KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY: FRIDAY PRAYERS 05/ 07/ 2024

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 4 июл 2024
  • KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY: FRIDAY PRAYERS 05/ 07/ 2024
    UJUMBE WA LEO: VITA YA KESHO YAKO
    [SEHEMU YA PILI]
    Hagai 2 : 9
    Yoshua 2 : 8 - 11
    Kutoka 16 : 7
    Mambo ya Walawi 9 : 6
    1 Wafalme 18 : 36
    Kutoka 24 : 16
    Isaya 58 : 8
    Nehemia 1 : 11
    Ester 3 : 7

    Hagai 2 : 9
    9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi.
    Yoshua 2 : 8 - 11
    8 Tena kabla hawajalala akawaendea juu darini,
    9 akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa nchi wanayeyuka mbele yenu.
    10 Maana tumesikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng'ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na Ogu, mliowaangamiza kabisa.
    11 Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini.
    Kutoka 16 : 7
    7 na asubuhi ndipo mtakapouona utukufu wa Bwana; kwa kuwa yeye asikia manung'uniko yenu mliyomnung'unikia Bwana; na sisi tu nani, hata mkatunung'unikia?
    Mambo ya Walawi 9 : 6
    6 Kisha Musa akasema, Neno aliloliagiza Bwana kwamba mlifanye ni hili; na huo utukufu wa Bwana utawatokea.
    1 Wafalme 18 : 36
    36 Ikawa, wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, Eliya nabii akakaribia, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo ya kuwa wewe ndiwe Mungu katika Israeli, na ya kuwa mimi ni mtumishi wako, na ya kuwa nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.
    Kutoka 24 : 16
    16 Na huo utukufu wa Bwana ukakaa juu ya mlima wa Sinai; lile wingu likaufunikiza siku sita; na siku ya saba akamwita Musa toka kati ya lile wingu.
    Isaya 58 : 8
    8 Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa Bwana utakufuata nyuma ukulinde.
    Nehemia 1 : 11
    11 Ee Bwana, nakusihi, litege sikio lako, uyasikilize maombi ya mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako, wanaofurahi kulicha jina lako; nakuomba sana; unifanikishe mimi, mtumishi wako, leo, ukanijalie rehema mbele ya mtu huyu. (Maana, nalikuwa mnyweshaji wa mfalme).
    Ester 3 : 7
    7 Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari.

    AGENDA ZA MAOMBI
    1. Kumshukuru Mungu na Kuomba Toba kwa nusu mwaka 2024
    2. Kuombea kila wazo la Kukufanikisha alilokupa Bwana.
    3. Omba Watu sahihi (Vision Connections)
    4. Omba Utukufu wa Bwana katika maisha yako.
    5. Kushughulikia Vifungo kwenye Miguu.
    Mhubiri: Mwl. Eng. Googluck Mushi.
    Kwa maombi na ushauri :
    Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
    Mch. Msaidizi: Anna Kuyonga
    Simu: +255 713 553 443
    RUclips: Kijitonyama Lutheran church
    Barua Pepe: Kijitonyamalutheran@gmail.com

Комментарии • 8