KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA MORNING GLORY (THE SCHOOL OF HEALING) 15/ 10/ 2024

Поделиться
HTML-код
  • Опубликовано: 14 окт 2024
  • KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA MORNING GLORY (THE SCHOOL OF HEALING)15/ 10/ 2024
    UJUMBE WA LEO: SIRI ILIYOJIFICHA KATIKA UTOAJI SADAKA
    Malaki 3 : 10A
    Mwanzo 4 : 3 - 7
    Mwanzo 21 : 14 - 19
    Mwanzo 22 : 6 - 7
    Mwanzo 15 : 7 - 13

    Malaki 3 : 10A
    10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
    Mwanzo 4 : 3 - 7
    3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.
    4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;
    5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
    6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
    7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
    Mwanzo 21 : 14 - 19
    14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.
    15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.
    16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.
    17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.
    18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.
    19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.
    Mwanzo 22 : 6 - 7
    6 Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.
    7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?
    Mwanzo 15 : 7 - 13
    7 Kisha akamwambia, Mimi ni Bwana, niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi.
    8 Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi?
    9 Akamwambia, Unipatie ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa.
    10 Akampatia hao wote, akawapasua vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua.
    11 Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza.
    12 Na jua lilipokuwa likichwa usingizi mzito ulimshika Abramu, hofu ya giza kuu ikamwangukia.
    13 Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.
    Mhubiri: Mwl. Keneth Mushi
    Kwa maombi na ushauri :
    Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
    Mch. Msaidizi: Anna Kuyonga
    Simu: +255 713 553 443
    RUclips: Kijitonyama Lutheran church
    Barua Pepe: Kijitonyamalutheran@gmail.com

Комментарии •