ASKARI ALIYEPOTEA MWILI WAKE WAKUTWA MSITUNI
HTML-код
- Опубликовано: 28 сен 2024
- Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Daniel Shillah, amesema askari wa Kikosi cha Valantia (KVZ), Haji Machano Mohamed, ambaye alidaiwa kupotea akiwa katika mafunzo ya uongozi, mwili wake umepatikana ukiwa umeharibika msituni.
Kamanda Shillah amesema uchunguzi wa awali uliofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, ulibaini mwili huo ukiwa na nguo na viatu ambavyo vinafanana na alivyokuwa amevaa askari huyo siku alipopotea.
Kamanda Shillah amesema askari huyo alipotea tangu Agosti 8, 2024 na taarifa iliyotolewa Kituo cha Polisi Dunga, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja Agosti 9, 2024, askari huyo alikuwa akihudhuria mafunzo ya uongozi katika Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) Dunda.#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania.#Follow @radioonetanzani.
Usisahau kutufuatilia katika mitandao yetu ;
Subscribe to our RUclips Channel : bit.ly/itvtanzania
Facebook : bit.ly/2KeQNl3
Twitter : bit.ly/2XG7aii
Instagram : bit.ly/34KItmg
Mnatafuta mbinu ya kuwazuga ndugu wa marehemu,hamna lolote