Это видео недоступно.
Сожалеем об этом.

Matendo 3:1-11|| Petro na Yohana wamponya Kiwete

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 25 апр 2024
  • MATENDO YA MITUME 3:1-11.
    "Petro na Yohana wamponya Kiwete"
    1 Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa.
    Matendo ya Mitume 3:1
    2 Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu.
    Matendo ya Mitume 3:2
    3 Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.
    Matendo ya Mitume 3:3
    4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.
    Matendo ya Mitume 3:4
    5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.
    Matendo ya Mitume 3:5
    6 Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.
    Matendo ya Mitume 3:6
    7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.
    Matendo ya Mitume 3:7
    8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.
    Matendo ya Mitume 3:8
    9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu.
    Matendo ya Mitume 3:9
    10 Wakamtambua, ya kuwa yeye ndiye aliyekuwa akiketi na kuomba sadaka penye mlango Mzuri wa hekalu; wakajaa ushangao wakastaajabia mambo yale yaliyompata.
    Matendo ya Mitume 3:10
    11 Basi alipokuwa akiwashika Petro na Yohana, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana.
    Matendo ya Mitume 3:11

Комментарии • 1