"Jella Mtagwa ameteseka sana nilikuwa naishi nae, sitaki kuogea nitalia" Tino, Tenga wafunguka
HTML-код
- Опубликовано: 17 май 2024
- Mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars , Pan Africa na Majimaji ya Songea Peter Tino amehudhuria mazishi ya Nguli Jella Mtagwa ambaye amezikwa mkoani Morogoro Mei 18, 2024.
Tino amesema kutokana na Mambo mengi aliyoyafanya Mtagwa enzi za uhai wake alitakiwa kuzikwa na bendera ya taifa lakini haikuwa hivyi. Amesisitiza kuwa Heshima aliyoiletea nchi hii mwaka 1974 hali iliyomfanya awekwe kwenye stempu ambapo alifahamika dunia nzima alipaswa kuzikwa kwa heshima zote.
Hata hivyo Tino amesema enzi za uhai wa rafiki yake Jella Mtagwa waliwahi kuishi nyumba moja jijini Dar es salaam na walikaa chumba kimoja hivyo kwake huu ni msiba mzito.
Nae, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo hapa nchini (BMT) na mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ ni miongoni mwa waliohudhuria mazishi ya Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa Jella Mtagwa aliyefariki jijini Dar ea aalaam.
Tenga amesema msiba huo kwake ni pigo kubwa kwaku amecheza nae katika timu ya taifa hata timu ya Yanga pia wamecheza pamoja.
Poleni Sana ndugu zetu mwenyezi mungu awape wepesi
"Ukiwa huna kitu,kinyama cha mwitu",nimekuckia kk Peter Tino umeongea kwa machungu ya marehem kk Jella Mtagwa,lkn yote kwa yote tumshkr Allah kk amesitirika,yalobakia bac tuyapokee,Rabbi awafariji familia/ndg/jamaa wote pia wa tz WALIOGUSWA.
Nchi ngumu saana hii.., Allah amstiri jella. Amfutie dhambi zote.. AMIN
Nchi imejaa upuuzi na haipendi watu wake
Suala la Stamp ya Jella Mtagwa lilikuwa mwaka 1982 wakati wa Kombe la Dunia zilizofanyika Hispania. Haikuwa mwaka 1974.
Sawa sawa stamp ilikuwa ni 1982,pia mchezaji mwingine aliewahi kuwekwa ktk stamp kama kumbukumbu zng zipo sahihi ni MOHD CHUMA wa Mtwara(cjui kama yu hai au alishatangulia),hapo kk Peter kapitiwa kiduchu,wajua tena yote sbb ya MACHUNGU/CMANZI na MAYONZI kwa kjn mwenzie wa hey days.
Chuma kafariki
R.I.P nahodha nimelia nakumbuka enzi zake.umeongea ukweli.tino Alistahili heshima ya kitaifa.
Hakika kila nafsi itaonja umauti,enzi za utoto nilikuwa namsikia sana. yani bongo mpaka uwe chawa unakumbukwa
TANGANYIKA VIONGOZI IMANI NA HURUMA HAKUNA😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢
INASIKITISHA KUONA HAYA YANATOKEA.
Tenga ww ndiyo taperi mkubwa
Leodger Tenga huwezi kukwepa lawama kuhusu kutomjali Rafiki yako Jella Mtagwa. Ulipaswa kutoa misaada ya kumhudumia na kumkatia Bima ya afya rafiki yako. Hukufanya hivyo. Sina hakika pia kama ulishawahi kumtembelea kwake wakati akiugua. Wewe Tenga na wenzio wenye nafasi nzuri kimaisha mlimtupa rafiki yenu.
Wakati akiwa kiongozi wa TFF alitakiwa atengeneze utaratibu wa kuwaenzi hawa wenzake lakini hakujali na hata walipokua wanamfuata kumuomba msaada alikua anawakimbia.