Hii aya ya Kun faya kun imetokea mara kadhaa kwenye Quran Hizi hapa namba ya surah na namba ya aya: 2:117- Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi, na anapotaka kitu hukiambia tu: Kuwa, kikawa. 3:47- Maryamu alijibu: 'Ewe Mola wangu! nitapataje mwana na hali hakuna mtu aliyenigusa? Akasema: Kama vile Mwenyezi Mungu huumba apendavyo. Anapoamua (kufanya) kazi fulani, Anaiamrisha tu 'Kuwa', na inakuwa. 3:59- Hakika mfano wa Isa (Yesu) mbele ya Mwenyezi Mungu ni sawa na ule wa Adam aliyemuumba kwa udongo, kisha akamwambia: Kuwa! Naye akawa. 6:73 Na Yeye ndiye Aliyeziumba mbingu na ardhi (kwa haki). Na Siku Atakaposema: Kuwa! Neno lake ni kweli. Na ufalme utakuwa wake Siku itakapo pulizwa Baragumu. Yeye (ndiye ambaye) ana elimu ya ghaibu na yanayoonekana, na ni Mwenye hikima, Mwenye khabari. 16:40 - Amri yetu kwa jambo si ila tu kwamba tunapo kusudia (kuwapo) tunakiambia: Kuwa, na huwa. 19:35- Si utukufu wa Mwenyezi Mungu kuwa amfanye yeyote kuwa mwana. Yeye ni Mtakatifu na Mtukufu (juu ya haya)! Anapohukumu jambo lolote huliambia tu: Kuwa, nalo huwa. 36:77-83 Je! Na wanabishana nasi - wamesahau kuwa wameumbwa - wakisema: "Ni nani atakayeihuisha mifupa iliyoharibika?" Sema, ewe Mtume, “Watahuishwa na aliye waumba mara ya kwanza, kwa kuwa Yeye ana ujuzi kamili wa kila kiumbe. ^Yeye ndiye anaye kupeni moto katika miti mibichi, na tazama, mnawasha moto kutoka kwayo. Je, hawezi aliyeziumba mbingu na ardhi kuwafufua hawa makafiri? Ndiyo ˹Anaweza! Kwani Yeye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi wa yote. Kinachohitajika, anapotaka kitu fulani kiwe ni kukiambia tu: “Kuwa!” Na ndivyo! Basi ametakasika Yule ambaye Mikononi Mwake umo uweza juu ya kila kitu, na Kwake Yeye peke yake mtarejeshwa. 40:68- Yeye ndiye anayehuisha na anayefisha. Basi anapo amua jambo huliambia tu: Kuwa, ndivyo kikawa.
Mashaallah 😢😢😢
Aya hio ni sura gani imamu
Hii aya ya Kun faya kun imetokea mara kadhaa kwenye Quran
Hizi hapa namba ya surah na namba ya aya:
2:117- Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi, na anapotaka kitu hukiambia tu: Kuwa, kikawa.
3:47- Maryamu alijibu: 'Ewe Mola wangu! nitapataje mwana na hali hakuna mtu aliyenigusa? Akasema: Kama vile Mwenyezi Mungu huumba apendavyo. Anapoamua (kufanya) kazi fulani, Anaiamrisha tu 'Kuwa', na inakuwa.
3:59- Hakika mfano wa Isa (Yesu) mbele ya Mwenyezi Mungu ni sawa na ule wa Adam aliyemuumba kwa udongo, kisha akamwambia: Kuwa! Naye akawa.
6:73 Na Yeye ndiye Aliyeziumba mbingu na ardhi (kwa haki). Na Siku Atakaposema: Kuwa! Neno lake ni kweli. Na ufalme utakuwa wake Siku itakapo pulizwa Baragumu. Yeye (ndiye ambaye) ana elimu ya ghaibu na yanayoonekana, na ni Mwenye hikima, Mwenye khabari.
16:40 - Amri yetu kwa jambo si ila tu kwamba tunapo kusudia (kuwapo) tunakiambia: Kuwa, na huwa.
19:35- Si utukufu wa Mwenyezi Mungu kuwa amfanye yeyote kuwa mwana. Yeye ni Mtakatifu na Mtukufu (juu ya haya)! Anapohukumu jambo lolote huliambia tu: Kuwa, nalo huwa.
36:77-83 Je! Na wanabishana nasi - wamesahau kuwa wameumbwa - wakisema: "Ni nani atakayeihuisha mifupa iliyoharibika?" Sema, ewe Mtume, “Watahuishwa na aliye waumba mara ya kwanza, kwa kuwa Yeye ana ujuzi kamili wa kila kiumbe. ^Yeye ndiye anaye kupeni moto katika miti mibichi, na tazama, mnawasha moto kutoka kwayo. Je, hawezi aliyeziumba mbingu na ardhi kuwafufua hawa makafiri? Ndiyo ˹Anaweza! Kwani Yeye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi wa yote. Kinachohitajika, anapotaka kitu fulani kiwe ni kukiambia tu: “Kuwa!” Na ndivyo! Basi ametakasika Yule ambaye Mikononi Mwake umo uweza juu ya kila kitu, na Kwake Yeye peke yake mtarejeshwa.
40:68- Yeye ndiye anayehuisha na anayefisha. Basi anapo amua jambo huliambia tu: Kuwa, ndivyo kikawa.
Yasin
MaashaAllah
Aamiin 🤲
Amiin