Alilipa Deni zangu | Song: Pendo Kuu | Mamajusi Choir | Lyrics

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 5 окт 2024
  • Song: Pendo Kuu
    Artist: Mamajusi Choir
    Song Lyrics:
    Verse 1
    Pendo kuu la Yesu
    lilitosha Kalvari
    Msamaha wa dhambi
    niliupata Kalvari
    Alinipenda Yesu
    Akaingia gharama
    Msamaha wa dhambi
    niliupata Kalvari
    Chorus:
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi
    niliupata Kalvari
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi
    niliupata Kalvari
    Verse 2
    Yesu Atuchunga,
    Mchunga Wetu
    Naye Atufuta
    machozi yetu
    Mkononi Mwake
    hatuna hofu
    Daima twapata
    kwake wokovu
    Chorus:
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari
    Verse 3
    Namtolea Yesu
    Nampa moyo wote
    Ntampenda Yesu namwandama kila saa
    Chini ya msalaba
    nataka simama
    Ndiye mwamba safarini
    Kwa kivuli chema
    Chorus:
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari
    Verse 4
    Nataka nifahamu
    nizidi kupambanua
    Mapenzi Yake nifanye
    yanayompendeza
    Nataka nikae naye
    kwa mazungumzo
    Nizidi kuwaonyesha
    wengine wokovu Wake
    Chorus:
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi
    niliupata Kalvari
    Alilipa deni zangu,
    kwa gharama ya mauti
    Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari Msamaha wa dhambi niliupata Kalvari

Комментарии • 1,1 тыс.

  • @eliamancharles-k3g
    @eliamancharles-k3g 9 месяцев назад +485

    wale tunasikiliza wimbo huu Bila kuchoka 2024 tujikusanye hapa❤❤

  • @philyskasaya7317
    @philyskasaya7317 Месяц назад +32

    Wale bado tuko hapa 23/8/2024 weka Tick ili niweze kurudi hapa na kuusikiliza huu wimbo tena

  • @stellaadhiambo2159
    @stellaadhiambo2159 4 месяца назад +53

    Team 15th May 2024 wapy likes za Yesu Christu kutufilia msalabani

  • @marselinadena7618
    @marselinadena7618 Год назад +102

    Kuna nyimbo wanadamu tunatunga na humpendeza Mungu saana. Ila kuna nyimbo pia Roho mtakatifu huziandaa na kutufundisha ili kumwimbia Mungu wetu, huu wmbo mtunzi naweza sema alishushiwa direct na Roho mtakatifu. ♥️ huu wimbo ukiusikia utaogopa kabisa kutenda dhambi

    • @moseskirimbay1791
      @moseskirimbay1791 6 месяцев назад +5

      Huu wimbo una hisia kali sana na unapenya mpaka rohoni

    • @IsayaGervas
      @IsayaGervas 6 месяцев назад

      ❤p​@@moseskirimbay1791

    • @AnnaBoniphace-dw7py
      @AnnaBoniphace-dw7py 6 месяцев назад +2

      Jmn kwel huu wimbo yaan ad unatamn kuacha mabay yote🙏😢

    • @LaurianMramba
      @LaurianMramba 6 месяцев назад +2

      Najikuta nalia ety😭

    • @sophiabernado2154
      @sophiabernado2154 5 месяцев назад +1

      😊😊😊

  • @MwanjoleMwatsuma-t2b
    @MwanjoleMwatsuma-t2b Месяц назад +8

    Eee MUNGU ni wa milele nyimbo hii imenikumbosha mbali sana hivyo ubarikiwe sana na MUNGU wa mbinguni atukumbuke soteni wenye imani ya kuamini ijili BWANA atutie nguvu ili tuushinde ulimwengu amen .

  • @jumahawa7272
    @jumahawa7272 2 месяца назад +8

    Mungu wangu 2024, ni mwaka wangu I need marriage family and blessing family........hakika bwana utatenda❤.....I believe and I trust Mungu wangu halali wala hachoki, pita kwangu bwana

  • @gracemushi5591
    @gracemushi5591 2 месяца назад +14

    Nabarikiwa sana na huu wimbo nasikiliza mara 10 zaidi kwa siku na sioni kutosheka Asante sana Yesu kwakunilipia Deni

  • @AngelinaMashaka
    @AngelinaMashaka 5 месяцев назад +2

    ❤❤ nabalikiwa sana na nyimbo hii

  • @moreenvinaywa3552
    @moreenvinaywa3552 6 месяцев назад +75

    Amen team 2024 bado mpo it's still fresh

  • @Sarahsnafulawamalwa
    @Sarahsnafulawamalwa Месяц назад +2

    Aki hii wimbo ni kama malaika ndio waliimba❤❤❤❤❤❤❤❤

  • @SamMbuvi-fp1wi
    @SamMbuvi-fp1wi 6 месяцев назад +18

    Yohana 19:30
    "Baada ya kuipokea hiyo siki, Yesu akasema 'imekwisha' akainamisha kichwa akakata roho."❤❤ Amen
    Kwa hakika yote yalikwisha msalabani mateso, laana, mashida, umaskini, mahaangaioko, chuki, visirani yote hayo alisena Yesu yamekwisha
    Don't give
    Keep praying
    "For our Lord God is mercyful and forgiving ". Daniel 9:9
    Be blessed God loves us 🤍🤍

  • @1stladyafrica402
    @1stladyafrica402 Год назад +105

    Nilikuwa nautafuta sana huu wimbo.Namshukuru Mungu ninausikiliza sasa hapa.Nampenda sana Yesu

  • @VannesaGasper-ph1kl
    @VannesaGasper-ph1kl 7 месяцев назад +34

    Naupenda Sana huu wimbo na unanibariki mno

  • @PriscillaMangale
    @PriscillaMangale 6 месяцев назад +2

    Alilipa deni zangu nimebarikiwa sana ❤❤❤

  • @geoffreylevi335
    @geoffreylevi335 4 месяца назад +12

    🙏🙏🙏🙏 ooh ooh ooh YESU YESU wangu...............hakika ingelikua sio wewe kunifia msalabani ningelikua wapi sasa hivi😭😭😭😭😭 Nikulipe nini Bwana Yesu wangu?????? Asante asante asante asante😭😭😭😭😭😭😭😭😭

  • @UninceOpiyo
    @UninceOpiyo 4 месяца назад +2

    Yesu alinilipia dhambi kweli ningekua wapi kama si yeye

  • @bumbuli4170
    @bumbuli4170 6 месяцев назад +30

    Here on Good Friday 2024 oh Lord have mercy on us 😭

  • @felexGidai
    @felexGidai 6 месяцев назад +4

    Kabisa pendo la MUNGU NI KUU

  • @dottymwats7535
    @dottymwats7535 Год назад +29

    Alilipa deni zangu. Msamaha wa dhambi zangu niliupata Kalvari. Kwa gharama ya mauti. Thank you Jesus

  • @StellamaketaMganda-im1qy
    @StellamaketaMganda-im1qy Год назад +1

    Msalaba kwetu ni ukombozi tunautazama huo tu

  • @MaryhannahMembe-ok4gu
    @MaryhannahMembe-ok4gu 2 месяца назад +3

    Msamaha wa dhambi niliipata calvary kwa Neema TU, 🙌🙌🙌🙌 alilipa deni zangu 😭😭😭😭🙇🙇, Asante Yesu.

  • @philisanyona8812
    @philisanyona8812 6 месяцев назад +17

    Mama yngu anapenda Sana wimbo huu, umejaa Sana baraka kila mda nikiieka mama huwa ana furahia❤🤍💖 nakupenda sana mama 🫶🫶

  • @mwanahamisiswedi3093
    @mwanahamisiswedi3093 6 месяцев назад +8

    Nimechelewa sana kuufahamu huu wimbo, nmebarikiwa 31/3/2024. Alilipa deni zangu kwa gharama ya mauti🙏

    • @amosnice1796
      @amosnice1796 6 месяцев назад

      We did on same day

    • @lydiamercy1121
      @lydiamercy1121 28 дней назад +1

      Yesu anakupenda sana mwanahamisi.Alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi.Problem is Muslims don't understand that Jesus is God alikuja duniani kama binadamu kutufia msalabani ili aweze kutusamehe tuweze kuenda mbinguni tuwe na yeye hujo milele.He died for you mpee moyo wako na utubu dhambi zako akusamehe.Yeye ni wa huruma mwingi.Be blessed kwa kuuskia huu wimbo

  • @FabiolaShirima
    @FabiolaShirima 5 месяцев назад +2

    Yani Kila ninapo usikiliza najikuta natikwa na machozi ya furaha hakika uu wimbo umeletwa kukutia faraja na amanin ya. Moyo❤️🙏

  • @aminambwambo622
    @aminambwambo622 Год назад +16

    YESU nakupenda sana nimejikana nimekuja kwako usiniache YESU

  • @ShakraaSam
    @ShakraaSam Месяц назад +1

    Msamaha wa dhambi tuliupata kalvali coz ya Upendo wa YESU kristo kwetu alikubali kudharauliwa kukataliwa na kutemewa mate...jamn! Tumsifu na kumtumikia na kumtukiza huyu YESU aliyetupenda na kuchukua makosa yetu 😢😢...❤ I love you Jesus

  • @EstherKamore
    @EstherKamore Год назад +12

    Tulipata msamaha Kalvari.Asante sana YESU🙏🙏🙏

  • @anzimsigwa6853
    @anzimsigwa6853 7 месяцев назад +8

    Msamaha wa dhambi niliupata calvary nakupenda YESU ❤

  • @nurumakweta1770
    @nurumakweta1770 Год назад +22

    Wimbo huu unagusa sn moyo wangu nampenda Yesu Kwa sababu ananipenda

    • @caritasmushi8896
      @caritasmushi8896 Год назад +1

      Asante Yesu kwa kutupenda jana leo na hata milele.Kama si wewe Yesu ningekuwa wapi mimi?🙏🙏🙏🤣

    • @josephmwasalanje2320
      @josephmwasalanje2320 Год назад +1

      Kabisa pastor yaani Sina la kusema

    • @nigananurunjema
      @nigananurunjema Год назад +1

      Angalia Garai neni Zimpraise kitu Cha Zimbabwe wamekopi Mamajusi wanafeli wapi?

  • @cyrillahmubatsi5743
    @cyrillahmubatsi5743 5 месяцев назад +2

    Alilipa deni zangu kwa gharama ya mauti msamaha wa dhambi niliupata kalvari ❤. Jesus Christ is the way the truth and the light.

  • @njerimuigai2703
    @njerimuigai2703 6 месяцев назад +17

    I love listening to this song as it Blesses my heart.. Listening on 30/03/2024 at 12:05am

  • @RiseImanueli
    @RiseImanueli 8 месяцев назад +6

    Jaman MUNGU awabaliki watu wote walio imba huu wimbo una nguv za mungu

  • @saverycyprian2879
    @saverycyprian2879 10 месяцев назад +10

    Hakika wimbo huu ni Roho Mtakatifu kiongozi amefurika

  • @ElizabethKinya-vx2kf
    @ElizabethKinya-vx2kf 6 месяцев назад +2

    Mm naupependa huu wimbo Sanaa

  • @RoseKapaya-w8r
    @RoseKapaya-w8r Год назад +11

    Wimbo unanikumbusha kuacha dhambi,🙏🙏🙏🙏

  • @LillianYatundu-yh2cn
    @LillianYatundu-yh2cn Год назад +7

    Moyo wangu wa kupenda yesu,,,, Asante kwa Kila kitu,, I bless you jesus

  • @praisetunes
    @praisetunes Год назад +75

    This song reminds me how God delivered me from alcohol and drug addiction. He transformed me to a healthy person ready to serve him. He indeed paid all my debts. I will serve him every single day of my life.

    • @livelyfacts
      @livelyfacts Год назад +3

      Same here 🙏fr God is good and sweet

    • @dottymwats7535
      @dottymwats7535 Год назад +1

      Amen

    • @mooney7704
      @mooney7704 Год назад +1

      Words me too.

    • @sethmartin6555
      @sethmartin6555 Год назад +1

      Praised be Lord Jesus, He fails at nothing when pursues someone. Praise Him, praise Him until it hurts.
      I too love Him so tenderly and am looking forward to obtain my healing that I need badly now. Thank You Jesus, thank You Holy Spirit, thank you Eternal Father. Blessed be Holy Trinity.

    • @salomegitau562
      @salomegitau562 Год назад +1

      Hallelujah 🙏🙏🙏🙏🙏

  • @QueenMainge
    @QueenMainge 10 месяцев назад +6

    Asanteee yesu kwa kulipa Deni zangu zotee asanteee Sana 💓

  • @gracedamas5883
    @gracedamas5883 Год назад +5

    Nampenda Yesu
    Alilipa deni zangu msamaha wa dhambi niliupata karvari
    Asante Bwana 👏👏👏

  • @CarolyneKaveza
    @CarolyneKaveza 7 месяцев назад +6

    Huu wimbo umeja upako Mungu tuone

  • @NANDIROSELYNE
    @NANDIROSELYNE 7 месяцев назад +10

    Wimbo huu ni baraka kwangu siku zote

  • @safiniasinyangwe4359
    @safiniasinyangwe4359 6 месяцев назад +5

    ♥️♥️♥️♥️ ASANTE YESU KWA KULIPA DENI LANGU 2024 🙏

  • @ruthandiba-wk7zc
    @ruthandiba-wk7zc 11 месяцев назад +9

    2023 Who else is here
    I will come back with a testimony

  • @catherinekambuamuthuka3641
    @catherinekambuamuthuka3641 Год назад +7

    Pendo kuu la Yesu lilitosha kalvari.

  • @JudithaJustine-b1u
    @JudithaJustine-b1u 10 месяцев назад +6

    Ilove jesus❤❤

  • @dianwilfred8541
    @dianwilfred8541 Год назад +5

    Asante Yesu kwa Nguvu zako sina cha kukulipa🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽

  • @esthercihenda958
    @esthercihenda958 Год назад +4

    Amen Amen nikweli kabisa apewesifa baba wa rehema Yesu Christ ni bwana.....

  • @victorkipkemboi7546
    @victorkipkemboi7546 Год назад +26

    Wimbo huu umejaa upako na roho mtakatifu anazungumza kupitia wimbo huu. Ubarikiwe sana nimepata utulivu moyoni mwangu

  • @KossyLidia-u3h
    @KossyLidia-u3h 6 месяцев назад +4

    Naupenda sana huu Wimbo na barikiwa sana,asante yesu

  • @RukiaSalum-z4l
    @RukiaSalum-z4l Год назад +6

    ❤❤Asante sana Mokozi Yesu mpe kila Mwenye huzuni furaha bwana. Kupitia wimbo huu

  • @MiriamRuguru-gl2tu
    @MiriamRuguru-gl2tu Год назад +13

    Kwa kweli Yesu ametulipia Kwa gharama kuu,nasikia kumpenda zaidi huyu Yesu ninaposikiza wimbo huu

  • @MonikaBakali
    @MonikaBakali 8 месяцев назад +5

    Sichoki kusikiliza huu wimbo siku miezi na miaka nakupenda sana

  • @rehemamwaka140
    @rehemamwaka140 6 месяцев назад +3

    Haleluyaa, msamaha tumeupata Kalvary hakika! Barikiweni wote mliouimba wimbo huu!

  • @SARAHMLANGA
    @SARAHMLANGA 6 месяцев назад +4

    Mlio tunga wimbo huu barikiwa sana unanikumbusha mbali sana huyu MUNGU aliko nitoa

  • @bettieluwuge
    @bettieluwuge 7 месяцев назад +7

    Kwa kweli wimbo huu unanigusa sana

  • @IucySalome
    @IucySalome 5 месяцев назад +1

    Naupenda huu wimbo Sana. Kaa si mungu singekua hapanilipo ❤❤ amen

  • @ROZALINENYIMBO-ke4jr
    @ROZALINENYIMBO-ke4jr 6 месяцев назад +4

    🙏🙏nabarikiwa sana , thanks Jesus for all you have done for me, nakumbuka mengi sana nikiusikiliza huu wimbo hakika Mungu mwema kwa kila jambo🥹🥹

  • @lucasalickmbila7748
    @lucasalickmbila7748 10 месяцев назад +3

    Kweli wokovu ni dhihilisho la pendo kuu la Yesu, kuamua kuwafia wenye dhambi. Tusichezee wokovu bali tuutunze

  • @Emanuel-fp5sy
    @Emanuel-fp5sy Год назад +7

    Ee Mungu wangu unisamehe baba yangu kwadhambi zangu zilizo kufanya uteseke mateso makali baba u2be roho yauruma hata 2kumbuke uliteseka kwajili yangu me naomba uruma yako baba

  • @NancyRichie-i6f
    @NancyRichie-i6f 10 месяцев назад +5

    nmekuwa nikitafuta huu wimbo sana thanks to God nimeupata

  • @rodahjuma8151
    @rodahjuma8151 6 месяцев назад +4

    Amen hakika alinipenda akalipia gharama😢😢😢😢😢😢

  • @catherinemdage4905
    @catherinemdage4905 11 месяцев назад +4

    Hakika wimbo mzuri sana, Mtunzi Mungu akubariki. Hapa ulitumika kwa viwango vya kimungu kabisa.

  • @glorykessy1797
    @glorykessy1797 7 месяцев назад +4

    Asante Yesu wangu Kwa kunipenda na kuchukua dhambi zangu na kunipa msamaha wa dhambi

  • @lensonmbilinyi4721
    @lensonmbilinyi4721 Год назад +14

    Baba yangu Danford Mbilinyi wakati wa uhai wake wake aliupenda sana huu wimbo na wakati wote aliuimba kwa ufundi mkubwa akishirikiana na marehemu bibi yangu daima ili nimkumbuke vyema hutumia wimbo huu kufanya meditation

  • @veronicamwandu-k4l
    @veronicamwandu-k4l Год назад +6

    Mungu awabariki sana na yesu awaone kwenye huduma yenu

  • @anettekandole8335
    @anettekandole8335 8 месяцев назад +3

    Amen Mutumishi wa Mungu tume bariki sana tena sana na wimbo

  • @TitusKinyaika
    @TitusKinyaika 8 месяцев назад +3

    Nllitafuta huu wimbo sana wimbo mtamu sana asante mungu kwa hekima ulio wafunulia hawa wana choir

  • @FortunataMacha-cl2to
    @FortunataMacha-cl2to 11 месяцев назад +6

    Napata amani sana ninaposikiliza huu wimbo Mungu awabariki

  • @AnneMwende-qj3gp
    @AnneMwende-qj3gp Год назад +8

    I love this song because Jesus died for me

  • @bupembonile8124
    @bupembonile8124 6 месяцев назад +1

    Asante sana Bwana Yesu. Tumepata ukombozi.

  • @flonachepkoech
    @flonachepkoech 6 месяцев назад +6

    Huu Wimbo unanibariki sana

  • @Yustina2002
    @Yustina2002 Год назад +4

    Naupenda san huu wimbo❤

  • @violetnasimiyu8718
    @violetnasimiyu8718 6 месяцев назад +3

    Haleluya sifana utukufu kwa BwanaYesu. Kazi uliyoifanya pale salabani imenifanya niwepo leo baba. I can'ttake it for granted it's by grace.

  • @AmiriJuma-pp2xf
    @AmiriJuma-pp2xf 5 месяцев назад +2

    nikisikiliza wimbo huu nafalijika sana mungu asante kwa kunips pumzi hii ambayo silipii hata mia mweche mungu aitwe mungu

  • @AlenAmon-fu6vz
    @AlenAmon-fu6vz 7 месяцев назад +3

    Namshukuru mungu nikiwa nausikiliza wimbo huu nasikia kuwa na upendo na kuzidii kumtumkiamungu aliye mbinguni,🎉

  • @Marrymassawe-mk3pe
    @Marrymassawe-mk3pe 4 месяца назад +1

    Napata bubujiko ndani ya Msamaha wa Yesu, nipe kibali chako Yesu kukujua zaidi kuliko wanadamu

  • @yasintawalyuba2444
    @yasintawalyuba2444 2 года назад +29

    Huu wimbo unipa faraja Sana ktk Hali zote .najikuta kuwa jasili Yesu Mwema Sana

    • @esthermoshili738
      @esthermoshili738 Год назад +1

      Yaaaani naaamka nao nashinda nao hauishi kichwani mwangu

  • @rebecaisemi8349
    @rebecaisemi8349 6 месяцев назад +5

    Mwenyezi Mungu ni mwema sana kumtoa mwanawe Yetu kristo kutufia msalabani kwa gharama kwa gharama ya kubwa ya mauti❤😅😅😅

  • @estherwaithera2376
    @estherwaithera2376 6 месяцев назад +5

    Kama sio kazi ya msalaba sijui ningekua wapi😢 Alilipa deni yangu 😭
    Thank you for this song

  • @godfreyhanda921
    @godfreyhanda921 Месяц назад +1

    Asante yesu kwa gharama ulioingia kwa ajili yangu sina la kukulipa ila kufungua roho yangu ukae ndani mwangu 🙏🙏

  • @paulkyule99
    @paulkyule99 6 месяцев назад +5

    Everytime I feel like I'm about to give this songs 🎵 reminds me alot and gives me strength ❤❤❤❤❤

  • @nellyakinyi4150
    @nellyakinyi4150 Месяц назад +1

    Msamaha....
    Gharama yangu ililipwa kwa Damu iliyo ya thamani🙏🙏
    Ahsante sana Kristo🙏

  • @ConjethaCharles
    @ConjethaCharles Год назад +6

    Nabarikiwa sana naposikiliza wimbo huu nazidi kufunguliwa kupitia wimbo huu🙏🙏

  • @kyarose609
    @kyarose609 9 месяцев назад +2

    Asante Yesu Kristo kwa kulipa dhambi zetu

  • @ayoubmwaitebele9174
    @ayoubmwaitebele9174 2 года назад +4

    Amina Amina Amina

  • @JanethNdalu
    @JanethNdalu 7 месяцев назад +1

    Na mimi nausikiliza bila kuchoka ,,nakupenda yeah

  • @ZenaisMosha-yo7gz
    @ZenaisMosha-yo7gz Год назад +4

    Nabarikiwa sana nahuu wimbo Mungu awabariki sana

  • @tinyblack-f7y
    @tinyblack-f7y 9 месяцев назад +1

    nabalikiwa sana kuusikia uuh wimbo asante yesu kwaajili ya wimbo uuh

  • @catherinemenganyi2645
    @catherinemenganyi2645 10 месяцев назад +3

    Alilipa deni zangu Bwana .
    So humbling to me ,my God is fairhful i beleive a testimony is being prepared for me God.
    You have been fairhful in my life and i thank you always❤

  • @bennjenga8641
    @bennjenga8641 Месяц назад +1

    Msamaha wa thambi kabisa,Mume wangu aliokoka baada ya kusikiza huu wimbo ..he cries every time he listens n sing along..thank you Holy Spirit for coming through this choir

  • @janekimani1170
    @janekimani1170 9 месяцев назад +4

    Amen and Amen. Lovely song

  • @BertaAtanasio
    @BertaAtanasio 2 месяца назад +1

    Nakupend yesu umenitua mbali kunamzigo alinitua nilikuwa nakufa lkn mungu amenifanya nionekane mpaya Tena asant yesu

  • @amosidavidjilili6572
    @amosidavidjilili6572 6 месяцев назад +4

    Mungu akubari kwa wimbo mzur

  • @MarthaKinya-l6i
    @MarthaKinya-l6i 12 дней назад

    Asante YESU kwa neema ya wokovu , Kama sio wewe YESU ningekuwa wa jehanam, Asante YESU,siwezi kukuchukuru ya kutosha , Asante YESU,.

  • @StellaRugazia
    @StellaRugazia 11 месяцев назад +6

    Nabarikiwa sana kuusikiliza huu wimbo roho mtakatifu mzima mzima

  • @BrianNjeru-vj7vw
    @BrianNjeru-vj7vw 3 месяца назад +2

    Huu wimbo n ujumbe mkuu na pia una ukombozi Dani yetu sisi

  • @marymafie1669
    @marymafie1669 9 месяцев назад +4

    Nausikiza muda huu! Bwana wetu Yesu Kristo atukuzwe kwa pendo ili kubwa kwetu

  • @lydiamercy1121
    @lydiamercy1121 28 дней назад

    Baba yangu mwema nisamehe dhambi zangu.Ulikufa msalabani kwa ajili yangu mimi.Nakupenda sana Yesu.Asante Yesu mwema😭😭😭😭😭😭😭

  • @victorkim1359
    @victorkim1359 7 месяцев назад +5

    The first time i had this song i was in a matatu and it really touched me till i cried. Such a powerful song indeed ❤. Glory to God forever

  • @Sarahsnafulawamalwa
    @Sarahsnafulawamalwa 2 месяца назад +2

    Kila siku asubui hiiii ndio alaam yangu❤❤❤❤❤❤❤❤❤