KWANINI HAVITOKEI KWA WAKATI (X) - PASTOR SUNBELLA KYANDO
HTML-код
- Опубликовано: 14 окт 2024
- Kuna wakati unamuomba sana Mungu na una uhakika kabisa kuwa amesikia lakini huoni akikujibu,wakati mwingine hadi vitu vyako vinakufa kabisa lakini humuoni akifanya chochote.Na watu wengi huumia sana na kufikiri kuwa Mungu amewaacha, kiuhalisia Mungu nyuma ya hayo maumivu yupo na anafanya kazi.Kuna wakati anaruhusu uaibike mbele za watu ili akija kukubariki akubariki mbele ya macho ya haohao walioshuhudia anguko lako.Mungu anasema kuwa ajapokuhuzunisha sana atakufurahisha sana.
Wakati Lazaro anaumwa na watu wakatumwa kwa Yesu kumuita humuoni Yesu akienda siku ile ile bali alikaa alipokuwa siku mbili zaidi,na hata alipoenda kwa Lazaro baada ya kuwaambia wanafunzi wake kuwa Lazaro ameshakufa,alienda wakati Lazaro ameshazikwa kwa siku nne.Katikati ya hiyo mauti na kuoza kabisa Yesu alirudisha uzima ndani yake.
Haijalishi unaona vitu vyako vimekufa kwa ukubwa gani,unachotakiwa kujua ni kuwa Mungu ana nguvu ya ufufuo..amefufua kwa wengine,atafufua na kwako pia.
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our RUclips: www.youtube.co....
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz
and Subscribe Pastor Sunbella Kyando RUclips
/ @pastorsunbellakyando
Amen mtumishi barikiwa sana
Kila ujumbe anayehubiri mchungaji huyu anayahubiri maisha yangu Mungu akubariki nayasikiza mahubiri yake kila siku from Mombasa Mungu akubariki Mungu amekutumia sana kwa ajili yangu naamini siku moja nitakuja ibada hapo kanisani nikitembea Tanzania
Mungu akubariki mnoooooo
Mungu aendeleekuinua huduma yenu inabariki inatufungua japo tuko mbali hakika yesu yuhai mahali hapo nimeona na kushuhudia nguvu za mungu zikinigusa.mungu aitizame na kuisimamia.
Amen🙏 Nami naamini ktk jina la Yesu Kristo vilivyo kufa vyote ktk maisha yangu vitafufuka Hallelujah.
Bishop naomba ukienda dodoma.nikuje Nam niweze kuonana na wewe.asante barikiwa Sana bishop Sanbella
Nimepata funzo Sana. Mungu akubariki mtumishi.
Uyo Ni mim kbsaa bishop Sanbella..NENO 📖 langu mwenyew.MUNGU amesema nam.ananifundishaa njia zake za uvumilivu.dah! Asante Sana pastor Sanbella 🙏🙏🙏🙏🙏 barikiwa Sana somo zuriii San.
Moyo wangu umetoa machozi mtumishi ubarikiwe neno limegusa maisha yangu Mungu anisaidie uvumilivu wa kiMungu mie siwezi kwa akili zangu
naamini kwamba mungu hajaniachilia gupo nami ata ndani ya shida zenyi nipo na pitilia bwana wangu atanivusha kwa ushindi,nakutumainia ee bwana mungu.
Asante sana kwa ujumbe mtumishi. Mimi naamini Mungu atanivusha.
Ameeen pastor
Powerful Word! Ubarikiwe Mtumishi 🙏🙏🙏
I'm really blessed with these teachings, be blessed Pastor Sunbella. I'm watching from Mbeya Tanzania 🙏💞
Amen, somo zuri sana
Amen