SONGA MBELE (Jikung'ute mavumbi) - Paradise choir Ruanda moravian mbeya
HTML-код
- Опубликовано: 14 окт 2024
- Usitarajie mambo mazuri tu, hata mambo mabaya yatakufika. watakaokutendea ubaya huo ni ndugu wa karibu na wewe, kama neno la Mungu lisemavyo katika "mika 7:6c "adui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe" mathayo 10:36 " na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
hivyo huna sababu ya kurudi nyuma.... SONGA MBELE TU.
#lyrics
Inuka simama jikung'ute mavumbi, sawa umedharauliwa, na umekataliwa.
Jifunge mkanda, piga moyo konde, safari iendee.
ni kazi ya Mungu aliyekupa yupo, ndugu usikate tamaa, nakusihi songa mbele.
Walifanya kwa Yesu, wewe u nani?
Aliyemsaliti mwanafunzi wake.
Aliyemkana Petro/Simoni
Wewe u nani?
Usitarajie mazuri tu, na mabaya yanakuja, Yale ya kuumiza moyo ni mengi.
Watakao tenda ni ndugu, tena wa karibu nawe, wale ulio waamini kwa dhati.
Walifanya kwa Yesu, wewe u nani?
Aliyemsaliti mwanafunzi wake.
Aliyemkana Petro/Simoni
Wewe u nani?
Majaribu yangalipo kwetu, kutuimarisha, tusonge mbele.
hilo la mwanzo tu, mengi yanakuja. (Mtumishi wake)
(Ni kama hadithi, omba yasikupate, maumivu yake hayaelezeki, ni bora ungesimuliwa ila usisalitiwe , maumivu yake hayaelezeki. aiyooo lelele - aiyoo lelelelelele)
(Aliyekuita ni Mungu usihangaishwe na ya wanadamu, timiza kusudi lake - aaahh songa mbele)
Songa Mbele, Songa Mbele, mtazame Bwana yesu pekee
(Ni hali gani aliyokuwa nayo yusufu,kuuzwa utumwani na ndugu zake tena kaka zake,
Uchungu gani alioubeba moyoni, kuuzwa kwa potifa na ndungu zake*kaka zake*.......
laiti wangejua wanatimiza kusudi la Mungu kwa kuota ndoto, Hawakutambua wanamfanya kuwa waziri mkuu wao na vizazi vyao...
Aliyekuita ni Mungu usihangaishwe na ya wanadamu, timiza kusudi lake - Bwana atakulinda, tena atakubariki, taji anaiandaa na uzima wa milele.... aaahh songa mbele)
songa mbele, songa mbele, mtazame Bwana yesu pekee
(aiyooo lelel - aiyoo lelelelelele)
Appreciation
Song Composer and Writer - James Frank Mwidunda
Drums - Emmanuel Mwakamele
Bass Guitar - Musa Mwakanyamale
Solo Guitar - Ezekiel Mpimba
Rhythm Guitar - Dr. Tuntufye
Main piano - Jerry Mwakanyamale
AUX 1 - Sam Kameta (meta king)
AUX 2 - Joshua
Tombs - Emmanuel Ngoloke
Waooh hii nyimbo mmejua kuimba hakika wanatuumiza watu wa karibu.Mung awabariki sana
Aiseee huu wimbo unanbariki mno natamani kila nikija mbeya nikija kanisani uimbwe kuna huu na mwingine aiseee
Nawapenda bureeee ❤❤❤❤
Nabarikiwa sana na huu wimbo jaman
Mungu aitunze paradise choir
Tusitarajie mazuri tu, Yale ya kuumiza moyo ni mengi😢
My favorite choir,,,, kazi nzuriiiii❤
Hakika Mwenyezi Mungu awabariki sana ninyi watu, wimbo mzuri, ujumbe mzuri, mmeimba na Mungu akiwa nanyi, aina hizi za nyimbo zimekua n adimu mnooo
Naisubilia Kwa hamu video ya wimbo huu jamani mwenyezi Mungu awasaidie❤❤❤❤❤
Nilikuwa naisubiri kwa hamu video yenye mwonekano murua km hii , barikiwa sana Kaka, huu wimbo nimekuwa nautumia kusonga mbele katika vikwazo mablimbali kwenye huduma, Lkn pia nautumia mara nyingi kuwatia moyo wenzangu, Barikiweni sana
Jamani huu wimbo unanibariki sio utani na nauhitaji kweli mweee❤❤❤❤❤❤
Nawapenda watu wa Mungu kazi zenu ni njema mbele za Mungu wetu.Mungu awafunike.
Maumivu ya kusalitiwa yanararua Moyo, lakini kwa uweza wa Mungu na Neema yake inakuwezesha kusonga mbele.
Mungu aendelee kuwainua kwa viwango vya juu zaidi
Hongereni sana
Nawapenda Bure mungu azid kuinua vipawa vyenu mfike mbali
Aiseee nawapenda sana hii kwaya Mungu awatunze
Mungu awabarik sana
jamniii huu wimbo unanibariki sanaaaah sas video yake inatoka liniii??!
Barikiwa sana
Nawakubali sana mungu haendelee kuwapa nguvu na umoja wenu udumu
Mubarikiwe sana
Mungu awabariki nabalikwa sana na hii nyimbo
Kuna mahali huu wimbo umenivusha, Can't wait for the official video..
Wimbo bora kabisaaa❤❤
Mungu awe nanyi katika huduma mko vizuri sana
Kwaya yangu pendwa. Nawapenda
Amina
MUNGU awatunze na awakumbuke
❤❤❤
Nawakubali sana
Mungu awabariki sana kwa nyimbo nzuri na zenye maana uwa natamani sana kila wakati nisikilize nyimbo zenu
Najisikia raha kila ninapo usikiliza huu wimbo mtunzi naomba ni mjue
Amina sana mtunz
Jamani huu Wimbo uwekwe audio mack ni Mzuri sana una utukufu
Watumishi nabarikiwa sana kuwepo katikati yenu
Mungu azid kukuinua mwl James
Napokea, naomb Uendelee kuniombea...
Nimiongon mwa kwaya iliyobarikiwa
Wimbo mzuri sana lkn sauti haipo vizuri.
Jamani Kwanini hamtoi albam?mnatukwaza wapenzi wenu
Nimebarikiwa sanq aisee na huu winbo... And i would like to ask kama wewe ndo James Frank wa "Tunamtaka Tabitha"
Yaani hii ni live 😊😊😊😊
Hii Co live official release from the choir... But karibu ushiriki nasi katika ibada ya kufanya live recording ya album ya kwaya hii mwaka huu tareh 31/10/2024 tughimbe hall mbezi...... Ubarikiwe
Wimbo safi kabisa...where is the video that has clear sound?
31/10/2024, kwaya itafanya live recording.. Huu ni wimbo ambao upo kwenye hii project.. Naomb nitumie fursa hii kukukaribisha ushiriki pamoja nasi... Ubarikiwe
🎉🎉🎉❤
Jamani video bado????? Hii nyimbo nimeipenda sana sipati audio wala video
Hongereni sana
❤❤❤
❤❤❤
❤️❤️❤️❤️
❤❤❤❤
❤❤
❤❤❤❤❤❤❤