brother

  • @Rugemalilatv1994
    @Rugemalilatv1994 5 лет назад

    Acheni kuichagua ccm wanakazna kuijenga dar es salaam huko mkoani mnadanganywa tu

  • @wahidashabaz5982
    @wahidashabaz5982 5 лет назад +1

    rais tafuta kabila linalotokea katika kijiji icho kama yupo katika serikal yako basi mpeleke huko marumba nae akale vumbi miaka yote hiyo wananchi wapo kama hawapo tanzania