AICT Chang'ombe Choir (CVC) - Patakatifu (Official Music Video)

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 окт 2024
  • Shalom Mpendwa Katika Bwana!
    Tumekuletea baraka nyingine tena kwako (neno kwa njia ya uimbaji). Patakatifu ni wimbo ambao unaelezea utukufu wa Mungu aketiye mahali palipoinuka mno.
    Ubarikiwe na wimbo huu kutoka AICT Chang'ombe Choir (CVC).
    #patakatifu #cvc
    PATAKATIFU
    Wote : Baba yetu uliye mbinguni
    Jina lako litukuzwe, litukuzwe
    Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe
    Hapa duniani kama huko mbinguni .
    Solo : Mmmh Baba yetu uliye mbinguni
    Jina lako litukuzwe, litukuzwe
    Ufalme wako uje
    Mapenzi yako yatimizwe
    Hapa duniani kama huko mbinguni (Ewe Baba).
    Wote: Baba yetu uliye mbinguni
    Solo : jina lako
    Wote : jina lako litukuzwe
    Solo: Eeeh YESU
    Wote: litukuzwe
    Solo : Ufalme wako
    Wote: Ufalme wako uje
    Solo :Mapenzi yako
    Wote: Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni x3.
    Solo: Wewe ni MUNGU peke yako x2
    Ustahiliye sifa pekee
    Maskani yako mahali palipoinuka mno (ooh)
    Solo: Panaitwa
    Wote : (patakatifu pa patakatifu)
    Solo: Wewe ni
    Wote : ( Mtakatifu )x13
    Wote: (Mtakatifu) x13.
    Solo: Viumbe wengi sana kama malaika wenye vyeo vikubwa waitwao maserafi
    Mchana na usiku kamwe hawatulii, wazunguka zunguka wakipalinda patakatifu
    ( Ooooh Halleluya)
    Na viumbe wengine kama malaika vyeo vya katikati waitwao makerubi oooh
    Mchana na usiku nao hawatulii wazunguka zunguka wakihudumu patakatifu.
    Solo : Wanasifu
    Wote: ( Mtakatifu )x13
    Solo : Wanasifu
    Wote: ( Mtakatifu )x13.
    Solo : Wazee ishirini na wanne wanaanguka mbele zako Baba wanakusujudia MUNGU wetu
    Hawapumziki wewe MUNGU, wewe MUNGU
    Wastahili, wastahili sifa na utukufu (uuuh) Bwana wewe wastahili
    Wenye uhai wanne nao wamekizunguka kiti chako Baba kwa pamoja hawapumziki
    Wenye uhai wanne nao wamekizunguka kiti chako Baba kwa pamoja hawapumziki.
    Solo : Wanasifu
    Wote: ( Mtakatifu )x13
    Solo : Umeketi
    Wote: Patakatifu
    Solo : Oooh, Oooh Baba umeketi
    Wote: Pa patakatifu
    Wote : patakatifu , pa patakatifu
    Solo : MUNGU umeketi
    Wote : Patakatifu pa patakatifu
    Wote : Amen.
    SONG CREDITS TO;
    Song Writer - Papaa Clement Buhembo
    Video Director - Elidadi
    Videographer - Amigo Johnson
    Lights - Sengati
    Audio - CVC Media
    Kaa Karibu nasi | CVC MEDIA
    / cvcchoirtz_official
    / cvcchoirtz_official
    ©2023 AICT Chang'ombe Choir (CVC) | All Rights Reserved.

Комментарии • 134

  • @ElizabethJohn-ls7ou
    @ElizabethJohn-ls7ou 6 месяцев назад +6

    Huyo mkaka aloimba mwanzo kajua kutuliza sauti ,,,,,adi moyo unafarijika❤

  • @emmanuelidafa2974
    @emmanuelidafa2974 4 месяца назад +2

    Nimebarikiwa sana na huu wimbo sana,
    nawapongeza kwa masifu haya makuu kwajili ya Mungu wetu, pongezi kwa Mwalimu mtunzi, sololist wote ila huyukijana wa mwisho amejua kumwinua kristo, hakika Mungu ni Mtakatifu. Mbarikiwe sana waimbaji wote

  • @RoseKisasi
    @RoseKisasi 6 месяцев назад +2

    Wimbo huu unaupako kwa kweli
    Mungu awatunze na kuwalinda waimbaji

  • @hezronbaraka206
    @hezronbaraka206 Год назад +2

    Ooh...patakatifu jamn Mungu azid kuwainua kwa viwango vingine...japo natamani nitumike nayie....Mungu awatie nguvu jaman na awainue kwa viwango vingine...

  • @justusekeno2262
    @justusekeno2262 Год назад +6

    Hakika mungu umeketi pahali patakatifu nimebarikiwa sana mungu awatumie nyie cvc

  • @AliceHatibu
    @AliceHatibu 3 месяца назад +2

    Naipenda sana hii nyimbo oh my God this is the best

  • @azizasamson1505
    @azizasamson1505 Месяц назад +1

    MAM aliyenyoa na kaka mwenye suti nyeusi you have an Angelic voice😍😍

  • @nicholouskyomo4960
    @nicholouskyomo4960 Год назад +3

    Yeye aliye mkamilifu atimizae agano....asiyeacha mwenye haki yake aangamieee.....hakika yu mtakatifuuu

  • @marynakei2621
    @marynakei2621 3 дня назад

    Ni kweli kabisa Hawa wamama watatu wana uwezo mkubwa

  • @VivianYusuph
    @VivianYusuph 3 дня назад

    Jamani huu wimbo daaah

  • @boazkitela6960
    @boazkitela6960 Год назад +3

    Amina mbarikiwe aki cvc ,,,,, From Kenya

  • @stanleyleonard4731
    @stanleyleonard4731 Год назад +2

    Kinara Cha masolorist... Ubarikiwe sana mama ✅✅✅

  • @kalindientertainment3216
    @kalindientertainment3216 Год назад +3

    wimbo mzuri sana. Mungu awape nguvu na awaneemeshe kifedha na kimawazo na kila kitu. tunabarikiwa sana na nyimbo zenu. mungu amubariki sana. mtazamaji mwenzangu kama umebarikiwa na wimbo huu tafadhali coment kwangu Amen kisha like comment yangu. asante.
    ❤❤❤❤❤

  • @soscreator
    @soscreator 3 месяца назад +1

    Huu wimbo ni sala yangu ya kila siku, Mbarikiwe sana

  • @miriamherman4499
    @miriamherman4499 Год назад +3

    Solo wa Kwanza sauti imetulia sana na Mungu azidi kuwainua masolo wote...nyimbo imetulia sana abarikiwe sana aliyetoa idea ya wimbo, na abarikiwe pia mtunzi wa wimbo kwa kweli mmebarikiwa kila eneo

    • @hawamdee8811
      @hawamdee8811 Год назад

      Miriam wote wamefanya vizuri sana

  • @stanleyleonard4731
    @stanleyleonard4731 Год назад +5

    Solo wa mwisho we mkaka umegusa hisia sana.... Ahsanteni CVC na watunzi wenu wako vizuri mno....

    • @atwijukireprize5090
      @atwijukireprize5090 Год назад

      But uyo sololist ni yule wa The survivors choir

    • @stanleyleonard4731
      @stanleyleonard4731 Год назад

      Survivors choir kahama, ndo amejiunga hiyo kwaya?? Mungu ambariki sana ameleta Radha mpya kwenye AIC CHOIR

    • @atwijukireprize5090
      @atwijukireprize5090 Год назад

      @@stanleyleonard4731 bona akatoka the survivors?

  • @zakariamsumba-gr8vr
    @zakariamsumba-gr8vr Год назад +3

    Mungu mtakatifu aketiye mahali pa juu patakatifu palipoinuka azidi kuwainua,,, nawaelewa sana chang'ombe tangu enzi za GUSA 2009's up to today,,, MUNGU awabariki sana🙌🙌🙏🎉

  • @francesmpangwa8801
    @francesmpangwa8801 Год назад +2

    Nasubiria sana ase nipate baraka za Mungu nawapenda sana CVC

  • @EvelineKilango-co1vc
    @EvelineKilango-co1vc Месяц назад

    Jaman huyu mdada mweupe ananibariku mm jaman napenda kuimba kama yeye jaman nilipoona amesolo yaan navurugwa mno nampenda nakuombea Mungu azid kuwalinda masolo wote WA Kwaya hii ila Zaid ❤❤❤ mno.

  • @jacklinemwandoloma285
    @jacklinemwandoloma285 Год назад +2

    Great....In love with you servants. Mungu azidi kuwaongeza ktk viwango vya juu

  • @annaelias1250
    @annaelias1250 Год назад +1

    Naupenda Sanaa huu wimbo,Mungu awabariki Sanaa watumishi wenzangu shambani mwa Bwana🙏kazi njema 🔥🔥🔥🔥🔥

  • @JustinaMasanja-kg5cg
    @JustinaMasanja-kg5cg 6 месяцев назад +2

    Hakika mnamtumikia MUNGU❤

  • @AbbysalumChiwanga
    @AbbysalumChiwanga Год назад +3

    GREAT SONG UTUKUFU KWA MUNGU

  • @mncheruiyot
    @mncheruiyot Год назад +2

    i got so much inspiration on the songs of the AIC keep the fire burning praising God, coz the same songs will be used to heal souls and lift spirits in worship God bless you and your ministry

  • @aziramartine252
    @aziramartine252 Год назад +2

    Nimebarikiwa na ujumbe,production iko on point waimbaji wamejua kutumia position zao za utumishi walionao Mungu azidi kuwainua🙏

  • @MagrethMagulu-pj3cm
    @MagrethMagulu-pj3cm Год назад +2

    Aiseee we mtoto nimekukubali sn,Mungu azidi kukutumia

  • @ednalameck9783
    @ednalameck9783 Год назад +3

    The cvc I know❤❤❤❤❤❤

  • @ruthjonathan4361
    @ruthjonathan4361 Год назад +1

    Hongrereni kazi nzuri Mungu awabarki

  • @yohanadaniel7030
    @yohanadaniel7030 Год назад +1

    Mungu awatunze, kazi nzuri sana hakika ni patakatifu

  • @vanipembe7819
    @vanipembe7819 Год назад +2

    Mungu awalinde na kuwatunza wapendwa

  • @estherapologise8280
    @estherapologise8280 Год назад +1

    Amen🙌hakika Mungu umeketi mahali PATAKATIFU🙏

  • @warrenhenrick5565
    @warrenhenrick5565 Год назад +1

    Hakika Mungu wetu ameketi mahali pa juu sana patakatifu amezungukwa na maserafi na makerubi wimbo mzuri sana barikiwa sana cvc❤

  • @lucypaulo9238
    @lucypaulo9238 Год назад +2

    Mbarikiwe sana watumishi

  • @trophywilson7211
    @trophywilson7211 9 месяцев назад +3

    Huo ndio Uimbaji wa nyimbo za kumwinua Mungu, Nabarikiwe Mno

  • @GetrudaPeter-k3p
    @GetrudaPeter-k3p 6 месяцев назад +2

    Mungu awatunze❤

  • @shedrackdaudi3403
    @shedrackdaudi3403 Год назад +2

    Niko apa nangoj jiwe lingine nawaamn san hawa watu hawajawahi kosea

  • @donaldjohn9103
    @donaldjohn9103 Год назад +1

    Amen cvc ahsantee kwa kwazi iliyo tukuka

  • @elishasamwel1783
    @elishasamwel1783 Год назад +2

    Mnatisha sana CVC kila baada ya miezi ata sita mngekuwa mnatubariki na wimbo njia vizuri balaa sina kwaya pendwa nyingine zaidi yenu

  • @moronayou5148
    @moronayou5148 Год назад +3

    Glory be to God 🙏

  • @priscamakwetta740
    @priscamakwetta740 Год назад +1

    Woooooow woooooow woooooow Kaz yenu Ni njema Sana...I'm happy to see my singer mfeloo... amaizing work..mnajua na mnajua Tena . MUNGU awabariki

  • @MageJoseph-b6i
    @MageJoseph-b6i 7 месяцев назад +2

    Barikiwa san wimbo mzuri

  • @victoriansolo3842
    @victoriansolo3842 Год назад +1

    Hongereni sana wanac.v.c nawapenda

  • @kalovwendunga8103
    @kalovwendunga8103 Год назад +1

    Wewe ni mtakatifu
    Wow

  • @isackkidaso9030
    @isackkidaso9030 Год назад +1

    Mungu awalinde zaidi

  • @allanlwambo9066
    @allanlwambo9066 Год назад +1

    Mungu aneishi Mahali Patakatifu Azidi Kuwainua na kuwapandisha viwango na viwango vya Juu. Mbalikiwe sana!!

  • @famaramedia
    @famaramedia Год назад +1

    Mungu awabariki kwa wimbo mzuri sana

  • @magrethmkemwa9287
    @magrethmkemwa9287 11 месяцев назад +1

    Watu waimbe nyimbo hizi❤,Shetan ataiba je,🔥🔥wimbo kama huu,Mbarikiwe Sana Chan'gombe

  • @bensonlobulu
    @bensonlobulu 11 месяцев назад +2

    Dah nimesikiliza nyingi Ila hii ni zaidi ya utukufu mbarikiwe sana

  • @widsonswalala9696
    @widsonswalala9696 Год назад +1

    Hakika ni Mungu pekee ndiye anastahili kuhimidiwa

  • @milkamanyanda7509
    @milkamanyanda7509 Год назад +1

    Mtakatifu,mtakatifu,hakika u mwema maishani.

  • @AnithaTrm
    @AnithaTrm 10 месяцев назад +2

    Patakativu ni nyimbo nzuri sana by ndibalema

  • @yasintaendaki654
    @yasintaendaki654 Год назад +1

    We blessed na Mungu azidii kuwabariki pia❤️🙏

  • @MistaToo
    @MistaToo Год назад +1

    Nawaenzi sana wanakwaya wa A.I.C Chang'ombe tangu enzi za Tunda la Roho mpaka sasa nyie ni wa baraka ❤

  • @leahjonathan9726
    @leahjonathan9726 Год назад +1

    Mungu wewe ni Mtakatifu hakika!!

  • @jeffchamah145
    @jeffchamah145 Год назад +1

    Amen...May God bless you all ...For the new song...Hongera

  • @Seniorcaptain
    @Seniorcaptain Год назад +1

    Mungu uketi katikati ya sifa,barikiwe CVC

  • @ruthmagulu4896
    @ruthmagulu4896 Год назад +1

    My Team Hongereni sana

  • @DanfordJohan-zd1cg
    @DanfordJohan-zd1cg 9 месяцев назад +7

    Hawa wamama huwa wanaimba vzr hasa uyu mama wakwanzaa jmn anaimba kwa utulivu. Lkn niliwai kuja kanisan kwenu nimehudhuria mwez mzima kila nikienda kanisan kwao nia yangu niwaone wakiimba live wakisoro lkn sikuona wakisoro je wameacha kuimba? Nilkua naona wanasoro wengne tu nilkua naumia maana mm nilikuwa nakuja kusali ili niwaone tu😂😂 mnijuze jmn wamestaafu ama

    • @AICTChangombeChoir_
      @AICTChangombeChoir_  8 месяцев назад

      Wapo mtumishi

    • @SeraphineLihimba
      @SeraphineLihimba 8 месяцев назад

      Hata mimi kwaya hii naipenda sana wabarikiwe wote. Mwenyezi Mungu anakusudi kuwaunganisha wao, natuinjilishe ktk Uumbaji. siku Moja nitakuja kuwatembelea.

  • @Nhabato5599
    @Nhabato5599 8 месяцев назад +1

    Nabarikiwa sana na kwaya hii CVC Mungu azidi kuwatunza nakuwainua, Mimi ni Muumini wa nyimbo za aina hii❤

  • @boazkitela6960
    @boazkitela6960 Год назад +2

    Mama Diana James wow❤

  • @livinohaule8442
    @livinohaule8442 Год назад +1

    Wimbo mzuri. Sanaa yake ya juu sana. Ahsante na mbarikiwe

  • @sylivansaaga366
    @sylivansaaga366 Год назад +1

    Hongereni sana cvc Mungu azidi kuwainua na kuwatumia

    • @hawamdee8811
      @hawamdee8811 Год назад

      Ninaomba mungu siku moja nije na niingie cvc tuimbe pamoja big up watumishi

  • @naahmkama8789
    @naahmkama8789 Год назад +2

    My favorite song

  • @dadysfavourite1963
    @dadysfavourite1963 Год назад +1

    Brove 🎉our might God keep u all

  • @yohananchama
    @yohananchama Год назад +1

    Nimebalikiwa sana

  • @aghatamaziku6173
    @aghatamaziku6173 Год назад +1

    Nimeipenda hii jmn Mungu awabariki sana ❤

  • @mathewanthony5819
    @mathewanthony5819 Год назад +1

    Waiting 😊😊😊

  • @lawrencekameja9730
    @lawrencekameja9730 Год назад +1

    Nimeipenda sana hii

  • @GoliamaAndrew
    @GoliamaAndrew 7 месяцев назад +2

    Jamani hii kwaya kwakweli Wana nipako sana nitakujiunga nanyi nafanyaje.

  • @ndindapurity1210
    @ndindapurity1210 Год назад +2

    I've been looking for this song for a long time, saw it in one of your previous albums but couldn't find it here. I'm blessed like very blessed

  • @alicemmbone2260
    @alicemmbone2260 Год назад +1

    Waiting❤❤❤

  • @ecabelmwai3474
    @ecabelmwai3474 Год назад +1

    Such a beautiful song beautiful composition

  • @salomegunga5300
    @salomegunga5300 Год назад

    AMEN mtakatifu ni Mungu pekee mbarikiwe sana

  • @metrojordan6387
    @metrojordan6387 Год назад +1

    Am blessed from this song 🙏🏼🙏🏼 God is great

  • @janewayua5333
    @janewayua5333 Год назад +1

    Such a nice song, congrats the changombes

  • @marcosyohana1605
    @marcosyohana1605 Год назад

    Baadaye mtuletee wimbo wa tumetumwa na ule wa samehe usamehewe

  • @clementlugoda7870
    @clementlugoda7870 Год назад +1

    Hongereni sana kwa utume!

  • @meshackwilson1909
    @meshackwilson1909 Год назад +1

    Utukufu kwa Mungu

  • @marthankola3316
    @marthankola3316 Год назад +2

    Glory to God🙌

  • @agapejosceline8262
    @agapejosceline8262 Год назад

    Mu batikiwe zaidi.
    Na kumbuka ule wimbo wa "gusa" nawa "jiwe"

  • @juntwakabete1664
    @juntwakabete1664 Год назад +1

    God bless you mmebadilisha maisha yangu🙏

  • @barnabasmollel8797
    @barnabasmollel8797 Год назад +1

    Sifa na Utukufu Kwa Mungu

  • @ecabelmwai3474
    @ecabelmwai3474 Год назад +1

    Mmeuwaaaaaaa what a beautiful song

  • @erickdoss7274
    @erickdoss7274 Год назад +1

    Kudos to you CVC for such an awesome worship masterpiece 👏

  • @micahmutinda3755
    @micahmutinda3755 Год назад +1

    Mungu ni mtakatifu.

  • @Rii_home_store
    @Rii_home_store Год назад +1

    weiting 🔥🔥🔥

  • @lucymukhavi1405
    @lucymukhavi1405 Год назад +1

    Isaiah 6. Revelation 4. Be blessed AICT as God uses y'all as His vessels. I'm so much blessed. ❤

  • @PatrickKavoo-b4y
    @PatrickKavoo-b4y Год назад +1

    Am blessed

  • @Yusufumoses-w5y
    @Yusufumoses-w5y 10 месяцев назад +1

    Ameeeeeeeen mbarikiwe sana

  • @felixkyalo2243
    @felixkyalo2243 Год назад

    Mtakatifu Mtakatifu ni Bwana! Amina

  • @thentuzumusic
    @thentuzumusic Год назад

    Ujumbe mzr

  • @ivonaaganyira8462
    @ivonaaganyira8462 Год назад +2

    😩❤️

  • @julietmoonka183
    @julietmoonka183 Год назад

    Blessings 🔥🔥🔥🔥 Please upload the first version of the song

  • @everinemusomba6787
    @everinemusomba6787 Год назад

    Mungu ni Mtakatifu asante Kwa wimbo nzuri bt video ya kwanza ya Patakatifu ilikuwa na kasoro kidogo neema ya Mungu iwe nanyi

  • @amospaul8473
    @amospaul8473 7 месяцев назад +1

    Nice song

  • @mubukuropceachurchchoir1617
    @mubukuropceachurchchoir1617 Год назад

    Waiting to be blessed

  • @EmmanuelythomasMponeja
    @EmmanuelythomasMponeja Год назад

    Mungu mwema

  • @Rii_home_store
    @Rii_home_store Год назад

    Patakatifu🎉

  • @andrewmatheka9749
    @andrewmatheka9749 Год назад

    Patakatifu kweli...
    My favorite choir ..

  • @pendongerageza6020
    @pendongerageza6020 Год назад +1

    Amina