KWANINI MTUME MUHAMMAD S.A.W HAITWI MAREHEMU..???
HTML-код
- Опубликовано: 7 фев 2025
- Jina lake ni Mohammad bin Abdallah bin Abdul mutwalib bin hashim bin Abdul manaf bin Quswai bin kilaab. Na ukoo wake mtukufu unamalizikia kwa mtume Ibrahiim (A.S)
MAMA YAKE.
Mama yake ni Amina binti Wahabi bin Abdul manafi bin zuhra bin kilaab.
KUNIA YAKE NI:
Abul qaasim, pia Abuu Ibrahiim.
JINA LAKE MASHUHURI.
1- Mustafa, na anayo majina mengine mengi yaliyo pokelewa ndani ya Qur’ ani tukufu kama:
2- Khaatamun nabiyyiin. 3- Al ummiyyi. 4- Al muzammil. 5- Al mudathir. 6- Al mubiin. 7-Al kariim.
8- An nuur. 9- An niima. 10- Ar rahmaan. 11- Ash shaahid. 12- Al mubashir.13- An nadhiir. 14- Abdur rauuf. 15- Ar rahiim. 16- Ad daai na mengine mengi.
TAREHE YA KUZALIWA KAKE.
Alizaliwa tarehe 17 mwezi wa Rabiiul awwal, mwaka wa tembo sawa na mwaka 571 H.D.kutokana na kauli iliyo mashuhuri kwa mashie, na kauli nyingine inasema ya kuwa alizaliwa tarehe 12 mwezi wa Rabiul awwal mwaka huo huo.
SEHEMU ALIPO ZALIWA.
Alizaliwa katika mji wa makkatul mukarramah ulioko katika nchi ya Saudi Arabia.
KUPEWA KWAKE UTUME.
Ali pewa rasmi utume tarehe 27 mwezi wa rajab katika mji wa makka baada ya kutimiza miaka 40 ya umri wake mtukufu.
MAFUNDISHO YAKE.
Mtume (s.a.w) alikuja na wito wa usawa kwa viumbe wote, na alikuwa akilingania udugu, na msamaha kwa kila mwenye kuingia kwenye Dini ya ki islaam, kisha aliweka sheria iliyo nyepesi, na kanuni za uadilifu alizo zipokea kutoka kwa Mwenyezi Mungu alie takasika, kisha waislaam wakazipokea kutoka kwa Mtume (s.a w).
MIUJIZA YAKE.
Muujiza wake pekee wa milele na milele ni Qur’ ani tukufu; ama miujiza yake iliyo dhihiri mwanzoni mwa uislaam ni mingi sana kwani hai hesabiki.
WITO WAKE.
Mtume (s.a.w) ali walingania watu kwenye upweke wa Mwenyezi Mungu katika mji wa makka na kwa njia ya siri kwa muda wa miaka mitatu, na baada ya kipindi cha siri ali waita watu kwa njia ya wazi kwa muda wa miaka kumi.
KUHAMA KWAKE.
Alihama kutoka katika mji wa makka kwenda madina mwanzoni mwa mwezi wa rabiul awwal baad ya kupita miaka 13 tangu kupewa utume, na kuhama huko kulitokana na maudhi mengi ya makuraishi, mushrikina na mkafiri kumuelekea yeye na maswahaba wake.
VITA VYAKE.
Mwenyezi Mungu alie takasika alimpa idhini ya kuwapiga vita mushrikina na makafiri na wanafiki, na baada ya idhini hiyo aliweza kuingia kwenye mapambano na watu hao kwenye vita vingi sana, na kati ya hivyo vilivyo kuwa mashuhuri ni Badri, Uhudi, Khandaq (Al ahzaab) Khaibar, na Hunain.
#KWANINIMTUMEMUHAMMADSAWHAITWIMAREHEMU #kifochamtumemuhammad #historiayamtumemuhammad #marehemu #maishayamtume #kufakwamtume #HAIFAIKUMITAMAREHEMU #HAIFAIMTUKUITWAMAREHEMU
WAKEZE MTUME (S.A W).
Mtume alikuwa na wanawake kadhaa: Wakwanza ni Khadija binti Khuwailid (Rehma za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake),na huyu ndie mwanamke wa kwanza wa Mtume (s.a.w), ama wengine ni : 2-Sauda binti zum’a, 3- Aisha binti abi baker, 4- Ghuzya binti dudaan (ummu shariik) 5- Hafswa binti omar, 6- Ramla binti abii sufyan (ummu habiibah), 7- Ummu salmah binti umayyah, 8- Zainab binti Juhsha, 9- Zainab binti Khaziimah, 10- Maimuna bintil Harithi, 11- Juwairia bintil Haarithi, 12- Swafia binti Hayyi bin Akhtwab.
WATOTO WAKE MTUME (S.AW).
Watoto wake ni kama wafuatao: 1- Abdallah. 2- Qaasim. 3- Ibrahiim (a.s) 4- Fatimatuz zahraa (a.s).na kuna kauli zingine zisemazo kuwa Zainab, Ruqayya, na ummu kulthum ni wanawe pia.
BABA ZAKE WADOGO.
Mtume (s.a.w) ana baba wadogo tisa (9), nao ni watoto wa abdul mutwalib kama wafuatao: 1- Al haarith. 2- Zubair. 3- Abu twalib. 4- Hamza. 5- Al ghidaaq, 6- Dharaar Al muqawwim, 7- Abu lahab. 8- Al abbas.
SHANGAZI ZAKE MTUME (S.AW).
Mtume (s.a.w) alikuwa na shangazi sita kutokana na akina mama tofauti nao ni kama wafuatao: 1- Umaimah. 2- Ummu hakiimah. 3- Burrah. 4- Aatikah. 5- Swafiyyah. 6- Arwy.
MAWASII WAKE MTUME (S.A.W).
Mawasii wake ni kumi na mbli,nao ni kama wafuatao: 1- Amirul muuminnina Ally bin abii twalib (a.s). 2- Hassan bin Ally (a.s) 3- Hussein bin Ally (a.s) 4- Ally bin Hussein (a.s). 5- Mohammad bin Ally ( a.s) 6- Jaafar bin Mohammad (a.s) 7- Mussa bin Jaafar (a.s) 8- Ally bin Mussa (a.s) 9- Mohammad bin Ally (a.s) 10- Ally bin Mohammad (a.s) 11- Hassan bin Ally (a.s) 12- Al hujjat binil Hassan (Mohammad mahdii ) (a.s).
MLINZI WAKE.
Mlinzi wake alikuwa ni Anas.
WAIMBAJI MASHAIRI WA MTUME (S.A.W).
1 - Hassan bin Thabiti. 2- Abdallah bin Rawaha. 3- Kaab bin Maalik.
WAADHINI WA MTUME (S.A.W).
1- Bilal Al -habashi 2- Ibnu ummu makhtuum. 3- Saad Al-qurt.
NEMBO YA PETE YA MTUME (S.A.W).
Nembo ya pete yake ilikuwa ni (( Mohmmad rasuulu llah)).
UMRI WAKE (S.A.W).
Ali ishi kwa muda wa miaka 63.