RC SERUKAMBA : BENKI WEKENI MAZINGIRA WEZESHI YA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 окт 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba Amezitaka Benki zote Nchini kuweka mazingira wezeshi ya Mikopo na Riba nafuu kwa Wananchi ili kuondokana na mikopo ya Kausha damu.
    Ameyasema hayo leo Oktoba 3, 2024 wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la CRDB Lililopo katika Halmashauri ya wilaya ya kilolo, Mji mdogo wa Ilula.
    Mhe.Serukamba amesema kuwa Benki zinaweza kuweka utaratibu wa upatikanaji wa mkopo kwa muda mfupi ili kutatua changamoto kwa Wafanyabiashara kuondokana na mikopo ya kausha damu inayowatesa wananchi wengi katika kipindi hiki,
    Aidha Mhe. Serukamba amewataka wafanyakazi wa CRDB kubuni mikakati ya utoaji Elimu kwa Wananchi kuhusu umuhimu wa kutumia huduma za Benki.
    Mhe. Serukamba ametoa wito kwa Watanzania kujenga tabia ya kuweka akiba kwenye Benki pamoja na kutumia Huduma za Benki.
    Hata hivyo Mhe. Serukamba amemaliza kwa kuipongeza benki ya CRDB kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kufikisha huduma nzuri kwa Wananchi na kuwataka kuongeza juhudi ili Benki hiyo iwe mfano wa mafanikio ya kitaasisi huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwa pamoja nao katika kila hali.

Комментарии • 1

  • @ndukulusudikucho_
    @ndukulusudikucho_ 10 дней назад

    Kuomba ushauri wa Kifedha bank ni Sawa na teja kuomba ushauri kwa muuza madawa. Riba ni Kharamu na ndio inayo angamiza Mataifa yote yalio endelea Sasa na hawajui Shida ni Nini