AICT Chang'ombe Choir (CVC) - Patakatifu (Official Music Video)
HTML-код
- Опубликовано: 14 окт 2024
- Shalom Mpendwa Katika Bwana!
Tumekuletea baraka nyingine tena kwako (neno kwa njia ya uimbaji). Patakatifu ni wimbo ambao unaelezea utukufu wa Mungu aketiye mahali palipoinuka mno.
Ubarikiwe na wimbo huu kutoka AICT Chang'ombe Choir (CVC).
#patakatifu #cvc
PATAKATIFU
Wote : Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe, litukuzwe
Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe
Hapa duniani kama huko mbinguni .
Solo : Mmmh Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe, litukuzwe
Ufalme wako uje
Mapenzi yako yatimizwe
Hapa duniani kama huko mbinguni (Ewe Baba).
Wote: Baba yetu uliye mbinguni
Solo : jina lako
Wote : jina lako litukuzwe
Solo: Eeeh YESU
Wote: litukuzwe
Solo : Ufalme wako
Wote: Ufalme wako uje
Solo :Mapenzi yako
Wote: Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni x3.
Solo: Wewe ni MUNGU peke yako x2
Ustahiliye sifa pekee
Maskani yako mahali palipoinuka mno (ooh)
Solo: Panaitwa
Wote : (patakatifu pa patakatifu)
Solo: Wewe ni
Wote : ( Mtakatifu )x13
Wote: (Mtakatifu) x13.
Solo: Viumbe wengi sana kama malaika wenye vyeo vikubwa waitwao maserafi
Mchana na usiku kamwe hawatulii, wazunguka zunguka wakipalinda patakatifu
( Ooooh Halleluya)
Na viumbe wengine kama malaika vyeo vya katikati waitwao makerubi oooh
Mchana na usiku nao hawatulii wazunguka zunguka wakihudumu patakatifu.
Solo : Wanasifu
Wote: ( Mtakatifu )x13
Solo : Wanasifu
Wote: ( Mtakatifu )x13.
Solo : Wazee ishirini na wanne wanaanguka mbele zako Baba wanakusujudia MUNGU wetu
Hawapumziki wewe MUNGU, wewe MUNGU
Wastahili, wastahili sifa na utukufu (uuuh) Bwana wewe wastahili
Wenye uhai wanne nao wamekizunguka kiti chako Baba kwa pamoja hawapumziki
Wenye uhai wanne nao wamekizunguka kiti chako Baba kwa pamoja hawapumziki.
Solo : Wanasifu
Wote: ( Mtakatifu )x13
Solo : Umeketi
Wote: Patakatifu
Solo : Oooh, Oooh Baba umeketi
Wote: Pa patakatifu
Wote : patakatifu , pa patakatifu
Solo : MUNGU umeketi
Wote : Patakatifu pa patakatifu
Wote : Amen.
SONG CREDITS TO;
Song Writer - Papaa Clement Buhembo
Video Director - Elidadi
Videographer - Amigo Johnson
Lights - Sengati
Audio - CVC Media
Kaa Karibu nasi | CVC MEDIA
/ cvcchoirtz_official
/ cvcchoirtz_official
©2023 AICT Chang'ombe Choir (CVC) | All Rights Reserved.
Huyo mkaka aloimba mwanzo kajua kutuliza sauti ,,,,,adi moyo unafarijika❤
Nimebarikiwa sana na huu wimbo sana,
nawapongeza kwa masifu haya makuu kwajili ya Mungu wetu, pongezi kwa Mwalimu mtunzi, sololist wote ila huyukijana wa mwisho amejua kumwinua kristo, hakika Mungu ni Mtakatifu. Mbarikiwe sana waimbaji wote
Wimbo huu unaupako kwa kweli
Mungu awatunze na kuwalinda waimbaji
Ooh...patakatifu jamn Mungu azid kuwainua kwa viwango vingine...japo natamani nitumike nayie....Mungu awatie nguvu jaman na awainue kwa viwango vingine...
Hakika mungu umeketi pahali patakatifu nimebarikiwa sana mungu awatumie nyie cvc
Naipenda sana hii nyimbo oh my God this is the best
MAM aliyenyoa na kaka mwenye suti nyeusi you have an Angelic voice😍😍
Yeye aliye mkamilifu atimizae agano....asiyeacha mwenye haki yake aangamieee.....hakika yu mtakatifuuu
Ni kweli kabisa Hawa wamama watatu wana uwezo mkubwa
Jamani huu wimbo daaah
Amina mbarikiwe aki cvc ,,,,, From Kenya
Kinara Cha masolorist... Ubarikiwe sana mama ✅✅✅
wimbo mzuri sana. Mungu awape nguvu na awaneemeshe kifedha na kimawazo na kila kitu. tunabarikiwa sana na nyimbo zenu. mungu amubariki sana. mtazamaji mwenzangu kama umebarikiwa na wimbo huu tafadhali coment kwangu Amen kisha like comment yangu. asante.
❤❤❤❤❤
Mpo vizuri natamani nijoyn
Huu wimbo ni sala yangu ya kila siku, Mbarikiwe sana
Solo wa Kwanza sauti imetulia sana na Mungu azidi kuwainua masolo wote...nyimbo imetulia sana abarikiwe sana aliyetoa idea ya wimbo, na abarikiwe pia mtunzi wa wimbo kwa kweli mmebarikiwa kila eneo
Miriam wote wamefanya vizuri sana
Solo wa mwisho we mkaka umegusa hisia sana.... Ahsanteni CVC na watunzi wenu wako vizuri mno....
But uyo sololist ni yule wa The survivors choir
Survivors choir kahama, ndo amejiunga hiyo kwaya?? Mungu ambariki sana ameleta Radha mpya kwenye AIC CHOIR
@@stanleyleonard4731 bona akatoka the survivors?
Mungu mtakatifu aketiye mahali pa juu patakatifu palipoinuka azidi kuwainua,,, nawaelewa sana chang'ombe tangu enzi za GUSA 2009's up to today,,, MUNGU awabariki sana🙌🙌🙏🎉
Nasubiria sana ase nipate baraka za Mungu nawapenda sana CVC
Mbarikiwe Sana 🥰cvc
Jaman huyu mdada mweupe ananibariku mm jaman napenda kuimba kama yeye jaman nilipoona amesolo yaan navurugwa mno nampenda nakuombea Mungu azid kuwalinda masolo wote WA Kwaya hii ila Zaid ❤❤❤ mno.
Great....In love with you servants. Mungu azidi kuwaongeza ktk viwango vya juu
Naupenda Sanaa huu wimbo,Mungu awabariki Sanaa watumishi wenzangu shambani mwa Bwana🙏kazi njema 🔥🔥🔥🔥🔥
Hakika mnamtumikia MUNGU❤
GREAT SONG UTUKUFU KWA MUNGU
i got so much inspiration on the songs of the AIC keep the fire burning praising God, coz the same songs will be used to heal souls and lift spirits in worship God bless you and your ministry
Nimebarikiwa na ujumbe,production iko on point waimbaji wamejua kutumia position zao za utumishi walionao Mungu azidi kuwainua🙏
Aiseee we mtoto nimekukubali sn,Mungu azidi kukutumia
Yupiii
The cvc I know❤❤❤❤❤❤
Hongrereni kazi nzuri Mungu awabarki
Mungu awatunze, kazi nzuri sana hakika ni patakatifu
Mungu awalinde na kuwatunza wapendwa
Amen🙌hakika Mungu umeketi mahali PATAKATIFU🙏
Hakika Mungu wetu ameketi mahali pa juu sana patakatifu amezungukwa na maserafi na makerubi wimbo mzuri sana barikiwa sana cvc❤
Mbarikiwe sana watumishi
Huo ndio Uimbaji wa nyimbo za kumwinua Mungu, Nabarikiwe Mno
Mungu awatunze❤
Niko apa nangoj jiwe lingine nawaamn san hawa watu hawajawahi kosea
Amen cvc ahsantee kwa kwazi iliyo tukuka
Mnatisha sana CVC kila baada ya miezi ata sita mngekuwa mnatubariki na wimbo njia vizuri balaa sina kwaya pendwa nyingine zaidi yenu
Siku hizi wanachelwa wanachelwa ... More blessed Cvc
Glory be to God 🙏
Woooooow woooooow woooooow Kaz yenu Ni njema Sana...I'm happy to see my singer mfeloo... amaizing work..mnajua na mnajua Tena . MUNGU awabariki
Barikiwa san wimbo mzuri
Hongereni sana wanac.v.c nawapenda
Wewe ni mtakatifu
Wow
Mungu awalinde zaidi
Mungu aneishi Mahali Patakatifu Azidi Kuwainua na kuwapandisha viwango na viwango vya Juu. Mbalikiwe sana!!
Mungu awabariki kwa wimbo mzuri sana
Watu waimbe nyimbo hizi❤,Shetan ataiba je,🔥🔥wimbo kama huu,Mbarikiwe Sana Chan'gombe
Dah nimesikiliza nyingi Ila hii ni zaidi ya utukufu mbarikiwe sana
Hakika ni Mungu pekee ndiye anastahili kuhimidiwa
Mtakatifu,mtakatifu,hakika u mwema maishani.
Patakativu ni nyimbo nzuri sana by ndibalema
We blessed na Mungu azidii kuwabariki pia❤️🙏
Nawaenzi sana wanakwaya wa A.I.C Chang'ombe tangu enzi za Tunda la Roho mpaka sasa nyie ni wa baraka ❤
Mungu wewe ni Mtakatifu hakika!!
Amen...May God bless you all ...For the new song...Hongera
Mungu uketi katikati ya sifa,barikiwe CVC
My Team Hongereni sana
Hawa wamama huwa wanaimba vzr hasa uyu mama wakwanzaa jmn anaimba kwa utulivu. Lkn niliwai kuja kanisan kwenu nimehudhuria mwez mzima kila nikienda kanisan kwao nia yangu niwaone wakiimba live wakisoro lkn sikuona wakisoro je wameacha kuimba? Nilkua naona wanasoro wengne tu nilkua naumia maana mm nilikuwa nakuja kusali ili niwaone tu😂😂 mnijuze jmn wamestaafu ama
Wapo mtumishi
Hata mimi kwaya hii naipenda sana wabarikiwe wote. Mwenyezi Mungu anakusudi kuwaunganisha wao, natuinjilishe ktk Uumbaji. siku Moja nitakuja kuwatembelea.
Nabarikiwa sana na kwaya hii CVC Mungu azidi kuwatunza nakuwainua, Mimi ni Muumini wa nyimbo za aina hii❤
Mama Diana James wow❤
Wimbo mzuri. Sanaa yake ya juu sana. Ahsante na mbarikiwe
Hongereni sana cvc Mungu azidi kuwainua na kuwatumia
Ninaomba mungu siku moja nije na niingie cvc tuimbe pamoja big up watumishi
My favorite song
Brove 🎉our might God keep u all
Nimebalikiwa sana
Nimeipenda hii jmn Mungu awabariki sana ❤
Waiting 😊😊😊
Nimeipenda sana hii
Jamani hii kwaya kwakweli Wana nipako sana nitakujiunga nanyi nafanyaje.
Karibu kanisani kwetu AIC CHANG’OMBE
I've been looking for this song for a long time, saw it in one of your previous albums but couldn't find it here. I'm blessed like very blessed
Waiting❤❤❤
Such a beautiful song beautiful composition
AMEN mtakatifu ni Mungu pekee mbarikiwe sana
Am blessed from this song 🙏🏼🙏🏼 God is great
Such a nice song, congrats the changombes
Baadaye mtuletee wimbo wa tumetumwa na ule wa samehe usamehewe
Hongereni sana kwa utume!
Utukufu kwa Mungu
Glory to God🙌
Mu batikiwe zaidi.
Na kumbuka ule wimbo wa "gusa" nawa "jiwe"
God bless you mmebadilisha maisha yangu🙏
Sifa na Utukufu Kwa Mungu
Mmeuwaaaaaaa what a beautiful song
Kudos to you CVC for such an awesome worship masterpiece 👏
Thanks for listening
Mmetisha Sasa mwenyezi mungu azidi kuwatumia kwaajili ya wengine.😊
Mungu ni mtakatifu.
weiting 🔥🔥🔥
Nice
Nimebarikiwa sana kazi nzur na mbarikiwe zaidii zaidii
Isaiah 6. Revelation 4. Be blessed AICT as God uses y'all as His vessels. I'm so much blessed. ❤
Am blessed
Ameeeeeeeen mbarikiwe sana
Mtakatifu Mtakatifu ni Bwana! Amina
Ujumbe mzr
😩❤️
Blessings 🔥🔥🔥🔥 Please upload the first version of the song
Mungu ni Mtakatifu asante Kwa wimbo nzuri bt video ya kwanza ya Patakatifu ilikuwa na kasoro kidogo neema ya Mungu iwe nanyi
Exactly 👍👍🤔
Nice song
Waiting to be blessed
Mungu mwema
Patakatifu🎉
Patakatifu kweli...
My favorite choir ..
Amina