MHE. RAIS AMETUTEUWA TUKATATUE KERO ZA WANANCHI: RC. NAWANDA

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 5 сен 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa wilaya zote za Mkoa wa Simiyu kutenga siku moja katika wiki ya kusikiliza kero na migogoro ya wananchi.
    Akiwa katika ziara yake ya Kwanza ya Kujitambulisha Wilayani Itilima Mhe. Dkt Nawanda alisema ya Kwamba Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametuteua tukasikilize na kutatua kero na migogoro ya Wananchi
    Aidha Mhe. Nawanda alitahadharisha Kwa kusema " isitokee siku, katika siku zilizopangwa Wananchi kuto sikilizwa, wasikikizwe hata kama ni Saa tisa usiku"
    Mkuu wa Mkoa huyo alitaka zoezi hilo kuanza mapema wiki ijayo na Kamati ya utatuzi wa kero za wananchi Mwenyekiti wake atakua Mkuu wa Wilaya na Katibu atakua Katibu tawala wa Wilaya.
    Aidha kamati hiyo itajumuisha wajumbe wengine wa Kisekta kama Maafisa Ardhi, Mwanasheria wa Halmashauri na Afisa Mipango wa Halmashauri.
    ‪@MsemajiMkuuwaSerikali‬

Комментарии •