SIMULIZI YA SAUTI : FEEL MY HEART ❤ SEHEMU YA: 01

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 21 окт 2024
  • Majira ya usiku mtulivu sana, wanakijiji walikuwa wamelala kwa utulivu mzuri hakukuwa na kelele wala vurugu za aina yoyote ile maana ilielekea saa nane hivi?
    Katika nyumba moja wapo za kijiji kimoja wapo huko Tanga kwa wabondei. Kijana aliefahamika kwa jina Khalfan alikuwa kalala kwa utulivu wa hali ya juu kitandani kwake. Nje ya nyumba yake ya mbuzi walianza kutoa sauti ya tahadhari, na Khalfan alikuwa na usingizi mwepesi sana hakuweza kustahimili kuwasikia mbuzi wakitoa sauti hovyo kisha alale, aliinuka na kwenda kushuhudia kinachoendelea huko.
    Alipofungua tu mlango atoke nje alikabwa kaba lake na mtu ambae hakumfahamu kwa haraka sana wakati huo. Mtu huyo alikuwa na nywele laini sana kwa asili isiyoeleweka Khalfan alihisi labda kavamiwa na jini.
    " nisitiri usiku huu, hakikisha unanipa hifadhi nzuri nitakuwa msaada wako hapo baadae, kwa leo tu na asijue yeyote nipo kwako" aliongea mtu huyo huku akihema kwa nguvu sana. Khalfan alimeza mate mfululizo na kuhisi labda kuna watu walikuwa wakimkimbiza huyo mtu. Alikuwa na wasiwasi sana je angempa hifadhi mwanadamu aliemuingilia Majira ya usiku wa manane kama hivyo? Au alifaa kufanya nini mbona mambo yalikuwa karibu kumuelemea tayari?.
    "Mhhkkh!" Khalfan aligugumia akitamani aachiwe shingo yake iliyokabwa. Baada ya kuachiwa alijiweka sawa kisha akasogea hadi mlangoni kwake akachungulia kwenye tobo dogo la mlango akagundua wazi kwamba mtu huyo alikuwa akikimbizwa na kundi la watu. Aliwaza apige kelele ama aache tu? Uoga ulimjaa maana mtu mwenyewe hakumfahamu hata kidogo.
    #ankojaysimulizi #diamondplatnumz #simulizimedia #simulizizamaisha #film #simulizimix #simulizizamapenzi #zuchu #wasafi #film #drama #storytime #shorts #channel

Комментарии • 13