Maporomoko ya ardhi Kimende, kaunti ya Kiambu

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 май 2024
  • Ili kutoa nafasi kwa juhudi za uokoaji kuwatafuta watu watatu wanaodhaniwa wamefukiwa kwenye maporomoko ya udongo yaliyotokea katika eneo la Matathia eneo bunge la Kimende Lari, barabara ya Kimende Matathia imefungwa kwa muda. Wenyeji waliripoti kuwa jana saa nane mchana, kuwa watu walioathirika hawakuweza kukimbia tukio hilo la kusikitisha, ambalo lilizua hofu na wasiwasi. Juhudi za kutafuta miili inayodhaniwa kusalia ndani ya udongo kwenye eneo la ukubwa wa ekari moja inaongozwa na kundi la kukabiliana na majanga ya kaunti. Gavana Kimani Wamatangi wa Kaunti ya Kiambu amewataka watu kuwa waangalifu ili kuepuka maafa zaidi ya mvua na mafuriko. Brenda wanga anaungana nasi kwa njia ya simu kutoka Kimende.

Комментарии • 3

  • @cloudinhoabdi868
    @cloudinhoabdi868 13 дней назад

    Makiwa kwa familia zao. Mungu awatie nguvu

  • @magdalinenyambura3404
    @magdalinenyambura3404 12 дней назад

    Blood sister move in naijaria

  • @160501959
    @160501959 13 дней назад

    Can it happen in Kiambu really? It is only known to happen in Muranga. That has been the folklore.